Kiranga sio atheist ni non-believer

Kiranga sio atheist ni non-believer

Tz mbongo ,

Mimi nadhani tufanye hivii,

Kwa sababu lengo kuu la uzi huu (hasa sisi third parties(tusio na upande)) ni kujifunza na kushare experiences, basi nitoe rai kwa wachangiaji wakuu (Kiranga , Mshana Jr et al) tujadili uwepo wa mungu bila kuegemea katika maandiko fulani ya dini fulani, kwa sababu, dini ziko nyingi na ninafikiri sio lengo la mwenye uzi ku critesize dini ya mtu!!
 
Hahaha haya, kumbe huna proof hata moja, basi endelea kuamini, acha kuchamba wenzako ambao wanaamini tofauti na wewe. Ni msimamo tofauti tu, sio wote wanafatafata tu mambo yasiyo na proof. Na unavyomsema jamaa kua anafuata wikipedia huku imeandikwa na binadamu, unasahau kua vitu vilivyoandikwa kwenye wikipedia tunaweza kuviprove, wewe unatumia simu unapost JF dunia nzima tunaona, hiyo ni proof enough kua tunachofanya tunakijua hatuendi kwa imani, tunaenda kwa proof.
 
Ni kama nianze kumfundisha sisimizi calculus kwa lengo la kumuelewesha Poincare's conjecture ili tuitumie katika ku solve equations za Calabi Yau manifold katika the eleventh spatial dimension and third temporal axis of string theory!

Ni kweli kujibu nilkichokuuliza kwamba kwenye kitu ulichoandika mwenyewe kunahitaji uelewa wa imminent critique?
Sio suala la kuonyesha unajua nini na uelewa wako ni wa kiwango gani, kama havisaidii au havina mchango vinapohitajika hakuna tija yeyote.
 
Tz mbongo ,

Mimi nadhani tufanye hivii,

Kwa sababu lengo kuu la uzi huu (hasa sisi third parties(tusio na upande)) ni kujifunza na kushare experiences, basi nitoe rai kwa wachangiaji wakuu (Kiranga , Mshana Jr et al) tujadili uwepo wa mungu bila kuegemea katika maandiko fulani ya dini fulani, kwa sababu, dini ziko nyingi na ninafikiri sio lengo la mwenye uzi ku critesize dini ya mtu!!
Itakuwa vizuri ikiwezekana kufanyika hivyo.
 
Hivi kumbe maneno yanaweza kuthibitisha?

Nimekuuliza mara kwa mara kwamba Mungu amedanganya? Unajibu amedanganya na kuleta maandiko.

Kwa kuwa unadai Mungu AMEDANGANYA, alikudanganya namna gani?

Ulichokileta hapa ni vitabu kisha unasema Mungu amedanganya.

Unaweza kuthibitisha alivyokudanganya? (Japo wakati huohuo unadai hayupo).
Kwa hiyo biblia au quran maneno ya nani
 
Hahaha haya, kumbe huna proof hata moja, basi endelea kuamini, acha kuchamba wenzako ambao wanaamini tofauti na wewe. Ni msimamo tofauti tu, sio wote wanafatafata tu mambo yasiyo na proof. Na unavyomsema jamaa kua anafuata wikipedia huku imeandikwa na binadamu, unasahau kua vitu vilivyoandikwa kwenye wikipedia tunaweza kuviprove, wewe unatumia simu unapost JF dunia nzima tunaona, hiyo ni proof enough kua tunachofanya tunakijua hatuendi kwa imani, tunaenda kwa proof.
Kuna watu wanashinda kesi mahakamani na kuonekana hawana hatia kwa kukosekana ushahidi ijapokuwa ni kweli walikuwa na unaweza ukawa huna makosa ila ushahidi ukaonesha una makosa.
 
Kwahiyo unataka kusema mungu hana uwezo wote,uwezo wake una mipaka hawezi kuumba vyovyote vile ajisikiavyo?

Hivyo ndiyo unamaanisha ama?
Sijui kama umenifuatilia toka mwanzo.

Nitasemaje uwezo wake una mipaka wakati kwanza hayupo!?

Mungu mwenye uwezo wote,upendo wote na ujuzi wote hayupo.

Na hatusemi hayupo kwa sababu hatumuoni,tunasema hayupo kwa sababu dhana ya uwepo wake inajipinga yenyewe hata kabla ya kupigwa na yeyote.

