Naomba unifahamishe msimu Bora wa kupanda ufuta bagamoyo mkuu
Kwanza huo ufuta ulitakiwa uukatie mashina yabaki kama matatu au manne ndio ungeona ukuaji wake, pili ujaupiga dawa hadi wadudu wanautafuna bado unalalamika tatizo mvua wakati wewe mwenyewe tatizo!!Mwaka 2019 nimelima ekari 20 hiki ndio ninachokiona halafu mvua hakuna yaani duh View attachment 1047900
Sent using Jamii Forums mobile app
Nanjilinji kwa mzee Lipetelo.Bora ninunue Na kuuza ila hili zao kulima ni pasua kichwa asikuambie Mtu, afu linatuma vibaya vibaya, ukiwa unalima usicheze mbali Na shamba lako, pia Kuna imani za kishirikina pia katika zao hili,
Mwaka Jana mwenz wa 6 niliingia chimbo mwenyewe huko Nanjilinji kununua Ufuta mashambani kwa wakulima wenyewe huko milimani kwenye makorongo, nilipata story nyingi za wakulima kuhusu zao hili..!!
Unaweza kutumia Pesa nyingi Na usirudishe pesa zako muda wa mavuno, pia unaweza ukatumia Pesa ndogo Sana ukapiga pesa saana Yani unaweza kulima heka mbili TU ukabutua, Ila unaweza ukalima heka 20 ukaja kupata gunia 5 TU,
Wengi wanaolima zao Hilo kwa wilaya ya kilwa Na kidogo vijiji vya Ruangwa mpakani mwa Kilwa Na Ruangwa, wengi wao huwa wanalala huko huko porini, kwa maana wanajenga Banda TU wanalala hapo kusimamia shamba,,au ukishindwa kulala mwenyewe, Una muajiri Mtu analala ni Kama analinda. ..!
Katika ulimaji wa zao hili naona Una changamoto nyingi kuliko korosho,, hasa hasa kipato chake kinaendana Na bahati,
Kwa mama Bahati?Nimeanza na kuchoma kichaka ekari 5 ili nianze upandaji katikati ya mwezi wa 12 maeneo ya mwaya, moro.
Vp ulifanikiwa kupata mashine ya kupandia ufuta mkuu?Wakuu nipo mkoani rukwa na ni mkuluma wa ufuta,lakini kwa kipindi kirefu nimekuwa nikipanda kwa njia za kienyeji sana ila baada ya kuona kuwa ufuta unanilipa vizuri nimeamua kuwekeza nguvu nyingi huko.
Nimeamua kutafuta mashine ya kupandia ili kurahisisha kazi lakini pia kuongeza tija katika kilimo.
Ninaomba msaada kwa yeyote anayefahamu upatikanaji wa mashine hiyo kwa hapa tanzania.
Asanteni sana wakuu.
Mkuu mashine za kupandia ufuta zinapatikana wapi? Na ni shs ngapi mkuu?Nimeku-PM unitafute zipo hutaki.
Vp maendeleo yapoje mkuu?Mwaka huu nimefanya majaribio ya kulima ufuta wilaya ya Malinyi. Nimelima hekari 10, sijalima kitaalamu badala yake nimelima kama wakulima wa maeneo hayo.
Gharama za uendeshaji kuanzia December 2019 hadi sasa March 2020 ziko kama ifuatavyo;
Kukodi eneo hekari 10@30000 = 300000
Kufyeka/Kusafisha eneo hekari 10@15000 = 150000
Mbegu debe 1 = 100000
Kulima hekari 10@ 50000 (Phase1: 30000@hekari, phase2: 20000@hekari) = 500000
Kupalilia hekari 10@25000 = 250000
Dawa ya kupulizia wadudu, kopo 5@5000 = 25000
Gharama za matumizi ya msimamizi hadi sasa 100000.
Jumla ya gharama zilizotumika kuhudumia hekari 10 hadi sasa ni Tsh 1425000.
Pia kuna gharama za uvunaji zitaongezeka msimu wa kuvuna ukifika.
NB: Sikutaka kuanza na kilimo cha kitaalamu kutokana na changamoto za usimamizi kwani usimamizi uko chini ya watu ambao mostly wanalima kilimo chetu cha kitanzania. Hivyo kwa majaribio nimeona nianze hivyo kwanza ili tuweze kuzungumza lugha inayoendana na wenyeji wangu walioko mashambani then huko mbele ndio ninaweza kulima kwa kufuata kanuni za kitaalamu kama nitaona inafaa.
Tunamshukuru Mungu maendeleo ya mazao yanatia moyo, tuna matumaini ya kupata.Vp maendeleo yapoje mkuu?
Kila la kheri mkuuTunamshukuru Mungu maendeleo ya mazao yanatia moyo, tuna matumaini ya kupata.
Kwa hali ya hewa bado inasapoti kulingana na nature ya maeneo niliyolima, japokuwa mvua zinanyesha sana ila maeneo niliyolima hayatuamishi maji ni maeneo ya juu kidogo hivyo athari za mvua hazijaonekana sana hivyo matumaini ya kupata yapo.
Changamoto ninayoiona saivi ni wadudu wameanza kuonekana kwenye ufuta ila ni wachache na nimeshanunua dawa na wiki hii nitapulizia ili kuwadhibiti.
Mkuu,kwa makadirio ekari Mona inaweza kutoa kias gan(debe ngapi) Cha ufuta?Tunamshukuru Mungu maendeleo ya mazao yanatia moyo, tuna matumaini ya kupata.
Kwa hali ya hewa bado inasapoti kulingana na nature ya maeneo niliyolima, japokuwa mvua zinanyesha sana ila maeneo niliyolima hayatuamishi maji ni maeneo ya juu kidogo hivyo athari za mvua hazijaonekana sana hivyo matumaini ya kupata yapo.
Changamoto ninayoiona saivi ni wadudu wameanza kuonekana kwenye ufuta ila ni wachache na nimeshanunua dawa na wiki hii nitapulizia ili kuwadhibiti.
Kwangu hii ni mara yangu ya kwanza kufanya kilimo hiki. Ila niliambiwa kuwa inaweza kutoa debe 12-18. Jibu sahihi kabisa nitakalokuwa na uhakika nalo nitalipata nitakapovuna maana hayo ndio yatakuwa matokeo halisi ya kutoka field kwa experience yangu mwenyewe.Mkuu,kwa makadirio ekari Mona inaweza kutoa kias gan(debe ngapi) Cha ufuta?
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuwepo lindi- Liwale huko wanapata debe 24- 36 kwa heka pia huku songwe maeneo ya mkwajuni napo kipato kipo hivyo pia ukienda maeneo ya bonde la ziwa rukwa napo wengi huwa kipato kina range kwenye debe 18-36Kwangu hii ni mara yangu ya kwanza kufanya kilimo hiki. Ila niliambiwa kuwa inaweza kutoa debe 12-18. Jibu sahihi kabisa nitakalokuwa na uhakika nalo nitalipata nitakapovuna maana hayo ndio yatakuwa matokeo halisi ya kutoka field kwa experience yangu mwenyewe.
Labda kwa wadau wenye experience na kilimo hiki wanaweza kutusaidia kupata jibu la uhakika zaidi maana wakati mwingine hali ya hewa, aina ya ulimaji pia inaweza kuchangia kupungua/kuongezeka kwa mazao.
Kwa upepo huu wa Corona ufuta utalipa kweli mwaka huu? Mana wanunuaji wakubwa ndo hao wanapata tabu.