Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,014
9,883
Dar es Salaam, Agosti 22, 2023

Abdulrahman Omari Kinana, mwanasiasa maarufu nchini Tanzania ambaye aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika Mashariki kuanzia mwaka 2001 hadi 2006, ametoa maoni yake kuhusu maendeleo ya demokrasia nchini humo. Akizungumza na katika mkutano wa wadau wa demokrasia nchini leo mjini Dar es Salaam, Kinana ameelezea jinsi demokrasia imekua na mwelekeo unaovutia.

Akiwa amegusia mabadiliko ya miaka iliyopita, Kinana amesema, 'Ukiniuliza kama demokrasia imekuwa, nitasema ukifananisha na miaka kadhaa iliyopita demokrasia imekua.' Ameangazia hasa mabadiliko katika uwakilishi wa wananchi katika bunge lao. Amekiri kuwa ingawa kuna changamoto katika sheria na usimamizi wa uchaguzi, hatua zimechukuliwa kuimarisha haki za kisiasa.

Akizungumza kuhusu uhuru wa kujieleza nchini, Kinana amesema, "Uhuru wa kusema upo lakini kila uhuru una mipaka yake. Uhuru bila nidhamu ni wendawazimu, nidhamu bila uhuru ni utumwa." Amesititiza umuhimu wa kudumisha usawa kati ya uhuru na wajibu wa kijamii.

Kuhusu mchakato wa kuunda katiba mpya, Kinana ametaja tume mbalimbali zilizoundwa ili kuandaa katiba hiyo mpya na kusema kuwa hatua kadhaa zimeshachukuliwa na nyingine bado zinaendelea. Kinana amemwelezea Rais Samia Suluhu Hassan kuwa amezungumza kwa uwazi kuhusu nia yake ya kuwa na katiba mpya. "Rais Samia ameshazungumza namna ambavyo serikali yake imejipanga kuwa na katiba," amesema Kinana. Ameeleza kuwa marekebisho ya sheria za uchaguzi na vyama vya siasa yatakuwa sehemu ya mchakato huo.

Katika mwaka 2024/25, Kinana anatarajia kuwa Tanzania itakuwa na uchaguzi ambao utaendeshwa kwa uwazi na kuheshimu kanuni za demokrasia.
 
Kauli hii ni kuwarushiwa fununu wanachama wa chama dola kongwe kuwa serikali ya CCM itakubali kubadili mkataba baada ya kusikiliza maoni ya wananchi na hivyo wanachama wa CCM wawe watulivu zama hizi za demokrasia siyo zama za chama kushika hatamu kungangania mkataba ni mzuri.
 
Demokrasia ipi wakati wakili Madereka yuko akishikiliwa na Polisi huko Arusha...kisa amekosoa na kupinga Mkataba wa DP-WORLD?

Ni Demokrasia ipi hiyo wakati Dk Slaa,wakili Mwabukusi na Mwanaharakati Mdude Nyagali bado wanasumbuliwa na Polisi kwa sababu wametoa maoni yao na kupinga Mkataba mbovu wa DP-WORLD?

Tunayo mifano mingi sana ya kuzuia wananchi kutoa maoni yao.

Mfano halisi ni huu wa sasa ambapo serikali imezuia vyombo vya habari kuchapisha waraka wa maaskofu wa madhehebu ya kikatoliki nchini TEC!

Kwa kupewa amri na serikali kupitia waziri wa habari huyu ambae ni Nape Nnauye.

Kinana hana hata aibu mbele ya watanzania anasimama kuongea pumba.

Watanzania wa sasa sio wa jana!
 
Dar es Salaam, Agosti 22, 2023

Abdulrahman Omari Kinana, mwanasiasa maarufu nchini Tanzania ambaye aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika Mashariki kuanzia mwaka 2001 hadi 2006, ametoa maoni yake kuhusu maendeleo ya demokrasia nchini humo. Akizungumza na katika mkutano wa wadau wa demokrasia nchini leo mjini Dar es Salaam, Kinana ameelezea jinsi demokrasia imekua na mwelekeo unaovutia.

Akiwa amegusia mabadiliko ya miaka iliyopita, Kinana amesema, 'Ukiniuliza kama demokrasia imekuwa, nitasema ukifananisha na miaka kadhaa iliyopita demokrasia imekua.' Ameangazia hasa mabadiliko katika uwakilishi wa wananchi katika bunge lao. Amekiri kuwa ingawa kuna changamoto katika sheria na usimamizi wa uchaguzi, hatua zimechukuliwa kuimarisha haki za kisiasa.

Akizungumza kuhusu uhuru wa kujieleza nchini, Kinana amesema, "Uhuru wa kusema upo lakini kila uhuru una mipaka yake. Uhuru bila nidhamu ni wendawazimu, nidhamu bila uhuru ni utumwa." Amesititiza umuhimu wa kudumisha usawa kati ya uhuru na wajibu wa kijamii.

