Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,513
- 113,641
Wanabodi,
Tukubali tukatae hadi sasa, watangaza nia ya urais kupitia CCM wameishavuka idadi ya watu 20, na inasemekana watakwenda hadi kufikia 30!, hivyo huu sasa ni utitiri wa watangaza nia ya urais kupitia CCM.
Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere aliwahi kupaita "Ikulu ni Mahali Patakatifu, ukimuona mtu anapakimbilia ikulu, huyo ni wa kuogopwa kama ukoma!", na kuuliza hivi Ikulu kuna bishara gani?!, sasa hadi watu zaidi ya 30 watake kupakimbilia?!.
Swali linakuja, je, utitiri huu ni uthibitisho wa wigo mpana wa demokrasia ndani ya Chama cha Mapinduzi, wenye kuthibitisha kila mwanachama mwenye sifa ya uongozi, yuko huru kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama ukiwemo urais?!.
Au utitiri huu, ni kufuatia JK kusemekani ndio amekuwa rais dhaifu kuliko rais mwingine yoyote wa Tanzania, na mfano mmoja tuu wa vitendo vya kuudhihirisha udhaifu wa JK kwenye taasisi ya urais, ni kile kitendo watu kukutwa na kuthibitishwa pasi shaka kuwa wamekwiba fedha za umma kupitia EPA, badala ya kushitakiwa na kuiachia sheria ifuate mkondo wake, JK kwa kutumia mamlaka ambayo hayapo mahali popote kikatiba, aliamua kuwasamehe kwa nia njema ili nchi isitikisike!.
Maamuzi kama haya yamepelekea taasisi ya urais kuonekana ni kitu cha kawaida tuu, yaani ni very cheap, na kuelezwa kuwa kama JK ameweza kuwa rais kwa miaka yote hii kumi, then every Tom, Dick and Harry can be a president, na hii ndio imepelekea utitiri huu wa watia kupitia CCM!. Jee kuna ukweli wowote katika hili?!.
Hawa ni baadhi ya watia nia na watia nia watarajiwa kupitia CCM. Hapa nawataja kwa prominence, power na electability:
Mimi binafsi yangu, nimewagawa watia nia hawa wa CCM kwenye makundi Saba...
Kundi la Kwanza ni ni wale nawaita ambao ni serious, hao ni wa kweli, wanautaka urais kiukweli kweli, wana mission na vision wanataka kuifanyia nini Tanzania, na wanautaka urais ili kuiondoa Tanzania hapa ilipo na kuipeleka kule ilikopaswa iwe. Kundi hili linaundwa na watu ambao ni presidential material. Kundi hili lina watu wachache na humu ndimo rais atatoka.
Kundi la Pili la watia nia, ni kundi la Wasindikizaji tuu, hawa nawaita 'pace makers' wameletwa ili kuonyesha urais una unashindani, ni wale ambao wanajijua kamwe kuchaguliwa hawawezi, lakini watagombea ili tuu kuwasindikiza baadhi ya wagombea wao makini just in case of anything can happen, mgombea wao asipopitishwa kwa sababu zozote zile, then watumike kama fall back positions.
Kundi la Tatu, ni ni la wagombea zuga au boshen, tuu ili kuzipooza hasira za watu, kundi hili mostly litahusisha wagombea kutoka Zanzibar, au wagombea wanawake. Kufuatia urais wa muungano ni suala la muungano na ulipaswa kupokezana kati ya Bara na Zanzibar, na pia kuna mpekezano wa Dini kati ya Mkristu na Muislamu.
Then, alipomaliza Mkapa ambaye ni Mkristu kutoka Bara, alipaswa afuatiwe na Muslamu kutoka Zanzibar, lakini kwa vile kitu kinachoitwa "Mtandao" kiliishabuniwa na kuwepo in place, kikaangalia aliyepaswa kumpokea Mkapa ni Muislamu kutoka Zanzibar, ili kubadili mchezo, Huyo Muislamu kutoka Zanzibar ilimbidi ashughulikiwe na kupotezewa kabla!, ili game liweze kurudi bara kwa excuse kuwa Zanzibar hakuna mtu!, kilichomkuta wengi mnakijua!,
Na "jamaa wa sehemu walihakikisha no post-mortem' ili kuthibitisha ni kazi ya Mungu!. Sasa kufuatia 1995 rais alitoka bara, 2005 rais akatoka tena bara, this time 2015 ki haki, kimuungano na kihalali ni zamu ya Zanzibar, lakini kwa vile mgombea wa CCM aliyemaliza ni Muislamu, na mgombea wa CCM wa 2015 tayari yupo, huu mchakato ni zuga tuu, then CCM wakituletea Muislamu mwingine, 'Kanisa' linaweza lisikubali.
