franksarry
JF-Expert Member
- Nov 9, 2009
- 1,284
- 481
Nukuu ya Sumaye... "Hatutaki Govt ya Magufuli...
Tunataka Govt ya Wananchi - CDM...
Tunataka Govt ya Wananchi - CDM...
Wakati anamponda Lowassa ulutheri na ukanda hakuwa nao?
Wakati EL na Sumaye wakiwa paka na panya hawakuwa wote walutheri? sasa ilikuwaje?
Mbona Mwigulu Mlutheri lakini anaendesha mashambulizi kwa EL?
Mbona Mangula Mlutheri lakini anaendesha mapambano dhidi ya EL?
Sitta... Mwakyembe je?
Hivi kwanini CCM mnapenda kukimbilia ajenda za kipuuzi zinazoweza wamaliza wenyewe?
Kuna walutheri wangapi wenye nguvu huko CCM ambao ndo mnawatumia kumpiga EL?
Unafikiri wote ni manyani kama wewe mnaokimbilia abracadabra za udini?
Daaah,tukifungia Jangwani itakuwa raha sana maana ule ufunguzi tu ulikuwa burudani tupu.
Ndugu wana JF,
Nimelazimika kumwandikia rafiki yangu kipenzi JK waraka huu wa swali kwamba sasa amemwelewa Sumaye? Ktk makundi ya wanafunzi tunazo aina tatu yaani gold...silver...stone.
Gold huweza kuelewa bila msaada wa mwalimu na kwa haraka sana... Silver huelewa mara moja akifundishwa na mwalimu na hahitaji nguvu ya ziada ... Stone yeye hata akifundisha ni ngumu kuelewa na huhitaji mbinu kali zaidi aelewe ikibidi kwa kurudia rudia somo lkn hawa hawafiki mbali kielimu.
Nimeanza na utangulizi huo nikiikumbuka kauli ya rafiki yangu JK pale jangwani kwenye ufunguzi wa kampeni za CCM aliposema amemsikiliza Sumaye hajamwelewa!! anasema mpaka siku hiyo anapokwenda uwanjani alikuwa hajamwelewa!!!!
Lakini ktk sokomoko hilo tumeshuhudia CCM ikibadili mbinu na sera... Bajeti ya kampeni ikiongezeka maradufu na hata kuwakumbatia wale JK aliowaita wanamiliki viwanda vya uongo ili tu kupunguza mvumo wa kauli na sumu za Sumaye majukwaani ndo nauliza sasa JK amemwelewa Sumaye?
Ndani ya vikao vya siri ajenda imekuwa Sumaye... ndugu yangu BM hana raha tangu Sumaye aondoke CCM...
Vilio na kutupiana lawama vimetawala ndani ya CCM juu ya kile Sumaye anafanya huko UKAWA!!!
Mafaili machafu dhidi yake yametafutwa yamekosekana!! hata hoja ya shamba halali la mvomero iliyoletwa na Makamba haijauza sasa wanaulizana ITAKUWAJE SUMAYE ANAYETUJUA SISI BINAFSI AKIAMUA KUFUNGUKA??
Siku anajitoa CCM Sumaye alisema huko CCM mmemuona ni sisimizi tu kiasi cha kuandika barua kutojibiwa hivyo wataona umuhimu wake akiwa Upinzani na ni dhahiri sasa anawatetemesha ndipo nauliza JK sasa umemwelewa Sumaye?
Nimeuliza kote walikopita wana UKAWA nimeambiwa watu wamekua na shauku kubwa mno yakumsikiliza bwana zero kuliko yeyote na amekuwa akitoa hamasa sana ....
Sumaye amejenga ujasiri sana kwa wapinzani na wapenda mabadiliko... ameondoa hofu na woga... amejenga kujiamini sasa vinaanza vitisho kuwa nchi haiendi upinzani!!!!
Nauliza tena JK uliyesema kwa dharau humwelewi Sumaye sasa umemwelewa au abadili mbinu za ufundishaji? umuulize na mdogo wako Makongoro ule mchezo wa CHANDIMU vipi mbona amechoka mapema??
Ahsante kwa kunisoma natumai umenielewa!!!
Ndimi LUSUNGO.
Sumaye anamsubiri mkuu wa malofa BM atie neno amtolee uvivu/amuumbue kwa matakataka aliyofanya wakiwa naye ikulu.
yale yaleeee
kila mtu kulalamika. mtu wa chini analalamika. mtu wa kati analalamika. na hata aliyeko juu analalamika. huku ni kukosa umakini na kutokuwa responsible tuuuu
sumaye waziri mkuu kwa miaka 10 kipindi cha akina iptl, meremeta na nk anakimbiaje madhaifu kipindi cha mkapa? huyu si msema kweli
kama huyu naye ni tegemeo la ukawa basi ukawa hamna kitu. huyu ilikuwa asikaribishwe hata huko ukawa
kama si sumaye wa kumlaumu kwa miaka 10 alipokuwa msaidizi nambari 1 wa mkapa mambo yalipokuwa yana haribika tumlaumu nani?
tumieni akili japo kidogo
Kama shida yako unatafuta wa kumlaumu kwani Mkapa kafa? Kwanini kumlaumu msaidizi wakati mwenyewe aliekuwa juu ya yote wakati wa kipindi chake yupo? Huoni alivyofunga mdomo wake? Hathubutu!
Akirogwa mbona mwenyewe mtamuonea huruma. Maana kipigo alichokipata, kile cha Arumeru kitakuwa "cha-mtoto".
Unajua kwanini summaye alikuwa anaitwa Mr ZIRO?
SUMMAYE AKILI ZAKE NI NDOGO SANA NA NDO MAANA ANAISHI KWA MITEGO YA KISIASA,
Kiburi cha JK kiko juu mno na matokeo yake ni anguko lake na chama cha mapinduzi.
Team ilio upande wa ccm wamebaki kujitumainisha tu kusiko na Tumaini halisi,wanajitia moyo na kujifariji kuwa Watashinda.
Wakati uhalisia wa Mambo chama tawala kuachwa na MAWAZIRI WAKUU WASTAAFU WAWILI NA KWENDA KUJIUNGA NA CHADEMA/UKAWA HILO NI PIGO KUBWA SANA,Maana hao wanajua SIRI NZURI NA MBAYA ZA SERIKALI YA CCM.
Midomoni mwa makada wa ccm walibakia kuenzi kijani WANACHEKA lakini Mioyoni mwao wanajaziba,hasira na wana uhakika ngoma imewashinda mwaka huu USHINDI SIO WAO.
SASA JK AMEMWELEWA SANA TENA SANA TU,NA AKIJIFANYA KUENDELEA KUBWABWAJA ANACHOFANYA SUMAYE/UKAWA NI KUBONYEZA MAHALI PENYE JERAHA TU Hapo utasikia MACCM WAKIANGUA KILIO TU.