Swali la msingi hawezi kulijibu kwa sababu lina mkanganyiko,linahitaji ufafanuzi kwanza!.....yeye anataka huo mkanganyiko umalizwe kwanza!
Kuweka msisitizo hapo, kuna watu wawili tayari (sio Mshana), washanijibu akili ni nini kwa tafsiri zao.
Na nishawajibu kama nina akili au sina.
Kuna mmoja kasema akili ni uwezo wa kutambua uwepo wa Mungu.
Nikamwambia kwa tafsiri hiyo sina akili, maana sijaweza kutambua uwepo wa Mungu.
Mwingine kaniambia akili ni uwezo wa kupambanua mambo negative na positive (I am paraphrasing). Nikamwambia kwa msingi huo akili ninazo maana nimeweza kudadavua hoja ya uwepo wa Mungu kwa "proof by contradiction" ambayo inaanza upande wa positive kwa assumption kwamba Mungu yupo, halafu nikaonesha contradictions katika imani hiyo, kwamba imetumia wrong assumptions, nikaishusha imani ikawa negative kwamba Mungu hayupo.
Hawa watu wawili walionipa tafsiri zao za akili ni nini, nimewambia nina akili au sina akili, kwa kuelezea kimantiki, kwa nini, kutokana na definition zaoza akili.
Sasa hapo utaona sina tatizo kujibu swali, nataka nielewe muktadha na definition ili nijikite kwenye swali linaloulizwa, si ninalotaka kujibu mimi.
Sasa Mshana kwa nini anaona ugumu kuniambia akili ni nini kwa mujibu wa definition na muktadha anaouliza?
Mbona wenzake wawili hao nimewajibu vizuri tu?
Yeye kwa nini hafunguki nimjibu?