Ni sawa na baba mzazi mwenye umri wa miaka arobaini akwambie mtoto wake wa kwanza ana umri wa miaka hamsini.
Sasa hapo utasemaje kwamba mzazi huyu hana uwezo wa kuzaa ajisikiavyo!?.

Jibu rahisi hapo ni kuwa huyo mzazi kwanza hayupo.Na hayupo si kwa maana hatumuoni(haonekani),hayupo kwa maana ya haiwezekani mzazi kuzaa (biologically) mtoto mwenye umri unaomzidi.
 
Sijui kama umenifuatilia toka mwanzo.

Nitasemaje uwezo wake una mipaka wakati kwanza hayupo!?

Mungu mwenye uwezo wote,upendo wote na ujuzi wote hayupo.

Na hatusemi hayupo kwa sababu hatumuoni,tunasema hayupo kwa sababu dhana ya uwepo wake inajipinga yenyewe hata kabla ya kupigwa na yeyote.

Ni sawa na baba mzazi mwenye umri wa miaka arobaini akwambie mtoto wake wa kwanza ana umri wa miaka hamsini.
Sasa hapo utasemaje kwamba mzazi huyu hana uwezo wa kuzaa ajisikiavyo!?.

Jibu rahisi hapo ni kuwa huyo mzazi kwanza hayupo.Na hayupo si kwa maana hatumuoni(haonekani),hayupo kwa maana ya haiwezekani mzazi kuzaa (biologically) mtoto mwenye umri unaomzidi.

Emmanuel J. Buyamba, sifa ya Mungu mwenye uwezo wote, upendo wote na nguvu zote, ni mafundisho ya baadhi ya dini kuelekea kile wanachokiamini.
Sifa hiyo, kama mtu sio wa imani (dini) hiyo, ni vigumu sana kuaminika kwa sababu ya mkanganyiko wake (hasa kwa wasiowaamini husika).

Kutokana na hilo, sidhani kama ni sahihi ku conclude general (kuwa mungu hayupo), from specific religion (hiyo inayoamini hivyo).

Nadhani bwana BUYAMBA , itapendeza kama utatoa fact za mungu kuwa hayupo, kwa kutumia general fact (zisizoegemea upande flani wa dini)
 
Mi naamini uwepo wa mungu aliye hai muumba bingu na ardhi lkn suala moja tu linalonitatizaga "Urithi wa dhambi"yaani makosa alifanyaga Babu yako huko nineteen kweusi Leo hii wewe unatakiwa uwajibike, hapo...Mkuu Mshana Jr hebu nipe kasomo kidogo kuhusu hili suala la kurithi dhambi limekaaje kiimani...maana inawezekana tunapambana Shaka lkn hatutoki kumbe tunalipa dhambi za wetu huko walipo....
 
Emmanuel J. Buyamba, sifa ya Mungu mwenye uwezo wote, upendo wote na nguvu zote, ni mafundisho ya baadhi ya dini kuelekea kile wanachokiamini.
Sifa hiyo, kama mtu sio wa imani (dini) hiyo, ni vigumu sana kuaminika kwa sababu ya mkanganyiko wake (hasa kwa wasiowaamini husika).

Kutokana na hilo, sidhani kama ni sahihi ku conclude general (kuwa mungu hayupo), from specific religion (hiyo inayoamini hivyo).

Nadhani bwana BUYAMBA , itapendeza kama utatoa fact za mungu kuwa hayupo, kwa kutumia general fact (zisizoegemea upande flani wa dini)
Unaweza ukanitajia dini ambazo haziamini kuwa Mungu wao hana uwezo wote,upendo wote na ujuzi wote!?

Ninayesema Mungu wa namna hiyo hayupo si wajibu wangu kuthibitisha hayupo.Ni wajibu wa wale wanaoamini yupo kuthibitisha uwepo wake.Mimi siwezi kuthibitsha hayupo maana kitu ambacho hakipo hakiwezi kuthibitishwa hakipo.

Kaka yangu Kiranga huwa anamfano mzuri sana wa kuwa, polisi wanapokutuhumu kwamba una madawa ya kulevya nyumbani kwako, hawaji na kukuamrisha uthibitishe kuwa nyumba yako haina madawa.