Waliangalia uwezekano wa kumshawishi Jaji Ramadhani, ili kumtumia tuu kama zuga kuwazuga Wazanzibari, akaishtukia hii dili, akawagomea kata kata na hakuna Mkristo mwingine Presidential materia kutoka Zanzibar, hivyo CCM itahakikisha inawachagiza baadhi ya wagombea kutoka Zanzibar kugombea ili kuzugia tuu!.
Kundi la Nne ni la watia madekio na madodoki ya kusafishia watu!. Kufuatia baadhi ya wagombea kusemekena sio safi, wako wenye kashfa za rushwa, wako wenye tuhuma za ufisadi, wako wenye tuhuma za usaliti ambao walihama chama na kuingia upinzani kisha wakaingia bungeni waliposhindwa wakarejea CCM, wako wenye tuhuma za kukataliwa na Baba wa Taifa.
Hivyo kuna wagombea wamechagizwa kugombea bila ya wao kujijua, huku anafahamika wazi sio presidential material, na wanajijua, ila wameshawishiwa na 'wenyewe' wagombee kwa kuahidiwa watapewa urais kwenye silver plater, kumbe lengo ni kuwatumia tuu kama ma dekio ya kusafishia wengine njia, au madodoki ya kusafishia wengine!.
Kundi la Tano ni Watangaza Nia Chinja chinja, Vichinjio, au visu vyenye makali kuwili!. Hili ni kundi ambalo wenyewe hawautaki urais, ila ni heavy guards, hawa wameshawishiwa kutangaza nia ili CCM iwatumie kama chinjio la kuchijia wale heavy guards wasiotakiwa!.
Kwa vile kwenye wasaka urais kwa udi na uvumba yupo mtu wa level fulani, mfano wa calibre ya Waziri Mkuu Mtaafu, huwezi kumchinja hivi hivi tuu, sasa ili kuhalalisha kumchinjia baharini, CCM imemshawishi Waziri Mkuu mwingine mstaafu nae agombee, na Waziri Mkuu incumbent pia agombee ili kwenye kikao cha maamuzi, ijengwe hoja hatuwezi kupitisha mawaziri wakuu wastaafu watatu, tutapitisha mmoja, huyu ni yupi.
Hatuwezi kumkata incumbent tukampitisha wa zamani, hivyo wa kwanza kuchinjwa atakuwa ni wazamani hadi wa sasa hivyo kitendo cha Waziri Mkuu au Makamo wa Rais kuchinjwa, kutakufanya kujikuta unatulia na kujichwa kimya kimya huku umetulia!.
Kundi la Sita, la wagombea la watangaza nia waoteaji , Akiba Uzeeni, hawa wanatumia mtindo unaoitwa the JK style. Hili ni kundi la vijana ambao umri bado sana, hivyo wanatangaza nia kwa kuotea tuu ili kujenga profile nzuri kwa 2025, kama alivyofanya JK 1995 na kuja kuchukua 2005.
Kundi la Saba, ni kundi la watia ni kujulisha "nipo nipo", au "Remember Me", hili ni kundi la watu ambao kwanza sio presidential material. wala urais hawautaki, bali wanagombea tuu ili kujenga profile za kujulikana, kukumbukwa, ili angalau angalau wataeuliwe uwaziri au post yoyote. Kwenye kundi hili humu ndimo wanagombea watu just for show off tuu kuwa na wao wanaweza!, yaani nao japo hawavumi lakini wamo!.
Kwa kumalizia, jee utitiri huu, ni healthy kwa ujenzi wa demokrasia ndani ya CCM au ndio aibu ya udhaifu wa JK kuufanya urais kuwa too cheap?!.
Wasalaam
Jumapili Njema.
Pasco
Tukubali tukatae hadi sasa, watangaza nia ya urais kupitia CCM wameishavuka idadi ya watu 20, na inasemekana watakwenda hadi kufikia 30!, hivyo huu sasa ni utitiri wa watangaza nia ya urais kupitia CCM.
Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere aliwahi kupaita "Ikulu ni Mahali Patakatifu, ukimuona mtu anapakimbilia ikulu, huyo ni wa kuogopwa kama ukoma!", na kuuliza hivi Ikulu kuna bishara gani?!, sasa hadi watu zaidi ya 30 watake kupakimbilia?!.
