Kikwete ajisafisha Dowans

Kikwete ajisafisha Dowans

Mbona naona kama JK amekuwa kama kinyonga leo anasema anakubaliana alichosema Waziri Mkuu, na alichosema Chiligati na baadaye kamati mkuu. Mbona mimi naona kama matamshi yote hayafanani?, au sikumbuki vizuri, naomba mwenye kumbukumbu za matamshi yote atujuze.
 
Sijawahi kusikia RAIS anasema "sasa tunatafuta manouver ya kisheria ili tujue la kufanya"!!! Tanzania haikuwahi kuongozwa namna hii, kama duka la viatu. Mungu wetu, Mungu wetu, MBONA UMETUACHA??
kweli whoever sent you here, sent a reason home

umeiweka vyema zaidi
 
sijawahi kuona kiongozi mbovu kama huyu wa kwetu.ati rais mzima anawaambia wananchi yeye sio wingu ati angekuwa wingu angeenda kukaa pale juu mvua inyeshe.
aliomba kuwa rais wetu ili aje afanye nini?
ninavyojua ukiona mtu ana mpango wa dharura ujue na mpango wa muda mrefu nao anao sasa toka jk aingie madaraka miaka sita iliyopita serikali yake imekuwa na mipango ya dharura ya kutosha sasa atuambie mipango ya muda mrefu ni ipi sio anatujia na maneno ya kwenye kanga.
tumeshajua uwezo wake wa kufikiri ni mdogo na ushahidi ni hatuba zake anazotoa kila wakati zina kuwa na maoungufu mengi.
wananchi amkeni tuingie barabarani tukomboe nchi yetu mikononi mwa mafisadi.
 
<font color="#4169e1"><font size="4">Sijawahi kusikia RAIS anasema &quot;sasa tunatafuta manouver ya kisheria ili tujue la kufanya&quot;!!! Tanzania haikuwahi kuongozwa namna hii, kama duka la viatu. Mungu wetu, Mungu wetu, MBONA UMETUACHA?? </font></font>
<br />
<br />

Duka la viatu lina bei zinaeleweka jukumu la mnunuzi unachagua kulingana na kiasi chako cha pesa, la sivyo unaomba msaada ili upunguziwe bei kwa kila unachokipenda. Lakini hili, mmmmmmh! Yaani jambo limejadiliwa kwenye baraza ambalo mhusika ni m/kiti bado m/kiti anasema halielewi barabara.
Kama Rich monduli ni feki ilopita ktk baraza hilo, inakuwaje dowans inakuwa halali mpaka yatafutwe mazingira hayo yanayoombewa na mh? Nani alimtuma waziri wa nishati kutangazwa kulipwa kwa dowans hata kabla ya kesi kusajiliwa mahakama kuu Tz? Ni lini suala hili la malipo lilijadiliwa na baraza la mawaziri mara baada ya uchaguzi wa mwaka jana? Ni nini sasa tamko la serikali baada ya kujitafakari - je ndo kuomba kufanyike mazingaombwe ili tusilipe au..... Je, ni nani mmiliki wa TANESCO tunapoambiwa kuwa ikishindikana itabidi ilipe, fedha za TANESCO zinztoka wapi? Ni lini na ni nani aliiwakilisha TANESCO ktk hatua ya Richmonduli kuhamisha mkataba wake kwenda dowans?
Eeh Mungu unayeishi milele umesema amelaaniwa yule amtegemeaye mwanadamu na kumfanya mungu wake; nawe ni mwenye wivu sala zetu zikufikiye utuondolee mazonge ndani ya nchi hii.
 
Hakuna jipya. Kikwete hawezi kusema kwa watanzania eti mimi siwafahamu wamiliki wa Dowans (Wezi wa Rasilimali za nchi tuliyomkabidhi ailinde). Ni kukosa maneno ya kuzungumza. Ndio maana Dr Slaa anasema eti Rais wetu anatoa majibu mepesi sana katika maswali magumu na ya msingi. Anaongoza nchi kisanii, kweli kweli!!!!
 
nilisema jana huyu anatuzingua tu.........anavyoongea hata mtendaji kata wangu anamzidi......
 
Yaani kwa kweli Kikwete anasikitisha sana!
 
Hawezi kuwa msafi usafi wake utatokana na mosi kuwachukulia hatua marafiki zake ambao wamelihujumu taifa na kuliingiza katika mikataba ya mfukoni. Pili kuwafilisi wahusika kwa nguvu alizopewa kikatiba bila kutumia mahakama.
 
utadhani anaongea na watoto wadogo, kasema hawajui Dowans? wkati live Rostam ana power of attorney? shame
 
"Huyo ndio JK..ingekuwa mtu mwingine ni 'Habari (News)...wanaofikiri wanajua angesema nini..kasema sasa!:clap2:
 
Anatengeneza kijisababu ili akishindwa kutekeleza ahadi aje aseme hata Nyerere hakuweza kutatua matatizo yote ya watz. Kweli huyu mtu ni kilaza.
 
