Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

As to 2010, wakristo ulimwenguni kote walikuwa asilimia 30 tu ya watu wote duniani, hii ni pamoja na mimi na Kiranga ambao tubatizwa lakini baadae tukagundua ni uzushi, ukituondoa, idadi inapungua zaidi, wewe 42_007 nani kakuambia believer ni wengi zaidi?
Anaweza kuwa kagundua chombo cha kuingia moyoni kwa kila mtu.

Tukiangalia matendo ya watu, wasioamini uwepo wa Mungu ni wengi sana.

Na hao wengi wao tunawaona wanasema Mungu yupo. Lakini matendo yao yanaonesha hawaamini wanachosema.

Wanaoamini Mungu wangekuwa wengi dunia isingekuwa na vita na mauaji hivi.
 
Ahahaa, kwa hiyo kuna maandiko ambayo Mungu kasema mwenyewe na kuna yale ambayo ameelezewa tu na waandishi wa biblia, na mtizamo wako, hayo aliyoelezewa tu na akina Yohana umeyakataa, sio ya kweli au ni kwa nini umeyakataa?
aliyoeleza yohana sijayakataa ni ya kweli kabisa sema kwa hoja aliyoijenga kwakua Mungu ni pendo basi asihukumu wenye dhambi icho ndo ninachokikataa ...uki relax utanielewa
 
aliyoeleza yohana sijayakataa ni ya kweli kabisa sema kwa hoja aliyoijenga kwakua Mungu ni pendo basi asihukumu wenye dhambi icho ndo ninachokikataa ...uki relax utanielewa
Kwa nini Mungu hakuumba ulimwengu ambao dhambi haiwezekani kufanyika?

Kama yupo, kaumba ulimwengu huu ambao watu hatuwezi kurudi nyuma katika muda.

Kwa nini hakuuwekea ulimwengu huu sheria ya asili kama hiyo ya kuzuia watu kurudi nyuma katika muda, ikataze dhambi kuwezekana?
 
u

Mungu ni roho siwezi kuithibitisha kwa kukuonyesha kwa kushika, je nawewe unaweza ukanionyesha roho yako?
Ume assume nakubali roho ipo na mimi nina roho.

Kama unavyo assume Mungu yupo.

Roho nayo haipo. Ndiyo maana wewe na mimi hatuwezi kuthibitisha ipo.

Unatumia uongo wa roho kuhalalisha uongo wa Mungu.

Thibitisha Mungu yupo. Thibitisha roho ipo.

Unajiongezea maswali tu.
 
Kwa nini Mungu hakuumba ulimwengu ambao dhambi haiwezekani kufanyika?

Kama yupo, kaumba ulimwengu huu ambao watu hatuwezi kurudi nyuma katika muda.

Kwa nini hakuuwekea ulimwengu huu sheria ya asili kama hiyo ya kuzuia watu kurudi nyuma katika muda, ikataze dhambi kuwezekana?
kumbe unaamini Mungu kaumba ulimwengu ila tuu hakuumba ulimwengu wa kutozuia dhambi kufanyika?
 
Mimi kichwani sio mweupe.. Nina nywele fupi nyeusi
Kila kitu katika maisha kina utaratibu wake... Hata kwenye kuhesabu huwezi kuanza na moja kisha ukaruka mbili na kuendelea na tatu... Vivyo hivyo kwenye kuulizwa unatakiwa kutoa jibu sio blah blah
Nakuuliza tena una AKILI ama huna AKILI!? Jibu ndio au hapana. Hayo mengine yatafuata
Una nywele sawa, lakini umetambua uweupe ktk ndonga yako ni kuwa haung,amui vitu kuvipa maana zaidi ya kile utakacho.

Wewe ni mzuri ktk kuandika makala likija suala la ujengaji hoja mae to man upo mweupe.

Unapozungumzia akili unazungumzia kwa maana hipi?

Haujatoa maana ya akili sasa ntajua una maanisha nini?

Wengne wametoa maana ya akili kuwa ni kudadavua vipi ktk postive na negative.

Mwingne kadai akili ni kutambua uwepo wa mungu nashangaa wewe hautaki kutoa maana ya akili.

Akili ni nini?

Ili ujibiwe kama ninazo, sina au sijui.
 
Ume assume nakubali roho ipo na mimi nina roho.

