Kikwete yuko Vietnam

Kikwete yuko Vietnam

Kikwete amepoteza utu wa mtanzania. Kuwa ombaomba siyo sifa, ni aibu, ni kukiri unyonge wa akili na moyo.

Kama Kikwete hawezi kufikiri atashindwa hata kutazamia? Wenzetu Kenye uchumi wao unazidi kuimarika kwa mipango thabiti ya Wakenya na Rais wao, sisi wa kwetu kila siku kiguu na njia, unadhani nyumbani kafukuzwa.

'Siku moja akapatikana kiongozi wa Taifa letu, akasema huko nje kuna pesa kuliko hapa nyumbani, mwambieni, wewe ni mpumbavu'. Rais wetu anaamini huko nje kuna pesa kuliko hapa nyumbani.

Kwa hiyo ingekuwa mwalimu yuko hai angemwambia jamaa "wewe ni mpumbavu!" Kwa vile kila siku viongozi wetu wanasema tuyaenzi maneno ya mwalimu hivyo hili nalo tulienzi? Mie simo!
 
Duh!!! we jamaa kweli huna akili kabisa, hiyo ziara ya Mh. Mbowe ilikuwa ni ya Kiserikali, ya kichama au ya kibinafsi? na je ziara hiyo imegharamiwa na fedha za serikali?

Chagua mwenyewe jibu sahihi...
 
Kwani anaomba kwa ajili ya familia yake msoga?#think wisely

Hapana. Ila ni sawa na kuwa na mke kila siku anaomba mboga kwa jirani ilihali friji imejaa mboga ila ni mvivu wa kupika. Atakuwa anakuaibisha wewe na familia yako.
 
ni aibu sana kuwa na viongozi wenye uwezo kidogo kifikra.

mimi ninaona aibu kuonekana mtanzania kila linapotajwa jina la Rais wa nchi ya Tanzania.

Rais wetu amekuwa wakala wa kutuaibisha kama taifa kwa kuwa ombaomba aliyevuka mipaka ya kuvumilika.

mimi ninawaonea wivu sana wakenya kwa sasa kwa kuwa na viongozi wenye fikira na mtazamo mpana kwa maslahi ya taifa lao.

taifa lao linajivunia sana Rais wao.

kila linapotajwa jina la Uhuru Kenyatta Wakenya wanajivunia sana na hata waafrika kwa ujumla wake.

na mimi najivunia sana kuwa na Kenyatta kama Rais anayebeba nembo na matumaini ya Afrika yaliyopotea miaka mingi.

TUJIFUNZE KWA VIONGOZI WA KENYA HASA UHURU KENYATTA NAMNA YA KUENDESHA NCHI NA SI KUKIMBILIA KUWA OMBAOMBA BADALA YAKE TUKAE KAMA TAIFA TUPANGE NINI TUFANYE ILI TUSITAWI.

HAKUNA NCHI ILIWAHI KUENDELEA KATIKA HISTORIA YA MAENDELEO KOTE DUNIANI KWA KUZUNGUKA DUNIA NZIMAKUOMBAOMBA.

HUYU RAIS ANATUABISHA KAMA TAIFA.

MAANA TUNAONEKANA UWEZO WA TAIFA WA KUFIKIRI KWA UJUMLA WAKE NI KIDOGO SANA KWA SABABU YEYE NDIYO NEMBO KWA TAIFA LETU NA AMESHINDWA KUTUONGOZA KUFANYA MAMBO YETU SISI WENYEWE BADALA YA KUWA OMBAOMBA

Hii habari ya kuomba umeipata wapi mkuu? Ivi unadhani bila kuwa na wawekezaji wakutosha tutapiga hatua za haraka? Jk anatafuta wawekezaje kwenye sekta muhimu,,china amepata wawekezaji kwenye reli ya kati,,tusubiri na Vietnam atakuja na wawekezaji wa aina gani ili tupige hatua..acheni kubeza kila kitu hizo nchi za asia mashariki hazikuendelea tu hivi hivi...
 
