Kikwete to USA (May 2009)

Kikwete to USA (May 2009)

Ni nafasi adhimu hiyo pamoja na dhihaka zenu kupata audience na US President sio mchezo, yes atatembeza bakuli na hatotoka mtupu.

Mmekalia majungu tu....
 
Kwa mujibu ya matangazo ya bbc idhaa ya kiswahili yanayosikika hapa dar es salam,

jk atakutana na obama ikulu ya marekani, ambapo watazungumzia maswala mbalimbali yanayohusu nchi zetu

kikwete anakuwa rais wa kwanza wa afrika kusini mwa jangwa la sahara kukutana na obama
Hivi kwenye kikao cha G20 London,kilichohudhuriwa na Obama, hakukuwa na marais kutoka Afrika Kusini mwa Sahara?Kama walikuwepo,hawakukutana na Obama?Kama walikutana nae,why now tuambiwe JK ndio rais wa kwanza kutoka eneo hilo kukutana na Obama?Labda,ungesema JK anakuwa rais wa kwanza kutoka eneo hilo kukutana na Obama White House.

By the way,JK ni kama amejipeleka tu because on the 10th of April (within his first 100 days in the White House),Obama called-not JK-but John Atta Mills wa Ghana.Na baadaye mwaka huu Obama will be visiting Ghana,not Tanzania.

Huyu mzururaji amebembeleza mpaka wamkubalie ili apate photocall na Obama.
 
Ni nafasi adhimu hiyo pamoja na dhihaka zenu kupata audience na US President sio mchezo, yes atatembeza bakuli na hatotoka mtupu.

Mmekalia majungu tu....
Surely he will...na wanaomdai michango yao kwenye kampeni ya 2005 (read as mafisadi) wanamsubiri arudi ili wapigane pasu kwa pasu from the bakuli.Any reason to be happy with that?
 
Namtakia kila la heri Rais kikwete maana pale anaenda kukutana na kichwa! Sana sana aangalie namna nzuri ya kutumia fursa hiyo nyeti kuwasaidia maskini tulio mgongoni mwake tunaoishi chini ya nusu dola moja. Hilo likiwa lengo tunamwombea afanikishe malengo yake.
Huo ndio mtazamo wangu wanajamvi. Maisha bora kwa kila mtanzania yanawezekana na yatapatikana.


Nimeshindwa kukupata vyema, unadhani umaskini wa watanzania unaweza kuondoka kwa JK kwenda kuombaomba? Fedha anazoomba kutoka kwa hao jamaa hazizidi zile mafisadi wanahamisha kila kukicha, fungua macho. Hatuwezi kuendelea kwa kutegemea misaada, na wala haya mataifa matajiri hayapo kwa lengo la kuondoa umaskini, ni mpaka wenyewe tutakapoamka na kuamua kuwa inatosha kuibiwa, tutalinda na kutetea nchi yetu, na kuiendeleza, ndipo maendeleo yatakuja. Kwa mtaji huu wa kuombaomba hatuwezi kufika popote, na hakuna nchi wala mtu aliyeendelea kwa stahili hiyo katika historia, labda anajaribu kuandika historia kwa kuwa Rais wa Kwanza kusini mwa Jangwa la Sahara kwenda kuomba kwa Obama.
 
Watz jamani yaani kila kitu ni lazima tumlaumu JK?

Tuwe wakweli..kuonana na Obama ni kupandisha chart yetu sisi Watz!

Je hilo pia kuna ubaya????????
 
Hamna cha muhimu atakachoongea zaidi ya kukenua meno kila sekunde. Hajui hata nini kinaendelea nchini mwake.
Obama ana-appreciate na ku-support wale wanao-fight for good citizens and not FISADIZ.
 