Swali linakuja, je, utitiri huu ni uthibitisho wa wigo mpana wa demokrasia ndani ya Chama cha Mapinduzi, wenye kuthibitisha kila mwanachama mwenye sifa ya uongozi, yuko huru kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama ukiwemo urais?!.
Au utitiri huu, ni kufuatia JK kusemekani ndio amekuwa rais dhaifu kuliko rais mwingine yoyote wa Tanzania, na mfano mmoja tuu wa vitendo vya kuudhihirisha udhaifu wa JK kwenye taasisi ya urais, ni kile kitendo watu kukutwa na kuthibitishwa pasi shaka kuwa wamekwiba fedha za umma kupitia EPA, badala ya kushitakiwa na kuiachia sheria ifuate mkondo wake, JK kwa kutumia mamlaka ambayo hayapo mahali popote kikatiba, aliamua kuwasamehe kwa nia njema ili nchi isitikisike!.
Maamuzi kama haya yamepelekea taasisi ya urais kuonekana ni kitu cha kawaida tuu, yaani ni very cheap, na kuelezwa kuwa kama JK ameweza kuwa rais kwa miaka yote hii kumi, then every Tom, Dick and Harry can be a president, na hii ndio imepelekea utitiri huu wa watia kupitia CCM!. Jee kuna ukweli wowote katika hili?!.
Hawa ni baadhi ya watia nia na watia nia watarajiwa kupitia CCM. Hapa nawataja kwa prominence, power na electability:
- Mhe. Edward Ngoyai Lowassa
- Mhe. Dr. Mohamed Gharib Bilal
- Mhe. Mizengo Kayanda Pinda
- Mhe. Dr Asharose Migiro
- Judg. Augustine Ramadhani
- Dr. Augustine Philip Mahiga
- Mhe. Bernard Kamilius Membe
- Mhe. Prof. Mark Mwandosya
- Mhe. Prof. Sospeter Muhongo
- Mhe. Samwel John Sitta
- Mhe. John Pombe Magufuli
- Mhe. January Yusufu Makamba
- Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba
- Mhe. Stephen Masatu Wassira
- Mhe. Lazaro Samuel Nyalandu
- Mhe. Mathias M Chikawe
- Mhe. Titus Mlengela Kamani
- Mhe. Dr. Hamisi Andrea Kigwangala
- Fredrick Tluway Sumaye
- Hassy Besen Kitine
- Mhe. Luhaga Joelson Mpina
- Mhe. Charles Makongoro Nyerere
- Balozi Amina Salum Ali
- Balozi Ali Karume
- Dr. Mwelecele Ntuli Malecela
- Dr Muzzamil Mussa Kalokola
- Monica Ngenzi Mbega
- Amos Robert Siyatemi
- Musa Godwin Mwapango
- Peter Isaiah Nyalali
- Boniface Thomas Ndengo
- Maliki Salum Marupu
- Leonce Nicholas Mulenda
- Lidephonce M Bilohe
Mimi binafsi yangu, nimewagawa watia nia hawa wa CCM kwenye makundi Saba...
Kundi la Kwanza ni ni wale nawaita ambao ni serious, hao ni wa kweli, wanautaka urais kiukweli kweli, wana mission na vision wanataka kuifanyia nini Tanzania, na wanautaka urais ili kuiondoa Tanzania hapa ilipo na kuipeleka kule ilikopaswa iwe. Kundi hili linaundwa na watu ambao ni presidential material. Kundi hili lina watu wachache na humu ndimo rais atatoka.
Kundi la Pili la watia nia, ni kundi la Wasindikizaji tuu, hawa nawaita 'pace makers' wameletwa ili kuonyesha urais una unashindani, ni wale ambao wanajijua kamwe kuchaguliwa hawawezi, lakini watagombea ili tuu kuwasindikiza baadhi ya wagombea wao makini just in case of anything can happen, mgombea wao asipopitishwa kwa sababu zozote zile, then watumike kama fall back positions.
Kundi la Tatu, ni ni la wagombea zuga au boshen, tuu ili kuzipooza hasira za watu, kundi hili mostly litahusisha wagombea kutoka Zanzibar, au wagombea wanawake. Kufuatia urais wa muungano ni suala la muungano na ulipaswa kupokezana kati ya Bara na Zanzibar, na pia kuna mpekezano wa Dini kati ya Mkristu na Muislamu.