Nii wajibu wao kuthibitisha tuhuma hizo kwa kufanya uchunguzi hadi wayaone.Hii ni kwa sababu hata ukitoa vitanda na makochi yote nje kuonesha madawa hayapo bado watakwambia umeyaficha mahala pengine.

Unaposema nyumba yako haina madawa hupaswi kuthibitisha kuwa hayapo.Ni wajibu wa wanaosema yapo kuonesha/kuthibitisha yalipo.
 
Mi naamini uwepo wa mungu aliye hai muumba bingu na ardhi lkn suala moja tu linalonitatizaga "Urithi wa dhambi"yaani makosa alifanyaga Babu yako huko nineteen kweusi Leo hii wewe unatakiwa uwajibike, hapo...Mkuu Mshana Jr hebu nipe kasomo kidogo kuhusu hili suala la kurithi dhambi limekaaje kiimani...maana inawezekana tunapambana Shaka lkn hatutoki kumbe tunalipa dhambi za wetu huko walipo....
Swali zuri sana.

Kwamba unasumbuka kuwatolea sadaka kina Mshana Jr kumbe tayari babu wa babu yako alishakukaanga zamani na hivyo una laana inayokusubiri ikupeleke motoni.

Kazi kwelikweli!!
 
Sijui kama umenifuatilia toka mwanzo.

Nitasemaje uwezo wake una mipaka wakati kwanza hayupo!?

Mungu mwenye uwezo wote,upendo wote na ujuzi wote hayupo.

Na hatusemi hayupo kwa sababu hatumuoni,tunasema hayupo kwa sababu dhana ya uwepo wake inajipinga yenyewe hata kabla ya kupigwa na yeyote.

Ni sawa na baba mzazi mwenye umri wa miaka arobaini akwambie mtoto wake wa kwanza ana umri wa miaka hamsini.
Sasa hapo utasemaje kwamba mzazi huyu hana uwezo wa kuzaa ajisikiavyo!?.

Jibu rahisi hapo ni kuwa huyo mzazi kwanza hayupo.Na hayupo si kwa maana hatumuoni(haonekani),hayupo kwa maana ya haiwezekani mzazi kuzaa (biologically) mtoto mwenye umri unaomzidi.
Tunazungumzia kuhusu mungu. Umeleta hoja ya kuhusu uwezo wote na upendo wote wa mungu,sasa nimehoji kutokana na unachokieleza unakuja kuniambia tunachokizungumzia hakipo!

Sasa kama ni hivyo kuna haja gani ya kuzungumzia hili suala?
 
Tunazungumzia kuhusu mungu. Umeleta hoja ya kuhusu uwezo wote na upendo wote wa mungu,sasa nimehoji kutokana na unachokieleza unakuja kuniambia tunachokizungumzia hakipo!

Sasa kama ni hivyo kuna haja gani ya kuzungumzia hili suala?
Thibitisha kwanza uwepo wa huyo Mungu maana unataka tuzungumzie uwepo wa baba mzazi mwenye miaka arobaini halafu mwanae eti ana miaka hamsini.

Thibitisha Mungu yupo ndiyo tuendelee na mengine sasa.
 
Unaweza ukanitajia dini ambazo haziamini kuwa Mungu wao hana uwezo wote,upendo wote na ujuzi wote!?

Ninayesema Mungu wa namna hiyo hayupo si wajibu wangu kuthibitisha hayupo.Ni wajibu wa wale wanaoamini yupo kuthibitisha uwepo wake.Mimi siwezi kuthibitsha hayupo maana kitu ambacho hakipo hakiwezi kuthibitishwa hakipo.

Kaka yangu Kiranga huwa anamfano mzuri sana wa kuwa, polisi wanapokutuhumu kwamba una madawa ya kulevya nyumbani kwako, hawaji na kukuamrisha uthibitishe kuwa nyumba yako haina madawa.

Nii wajibu wao kuthibitisha tuhuma hizo kwa kufanya uchunguzi hadi wayaone.Hii ni kwa sababu hata ukitoa vitanda na makochi yote nje kuonesha madawa hayapo bado watakwambia umeyaficha mahala pengine.

Unaposema nyumba yako haina madawa hupaswi kuthibitisha kuwa hayapo.Ni wajibu wa wanaosema yapo kuonesha/kuthibitisha yalipo.
Mbona umejikita kwenye dini tu wakati huko ndio tunataka tutoke? njoo tujadili imani ya uwepo mungu na si kujadili dini inasema nini kuhusu mungu.

