Kikwete ajisafisha Dowans

Kikwete ajisafisha Dowans

Sawa si kaongea yeye kama Kikwete, ningependa sasa kusikia msimamo wake kama Rais! kama raisi nae anaongea kama mpita njia sasa sisi wananchi wake tumueleweje? sijaona alichoongea zaidi ya kupoteza muda, sisi hatuhitaji ufafanuzi, tunahitaji decision, the way forward sio kutafuta public sympathy! aseme kama rais na sio mpayukaji!!!

Huu sasa ni umbumbumbu. Rais amekuwa wazi kwamba kwa upande mmoja kuna uamuzi uliwapa haki ICC na upande mwingine kuna kilio cha wengi kwamba deni hili halistahili kulipwa. lakini ili deni lisilipwe ni lazima kuwe na hoja makini za kisheria na hapa ndipo ulipokuja umuhimu wa kuunda jopo la wataalam ili kuona namna ya kukwepana na hili. Hiyo phobia yako kwa Rais ndiyo inayokufanya usielewe hata kilichozungumzwa. pengine hata hotuba hukuisikiliza kwa sababu ya chuki zako kwake! Usituletee chuki binafsi katika issue nyeti kama hizi. Ungekuwa wewe Rais ungefanya nini tofauti na hicho?
 
Amezungumza kama mwananchi wa mtaani lakini siyo kama Rais. Kwa sisi tuliosikiliza hotuba ile, ilikatisha tamaa maana ilidhihirisha kuwa hatuna kiongozi mkuu wa nchi ambaye anayweza kutoa jibu nchi inapokuwa katika utata. MIAKA HII 10 YA JK, KWA KWELI TUTAKUWA TUMEPOTEZA MUDA, MAANA HATUTAKUWA NA LA MAANA LA KUJIVUNIA KAMA TAIFA.
 
Mkubwa wa nchi hajui uhalali wa kampuni ambayo watendaji wake wanaipinga kutokuwa halali. Tutalipa tu kwa kuwa nguvu ya kulipa ni kubwa kuliko ile ya kutolipa. Haya ni hekaya za adili na nduguze...
 

Du sasa punguani wameanza, hivi ulitaka nani akakae Ikulu ataiondoa hali hii ya uchumi? Juzi mwenzako wameshikana mikono wakati wa siku ya Sheria, wanamtambua wwunasema hatuna Rais tena unatumia herufi ndogo wakati tumempa kura haya pasuka kama unauwezo weka mtu wako.
Afrika sasa hali ni mbaya kz mnataka mkaajiriwe bado vyuoni mkasomeshwe uzalendo wa JKT hamna unajiita haki kwanza basi andamana
km Tunisia au Misri hali ni ngumu acha matusi subiri 2015 simenti itakuwa sh. 5,000/=[/QUOTE

tunasomeswa??? tunajisomesha,hela ni kodi zetuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu!sio riziki nn
 
Amezungumza kama mwananchi wa mtaani lakini siyo kama Rais. Kwa sisi tuliosikiliza hotuba ile, ilikatisha tamaa maana ilidhihirisha kuwa hatuna kiongozi mkuu wa nchi ambaye anayweza kutoa jibu nchi inapokuwa katika utata. MIAKA HII 10 YA JK, KWA KWELI TUTAKUWA TUMEPOTEZA MUDA, MAANA HATUTAKUWA NA LA MAANA LA KUJIVUNIA KAMA TAIFA.

miaka kumi bila rais tz inawezekana
 
"Kafulila adai JK hawajui Dowans, Ngeleja anawajua

Kwa upande wa mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.

“Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,”alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.

Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.

“Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua,” alisema Kafulila na kuongeza:

Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?

Source: Mwananchi
 
'Hawajui wamiliki wa DOWANS' hii inaweza kuwa na maana nyingi tu, lakini mojawapo ni kuwa wale ambao yeye kikwete alikutana nao sio wale wanaotajwa na ngeleja, kwa maana hiyo ni wazi kuwa hawajui, lakini kwa sababu wale aliowai kukutana nao akiwemo swahiba wake RA basi kweli hawajui, tusimlazimishe kukubaliana na majina yanayotajwa na ngeleja.
 
Hii inaitwa "FUNIKA KOMBE MWANAHARAMU APITE" akudanganganyaye hakuchagulii uongo.
 
"Kafulila adai JK hawajui Dowans, Ngeleja anawajua

Kwa upande wa mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.

"Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,"alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.

Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.

"Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua," alisema Kafulila na kuongeza:

Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?

Source: Mwananchi


JK ameshindwa kazi....watanzania hawadanganyiki teena!

Hii akili ya uchambuzi ktk Gazeti la Mwananchi na Kafulila mwenyewe ni zaidi ya akili ya JK kuweza kutoa hata ufafanuzi kidogo kujisafisha mbele ya umma.

Kumbuka kuwa awali alipokuwa anaanza kuelezea ktk hotuba JK alisema....kuhusu suala la Dowans, naona niseme...." mimi siwajui Dowans, wala Wamiliki wake, na wala hawana haja ya kunifahamu au kunihusu ili niwafahamu...na wala sina uhusiano wowote nao, sina hisa nao na hawanihitaji niwafahamu...nk"
Jamani....hii ndiyo kauli ya 'Rais' ambaye Waziri aliyemteua yeye alisema kuwa ..."wamiliki wa kampuni ya Dowans SA, ni kama ifuatavyo....(akawataja Maruhani wake wote ambao hata JK alipelekewa copy, ila RA hakutajwa!) " ... njia ya mwongo siku zote ni fupi!

Kama JK hawajui, je Ngeleja anasubiri nini ofisini asijiuzulu kwa kubuni wamiliki, au hawajibiki kumpa taarifa JK??

Na ktk kuthibitisha kuwa JK anajikanyaga (kudhihirisha uongo, au usanii wake) kila anapoongea maneno mawili au matatu zaidi mbele ya umma, midomo ilikuwa inamkauka kila baada ya dakika, (ambayo ni tabia ya mtu anayesema au kutetea uongo), hivyo ilimbidi kunywa maji au kujilamba-lamba! Na ktk kudhihirisha kuwa alikuwa anachonga uongo, alifikia pahala akajisahau au kwa kutokujua kuwa 'anajifunua' ndipo akasema...."ngoja tukumbuke historia ya jambo hili.....(ndipo akaeleza kila kitu kuhusu kampuni feki ya mfukoni - Richmond, na jinsi ilivyokuja kuuza mkataba wake kwa Dowans', na haya aliyaeleza kwa mtiririko kuliko akina Pinda na Chiligati walivyojitahidi hapo awali)..., " Na hadi akaitetea Dowans kuwa "....baada ya kupokea mkataba toka Richmond, ndipo Dowans maana walikuwa na mtaji mkubwa, wakaingiza mitambo mikubwa-mikubwa, ambayo ndiyo iliyotusaidia kuondoa kiza na tatizo lililokuwepo...."

Hapo ndipo tukagundua kuwa...jamaa anayesema 'siijui Dowans hii' kama Petro alivyomkana Yesu, 'simjui mtu huyu' ili naye asisulubiwe!....ila hapa JK ni zaidi, anaikana DOWANS, kumbe sio tu asisulubiwe -ambayo ni haki kama kiongozi, bali pia anawaficha wananchi wasiujue ukweli maana yeye kama 'mkuu wa nchi' alitakiwa atoe dira na ufahamu na udhalimu unaofanywa kwa umma na kuwa hata kama ikitokea awepo 'tapeli' atafichuliwa na mkuu wa nchi, kumbe ni ZERO!. Tofauti yake ni kuwa, hata mkuu wa nchi ameshiriki kuuficha ukweli....Hatari sana!
SWALI: Je; Na hapo baadaye ikijulikana kuwa alikuwa anawafahamu ataruhusu afanyiwe nini?? kifungo au umma utaamuaje? (Au, Labda kasema hawajui maana anajua 'nyaraka nyeti zitakuwa zimesachomwa na hivyo hakuna wa kuzipatana kum-link na udhalimu huu!!!);

Ila nguvu ya umma itatawala ukweli tu...Mungu ndiye mtawala....! hata siku ya mwisho hata Mfalme Suleimani alianguka....sembuse JK! hatajiepusha na anguko kutokana na matendo yake mwenyewe, kama kuudanganya umma ndio mafanikio, basi anaelekea asipojua bado...uongo haudumu, utafichuliwa punde. Ndio maana tunasema, Kwa sasa mpira JK kautupa mwenyewe kati uwanjani....'umma wa wananchi' uamue mwelekee, kama ni upande upi...kama uelekee upande wa 'Timu ya Umma' kwa ushindi wa haki, ukweli na nguvu au kwa 'Timu ya JK' inayotetea udhalimu na uozo??
.................Watanzania hawadanganyiki tena ng'o!
 
