Kikwete ameingia Vietnam kwa ziara na msusururu wa Mtu kama miaa hivi, kudadeki... halafu kama hiyo haitoshi Pinda naye yuko Ulaya naye kabeba mtu kama 100 hivi na hiyo ni kwa wiki mbili sasa, huku nako Mwandosya yuko Zambia, achilia hao wengine ambao wala Ziara zao hazitangazwi kudadeki... hivi hakuna Mtu wa kumpindua huyu Jamaa arghhhhhhhhhh!
ni aibu sana kuwa na viongozi wenye uwezo kidogo kifikra.
mimi ninaona aibu kuonekana mtanzania kila linapotajwa jina la Rais wa nchi ya Tanzania.
Rais wetu amekuwa wakala wa kutuaibisha kama taifa kwa kuwa ombaomba aliyevuka mipaka ya kuvumilika.
mimi ninawaonea wivu sana wakenya kwa sasa kwa kuwa na viongozi wenye fikira na mtazamo mpana kwa maslahi ya taifa lao.
taifa lao linajivunia sana Rais wao.
kila linapotajwa jina la Uhuru Kenyatta Wakenya wanajivunia sana na hata waafrika kwa ujumla wake.
na mimi najivunia sana kuwa na Kenyatta kama Rais anayebeba nembo na matumaini ya Afrika yaliyopotea miaka mingi.
TUJIFUNZE KWA VIONGOZI WA KENYA HASA UHURU KENYATTA NAMNA YA KUENDESHA NCHI NA SI KUKIMBILIA KUWA OMBAOMBA BADALA YAKE TUKAE KAMA TAIFA TUPANGE NINI TUFANYE ILI TUSITAWI.
HAKUNA NCHI ILIWAHI KUENDELEA KATIKA HISTORIA YA MAENDELEO KOTE DUNIANI KWA KUZUNGUKA DUNIA NZIMAKUOMBAOMBA.
HUYU RAIS ANATUABISHA KAMA TAIFA.
MAANA TUNAONEKANA UWEZO WA TAIFA WA KUFIKIRI KWA UJUMLA WAKE NI KIDOGO SANA KWA SABABU YEYE NDIYO NEMBO KWA TAIFA LETU NA AMESHINDWA KUTUONGOZA KUFANYA MAMBO YETU SISI WENYEWE BADALA YA KUWA OMBAOMBA