Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,194
- 10,929
Katika historia ya dunia hakujawahi kuwepo utulivu .Ni vita tu kwa mitindo tofauti kulingana na muda.
Vita hivyo viko vya aina mbili.Vile vya kiuchumi na maslahi ya kidunia ambavyo hupiganwa na mashetani wawili wote wenye malengo ya kidunia.
Vita vya aina ya pili ni vya kidini ambavyo hupiganwa na wafuasi wa shetani kuwaweka mbali watu na Mungu na upande wa pili hupiganwa na wafuasi wa Mungu ambao huwa wana matarajio ya masiha mazuri baada ya kufa kwao.
Vita vya kidini daima vimekuwa baina wafuasi wa shetani dhidi ya waislamu ambao wanafuata Uislamu.
Historia inaanza mbali sana tangu dunia kuumbwa kwake.Historia ya karibu ni pale alipotumwa mtume Muhammad rehma na amani zimshukie.
Mtume Muhammad s.a.w alikuta dola za jirani za kifursi na roma pamoja na dola nyengine za kishirikina mbali na Makka na Madina.Dola zote hizo zilikwishaacha kufuata Uislamu na ikawa zinaendeshwa na shetani.Dola hizo hazikuacha kufanya uadui na dola ya kiislamu chini ya mtume huyo wa mwisho.
Vita vilivyoanzishwa na dola hizo havikuweza kuzuia ushindi wa waislamu.Uislamu ukafika Ulaya,nchi zote za Asia ikiwemo China,India na Urusi. Ilipoonekana kwa njia ya vita Uislamu haukushindikana,mfumo wa kufanya vita vya kiakili ukashika kasi na umeendelea kwa muda mrefu katikati yake pakaingia mchanganyiko wa vita vya kimaslahi ya dunia vikichanganywa na malengo ya dini kwa uongozi na fikra za kishetani.
Ukoloni kwa malengo ya kidunia ukaondoshwa hatua kwa hatua lakini vita vya kiakili kwa kutumia maendeleo ya kielimu ya kisasa bado havikusita.Katika vita hivyo waislamu wameshindwa pakubwa na kurudishwa nyuma wakibakiwa na maeneo madogo sana.
Upande wa vita vya kiakili dini za kikristo na nyenginezo zimefanikiwa kuwashinda waislamu kwa mbinu ya kuwatayarishia watawala watakaokuwa wakifanya kazi zilizo dhidi ya waislamu na kuwakandamiza waislamu wenye malengo ya kidini kwa maslahi ya akhera.
Mafanikio hayo yamekuwa makubwa kwa kuzishika nchi zote ambazo ni kitovu cha nguvu za waislsmu waliotawala kwa maongozi wa Mtume Muhammad s.a.w.Mbinu hiyo imechanganywa na kuzigombanisha nchi hizo na kuzifanya zisiwe na umoja wa aina yoyote ile. Kuna maeneo machache ambayo yamebaki katika maongozi hayo ambayo kwa kutumia vita vya kiakili wakristo na mayahudi wamekuwa wakishirikiana kuyamaliza kama wataweza.
Maeneo hayo ni kama vile Gaza ambako Israel akishirikiana na Marekani na Uiengereza wamekuwa wakipiga kwa nguvu na kwa silaha nzito sambamba na kuwalaza viongozi wa mataifa jirani kwa ulaghai tofaujti.
Ulaghai na diplomasia za ujanja na undumilakuwili umekuwa na mafanikio makubwa kwani viongozi wa nchi ziizo jirani ni wale waliotayarishwa kwa ajili ya muda kama huu.
Mfano wa mafanikio hayo ni kupigwa kwa eneo la Gaza na kuzuia chakula lakini nchi zote za kiislamu zimeshindwa kuzuia balaa hilo na hata kulaani kwa sauti ya juu.
Wakati huo huo Marekani inajitia huruma za mamba ikijifanya kujenga bandari ambayo irapeleleka chakula japo wana ratiba ya miezi miwili mbeleni .
Hatimae bandari hiyo itaondolewa kwenye kuwa ya muda na itapewa jukumu tofauti na hatimae kukamilisha malengo ya Israel ambaye ni mshirikia mkubwa wa Marekani na Uiengereza katika vita hivyo
Malengo mapana ya Israel kuimeza Gaza yote kama ilivyofanya kwa maeneo ya ukingo wa Magharibi yatakuwa yametimia.
Mataifa yaliyotarajiwa kuokoa janga hilo kwa vile hawajaweza kufanya muda huu mahitaji yake ni muda muafaka hawataweza kamwe kufanya jambo hilo baada ya kukamilika kwa malengo ya wapiganaji maadui wa Uislamu.
Kitakachobaki ni rehma za Allah subhanahu wa taala ambaye ana uwezo wa kubadili mwenyewe bila msaada wa yoyote muda huu kabla kufikia huko.
