Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Nimekaa chini na kujiulizahivi Kikwete anafanya kazi kwa manufaa ya nani?
Kabla ya uchaguzi na hata kesho hii kuna Wakisto wengi wanaoamini kwa nguvu kubwa kuwa Kikwete yupo pale Ikulu Kui-Silimisha Tanzania na kufanya kazi kwa maslahi ya Waislamu.
Mnaodhania hivyo, Mchungaji anawapasha kuwa Kikwete hata hao nduguze katika imani kaka na dada zetu wa Kiislamu, kawasahau maana yeye anatumikia matumbo na kutimiliza matakwa ya Mafisadi, Wawekezaji na Mabeberu anaowaita Wakubwa!
Kwa ufahamu wangu mdogo wa Uislamu, ni dini inayolenga kwenye kuleta haki, kuboresha maisha na zaidi kuondoa unyonge, umasikini, dhiki, magonjwa na ujinga.
Waislamu wa Tanzania kwa muda mrefu wamekuwa wakitoa kilio cha kuachwa nyuma kimaendeleo, kuwa na maisha ya hali ya chini na hata kusahauliwa ukilinganisha na wenzao Wakristo.
Kama jinsi Wakristo wanavyojisahau na kudhani kuwa na Rais Mkristo ni tija (Ben Mkapa) ndivyo ndugu zangu Waislamu na sisi Wakristo na Wapagani tulivyopotoka na kudhani kuwa Kikwete ataleta mambo ya Uislamu na kutumia mafundisho ya Uislamu kumuongoza katika uongozi wake kuliongoza Taifa letu. Ama tulidhania kuwa ataleta upendeleo wa kimaendeleo kwa Waislamu pekee!
Ni heri angefanya mambo kwa manufaa ya Waislamu, ningemvulia kofia na kumpa sifa. Ningemuelewa na kukubaliana naye.
Lakini Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete, ni Mwislamu jina na si wa matendo kama vile Ben Mkapa alivyokuwa Mkristo jina na si kwa matendo.
Niliandika awali sana kuwa Waislamu wanaweza kufanya kosa kuamini kuwa kuwepo kwa Kikwete Ikulu, basi ni suluhisho la matatizo yao.
Matatizo ya Waislamu ni matatizo ya Watanzania wote, sema tofauti ni kuna waliopiga hatua na kuna walioachwa nyuma.
Kama leo hii Kikwete angewatumikia Waislamu na hivyo viwango vyao vya maisha kuboreka na kupiga hatua hata kukaribiana na Wakristo ( hisia kuwa Wakristo wana maisha bora) ningepiga vigelegele na kushangilia mageuzi na kuna mafanikio ya Maisha Bora kwa Mtanzania hata kama ukweli ungebakia kuwa ilikuwa ni Maisha Bora kwa Wasilamu.
Leo hii ningeona kwa macho na kusikia kuwa Waislamu kwa kutumia upendeleo maalumu uliofanywa na Rais Kikwete, wameongezeka idadi mashuleni na wanafaulu kwa kiwango kikubwa nimgepiga makofi. Leo hii tungeambiwa idadi ya kina mama, watoto na wazee wa kiislamu ambao wanatibiwa bila shida na wanaanza kuwa na afya njema imeongezeka marudufu, ningeangua like keleuwii la kichagga la kushangilia.
Leo ningesikia Waislamu kutokana na upendeleo maalumu, wana nyumba bora, ajira, mazao yao yananunulika kwa wingi na wanaweza kuzalisha kwa mfumo wa kisasa wa uzalishaji, ningekusanya bendi na tuanze mdumange kumsifia Kikwete.
Lakini kama alivyoingia madarakani, hali ya Mtanzania iwe ni Muislamu, Mkristo au Mpagani haiajabadilika, wamebakia pale pale wakisuasua na kukodoleana macho na kushutumiana.
Anayefaidika na sera na utawala wa Kikwete ni mtu fisadi, ni mwekezaji, ni yule aliye na madaraka, ni yule aliyeahidiwa nyongeza ya mapato kwa kuonyesha utii na mapenzi bila kumkosoa Kikwete au kuhoji anayotenda.
Mbaya zaidi wanaoneemeka kwa shibe kubwa ni Mabepari ambao tuliwapiga vita wakiwa wakoloni wetu. Mabepari hawa na Makuwadi wao ambao ndio kuna wapambe, mafisadi na wanaoshangilia kutesa kwa zamu na kuneemeka, hawana dini ya imani ya Ukristo au Uislamu ambazo zinampa tukuzo na thawabu mtu masikini.
Hawa dini yao ni ulafi na kuvimbiwa. Humo wako Wakristo, Wapagani, Waislamu na dini nyingine ambao ibada na imani yao iko kwenye fedha na vitu vya kidunia.