Nimekua nikifutilia kila Jk akiwa anajibu kirahisi hoja nzito kama ya Dowans anafikia anasema hao wanaovalia njuga suala hilo na mengine kama hayo eti anawaomba wananchi wawapuuze.! Hv Jk hajajitambua bado, anafikiria huu upepo ni kama wa 2005. Nashukru alilitambua kuwa siku CCM inashindwa itakuwa ni ghafura mnoo..! Lakn pia alimwambia Dr kama hakupata leo atapata kesho. Peoplezzz! Power!. Kumbe eti wao ccm peoples power wanayo jaman jk?
 
Hata siku moja mwizi hawezi kukubali kuwa ni mwizi, JK hata aseme kwa lugha ya malaika hawezi kutughilibu sisi yeye ni mnufaika wa dowans, kwani huwezi kupiga mstari kati ya JK na RA. Kama kuna mtu wa kupuuzwa ni yeye kwani mipasho yake imezidi kumvua nguo kuwa kumbe hana hoja yeye ni mzee wa vijembe tu.Huyu ni wa kumpotezea tuu hana ishu
 
Wananchi tuliongea kwa sauti kubwa kwamba hatuko tayari kuona serikali inalipa deni la Dowans. Raisi ailikaa kimya. Watu takaanza kupaza sauti kwamba hana uwezo wa kutawala kwa kushindwa kutoa tamko lolote. Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali walitoa tamko linalofanana na la Waziri wa Madini na Nishati wakisisitiza umhimu wa serikali kuilipa Dowans. Wananchi tukapiga kelele na kusema deni likilipwa hapatatawalika. Kauli ya Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikaonekana sio kauli ya serikali. Tukazidi kumlaumu Raisi kwa kukaa kimya. Wengine tukafikia kusema kwamba Raisi hawezi kusema lolote maana ana maslahi binafsi katika sakata la Dowans. Ana hisa katika Dowans. Anawalinda marafiki zake.

Raisi baadae anaibuka katika kikao cha chama. Anaelezea historia ya sakata la Dowans. Anajisafisha kutohusika binafsi katika kashifa hiyo. Anauchukua ushauri wa watu wengi kwamba serikali isikurupuke kulipa. Anawataka wanasheria waangalie kama kuna mianya ya kisheria ya kutolipa deni. Wananch hao hao tunageuka na kusema hawezi kuongoza nchi. Angekaa kimya pia tungesema hawezi kuongoza nchi. Suala la IPTL lilitokea miaka kadhaa kabla huyo bwana hajawa Raisi. Mpaka sasa serikali inalipa mabilioni ya fedha kwaajili ya uzembe wa serikali. Hayo hayazungumzwi wala uwezo wa aliyekuwepo hauonekani. Naona kama tunamchanganya Raisi na Serikali badala ya kumsaidia sijua kwa maslahi ya nani?

Ni kweli suala la Dowans ni kashifa. Ni kashifa iliyogarimu baraza la mawaziri kuvunjwa kwa kuzingatia utafiti na ushauri uliotolewa na kamati ya Bunge. Haya ya kulipa au kutolipa fidia kwa Dowans ni matokeo ya tatizo lile lile la Dowans ambalo kisiasa lilimalizwa na kamati ya Mwakyembe kwa mapendekezo yaliyotolewa. Kisheria, ICC imeshatoa uamuzi. Raisi anawataka wataalamu waangalie kama kuna nafasi ya kuepuka kulipa au kupunguza kiwango cha fidia kisheria. Sisi bado tunarudi katika masuluhisho ya kisiasa. Kwa hali hii tatizo hili haliwezi kufikia ukomo ili serikali ikakaa na kufanya kazi zake.

Ni jambo la kuzingatia kwamba wakati uchaguzi mkuu wa 2010 unafanyika suala la Dowans lilishatokea na wabunge kufanya uamuzi wao. Vyama mbali mbali vya siasa vilitumia tatizo hilo kukipinga chama tawala na mheshimiwa Kikwete. Licha ya yote hayo wananchi walimchagua Kikwete na chama chake kuongoza nchi. Mimi nadhani tufikie wakati tuseme suala la Dowans limefikia ukomo wake. Kama kuna njia za kisheria za kutolipa deni zitumike na serikali imekubali. Kama hamna tukubali matokeo kama tulivyokubali katika sakata la IPTL. Tuweke mikakati ya kutoruhusu kashifa kama hizi baadae. Bahati nzuri mjadala wa katiba mpya uko mbele yetu na kama tukiutumia vizuri tunaweza kupata suluhisho la kudumu la matatizo kama haya.
 
