Kikwete yuko Vietnam

Kikwete yuko Vietnam

Nahisi dr alienda kumwombe ajira vasco da gama ili awe dereva wa Apolo maana tumechoka kuona kodi zetu zinamalizwa na ki gulf stream,kindege hakitulii kila dakika unakiona kinakatiza kipawa utafikiri daladala bwana

Nimecheka saba hii. ..dah mkuu you have made my day!
 
Watu mna majibu humu ndani ...aisee yaan JF is never boring
 
huyu rais wetu alianza mchezo huu mapema sana wa kutembelea kila kona ya nchi na watu walipohoji toka awamu ya kwanza wakajibiwa Rais wetu anatafuta misaada.

na safari hizi hazijawahi kukoma na zaidi zinaongezeka kila siku.

hata wewe unanipa picha ya aina ya watu waliopo ambao wanakatisha tamaa watanzania kama nchi ina watu wenye fikra za kulisaidia taifa.

sekta muhimu ni viwanda. safari za Rais wetu sasa zinakaribia kuwa miaka miwili katika miaka 10.

kwa wingi wa safari zote hizo ni kiwanda gani ambacho mpaka sasa kimepatikana kwa mamia ya safari zilizopita?

kama kasafiri ndani ya miaka 9 na hajapata wawekezaji wa maana je huu mwaka mmoja una matumaini kushinda miaka 9 aliyopoteza?

NIMESEMA HAKUNA NCHI ILIYOWAHI KUENDELEA KWA MISAADA.

umetaja nchi za Asia mashariki.

unaweza kunimbia China na India zilipata msaada toka kwa nchi gani ?

Rais Kenyatta alipoingia tu madarakani alipiga marufuku misaada ya nje katika serikali yake na asasi zote za kiraia.

lakini kasi yao ya maendeleo kwa muda mfupi ni yakutisha.

hata mtangulizi wa Kenyatta ambaye ni Mwai Kibaki sidhani kama alifikisha hata safari 20 kwenda ughaibuni ndani ya miaka 10 ya uongozi wake.

na juzi taifa lao limekuwa la uchumi wa kati duniani.

ndio maana wengine wamefikia hatua ya kumuita huyu rais ni RAIS MTALII

Mkuu hoja zako ni nzito sana...endelea kutoa elimu kaka!
 
Kwa hivyo Great Thinker unashauri Rais awe anabaki humu humu nchini ?? Halafu Marais wa hizo nchi za Ulaya, Marekani na Asia ndiyo waje wamtembeleee ? Wafanyabiashara na Wawekezaji waje kumtembelea ? Hiyo nayo SHULE !

Mbona we huwa unatoka nyumbani na kwenda dukani kununua vitu? kama huyu mfanyabiashara kaona biashara inayo mfaa iko Tanzania ataifuata tuu, ilimradi aone matangazo.
 
Ritz nahisi ID yako imeingiliwa siku za karibu post zako zinaleta walakini. Hivi ni nchi gani ambayo Raisi yupo kule na Waziri mkuu yupo kule? kumbuka wote wapo na misafara ya kufa mnyama ni mawaziri wangapi wapo nje ya nchi kwa sasa? halafu tunasema tutaendelea! Gharama wanazotumia na hicho wanachokileta haviwiani.

Huyu ndugu yangu,huyu kuna siku atakuja KUOKOKA yaani shateni CCM akae mbali naye.Wajua kaka muda ni dawa,tumsubiri tu.
 
Mbona we huwa unatoka nyumbani na kwenda dukani kununua vitu? kama huyu mfanyabiashara kaona biashara inayo mfaa iko Tanzania ataifuata tuu, ilimradi aone matangazo.

Kaka huyo anakichwa kigumu itamuwia ngumu sana kukuelewa kabeba bichwa tu.
 
Huyu aliyefuatana naye ni nani (ktk picha) mbona amechoka sana. Hataki kulea wajukuu?
 