Watu hawa hutumia mazingaombwe kwenda Makanisani na Misikitini na kupewa mapokezi ya zulia kama wao ndio Miungu, na hawaishi kufadhili Makanisa na Misikiti kwa kutoa Tujisenti vyao vilivyotokana na dhuluma waliofanya dhidi ya Watanzania; Waislamu na Wakristo na kutambakuwa wanasaidia umma.
Ikiwa leo hii bado watu wa Chanika hawana maji ya Bomba na kule Manyara watoto wanakalia mawe kwenye darasa chini ya mti, huku Kikwete na wapambe wanagombania viwanja na mapato ya miradi ya kuwakumbatia Mafisadi na Wawekezaji, iweje ndugu Watanzania tudhanie kuwa tukiwa na Rais wa Dini yetu basi tumepona na tunahemea mavuno?
Maisha bora kwa Mtanzania hayatapatikana kutokana na Kiongozi Mkuu kuwa wa dini fulani au kutoa upendeleo maalumu kwa dini fulani!
Maisha bora yatapatikana kutokana na Kiongozi anayewajali wananchi wake, watu waliompa dhamana ya kuongoza kwa kuwaffanyia kazi na kuhakikisha kuwa Wananchi hawa hawateseki na hawaishi katika umasikini na udun wa kupindukia.
Maisha bora yatakuja Tanzania pale Kiongozi wetu atakapoamua kufanyia kazi na kutafutia ufumbuzi wa kudumu matatizo ya Watanzania wote bila kujali dini, imani, rika, jinsia au kabila.
Maisha bora yatakuja siku Kiongozi Mkuu atakapoamka na kuuchukia Umasikini, Ujinga na Maradhi yanayowazunguka Watanzania na kuanzisha mfumo mpya wa kijamii, kiuchumi na kisasa mabo utaijeng nchi upya na kutoa nafasi sawa za kuleta maendeleo kwa kila mtu.
Hivyo mnaodhania kuwa Kikwete ataleta ajenda za Kiislamu, mmelogwa na mmepungukiwa. Kawapiga changa la macho pale alipoteua Waislamu wachache hapa na pale na mkafutuka kusifia na wengine kulaani, kumbe mwenzenu maslahi anayoyafanyia kazi kwa udi na vumba na hata kuyalinda ni ya Mafisadi, Wawekezaji na Mabeberu!
Kabla ya uchaguzi na hata kesho hii kuna Wakisto wengi wanaoamini kwa nguvu kubwa kuwa Kikwete yupo pale Ikulu Kui-Silimisha Tanzania na kufanya kazi kwa maslahi ya Waislamu.
Mnaodhania hivyo, Mchungaji anawapasha kuwa Kikwete hata hao nduguze katika imani kaka na dada zetu wa Kiislamu, kawasahau maana yeye anatumikia matumbo na kutimiliza matakwa ya Mafisadi, Wawekezaji na Mabeberu anaowaita Wakubwa!
Kwa ufahamu wangu mdogo wa Uislamu, ni dini inayolenga kwenye kuleta haki, kuboresha maisha na zaidi kuondoa unyonge, umasikini, dhiki, magonjwa na ujinga.
Waislamu wa Tanzania kwa muda mrefu wamekuwa wakitoa kilio cha kuachwa nyuma kimaendeleo, kuwa na maisha ya hali ya chini na hata kusahauliwa ukilinganisha na wenzao Wakristo.
Kama jinsi Wakristo wanavyojisahau na kudhani kuwa na Rais Mkristo ni tija (Ben Mkapa) ndivyo ndugu zangu Waislamu na sisi Wakristo na Wapagani tulivyopotoka na kudhani kuwa Kikwete ataleta mambo ya Uislamu na kutumia mafundisho ya Uislamu kumuongoza katika uongozi wake kuliongoza Taifa letu. Ama tulidhania kuwa ataleta upendeleo wa kimaendeleo kwa Waislamu pekee!
Ni heri angefanya mambo kwa manufaa ya Waislamu, ningemvulia kofia na kumpa sifa. Ningemuelewa na kukubaliana naye.
Lakini Jakaya Mrisho Khalfani Kikwete, ni Mwislamu jina na si wa matendo kama vile Ben Mkapa alivyokuwa Mkristo jina na si kwa matendo.
Niliandika awali sana kuwa Waislamu wanaweza kufanya kosa kuamini kuwa kuwepo kwa Kikwete Ikulu, basi ni suluhisho la matatizo yao.
Matatizo ya Waislamu ni matatizo ya Watanzania wote, sema tofauti ni kuna waliopiga hatua na kuna walioachwa nyuma.