Kama unavyo assume Mungu yupo.

Roho nayo haipo. Ndiyo maana wewe na mimi hatuwezi kuthibitisha ipo.

Unatumia uongo wa roho kuhalalisha uongo wa Mungu.

Thibitisha Mungu yupo. Thibitisha roho ipo.

Unajiongezea maswali tu.
Mungu yupo kwakua ameumba ulimwengu

roho ipo maana isinge kuepo kiumbe kinge ishi milele
 
Una nywele sawa, lakini umetambua uweupe ktk ndonga yako ni kuwa haung,amui vitu kuvipa maana zaidi ya kile utakacho.

Wewe ni mzuri ktk kuandika makala likija suala la ujengaji hoja mae to man upo mweupe.

Unapozungumzia akili unazungumzia kwa maana hipi?

Haujatoa maana ya akili sasa ntajua una maanisha nini?

Wengne wametoa maana ya akili kuwa ni kudadavua vipi ktk postive na negative.

Mwingne kadai akili ni kutambua uwepo wa mungu nashangaa wewe hautaki kutoa maana ya akili.

Akili ni nini?

Ili ujibiwe kama ninazo, sina au sijui.
Hawezi kujibu.

Hata anachokiulizia hajui ni kipi.
 
Mungu yupo kwakua ameumba ulimwengu

roho ipo maana isinge kuepo kiumbe kinge ishi milele
Unawezaje kuthibitisha Mungu kaumba ulimwengu? Unawezaje kuthibitisha hii si hadithi tu?

Unahakikishaje kiumbe kinaishi milele? Unawezaje kuthibitisha hii si hadithi tu?
 
Kwa nini Mungu hakuumba ulimwengu ambao dhambi haiwezekani kufanyika?

Kama yupo, kaumba ulimwengu huu ambao watu hatuwezi kurudi nyuma katika muda.

Kwa nini hakuuwekea ulimwengu huu sheria ya asili kama hiyo ya kuzuia watu kurudi nyuma katika muda, ikataze dhambi kuwezekana?
hapa umekubali Mungu kaumba ulimwengu ila tu umetaka ulimwengu ambao binadamu ashinde dhambi,turudi nyuma kutubbu
 
Ukishamwambia mtu mwingine Mungu yupo as a statement if fact, ushaindoka kwenye imani. Umeingia kwenye mjadala wa fact.

Unaelewa hilo?
Wewe unaposema hakuna mungu huwa hausemi kuwa hakuna mungu kwa wale wenye kusema uwepo wa mungu ni fact.
 
hapa umekubali Mungu kaumba ulimwengu ila tu umetaka ulimwengu ambao binadamu ashinde dhambi,turudi nyuma kutubbu
Neno gani linakufanya ufikiri nimekubali hivyo?

Unafahamu immanent criticism ni nini?
 
Day 6.
Mjadala umekwama ktk swali la msingi la akili ni nini? Wafuatiliaji wakitamani kuona majibu na swali litakalo fuata kutoka katika pande mbili vutani za mjadala.

AKILI NI NINI?
 
Unawezaje kuthibitisha Mungu kaumba ulimwengu? Unawezaje kuthibitisha hii si hadithi tu?

Unahakikishaje kiumbe kinaishi milele? Unawezaje kuthibitisha hii si hadithi tu?
nathibitisha kwa maandiko soma mwanzo 1;1
swali la pili unijibu wewe unaekataa roho kuwepo
 
Day 6.
Mjadala umekwama ktk swali la msingi la akili ni nini? Wafuatiliaji wakitamani kuona majibu na swali litakalo fuata kutoka katika pande mbili vutani za mjadala.

AKILI NI NINI?
Mshana kakimbia mjadala. Naendelea na wengine.

Kuna wawili wamejibu swali hilo na nimewajibu kama nina au sina akili kwa myktadha wao na tymeendelea na mjadala.

Mshana kakimbia mjadala.
 
As to 2010, wakristo ulimwenguni kote walikuwa asilimia 30 tu ya watu wote duniani, hii ni pamoja na mimi na Kiranga ambao tubatizwa lakini baadae tukagundua ni uzushi, ukituondoa, idadi inapungua zaidi, wewe 42_007 nani kakuambia believer ni wengi zaidi?
vp kuhusu hao 70%...???
 
Back
Top Bottom