Kikwete awaachia huru Polisi waliomuua Jenerali Kombe

Kwa maelezo yako Hao askari wawili hawakumuuwa huyo Jenerali kombe kwa Makusudi kama ni hivyo Rais J.K . Ana haki ya kuwaachia huru ingawa Mahakama kuu ilitoa Adhabu ya kifo. Je Tuangalie Sheria yetu inasemaje je mtu akiuwa kwa bahati mbaya anaweza kuhukumiwa Adhabu ya Kifo? Na hata kama atahukumiwa na Mahakama Kuu adhabu ya kifo mwamuzi wa mwisho ni Rais ,Rais akitia saini ndipo anaweza huyo mtu kuuwawa Natanguliza hivyo asanteni...
 
Ulijuaje walimwuua kwa bahati mbaya? Unawezaje kumpiga risasi "mhalifu au mtuhumiwa" ambaye kishaweka juu mikono yake? It was cold blooded murder ordered by someone. Otherwise kwa nini wapewe msamaha sasa na hela za kuanzishia biashara?
 
Ni shinikizo toka kwa kikosi cha mauaji, ni kama vile hakikuwa active na sasa kimeibukia kwa akina Mwakyembe baada ya ya shinikizo lao la kutaka wenzao waachiwe kutimizwa......sasa chizi kapewa rungu tutashuhudia mengi....
 
waliohukumiwa kifo ni hawo tuu mbona kuna wengine wamekaa zaidi ya miaka 30 hawo vip????
 
Mimi nasema hivi Kikwete anataka tulipize visasi.SASA BASI UWEZO WA VISASI TUNAO,NIA TUNAYO NA SABABU TUNAYO.
 

una ushahidi kuwa babu seya alimkazia jk mke wake?.
 

Nadhani sasa unapotoka.. kwani kwa kuwa umepewa madaraka ndio huyatumie bila busara? Hapa kwa kweli raisi amechemka na anaonekana kabisa amefanya uamuzi kwa shinikizo fulani kitu ambacho kinazidi onyesha udhaifu wake kuwaogopa wasio na madaraka. Nadhani kuna mauaji mengine yanapangwa ila ukweli utakuja tuu kujionyesha.
 

Babau Seya he has never been a national , regional wala street threat to the secuirty mkuu .Kama amewahi thibitisha hapa ni kivipi .
 
Tusinhangaike bure hiyo ni system ya nchi yetu ndivyo wanavyojiendeshea mambo,walishauwawa wengi sana tu.Wakati mwingine tuweke chuki pembeni, hao jamaa waliua mwaka 1996 akiwepo Mkapa....leo 2011 JK anawasemehe manake kazi iliyoanza katika serekali iliyopita JK kafanya kuimalizia tu.Pia inaonekana anaujua ukweli kwamba hawa jamaa waliua na si kwa makusudi kwa mantiki kwamba walitumwa na watu wenye mamlaka nafikiri mna idea na mambo ya Jeshi yalivyo amri kwanza matokeo baadaye.Jifikirie wewe ndio ungekuwa askari hao waliopelekwa kwenye hilo zoezi ukaambia ukauwe watakukinga ..... jaribu kufikiria ungetaaa kingetokea nini?

Cha msingi hapa ni waliotoa hiyo amri ya hayo mauaji ndio wa wakutafutwa...ndio maana mnasikia watu wanapelekwa huko the HAGUE mnafikiri wao ndio walishika bunduki wakamwaga damu?Tafakari..
 

Kama wasema Mkapa hakusaini karatasi hiyo na hukumu ilisha pita JK alikuwa na mamlaka gani ya kuingilia hukumu iliyo pita na kuwa toa? kama wewe wakataa sisi tusimlaumu kwanini asiache nayeye kuingilia jambo hilo. Maana kama JK ame sign watoke basi wamekinzana na hukumu ya mahakama kumbuka mwenzio alipo kuwa kwenye urais haku sign wewe umekuja ukasign watoke mbona hapo mwatukanganya zaidi.

