Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Hivi kuna uzi wako full ukielezea hicho ulichosema?

Kama upo naomba link
Kuna maandiko mengi sana...google andiko moja LA MTU anaitwa Bertrand Russell " Why I am Not a Christian" itakusaidia kuanza kuona contradictions
 
Uasi wa adamu na hawa ndio ulioleta kifo cha kimwili ila halikua kusudi la Mungu binadamu kufa
Kwa nini mungu mwenye uwezo wa yote,upendo wa yote na ujuzi wa yote aruhusu uasi wa adam na hawa???!
 
..mjadala wa kufikirisha huu...najua kiranga amemshika mshana pabaya....kudos ngosha!

..ngoja tumsaidiege mshana...Ili aweze kuendelea na alichotaka toka kwa kiranga..

..kwa uelewa wangu...akili au kwa kimombo ' intelligence' au 'intellect'au 'intellectual capacity' au 'mental capacity' au hata wengine humu wameita mind.......Ni uwezo wa kufikiri, kuelewa na kufanya maamuzi sahihi kwa kiwango kikubwa....
..akili (intelligence) hutofautiana Kati ya mtu na mtu na kwa maana hiyo kila mtu ana kiwango Fulani cha akili....na kwa maana hiyo swali la je mtu ana akili ama la si sahihi....

....kwasababu watu hutofautiana akili....basi kumewekwa kipimo cha akili ambacho huitwa intelligence quotient (ama IQ)....ambacho huonesha viwango tofauti vya akili Kati ya mtu na mtu....
...hii ni namna mimi navyoelewa akili....kama itawasaidia kwenye mjadala wenu...
......
......ole Ngika ole Ngalo ole Nzubha cho!
 
Sasa ukijibu kwamba huna/unazo akili utakuwa umekosea nini?

Jibu kwa muktadha wako!

Mshana Jr akisema si hivyo ndio aseme alikuwa anamaanisha akili kwa maana gani?
Nishajibu swali mara mbili.

Kwa watu walionipa muktadha wa swali.

Sina shida kujibu swali.

Nina shida kujibu pasipo na swali.

Mshana hajauliza swali. Ameshindwa kuuliza sali.
 
Kuna maandiko mengi sana...google andiko moja LA MTU anaitwa Bertrand Russell " Why I am Not a Christian" itakusaidia kuanza kuona contradictions

Kuna andiko lingine ambalo linaelezea hizo contradictions apart from basing on christian/jew/muslim?
 
Hapo naona umesema hayupo

Unaweza thibitisha hayupo?
Mungu muweza yote, mwenye upendowote na ujuzi wote hayupo.

Hayupo kwa sababu dhana ya kuwepo kwake ina contradiction.

Ina contradiction kwa sababu Mungu huyo angekuwepo, duniaisingekuwa na mabaya yoyote.

Lakini dunia imejaa mabaya.

Kwa sababu Mungu huyo hayupo.

Angekuwepo, asingeumba dunia inayowezekana kuwa na mabaya kamahii.

Ukisema yupo, thibitisha kwamba yupo.
 
Unabishana na watu ambao hata basics tu za philosophy of religion hawajui...watu wanakuja kwenye debate wakati hawajawasoma kina St. Aquinas kujua hoja zao za uwepo Wa mungu. Wanakuja na majibu ya Katekisimu Yetu.
ST. Aquinas mbali kote huko, Alvin Plantinga tu hawajawahi hata kumsikia.
 
Kuna andiko lingine ambalo linaelezea hizo contradictions apart from basing on christian/jew/muslim?
Nimeandikasana hapa contradiction za omnipotent, omniscient, omni benevolent godhead ambaye kaumba ulimwengu huu wenye mabaya.

Tafuta kitabu kinaitwa "The Philosophy of Religion: An Anthology"

Humo wamekusanya arguments zaote za kutetea kuwepo kwa Mungu na za kupinga kuwepokwa Mungu.

Kutoka dini zote kubwa na tamaduni zote kubwa za dunia.

Sasa ukisoma vitabu kama hivyo halafu ukaja kubishana na kina Mshana, unaona tofauti kama usiku na mchana katika level ya debate.

Unatoka kusomadebates za Aquinas, Anselm,Augustine, Plantinga, Russell etc.

Unaenda kubishana na mtu ambaye akiulizwa "akili ni nini?" anaogopa kujibu!
 
Malumbano ya kipumbafu yanachosha.Mungu awepo asiwepo nyie mtaishi miaka yenu 70 kisha mtakufa tu.Mavumbini mtarudi.
Kufa ni ushahidikwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo angeumba ulimwengu ambao kifo hakiwezekani kuwepo kwa viumbe wake vipenzi.
 
Back
Top Bottom