05_09_xh01pn.jpg


Mchambuzi wa Sera wa Kampuni ya Google ya Marekani, Jake Hubert, akielezea mtandao wa kampuni hiyo unavyofanya kazi kwa Rais Juma Kilaza aliyetembelea kampuni hiyo juzi mchana katika eneo la Silicon Valley, San Jose, California

Wabongo tunanufaikaje hapo? SteveD alisema ni sawa unapotembelea kiwanda cha soda unashangaa jamaa machine zinavyofanya kazi https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/29125-kikwete-usa-again-may-2009-a-11.html#post458572 ! Hapa kweli tumeliwa haswa!

Faida ipo kubwa upande wa mafisadi kama hamjui, unajua kwa sasa maendeleo ya IT yamekuwa mwiba mkubwa sana kwao hawa jamaa. Kwa akili zao wao wanadhani wanajenga uhusiano mzuri ili iwe rahisi kuwakamata wale wanaoitumia technolojia kuwaanika. Ila kilichopo hapo ni kama Busanda kupiga picha za kuja kuwatishia wadanganyika kuwa mkiwatoa tena kama vile kule lambalamba watawapata tu, japo ukweli ni kwamba hilo haliwezekani, si mlisikia hotuba ya Msola kuhusu matumizi mabaya ya IT.

Huenda mpango wa kuonana na Obama pia ni kumuomba awashughulikie watu wanaomuangaisha katika mtandao kutokea USA- Mkjj et al mpo? hahahaa! angalieni picha ya simba inaweza uma siku moja.
 
Watz jamani yaani kila kitu ni lazima tumlaumu JK?

Tuwe wakweli..kuonana na Obama ni kupandisha chart yetu sisi Watz!

Je hilo pia kuna ubaya????????

Kweli kupanda chart.....!! Wakati wananchi wa TZ walio wengi wanashindwa kupata milo hata miwili kwa siku!!
 
Nchi hii... Semina Elekezi haziiishi...Wakuu wa wilaya wooote nchini (isipokuwa wa Busanda na kule kwa marehemu MB.wa TLP (RIP)wapo Dar, tunasuguana katika foleni,ndio maana sasa hivi magari hayasogei... Rais wetu yupo GOOGLE iviiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.....
 
Mara nyingi kama utakutana na rais wa Marekani sio ki - Official mwombaji huwa analipa fedha kwa Agent ambaye huandaa makutano kama haya. Je, sisi tumelipa ngapi!..
 
Mara nyingi kama utakutana na rais wa Marekani sio ki - Official mwombaji huwa analipa fedha kwa Agent ambaye huandaa makutano kama haya. Je, sisi tumelipa ngapi!..

Mkandara,
Kama nauli na matumizi ya JK anapojirusharusha hatuambiwi unafikiri hii ndio tutafahamishwa kama ipo?


JK kaipanga hii safari ili picha atakazopigwa na Michuzi zitumike kwenye kampeni ya 2010. Bila ya kuwaghiribu wadanganyika na ahadi za uongo ataimba wimbo gani kwa wakati kazi alizofanya ni mbili tu;
  1. Ya uVasco Dagama tu na
  2. Kuwakingia Wahindi kifua kwenye ufisadi wao?
Hiki ndio kilichompeleka kujichombeza chombeza kwa Obama bila ya kualikwa.
 
That's the way it is, Kikwete is cruising internationally at the moment, now whether he's a flop at home that is a different matter for a different debate.

But, I would think Obama's choice of Kikwete to visit him at the White House is aimed at launching a plan to help majirani zetu Kenya, kama groundwork ya kumwezesha Obama kuzuru Kenya kabla ya kumalizika 2010. Kumbuka kwake beyond 2010 ni kampeni ya uchaguzi wa USA.
 
Hamna shida ngoja apite kumsabai Jaluo jirani yetu... lakini lazima akumbuke kuwa hata Russia ni marafiki zetu na inabidi kumtembelea na Medvedev siku moja! Who knows labda Russia ndio wanajua nani katuloga Tanzania na wanaweza kutupepea.
 
Mara nyingi kama utakutana na rais wa Marekani sio ki - Official mwombaji huwa analipa fedha kwa Agent ambaye huandaa makutano kama haya. Je, sisi tumelipa ngapi!..

