Titicomb
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 16,692
- 30,967
Nafikiri hapo kwenye kumtaka Mshana Jr akufafanulie maana ya akili anayokusudia ina hoja yenye mashiko.Mpakasasa sijaelewakwa niniMshana anaona ugumu kujibu swali langu.
Kuna watu wanafikiri akijibu swali languanakuwa kashajijibu swali lake mwenyewe kwangu.
Fikra hizi ni potofu.
Swali la Mshana kwangu ni kama nina akili. Swali langu kwake ni akili ninini.
Akinipa maelezo ya akili ni nini, bado nitakuwa na swali la kujibu kama ninayo hiyo akili au sina.
Hata sioni kwa nini anaona ugumu kunijibu.
Kwa sababu mtu anaweza kukuuliza vipi jana ulikula bata?
Unaweza kujibu ndio ukidhania bata yule ndege kitoweo kumbe anaekuuliza anakusudia bata kama kitendo cha kufanya starehe kama vijana wa sasa wanavyosema kwa lugha ya mtaani.