Hamna wakulima humu??Habari wadau,
Baada ya kuangukia pua mara kadhaa kwenye kilimo cha tikiti-maji nimeamua kuhamia kwenye Kilimo cha UFUTA.
Shamba langu liko wilaya ya Mkuranga, eneo ambalo lina mchanga mwingi sana. Huu mchanga ndio umenifanya nipate hasara sana kipindi cha jua kali kwenye kilimo cha tikiti-maji sababu jua likiwa kali maji yanakauka haraka na mchanga unaunguza matunda naishia kuvuna matunda madogo. Changamoto ni nyingi sana kwenye tikiti-maji ambazo ofcoz zina utatuzi ni ni kama unacheza Kamari.
Msaada naoomba ni kama kuna mdau yeyote kashalima na kufanikiwa na kilimo hiki kwenye ardhi yenye mchanga mwingi.
Na je, ni vitu gani vya msingi zaidi ili kufanikiwa na kilimo hiki.
Pia - kilimo gani kingine chenye faida ukanda huu wa Pwani??
Natanguliza shukrani.
Sent using Jamii Forums mobile app
Tupo na mpango wa kulima ufuta mkuu ngoja nije pm kwa msaada zaidiSoko la mazao ya biashara ni zuri sana tu kama unakuwa mbunifu wa kuzindika mwenyewe badala ya kutegemea uwauzie wengine mazao yako. Kama una mpango wa zao la ufuta ni bora kama unaamua kuwa na kinu cha kukamua mafuta na katu hutakosa soko la mafuta.
Binafsi nakushauri sana kulima zao la ufuta iwapo utakuwa na mipango ya kuzindika na kupata mafuta wewe mwenyewe na kisha uuze mafuta yake, hapo utakomba faida yote badala ya kudanganywa na wanunuzi wa middles ambao hula faida ya wa juu na wa chini.
Vipi mkuu ulifanikiwa kulima ufuta?Habari zenu wadau,
Leo nimeona nije na mada ili kama kuna watu wenye information zinazoweza kusaidia basi na wachangie ili tuweze kupata faida. Kwa kifupi ni kuwa ninashawishika kujishughulisha na kilimo ili kuongeza kipato na nimeamua kujishughulisha na kilimo cha ufuta.
Ufuta kama zao lingine lolote lina mahitaji yake muhimu. Ninaomba kama kuna yeyote anayeweza kutoa maelezo kuhusu zao hili kwenye vipengele vifuatavyo basi anisaidie.
Wakuu wenye hizi habari tunaomba mfunguke kwa faida ya wengi.
- Je ni aina gani ya mbegu zinazopatikana na kustawi Tanzania, na katika hizo ipi ni bora zaidi.
- Kwa ekari moja, kama ukifuata ushauri wa kitaalamu unaweza kupata kiasi gani cha ufuta katika mavuno assuming normal conditions?
- Je ufuta unahitaji dawa za kuua wadudu, na kama ni ndivyo inahitajika kufanya zoezi hilo mara ngapi ili kupata mavuno mengi na bora? Pia gharama za kupiga dawa kwa ekari inaweza kufikia kiasi gani?
- Je zao hili ustawi katika mazingira gani? Hapa nina maana hali ya hewa, udongo n.k.
- Ni mbinu gani za kilimo naweza kutumia kuongeza wingi na ubora wa zao hili.
Sikulima si unaona kama hivi hakuna elimu ya kutosha.
Kuna kampuni walikuwa wanajiita Amsha. Sijui kama wapo. Watafute.Naombeni anayejua wapi napata mbegu za ufuta dsm, au morogoro
Sorry hivi heka1 ya ufuta inahitajika kupanda kilo ngapi za mbegu?Kuna kampuni walikuwa wanajiita Amsha. Sijui kama wapo. Watafute.
Au kama kuna mtu unamfaham ambae yuko Lindi mwambie akutafutie huko ziko nyingi
Sent using Jamii Forums mobile app
Sio mchezo mkuu halafu kilimo cha mitandaoni hatari sana. Watu nendeni field Mjionee.3 yrs later watu bado wana vilio mbaya kabisa.ufuta sio mchezo unatoboa mifuko
Usikate tamaa mkuu
Matokeo mwaka huu yamewaliza wengi sana. Nadhani mvua zilichangia kuzorotesha uzalishaji. Wewe ni mtu kama wa kumi unaelalamika.
Ulipanda mwezi wa ngap mkuu?Mwaka 2019 nimelima ekari 20 hiki ndio ninachokiona halafu mvua hakuna yaani duh View attachment 1047900
Sent using Jamii Forums mobile app
Umelimia wapi MKUU,kwani Mimi bado sijapanda mpaka sasahiviMwaka 2019 nimelima ekari 20 hiki ndio ninachokiona halafu mvua hakuna yaani duh View attachment 1047900
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu sijui km ulifanikiwa kuzipata naona watu hawajakujibu. Mm nilinunua Mtwara ila nalima Kisarawe, kama una mtu kule unaeza kuomba akusaidie kununua afu akutumie kwa garwapi naweza pata mbegu za white seseme seed{ufuta}
tuwasiliane kwa 0652472486
Sent using Jamii Forums mobile app