My Take;

Jk ni wakulaumiwa tuuu period
 
Nina wasiwasi na uwezo wako wa kufikiri. Si kila kitu ni siasa, mengine ni sheria zaidi. Ni bora usichangie kuliko kuchangia pumba. Hapa mzembe si Jk bali ni wewe nngu007. Katiba inampa uwezo rais kufuta au kupunguza adhabu yoyote. Rudi darasani!!!

Hili li f a l a nilishabiki la kijinga. Utaona ujinga wa mtu pale mapenz yake yanapozidi na anashabikia hata upuuzi.
Kwani si tunajua uwezo wa kiongozi wako.
 

sasa wewe ulitaka tu wakae gerezani bila kujua hatima yao. Je huoni huo ni kuvunja haki za binadamu kwa kumuweka mtu gerezani bila kumuhukumu?

Kosa la mkapa kwanini alikataa kusaini wakti hukumu hiyo bado ipo katika sheria za nchi yenu.
 
Mauaji ya Kombe hayakuwa ya bahati mbaya; yalikusudiwa. Nakumbuka magazeti mengi yalivyoripoti wakati ule:
Kwamba askari walikuwa wanamfukuza mwizi wa magari
Kombe alikuwa na mkewe nadani ya gari
Kombe baada ya kuona akikimbizwa alisimamisha gari na kutoka nje ya gari
Alinyosha mikono juu ya kujitambulisha, ndyo maana risasi ziliingia kifuani si mgongoni
Askari walimjua vyema kwani alikuwa bosi wao katika masual ya usalama wa Taifa
Kome alikuwa ametoa taarifa rasmi kuwa atasafiri kwa gari hilo kwenda Kilimanjaro,
Mkewe aliyashuhudia yote hayo, na kama askari wangekuwa wanamfuatilia mwizi magari, huyu mama wangemu-arrest baada ya kumuua huyo "mwizi wa magari' ili asaidie upelelezi; lakini huyu mama aliachwa hapo hapo.
Kombe alituhumiwa kumpa Mrema Lyatonga habari za kijasusi za mipango ya kumdhuru na ndiyo maana mitego mingi waliyoweka ilijulikana mapema kwa Mrema na kuweza kuikwepa. Nadhani mtu akienda maktaba anaweza kupata baadhi ya magazeti.
Katika hali hiyo, hawa askari wawili walikuwa wakitekeleza agizo la wakuu ndiyo maana JK kawaachia. Msishangae kuona wanalipwa kinyemela mafao yao!
 
Mie naona yafuatayo:
1. Katiba inayompa Rais madaraka ya kusamehe KOSA LOLOTE, itamke wazi kuwa adhabu ya kifo tunayoipigia kelele, IONDOLEWE KIKATIBA! Hii itaondoa manung'uniko ya Rais kusamehe pale anapojisikia kuna maslahi yake binafsi.
2. Serikali iILIPE familia ya Kombe hayo madai yaliyokubaliwa na Mahakama zetu! Tunaomba Rais alisimamie hili.
3. Maslahi ya Rais hapa, nionavyo mimi, ni kuwagawa wanaharakati wanaounga mkono kuondolewa adhabu ya kifo, ili waone kosa la kuwasamehe askari hawa 2 halikustahili.
4. Tunahitaji KATIBA MPYA SASA!
 


Hapo kwenye bold vipi kuhusu Govenor Of state?? Usilinganishe mataifa mawili tofauti yenye Judicial systems tofauti
 
@barubaru
vipi kazi ya kumuondoa gadaffi mmekamilisha? ukimaliza utaenda syria? huku kwetu pia kazi zako za kijasusi zinahitajika
 

Mkuu katika watu wote waliochangia hapa wewe ndio umenena maneno ya ukweli ukweli kabisa, maana naona wote hapa wanazunguka tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…