Wapumbavu acheni kudhihirisha chuki zenu huyo JK hana shida ya kwenda kutembea kokote na kishatembea sana nchi kibao tokea enzi zile ambazo hakuwa busy kama sasa hivi, ni huruma yake kwenu mapimbi nyie halafu mnajifanya mnajua. siku hizi kila mtu ana mdomo mrefu kawaachia uhuru wa kuongea basi ndo mnataka kuongea kwa kutumia makalio. Mmepata vielimu kidogo mnajianya hamna shukrani huko vijijini kwenu mlikotoka wengine tangu mmekuja mjini hamjarudi na huku mjini ndo hata ugali hamli eti mmejua BURGER NA PIZZA kumbukeni mlikotoka. huyu jamaa kajitahidi kinoma kwanza aliingia madarakani wakati hali ya uchumi dunia nzima ilikuwa mbovu halafu alikuwa na maadui ambao wamemganda (chui ndani ya ngozi za kondoo). magazeti yenu ya kikuda karuhusu yafanye biashara ya kuuza habari za kipumbavu kwenu wapumbavu mnataka nini awalambe miguu? Hali sio mbaya sana hata kama ni mbaya sio kivile na hata mkiuliza waganga wenu huko vijijini na bibi zenu wana kanamba ka tigo pesa au M-pesa bado mnapiga kelele hatujapiga kahatua.

So whaaaaaat!? Ndo aendelee kuzurura tu sasa sio? Kisa vijijini wana tigo-pesa na m-pesa? Mawazo ya mtu aliyelewa mbege kabisa!
 
Kwa hivyo Great Thinker unashauri Rais awe anabaki humu humu nchini ?? Halafu Marais wa hizo nchi za Ulaya, Marekani na Asia ndiyo waje wamtembeleee ? Wafanyabiashara na Wawekezaji waje kumtembelea ? Hiyo nayo SHULE !

shida si kusafiri ila safati zilizoptiliza na zenye msafara mkubwa

na kuna safari zingije si za kwenda rais.. Waziri tu atosha
 
Wapumbavu acheni kudhihirisha chuki zenu huyo JK hana shida ya kwenda kutembea kokote na kishatembea sana nchi kibao tokea enzi zile ambazo hakuwa busy kama sasa hivi, ni huruma yake kwenu mapimbi nyie halafu mnajifanya mnajua. siku hizi kila mtu ana mdomo mrefu kawaachia uhuru wa kuongea basi ndo mnataka kuongea kwa kutumia makalio. Mmepata vielimu kidogo mnajianya hamna shukrani huko vijijini kwenu mlikotoka wengine tangu mmekuja mjini hamjarudi na huku mjini ndo hata ugali hamli eti mmejua BURGER NA PIZZA kumbukeni mlikotoka. huyu jamaa kajitahidi kinoma kwanza aliingia madarakani wakati hali ya uchumi dunia nzima ilikuwa mbovu halafu alikuwa na maadui ambao wamemganda (chui ndani ya ngozi za kondoo). magazeti yenu ya kikuda karuhusu yafanye biashara ya kuuza habari za kipumbavu kwenu wapumbavu mnataka nini awalambe miguu? Hali sio mbaya sana hata kama ni mbaya sio kivile na hata mkiuliza waganga wenu huko vijijini na bibi zenu wana kanamba ka tigo pesa au M-pesa bado mnapiga kelele hatujapiga kahatua.

Ni kweli siye tuliyetoka VIJIJINI tukaja mjini tukula burger na pizza badala ya ugali na maharagwe.

Naomba nikupe nukuu hii toka kwa JK Nyerere,huyu aliyekuwa mwanzilishi wa hiyo CCM yenu..Alisema nanukuu"Siku moja akitokea kiongozi wa TAIFA letu akatuambia huko nje kuna hela nyingi kuliko hapa nyumbani,mwambieni wewe ni mpumbavu" mwisho wa kunukuu.

Na hii nukuu ya pili ni ya Rais wetu mpendwa nitanukuu ..."Unapoenda kuomba siyo kwamba wewe unapenda kuomba ,huko nje kuna mataifa yenye hela nyingi tu!Unachotakiwa ni kujieleza wakikuelewa watakupa"

Ukiweza kuzitafakari hizi nukuu mbili hautakaa uandike tena hiyo post yako.Pole.
 