Then, alipomaliza Mkapa ambaye ni Mkristu kutoka Bara, alipaswa afuatiwe na Muslamu kutoka Zanzibar, lakini kwa vile kitu kinachoitwa "Mtandao" kiliishabuniwa na kuwepo in place, kikaangalia aliyepaswa kumpokea Mkapa ni Muislamu kutoka Zanzibar, ili kubadili mchezo, Huyo Muislamu kutoka Zanzibar ilimbidi ashughulikiwe na kupotezewa kabla!, ili game liweze kurudi bara kwa excuse kuwa Zanzibar hakuna mtu!, kilichomkuta wengi mnakijua!,
Na "jamaa wa sehemu walihakikisha no post-mortem' ili kuthibitisha ni kazi ya Mungu!. Sasa kufuatia 1995 rais alitoka bara, 2005 rais akatoka tena bara, this time 2015 ki haki, kimuungano na kihalali ni zamu ya Zanzibar, lakini kwa vile mgombea wa CCM aliyemaliza ni Muislamu, na mgombea wa CCM wa 2015 tayari yupo, huu mchakato ni zuga tuu, then CCM wakituletea Muislamu mwingine, 'Kanisa' linaweza lisikubali.
Waliangalia uwezekano wa kumshawishi Jaji Ramadhani, ili kumtumia tuu kama zuga kuwazuga Wazanzibari, akaishtukia hii dili, akawagomea kata kata na hakuna Mkristo mwingine Presidential materia kutoka Zanzibar, hivyo CCM itahakikisha inawachagiza baadhi ya wagombea kutoka Zanzibar kugombea ili kuzugia tuu!.
Kundi la Nne ni la watia madekio na madodoki ya kusafishia watu!. Kufuatia baadhi ya wagombea kusemekena sio safi, wako wenye kashfa za rushwa, wako wenye tuhuma za ufisadi, wako wenye tuhuma za usaliti ambao walihama chama na kuingia upinzani kisha wakaingia bungeni waliposhindwa wakarejea CCM, wako wenye tuhuma za kukataliwa na Baba wa Taifa.
Hivyo kuna wagombea wamechagizwa kugombea bila ya wao kujijua, huku anafahamika wazi sio presidential material, na wanajijua, ila wameshawishiwa na 'wenyewe' wagombee kwa kuahidiwa watapewa urais kwenye silver plater, kumbe lengo ni kuwatumia tuu kama ma dekio ya kusafishia wengine njia, au madodoki ya kusafishia wengine!.
Kundi la Tano ni Watangaza Nia Chinja chinja, Vichinjio, au visu vyenye makali kuwili!. Hili ni kundi ambalo wenyewe hawautaki urais, ila ni heavy guards, hawa wameshawishiwa kutangaza nia ili CCM iwatumie kama chinjio la kuchijia wale heavy guards wasiotakiwa!.
Kwa vile kwenye wasaka urais kwa udi na uvumba yupo mtu wa level fulani, mfano wa calibre ya Waziri Mkuu Mtaafu, huwezi kumchinja hivi hivi tuu, sasa ili kuhalalisha kumchinjia baharini, CCM imemshawishi Waziri Mkuu mwingine mstaafu nae agombee, na Waziri Mkuu incumbent pia agombee ili kwenye kikao cha maamuzi, ijengwe hoja hatuwezi kupitisha mawaziri wakuu wastaafu watatu, tutapitisha mmoja, huyu ni yupi.
Hatuwezi kumkata incumbent tukampitisha wa zamani, hivyo wa kwanza kuchinjwa atakuwa ni wazamani hadi wa sasa hivyo kitendo cha Waziri Mkuu au Makamo wa Rais kuchinjwa, kutakufanya kujikuta unatulia na kujichwa kimya kimya huku umetulia!.
Kundi la Sita, la wagombea la watangaza nia waoteaji , Akiba Uzeeni, hawa wanatumia mtindo unaoitwa the JK style. Hili ni kundi la vijana ambao umri bado sana, hivyo wanatangaza nia kwa kuotea tuu ili kujenga profile nzuri kwa 2025, kama alivyofanya JK 1995 na kuja kuchukua 2005.
Kundi la Saba, ni kundi la watia ni kujulisha "nipo nipo", au "Remember Me", hili ni kundi la watu ambao kwanza sio presidential material. wala urais hawautaki, bali wanagombea tuu ili kujenga profile za kujulikana, kukumbukwa, ili angalau angalau wataeuliwe uwaziri au post yoyote. Kwenye kundi hili humu ndimo wanagombea watu just for show off tuu kuwa na wao wanaweza!, yaani nao japo hawavumi lakini wamo!.
Kwa kumalizia, jee utitiri huu, ni healthy kwa ujenzi wa demokrasia ndani ya CCM au ndio aibu ya udhaifu wa JK kuufanya urais kuwa too cheap?!.
Wasalaam
Jumapili Njema.
Pasco