Kuhusu mchakato wa kuunda katiba mpya, Kinana ametaja tume mbalimbali zilizoundwa ili kuandaa katiba hiyo mpya na kusema kuwa hatua kadhaa zimeshachukuliwa na nyingine bado zinaendelea. Kinana amemwelezea Rais Samia Suluhu Hassan kuwa amezungumza kwa uwazi kuhusu nia yake ya kuwa na katiba mpya. "Rais Samia ameshazungumza namna ambavyo serikali yake imejipanga kuwa na katiba," amesema Kinana. Ameeleza kuwa marekebisho ya sheria za uchaguzi na vyama vya siasa yatakuwa sehemu ya mchakato huo.

Katika mwaka 2024/25, Kinana anatarajia kuwa Tanzania itakuwa na uchaguzi ambao utaendeshwa kwa uwazi na kuheshimu kanuni za demokrasia.
Hakuna DEMKRASIA TANZANIA.UTAKUAJE NA DEMOKRASIA WAKATI CHAGUZI ZOTE ZINASIMAMIWA NA TUME ISIYO HURU NA HAKI?
Watendaji wa Serikali ambao ni Makada wa Ccm
 
Kauli hii ni kuwarushiwa fununu wanachama wa chama dola kongwe kuwa serikali ya CCM itakubali kubadili mkataba baada ya kusikiliza maoni ya wananchi na hivyo wanachama wa CCM wawe watulivu zama hizi za demokrasia siyo zama za chama kushika hatamu kungangania mkataba ni mzuri.
Umemaliza?

Una uhuru wa kujieleza halafu umeandika kama unakimbizwa, hiki ni nini "kuwarushiwa"?
 
Jenerali Ulimwengu - Tumepoteza uwezo wa kujadili hoja


View: https://m.youtube.com/watch?v=cptVEkJpJ6A

Hayo yamejiri katika kongamano lililotayarishwa na kituo cha demokrasia Tanzania wakati Jenerali Ulimwengu alipofafanua hali hiyo ya kutia simanzi na sikitiko ya umma kushindwa kujikita kujadili hoja nchini Tanzania....

utamaduni huu wa kushindwa kujadili hoja hauhitaji karipio, miongozo au sheria anasisitiza Jenerali Ulimwengu bali unahitaji kubadilisha fikra yaani mindset za waTanzania kuchukia kujadili hoja na kuzua mkabiliano usio zingatia hoja inayojadiliwa ...
 
Demokrasia feki ya kutojibu unachoulizwa haina maana, uzuri wa demokrasia ni kutoa majibu kwa yale unayoulizwa na uyafanyie kazi.
 
Dar es Salaam, Agosti 22, 2023

Abdulrahman Omari Kinana, mwanasiasa maarufu nchini Tanzania ambaye aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Afrika Mashariki kuanzia mwaka 2001 hadi 2006, ametoa maoni yake kuhusu maendeleo ya demokrasia nchini humo. Akizungumza na katika mkutano wa wadau wa demokrasia nchini leo mjini Dar es Salaam, Kinana ameelezea jinsi demokrasia imekua na mwelekeo unaovutia.

Akiwa amegusia mabadiliko ya miaka iliyopita, Kinana amesema, 'Ukiniuliza kama demokrasia imekuwa, nitasema ukifananisha na miaka kadhaa iliyopita demokrasia imekua.' Ameangazia hasa mabadiliko katika uwakilishi wa wananchi katika bunge lao. Amekiri kuwa ingawa kuna changamoto katika sheria na usimamizi wa uchaguzi, hatua zimechukuliwa kuimarisha haki za kisiasa.

Akizungumza kuhusu uhuru wa kujieleza nchini, Kinana amesema, "Uhuru wa kusema upo lakini kila uhuru una mipaka yake. Uhuru bila nidhamu ni wendawazimu, nidhamu bila uhuru ni utumwa." Amesititiza umuhimu wa kudumisha usawa kati ya uhuru na wajibu wa kijamii.

Kuhusu mchakato wa kuunda katiba mpya, Kinana ametaja tume mbalimbali zilizoundwa ili kuandaa katiba hiyo mpya na kusema kuwa hatua kadhaa zimeshachukuliwa na nyingine bado zinaendelea. Kinana amemwelezea Rais Samia Suluhu Hassan kuwa amezungumza kwa uwazi kuhusu nia yake ya kuwa na katiba mpya. "Rais Samia ameshazungumza namna ambavyo serikali yake imejipanga kuwa na katiba," amesema Kinana. Ameeleza kuwa marekebisho ya sheria za uchaguzi na vyama vya siasa yatakuwa sehemu ya mchakato huo.

Katika mwaka 2024/25, Kinana anatarajia kuwa Tanzania itakuwa na uchaguzi ambao utaendeshwa kwa uwazi na kuheshimu kanuni za demokrasia.
Demokrasia ni pana sana na ina watu wenye majukumu mbalimbali katika kuitekeleza. Jukumu moja ambalo halina watu ni kula pamoja. Ndio sababu sasa wanasheria wameamua kuongoza Ili watu kuujua ukweli, kuuishi ukweli, kuutetea ukweli, kufundisha watu kuwa wa kweli na kuteseka kwa kupigania ukweli. Ili kuilinda demokrasia wakweli wawe huru.
 
Back
Top Bottom