Kikwete yuko Vietnam

Kikwete yuko Vietnam

10402379_811523085578354_4082408879449939251_n.jpg


Kikwete ameingia Vietnam kwa ziara na msusururu wa Mtu kama miaa hivi, kudadeki... halafu kama hiyo haitoshi Pinda naye yuko Ulaya naye kabeba mtu kama 100 hivi na hiyo ni kwa wiki mbili sasa, huku nako Mwandosya yuko Zambia, achilia hao wengine ambao wala Ziara zao hazitangazwi

my president is 65 years old boy ndio tatizo la kuchagua kijana kama huyu kuwa rais.
 
Mmeshindwa kumpindua kwa kutumia sanduku la kura katika chaguzi kuu mbili za kidemokrasia, kwa sasa ndiyo mtaweza kwa njia nyingine.

Waulize wale walidai na kusema hawamtambui lakini cha kushangaza kila mara wanakwenda Ikulu kuomba msaada wa kisiasa pale maji ya kisiasa yanapowafika shingoni.

Kazi za Rais Kikwete hazihitaji kutumia darubini ili uzione.

The President is delivering on his promises to make Tanzania so much the better.

Watanzania hawawezi kuishi kwa kutegemea maneno ya wanasiasa pekee kama wale waliodai hawamtambui, bali Watanzania wataishi kwa kutegemea matendo ya wanasiasa.

Tukipata marais watatu kama jk tutakwisha kabisa, yani Nyerere angekuwa kama jk sijue ingekuwaje, nadhani tungekuwa kwenye human zoo someone in the middle of nowhere.
 
Hii habari ya kuomba umeipata wapi mkuu? Ivi unadhani bila kuwa na wawekezaji wakutosha tutapiga hatua za haraka? Jk anatafuta wawekezaje kwenye sekta muhimu,,china amepata wawekezaji kwenye reli ya kati,,tusubiri na Vietnam atakuja na wawekezaji wa aina gani ili tupige hatua..acheni kubeza kila kitu hizo nchi za asia mashariki hazikuendelea tu hivi hivi...

huyu rais wetu alianza mchezo huu mapema sana wa kutembelea kila kona ya nchi na watu walipohoji toka awamu ya kwanza wakajibiwa Rais wetu anatafuta misaada.

na safari hizi hazijawahi kukoma na zaidi zinaongezeka kila siku.

hata wewe unanipa picha ya aina ya watu waliopo ambao wanakatisha tamaa watanzania kama nchi ina watu wenye fikra za kulisaidia taifa.

sekta muhimu ni viwanda. safari za Rais wetu sasa zinakaribia kuwa miaka miwili katika miaka 10.

kwa wingi wa safari zote hizo ni kiwanda gani ambacho mpaka sasa kimepatikana kwa mamia ya safari zilizopita?

kama kasafiri ndani ya miaka 9 na hajapata wawekezaji wa maana je huu mwaka mmoja una matumaini kushinda miaka 9 aliyopoteza?

NIMESEMA HAKUNA NCHI ILIYOWAHI KUENDELEA KWA MISAADA.

umetaja nchi za Asia mashariki.

unaweza kunimbia China na India zilipata msaada toka kwa nchi gani ?

Rais Kenyatta alipoingia tu madarakani alipiga marufuku misaada ya nje katika serikali yake na asasi zote za kiraia.

lakini kasi yao ya maendeleo kwa muda mfupi ni yakutisha.

hata mtangulizi wa Kenyatta ambaye ni Mwai Kibaki sidhani kama alifikisha hata safari 20 kwenda ughaibuni ndani ya miaka 10 ya uongozi wake.

na juzi taifa lao limekuwa la uchumi wa kati duniani.

ndio maana wengine wamefikia hatua ya kumuita huyu rais ni RAIS MTALII
 
Hii habari ya kuomba umeipata wapi mkuu? Ivi unadhani bila kuwa na wawekezaji wakutosha tutapiga hatua za haraka? Jk anatafuta wawekezaje kwenye sekta muhimu,,china amepata wawekezaji kwenye reli ya kati,,tusubiri na Vietnam atakuja na wawekezaji wa aina gani ili tupige hatua..acheni kubeza kila kitu hizo nchi za asia mashariki hazikuendelea tu hivi hivi...

Wewe pia ni zuzu kama Ritz1, tena wewe ni zuzu kabisa
 
hawa jamaa wanasema wanamuenzi Nyerere,Nyerere sera yake ni ujamaaa na kujitegemea wao ni KUTEMBEA NA KUOMBA

kumuenzi nyerere ni kwa ajili ya kuomba kula tu kutoka kwa watz wazuzu, ina wakati wake
 
Kwa akili yako unaona hili jambo ni siasa! Hapa tunazungumzia kikweta rais wa tanzania, gharama ya safari ya rais si sawa na hata ya waziri, sasa wewe unaleta mambo ya mbowe m/k wa chadema wakati hapa anazungumzia kikwete rais wa tanzania, una akili wewe?
Hewe punguani unabisha au unapinga tu bila kujua, Mbowe alikwenda Oman yeye na Lukuvi pamoja na Anna Makinda, Mbowe alitoa pesa yake mfukoni? wewe utakuwa Chadema-Kata.
 
Pesa zawalalahoi zinaliwa ovyo

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
huyu jamaa kiukweli kazidi utembezi yaan km mtt wa mtaani asiye na kwao!!! Msitetee ujinga kimsingi jamaa kazidi utembezi.
 
Dah! viongozi wetu wanakula bata mpaka kuku wanaona gere........kudadadeki.
 
Daaah Wabongoooo, hii jitihada tunayoifanya ya kukesha mitandaoni na kupondeana ingekuwa ni shughuli ya uzalishaji mali ,basi tungekuwa mbali sanaa.
 
Hivi katika nchi za kiafrika hakuna wawekezaji? Mbona sijawahi kusikia katembelea huko??
 
Kwa hivyo Great Thinker unashauri Rais awe anabaki humu humu nchini ?? Halafu Marais wa hizo nchi za Ulaya, Marekani na Asia ndiyo waje wamtembeleee ? Wafanyabiashara na Wawekezaji waje kumtembelea ? Hiyo nayo SHULE !
tujadili gharama na tija za safari hizo
 
Nahisi dr alienda kumwombe ajira vasco da gama ili awe dereva wa Apolo maana tumechoka kuona kodi zetu zinamalizwa na ki gulf stream,kindege hakitulii kila dakika unakiona kinakatiza kipawa utafikiri daladala bwana

Urais si kazi ya kukaa ofisini.

Wenye macho manufaa yake tunayaona.
 
Back
Top Bottom