Vita hivyo viko vya aina mbili.Vile vya kiuchumi na maslahi ya kidunia ambavyo hupiganwa na mashetani wawili wote wenye malengo ya kidunia.
Vita vya aina ya pili ni vya kidini ambavyo hupiganwa na wafuasi wa shetani kuwaweka mbali watu na Mungu na upande wa pili hupiganwa na wafuasi wa Mungu ambao huwa wana matarajio ya masiha mazuri baada ya kufa kwao.
Vita vya kidini daima vimekuwa baina wafuasi wa shetani dhidi ya waislamu ambao wanafuata Uislamu.
Historia inaanza mbali sana tangu dunia kuumbwa kwake.Historia ya karibu ni pale alipotumwa mtume Muhammad rehma na amani zimshukie.
Mtume Muhammad s.a.w alikuta dola za jirani za kifursi na roma pamoja na dola nyengine za kishirikina mbali na Makka na Madina.Dola zote hizo zilikwishaacha kufuata Uislamu na ikawa zinaendeshwa na shetani.Dola hizo hazikuacha kufanya uadui na dola ya kiislamu chini ya mtume huyo wa mwisho.
Vita vilivyoanzishwa na dola hizo havikuweza kuzuia ushindi wa waislamu.Uislamu ukafika Ulaya,nchi zote za Asia ikiwemo China,India na Urusi. Ilipoonekana kwa njia ya vita Uislamu haukushindikana,mfumo wa kufanya vita vya kiakili ukashika kasi na umeendelea kwa muda mrefu katikati yake pakaingia mchanganyiko wa vita vya kimaslahi ya dunia vikichanganywa na malengo ya dini kwa uongozi na fikra za kishetani.
Ukoloni kwa malengo ya kidunia ukaondoshwa hatua kwa hatua lakini vita vya kiakili kwa kutumia maendeleo ya kielimu ya kisasa bado havikusita.Katika vita hivyo waislamu wameshindwa pakubwa na kurudishwa nyuma wakibakiwa na maeneo madogo sana.
Upande wa vita vya kiakili dini za kikristo na nyenginezo zimefanikiwa kuwashinda waislamu kwa mbinu ya kuwatayarishia watawala watakaokuwa wakifanya kazi zilizo dhidi ya waislamu na kuwakandamiza waislamu wenye malengo ya kidini kwa maslahi ya akhera.
Mafanikio hayo yamekuwa makubwa kwa kuzishika nchi zote ambazo ni kitovu cha nguvu za waislsmu waliotawala kwa maongozi wa Mtume Muhammad s.a.w.Mbinu hiyo imechanganywa na kuzigombanisha nchi hizo na kuzifanya zisiwe na umoja wa aina yoyote ile. Kuna maeneo machache ambayo yamebaki katika maongozi hayo ambayo kwa kutumia vita vya kiakili wakristo na mayahudi wamekuwa wakishirikiana kuyamaliza kama wataweza.
Maeneo hayo ni kama vile Gaza ambako Israel akishirikiana na Marekani na Uiengereza wamekuwa wakipiga kwa nguvu na kwa silaha nzito sambamba na kuwalaza viongozi wa mataifa jirani kwa ulaghai tofaujti.
Ulaghai na diplomasia za ujanja na undumilakuwili umekuwa na mafanikio makubwa kwani viongozi wa nchi ziizo jirani ni wale waliotayarishwa kwa ajili ya muda kama huu.
Mfano wa mafanikio hayo ni kupigwa kwa eneo la Gaza na kuzuia chakula lakini nchi zote za kiislamu zimeshindwa kuzuia balaa hilo na hata kulaani kwa sauti ya juu.
Wakati huo huo Marekani inajitia huruma za mamba ikijifanya kujenga bandari ambayo irapeleleka chakula japo wana ratiba ya miezi miwili mbeleni .
Hatimae bandari hiyo itaondolewa kwenye kuwa ya muda na itapewa jukumu tofauti na hatimae kukamilisha malengo ya Israel ambaye ni mshirikia mkubwa wa Marekani na Uiengereza katika vita hivyo
Malengo mapana ya Israel kuimeza Gaza yote kama ilivyofanya kwa maeneo ya ukingo wa Magharibi yatakuwa yametimia.
Mataifa yaliyotarajiwa kuokoa janga hilo kwa vile hawajaweza kufanya muda huu mahitaji yake ni muda muafaka hawataweza kamwe kufanya jambo hilo baada ya kukamilika kwa malengo ya wapiganaji maadui wa Uislamu.
Kitakachobaki ni rehma za Allah subhanahu wa taala ambaye ana uwezo wa kubadili mwenyewe bila msaada wa yoyote muda huu kabla kufikia huko.