Miraisi mingine bwana!!, inakesha angani kama popo.:smokin::smokin:
 
Nadhani siku hizi Serikali inaona aibu kutangaza baadhi ya ziara za JK. Hii ziara ya Vietnam sijaisikia bali nimeionea humu.

Jana jioni nilifuatilia kipindi Radio One kuhusu Mikopo ya Wanafunzi Vyuo vikuu. Viongozi wa TAHLISO walikuwa wakilalamikia serikali kushindwa kuwapa mikopo wanafunzi wanaostahili kwa madai ya ukosefu wa fedha wakati raslimali ni nyingi na matumizi serikali ni makubwa sana.

Mmoja wao akasema anashangaa kuwa serikali inadai haina pesa wakati wakienda Bodi ya Mikopo kufuatilia wanakuta magari ya Bodi ni ya kifahari mno, mashangi yanayoanzia milioni 200 ndio yanayotumiwa na wakurugenzi wa vitengo wa Bodi. Kuna mmoja wa watetezi Assenga Abubakar akadai kuwa inaipasa bodi kuwa na magari ya gharama hiyo ili kufanya kazi vizuri kwa kuwa miundombinu ya Tanzania sio mizuri, hiyo magari hayo yanawawezesha kutembelea vyuo vilivyo mikoani! Nilimshangaa sana.

Vv
 
huyu dada naona jk atakuwa ndg yake hampingi hata siku moja kutwa kumtetea aise.....
 
Yupo kazini. Sasa afanyeje wakati ndio moja ya majukumu yake makubwa?
 
Mwacheni JK ale bata... Maisha mafupi jamani.... subirini zamu yenu... BTW: hao wazungu waliogoma kutupatia misaada walifikiri JK hata safiri? Sasa ni China na Asia kwa kwenda Mbele deals za UK na USA zinaboa sana ... Wanabana misaada wakati ni fedha ambazo CCM walikubaliana nao wazifiche kwenye mikataba!!! Kidumu Chama Cha Mapinduzi ....
 
mbowe alikuwa south africa akaunganisha oman kisha akarudi dar es salaa, leo kaenda hai.

stop being cynucal.ziara zote za mbowe(ukijumlisha alizoenda kama kiongozi wa upinzani bungeni na alizoenda kama mfanyabiashara na hata kamam mtalii) hazifiki hata asimia kumi ya zile jk ameenda kama rais
 
Mmeshindwa kumpindua kwa kutumia sanduku la kura katika chaguzi kuu mbili za kidemokrasia, kwa sasa ndiyo mtaweza kwa njia nyingine.

Waulize wale walidai na kusema hawamtambui lakini cha kushangaza kila mara wanakwenda Ikulu kuomba msaada wa kisiasa pale maji ya kisiasa yanapowafika shingoni.

Kazi za Rais Kikwete hazihitaji kutumia darubini ili uzione.

The President is delivering on his promises to make Tanzania so much the better.

Watanzania hawawezi kuishi kwa kutegemea maneno ya wanasiasa pekee kama wale waliodai hawamtambui, bali Watanzania wataishi kwa kutegemea matendo ya wanasiasa.

Hivi tuseme rais akikaa hapa tz na kutumia rasilimali zilizopo hapa hapa hatuwezi kupata maendeleo,MSD wamesitisha kutoa dawa ila jk hii ziara atatumia hata bl 10.
mmelishwa nini hadi muwe na mahaba ya kussuport ujinga huu wa ccm??
 
10402379_811523085578354_4082408879449939251_n.jpg


Kikwete ameingia Vietnam kwa ziara na msusururu wa Mtu kama miaa hivi, kudadeki... halafu kama hiyo haitoshi Pinda naye yuko Ulaya naye kabeba mtu kama 100 hivi na hiyo ni kwa wiki mbili sasa, huku nako Mwandosya yuko Zambia, achilia hao wengine ambao wala Ziara zao hazitangazwi.
Hivi anajua kuwa hospital hazina dawa kweli?China si aliomba reli, huko Vietnam tunamuomba atuombee dawa za matibabu maana huku hakuna kabsa
 
Back
Top Bottom