Kwa nini mungu mwenye uwezo wa yote,upendo wa yote na ujuzi wa yote aruhusu uasi wa adam na hawa???!
Mungu ni muanzilishi wa Democrasia.
Na sio Dicteta, hivyo toka uumbaji alitaka kuunda utawala wa hiari yani wa kidemocrasia.
Alipomuumba Malaika akampa uhuru wa kuchagua kumwabudu yeye na kuwa chini ya himaya yake au kufuata anachopenda yeye.
Lusifer akaiona hiyo fulsa ya kuasi na akaichagua ili asilazimike kumwabudu Mungu, Mungu akamruhusu kuunda makao na mamlaka yake na pia kuweza kuwashawiishi watu wamtii.
Kwa binadamu pia,
Mungu alipomwumba Adam hakumficha kitu, alimwambia kuna matunda ya aina tatu nimeyapanda huko bustanini utakapo ishi.
Kuna tunda la chakula unaruhusiwa kula,
Kuna tunda la Uzima nalo pia kula ili uwe mzima mda wote.
Kuna tunda la kujua mema na mabaya, hili usile, ukila hakika utakufa.
Adam alitii vyote akaishi vizuri tu akiwa na afya njema na asiyekufa.
Mungu alipomuumbia Adam mke Hawa au Eve kwa kimombo, Eva alielezwa kila kitu kuhusu matunda yale, lipi ale na lipi asile na kwasababu gani.
Ili kuendeleza utawala wa Democrasia Mungu alimruhusu Lusifer kumshawishi Eva ili aamue kumtii Mungu au Roho nyingine.
Eva akashwawishika na maneno ya Lusifer akamshawishi na Adam mumewe wote wakala tunda la kutambua mema na mabaya na baada ya kula tu wakajiona wako uchi.
Mungu akawafukuza Adam na Eva katika bustani yake kwani hakutaka wale tunda la uzima ili wasije wakaishi milele katika hali yao ya uovu.
Pamoja na kumkaidi Mungu, bado Mungu alikuwa anawapenda akawapa mavazi na kuwapa chakula ambacho kitazalishwa na wao kwa kuilima ardhi.
Wakaanza maisha ya kujitegemea.
Mungu akaendelea kuwasilina nao ili kuwafundisha kuwa wakitaka kuurudia tena ufalme wa Mungu lazima wafe kwanza ili kuuacha mwili wao wa awali na kuuvaa mpya.
Baadae wakaletewa na Manabii ili wazidi kuwakumbusha namna ya kumrudia Mungu.
Hata hii leo binadamu halazimishwi kumtii Mungu, anahiari kumtii Mungu,
NIPO AMBAYE NIPO, au Shetani Lusifer.
Ndivyo Mungu anavyotaka iwe na imekuwa.
Kuna watu wanalalamika eti mbona Mungu hazuii mauaji yanayotendeka sasa.
Jibi ni kuwa Mungu amemwumba Binadamu na kumpa mamlaka ya kutawala dunia na vilivyomo, na amempa maelezo kuwa ili atawale vizuri inabidi afuate amri zake zinazoongoza kufanya amani hapa duniani.
Binadamu hawataki kufuata hizo amri na kuamua kufanya uasi kama,
Kuua
Kuroga
Kuharibu
Kuiba
Nk.
Hayo mambo yapo ktk mamlaka ya binadamu na yeye ndiye wa kulaumiwa panapotokea shida kama hizo.
Hivyo binadamu tutimize majukumu yetu ya kuleta amani duniani na sio unamchinja mtu bila hatia halafu unamsingizia Mungu.
Viungo vya mwili tulivyopewa ni vya kutuwezesha kujenga jamii na sio kuiharibu.