Kama leo hii Kikwete angewatumikia Waislamu na hivyo viwango vyao vya maisha kuboreka na kupiga hatua hata kukaribiana na Wakristo ( hisia kuwa Wakristo wana maisha bora) ningepiga vigelegele na kushangilia mageuzi na kuna mafanikio ya Maisha Bora kwa Mtanzania hata kama ukweli ungebakia kuwa ilikuwa ni Maisha Bora kwa Wasilamu.
Leo hii ningeona kwa macho na kusikia kuwa Waislamu kwa kutumia upendeleo maalumu uliofanywa na Rais Kikwete, wameongezeka idadi mashuleni na wanafaulu kwa kiwango kikubwa nimgepiga makofi. Leo hii tungeambiwa idadi ya kina mama, watoto na wazee wa kiislamu ambao wanatibiwa bila shida na wanaanza kuwa na afya njema imeongezeka marudufu, ningeangua like keleuwii la kichagga la kushangilia.
Leo ningesikia Waislamu kutokana na upendeleo maalumu, wana nyumba bora, ajira, mazao yao yananunulika kwa wingi na wanaweza kuzalisha kwa mfumo wa kisasa wa uzalishaji, ningekusanya bendi na tuanze mdumange kumsifia Kikwete.
Lakini kama alivyoingia madarakani, hali ya Mtanzania iwe ni Muislamu, Mkristo au Mpagani haiajabadilika, wamebakia pale pale wakisuasua na kukodoleana macho na kushutumiana.
Anayefaidika na sera na utawala wa Kikwete ni mtu fisadi, ni mwekezaji, ni yule aliye na madaraka, ni yule aliyeahidiwa nyongeza ya mapato kwa kuonyesha utii na mapenzi bila kumkosoa Kikwete au kuhoji anayotenda.
Mbaya zaidi wanaoneemeka kwa shibe kubwa ni Mabepari ambao tuliwapiga vita wakiwa wakoloni wetu. Mabepari hawa na Makuwadi wao ambao ndio kuna wapambe, mafisadi na wanaoshangilia kutesa kwa zamu na kuneemeka, hawana dini ya imani ya Ukristo au Uislamu ambazo zinampa tukuzo na thawabu mtu masikini.
Hawa dini yao ni ulafi na kuvimbiwa. Humo wako Wakristo, Wapagani, Waislamu na dini nyingine ambao ibada na imani yao iko kwenye fedha na vitu vya kidunia.
Watu hawa hutumia mazingaombwe kwenda Makanisani na Misikitini na kupewa mapokezi ya zulia kama wao ndio Miungu, na hawaishi kufadhili Makanisa na Misikiti kwa kutoa Tujisenti vyao vilivyotokana na dhuluma waliofanya dhidi ya Watanzania; Waislamu na Wakristo na kutambakuwa wanasaidia umma.
Ikiwa leo hii bado watu wa Chanika hawana maji ya Bomba na kule Manyara watoto wanakalia mawe kwenye darasa chini ya mti, huku Kikwete na wapambe wanagombania viwanja na mapato ya miradi ya kuwakumbatia Mafisadi na Wawekezaji, iweje ndugu Watanzania tudhanie kuwa tukiwa na Rais wa Dini yetu basi tumepona na tunahemea mavuno?
Maisha bora kwa Mtanzania hayatapatikana kutokana na Kiongozi Mkuu kuwa wa dini fulani au kutoa upendeleo maalumu kwa dini fulani!
Maisha bora yatapatikana kutokana na Kiongozi anayewajali wananchi wake, watu waliompa dhamana ya kuongoza kwa kuwaffanyia kazi na kuhakikisha kuwa Wananchi hawa hawateseki na hawaishi katika umasikini na udun wa kupindukia.
Maisha bora yatakuja Tanzania pale Kiongozi wetu atakapoamua kufanyia kazi na kutafutia ufumbuzi wa kudumu matatizo ya Watanzania wote bila kujali dini, imani, rika, jinsia au kabila.
Maisha bora yatakuja siku Kiongozi Mkuu atakapoamka na kuuchukia Umasikini, Ujinga na Maradhi yanayowazunguka Watanzania na kuanzisha mfumo mpya wa kijamii, kiuchumi na kisasa mabo utaijeng nchi upya na kutoa nafasi sawa za kuleta maendeleo kwa kila mtu.
Hivyo mnaodhania kuwa Kikwete ataleta ajenda za Kiislamu, mmelogwa na mmepungukiwa. Kawapiga changa la macho pale alipoteua Waislamu wachache hapa na pale na mkafutuka kusifia na wengine kulaani, kumbe mwenzenu maslahi anayoyafanyia kazi kwa udi na vumba na hata kuyalinda ni ya Mafisadi, Wawekezaji na Mabeberu!