Halafu watu hawataki uthibitishe kisicho kuwepo bali wanataka uthibitishe kuwa hicho kitu hakipo,mfano hao polisi wakija na kusearch wasipokuta walichokutuhumu nacho maana yake imethibitika kuwa kweli hakuna hicho kitu hakipo.
 
Unaweza ukanitajia dini ambazo haziamini kuwa Mungu wao hana uwezo wote,upendo wote na ujuzi wote!?

Ninayesema Mungu wa namna hiyo hayupo si wajibu wangu kuthibitisha hayupo.Ni wajibu wa wale wanaoamini yupo kuthibitisha uwepo wake.Mimi siwezi kuthibitsha hayupo maana kitu ambacho hakipo hakiwezi kuthibitishwa hakipo.

Kaka yangu Kiranga huwa anamfano mzuri sana wa kuwa, polisi wanapokutuhumu kwamba una madawa ya kulevya nyumbani kwako, hawaji na kukuamrisha uthibitishe kuwa nyumba yako haina madawa.

Nii wajibu wao kuthibitisha tuhuma hizo kwa kufanya uchunguzi hadi wayaone.Hii ni kwa sababu hata ukitoa vitanda na makochi yote nje kuonesha madawa hayapo bado watakwambia umeyaficha mahala pengine.

Unaposema nyumba yako haina madawa hupaswi kuthibitisha kuwa hayapo.Ni wajibu wa wanaosema yapo kuonesha/kuthibitisha yalipo.
@Buyamba , mimi siko mbali sana na wewe, mifano inayoitoa ni dhahiri kabisa inathibitisha umantiki wa hoja zako unazozijenga.

Point yangu kubwa ni kwamba, mtu anaweza akaamini kuwa Mungu yupo pasipo kuwa muumini wa dini yoyote!

Sasa, ili wote tuwe tunaenda pamoja, ni vema tusikatae kuwa Mungu hayupo kwa kigezo cha hoja au imani za dini flani.

Kuna mtu alisema, dini sio uthibitisho kuwa mungu yupo. Kwa maana hiyo, dini ni jambo moja na Mungu ni jambo lingine!!
 
Hapana mkuu,bali inaonesha ya kwamba mie ni binaadamu na si mungu na ndiyo maana ninaomba kwa sababu sina uwezo wote na ujuzi wote,ila Mungu mwenye uwezo wote na ujuzi wote ndio haombi kwa sababu yeye ana ujuzi wote na uwezo wote.
Mungu wako angekuwepo, usingekuwa na haja ya kuniomba chochote.

Unaniomba kwa sababu hayupo, unaelewa hilo?
 
Thibitisha kwanza uwepo wa huyo Mungu maana unataka tuzungumzie uwepo wa baba mzazi mwenye miaka arobaini halafu mwanae eti ana miaka hamsini.

Thibitisha Mungu yupo ndiyo tuendelee na mengine sasa.
Mkuu mara zote huwa nasema sipo hapa kuthibitisha uwepo wa mungu,kwa sababu hakuna anayeamini mungu kwa sababu amethibitishiwa uwepo wa mungu na si kwamba watu wanaamini mungu kwa sabubu kumekosekana uthibitisho.

Sasa una uhakika hakuna mungu basi tueleze sie tunaoamini.
 
Tz mbongo ,

Mimi nadhani tufanye hivii,

Kwa sababu lengo kuu la uzi huu (hasa sisi third parties(tusio na upande)) ni kujifunza na kushare experiences, basi nitoe rai kwa wachangiaji wakuu (Kiranga , Mshana Jr et al) tujadili uwepo wa mungu bila kuegemea katika maandiko fulani ya dini fulani, kwa sababu, dini ziko nyingi na ninafikiri sio lengo la mwenye uzi ku critesize dini ya mtu!!
Tangu mwanzo, nimeandika Mungu kwa sifa, sijaandika kwa dini.

Nimeandika "Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote, upendo wote".

Kama umekubali huyu hayupo, na unaamini yupo mwingine, mlete tumjadili.

Kuna watu wanaamini Beyonce ni Mungu wao, kwa vigezo vyao. Inawezekana na wewe ni mmoja wao.
 
Back
Top Bottom