Wanapishana na Mbowe alikuwa hapo Oman kwa sultan anakula bata kwenda mbele.

teh teh teh

Kwa akili yako unaona hili jambo ni siasa! Hapa tunazungumzia kikweta rais wa tanzania, gharama ya safari ya rais si sawa na hata ya waziri, sasa wewe unaleta mambo ya mbowe m/k wa chadema wakati hapa anazungumzia kikwete rais wa tanzania, una akili wewe?
 
hawa jamaa wanasema wanamuenzi Nyerere,Nyerere sera yake ni ujamaaa na kujitegemea wao ni KUTEMBEA NA KUOMBA
 
Hapana. Ila ni sawa na kuwa na mke kila siku anaomba mboga kwa jirani ilihali friji imejaa mboga ila ni mvivu wa kupika. Atakuwa anakuaibisha wewe na familia yako.

Hata kama anaomba kwa ajiri yetu,tumemtuma akaombe?.Kwanini asituulize kwanza kama hili jambo tunalifurahia?.Na mbona akipata ha itishi vyombo vya habari kutuonyesha alicholeta?
 
10402379_811523085578354_4082408879449939251_n.jpg


Kikwete ameingia Vietnam kwa ziara na msusururu wa Mtu kama miaa hivi, kudadeki... halafu kama hiyo haitoshi Pinda naye yuko Ulaya naye kabeba mtu kama 100 hivi na hiyo ni kwa wiki mbili sasa, huku nako Mwandosya yuko Zambia, achilia hao wengine ambao wala Ziara zao hazitangazwi

Halafu Zitto anashangaa uKAWA kufanya mkutano jangwani na kudai ndio walitakiwa kutafuta masoko ya mazao ya wakulima. Zitto and CCM are pathetic!
 
Mbowe alikuwa South Africa akaunganisha Oman kisha akarudi Dar es Salaa, leo kaenda Hai.

Mbowe anatumia hela yake. Huyo 'baba' yako na wajimba zako wanatumia hela ya walipa kodi. Halafu eti hajui kuwa yeye ndiyo sababu kwa nini Tanzania ni maskini.
 
Na wewe nenda Kenya ukiwa ndugu zakk kama 200 hivi ili umpiku Kikwete maana naona unawasha sana kila ukisiki Rais kasafiri.

Safari zake zina faida ndogo kwa wananchi ambao hawapati mlo wa uhakika kwa siku. Na zinatumia gharama nyingi zisizo za lazima. Sasa kama kwa wakati mmoja kuna misafara ya watu 300 wote kwa gharama za walipa kodi unadhani kwa nini nchi isiwe maskini? Kifupi nchi haina vipaumbele, ni ubinafsi tu ndio umetawala. Yawezekana na wewe ndio miongoni mwa wale waliopo kwenye misafara kila siku hupati muda wa kuona wala kujua kama kuna watanzania wanakosa mahitaji ya kila siku.
 
Ahhha Tafadhali bhana! Yaani Kikwete aajiriwe na NASA? Niijuavyo NASA hakuna hata kitengo kimoja ambacho Kikwete anaweza kushiriki ndani ya NASA hata kama NASA wanatafuta mtu tu wa kubonyeza kitufe kila atakapoona ishara fulani tu kwenye Kompyuta, huyu jamaa hawezi kupita huo Usaili!
NASA wangemweka kuwa dereva wa Apolo ili apasue anga vizuri
 
Na wewe nenda Kenya ukiwa ndugu zakk kama 200 hivi ili umpiku Kikwete maana naona unawasha sana kila ukisiki Rais kasafiri.

Kwa mawazo yako, hatuna haki ya kuhoji safari zake?hatuna haki ya kujua safari hizo zina tija kiasi gani kwa watz?unadhani JK anasafiri kwa pesa za nani kama si zetu...sisi ndo walipakodi tunatakiwa kuhoji kila kitu.Hii siyo maisha binafsi ya mtu Tunazungumzia taasisi inayotumia pesa zetu...fikiri kabla ya ku...
 
Back
Top Bottom