Sio mara ya kwanza kulisema hili.
Inapokuja suala la Mungu, ni la imani.
Kama unaamini, unaendelea na huo mrengo na kama hauamini, uko sawa kuendelea na mambo mengine.
Pili, huyo Mungu ambae anataka atetewe na Samaritan ndio awe Mungu, hawezi kujithibitisha mwenyewe, hata mimi simtaki na sio wajibu wangu kuthibitisha.
Mwisho, tofauti kati ya wanaoamini au kutoamini uwepo wa Mungu, haionekani thahiri moja kwa moja. Wote tunasoma, tunavuta hewa ileile, tunaugua, tunakufa, tunaajiriwa na kufanya kazi bila kubaguliwa kwa vigezo vya imani kuhusu uwepo wa Mungu. Hapo ndio nnaposhindwa kuelewa wasioamini kysema wanaoamini wana upeo mdogo au wanaamini uongo. Sijaelewa hii inawaathiri vipi wao. Binafsi asiyeamini uwepo wa Mungu hanipi shida.
Sasa
Kiranga hizo sifa za Mungu hapo juu umezipata wapi?
Naona umeamua tuendelee kujibizana.