- Angalau dola laki moja, hata ikiwa official lazima hiyo hela ilipwe rais wa US ana shughuli nyingi sana hana muda wa ku-chat na rais wa Africa, lazima nchi yenu itoe hela angalau lakini moja mpaka na nusu, na nusu ya hizo zinaenda kwenye chama chake cha siasa zingine ni za agent,

- Tena huyu agent ni permannet, analipwa on monthly bases au annually depending na contract yake na taifa, kwa mfano bongo tukitaka kuomba msaada toka US, huyu agent lazima awe wa kwanza kufahamishwa na atoe input yake kwanza, hawa ma-agent wanaitwa ma-lobbyist na wengi wao ni viongozi wa zamani mashuhuri wa US kama Gingrich former speaker.

Respect.

FMES!
 
That's the way it is, Kikwete is cruising internationally at the moment, now whether he's a flop at home that is a different matter for a different debate.

But, I would think Obama's choice of Kikwete to visit him at the White House is aimed at launching a plan to help majirani zetu Kenya, kama groundwork ya kumwezesha Obama kuzuru Kenya kabla ya kumalizika 2010. Kumbuka kwake beyond 2010 ni kampeni ya uchaguzi wa USA.

Sidhani kama Obama amemwita JK, hakuna dalili zozote za kuashiria hilo.

  • Mkutano muhimu kihistoria kama huo kati ya two black presidents, the first US black president na an African head of state ungepigiwa mabango kitambo, huko US na TZ-Daily News kwa angalau wiki mbili hivi mfululizo. Lakini ni mpaka JK alipokuwa West Coast ndio tangazo likatolewa na White house hapo jana, ikionyesha kabisa hii ni kama mgeni asiyekuwa na mpango.
  • Umuhimu wa TZ kwa serikali ya Obama ni mdogo sana au haupo kabisa otherwise angeshateua balozi mwenye uzito kama alivyofanya Bush.
  • Obama hamhitaji JK ili aongee na ndugu zake Kenya, after all amekuwa anaongea nao kila siku directly au through dada yake ambaye alikuwa naye tokea kwenye kampeni.
  • Zaidi ya hayo, Odinga na Obama ni ndugu na wanafahamiana vizuri sana kabla hata Obama hajawa raisi. Kwa hiyo hakuna dalili zozote za Obama kumhitaji JK kwa ajili ya kuongea na Wakenya.
Obviously kwenye hii safari, ni JK aliyejipendekeza na ni kwa manufaa yake binafsi na wala sio kwa ajili ya Watanzania. JK amebembelezea mpaka White House wakampa nafasi ya kupiga picha na Obama ili akaitumie Mwakani kwenye uchaguzi.
 
michuzi full kutinga oval office... maswala ya kiutani haya wtf...lol
 
Angalau dola laki moja, hata ikiwa official lazima hiyo hela ilipwe rais wa US ... lazima nchi yenu itoe hela angalau lakini moja mpaka na nusu, na nusu ya hizo zinaenda kwenye chama chake cha siasa zingine ni za agent,

... kwa mfano bongo tukitaka kuomba msaada toka US, huyu agent lazima awe wa kwanza kufahamishwa na atoe input yake kwanza, hawa ma-agent wanaitwa ma-lobbyist

Lobbyist toka lini akatoa input kuhusu nani wa kupewa foreign aid wewe mtu Field Marshall wewe?

Foreign governments lobbyist unamlipa kukuunganishia audience na Whitehouse tu, he can care less kama mtapata mnachoenda kuomba huko. Na anaelipwa ni yeye lobbyist, sio DNC wala GOP, wala Whitehouse.

Kuilipa Whitehouse ili ukutane nao ndio hizo unethical "cash for access" scandals zilizowazamisha kina Stephen Payne na Jack Abramoff. Eti Kikwete kamlipa Obama at least dola laki kukutana nae...usitoe shule potofu hapa.
 
Back
Top Bottom