Mwakyembe kasema Dowans ni Rostam. Rostam alikuwa meneja wa kampeni za Kikwete 2005. TAKUKURU wakasema Richmond safi. Mbona huyo bosi wa TAKUKURU bado anapeta?
 
Nashangaa kusikia kuwa hili suala lilizungumziwa kwenye kamati kuu ya ccm hivyo maneno ya Pinda na Chiligati yalikuwa ndio msimamamo wa CCM!! Mambo yanayohusu Tanesco sio mambo ya chama bali ni ya serikali ,kwanini yakazungumziwe kwenye kamati kuu ya ccm badala ya kuzungumziwa kwenye baraza la mawaziri?
 
rais kasema baada ya kusikiliza ushauri mbalimbali wengine wakitaka tulipe,wengine tusilipe,wengine tusiharakishe... "uamuzi wangu ukawa tusiharakishe kulipa( please note hajasema tusilipe ...amesema tusiharakishe..).

Maswali yangu kwa kikwete:


1.chiligati alisema mmekubaliana kulipa dowans kwa kuwa ndio uungwana kuheshimu sheria na hicho kikao wewe ndio ulikuwa mwenyekiti na hatujasikia kuwa ulikana ile statement ya chiligati. Je sasa ile statement ya chiligati ni kweli au la?manake kama ulivyosema mwenyewe wewe ndio ulikuwa mwenyekiti wa hicho kikao na mlisema mtalipa ..


2.pinda alisema kuwa dowans italipwa kwa kuwa tumeshindwa kesi .nini maoni yako >? Manake umetuambia kuwa ulikuwa kimya kwa kuwa waziri mkuu kashaongea.


3.watu pekee ambao wamesema kuwa dowans isilipwe ni sita na mwakyembe .. Wewe umesema tusiharakishe kulipa hujasema tusilipe ila tusiharakishe wenzako wamesema wazi tusilipe.


4. Vipi kuhusu ngeleja .. Alisema tulipe ...vipi utamfukuza kazi?


5. Vipi kuhusu mwanasheria mkuu amesema tulipe wewe unasema tusiharakishe( nasisitiza hujasema tusilipe)..nae vipi utamfukuza kazi?


6. Aisee....




halsu waandidhi wa habari hasa television hivi hamuwezi kuandaa taarifa hivi kuonyesha mtililiko wote wa hii issue kwa ubunifu?kwa mfano mnaanza pale ngeleja aliposema tunalipa,kisha mnamuweka chiligati aliposema tunalipa,kisha pinda ..kisha mnamuweka pinda tena baada ya kikao cha wabunge...halfu mnamweka jk..kaclip kama cha dakika tano hivi kwenye taarifa ya habari ..kwani zile recordings si bado zipo?au mnaogopa ...



aisee....


yaani hapo ndipo nashindwa kuelewa, scoring points ziko kibao. Kwa kuweka wazi hizo clips ni kuvuta carpet kutoka miguu ya kikwete. Vipi waandishi tusaidieni jamani...!!!
 
Kikwete must leave..now
Enough is enough, asingojee yaliyotokea huko Afrika Kaskazini, maana ndiyo kitakachofuatia hapa Tanzania
 
Rais kakubali kuwa Richmond ni Briefcase company. Sasa Dowans nao vipi?? Rais anaweza kutueleza hiyo Dowans Costa Rica. Dowans Tanzaia blah blah imefanya kazi nchi gani nyingine?? Imewahi kuzalisha umeme nchi nyingine yeyote??

Hili suala ni very easy kama rais anhgekuwa serious. Rostam angeambiwa Dowans watalipwa sababu ya upuuzi wa ICC, lakini siku wanayolipwa na yeye anapelekwa mahakamani kwa kuhujumu uchumi kwenye issue mbalimbali ikianzia EPA, Import/Support a Tax evasion.

Oops by the way kesi za EPA zimeishia wapi??
 
Rais haongelei haongelei...sasa kaongelea, kuna jipya lolote?

Wote tulikuwa tunajua kuwa hawezi kuwa na jipya, hapa kinachodiskasiwa ni kaongeaje, si kaongea nini. Any way, he made people have something to pass time kabla vikao vya bunge havijaanza, ukizingatia kuwa this time baraza la mawaziri ni leak-proof.
 
Kesi gani ya EPA ?hamna case kuna kashifa ya epa ambayo imefunikwa na kashifa ya dowans by da time u stop toking about dowans ,epa will be a history and it was intended to be that way.
While you are there just put into your mind that you could go on whinning,complaining till Ramadan it is decided to pay dowans so go HUG A TREE and cry me a river.
Sorry it is the way it is this world is so fkdup
 
Back
Top Bottom