Hiv kaka kweli hii Nchi inarais au kituko...unajua katika marais wote waliopita huyu tulienae sasa ajielewi na wala ajitambu,,sasa kama ww ndo rais wa nchi na mwenye zamani unawezaji kutamka maneno kama hayo mbele ya kadamnasi....yaani mpaka hapo inaonekana jamaa ana maamuzi yalio sahihi..na yupo tayali nchi iangamie ...daaaah inauma sana jombaaaaa


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amejisafisha kuwa si mmliki wala hawalindi marafiki zake katika sakata la DOWANS. Ameeleza kila kitu kuhusu mchakato wa Richmond hadi Dowans. Aisee naona sasa jamaa ameshutuka amefafanua mpaka basi, ameweka bayana Richmond ni kampuni ya mfukoni na kugusia maamuzi ya CC ya CCM.
Walioona taarifa hiyo jamani tuijadili kidogo.

Source TBC1 Time 02:19
 
Last edited by a moderator:
Wananchi tuliongea kwa sauti kubwa kwamba hatuko tayari kuona serikali inalipa deni la Dowans. Raisi ailikaa kimya. Watu takaanza kupaza sauti kwamba hana uwezo wa kutawala kwa kushindwa kutoa tamko lolote. Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali walitoa tamko linalofanana na la Waziri wa Madini na Nishati wakisisitiza umhimu wa serikali kuilipa Dowans. Wananchi tukapiga kelele na kusema deni likilipwa hapatatawalika. Kauli ya Waziri Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikaonekana sio kauli ya serikali. Tukazidi kumlaumu Raisi kwa kukaa kimya. Wengine tukafikia kusema kwamba Raisi hawezi kusema lolote maana ana maslahi binafsi katika sakata la Dowans. Ana hisa katika Dowans. Anawalinda marafiki zake.

Raisi baadae anaibuka katika kikao cha chama. Anaelezea historia ya sakata la Dowans. Anajisafisha kutohusika binafsi katika kashifa hiyo. Anauchukua ushauri wa watu wengi kwamba serikali isikurupuke kulipa. Anawataka wanasheria waangalie kama kuna mianya ya kisheria ya kutolipa deni. Wananch hao hao tunageuka na kusema hawezi kuongoza nchi. Angekaa kimya pia tungesema hawezi kuongoza nchi. Suala la IPTL lilitokea miaka kadhaa kabla huyo bwana hajawa Raisi. Mpaka sasa serikali inalipa mabilioni ya fedha kwaajili ya uzembe wa serikali. Hayo hayazungumzwi wala uwezo wa aliyekuwepo hauonekani. Naona kama tunamchanganya Raisi na Serikali badala ya kumsaidia sijua kwa maslahi ya nani?

Ni kweli suala la Dowans ni kashifa. Ni kashifa iliyogarimu baraza la mawaziri kuvunjwa kwa kuzingatia utafiti na ushauri uliotolewa na kamati ya Bunge. Haya ya kulipa au kutolipa fidia kwa Dowans ni matokeo ya tatizo lile lile la Dowans ambalo kisiasa lilimalizwa na kamati ya Mwakyembe kwa mapendekezo yaliyotolewa. Kisheria, ICC imeshatoa uamuzi. Raisi anawataka wataalamu waangalie kama kuna nafasi ya kuepuka kulipa au kupunguza kiwango cha fidia kisheria. Sisi bado tunarudi katika masuluhisho ya kisiasa. Kwa hali hii tatizo hili haliwezi kufikia ukomo ili serikali ikakaa na kufanya kazi zake.

Ni jambo la kuzingatia kwamba wakati uchaguzi mkuu wa 2010 unafanyika suala la Dowans lilishatokea na wabunge kufanya uamuzi wao. Vyama mbali mbali vya siasa vilitumia tatizo hilo kukipinga chama tawala na mheshimiwa Kikwete. Licha ya yote hayo wananchi walimchagua Kikwete na chama chake kuongoza nchi. Mimi nadhani tufikie wakati tuseme suala la Dowans limefikia ukomo wake. Kama kuna njia za kisheria za kutolipa deni zitumike na serikali imekubali. Kama hamna tukubali matokeo kama tulivyokubali katika sakata la IPTL. Tuweke mikakati ya kutoruhusu kashifa kama hizi baadae. Bahati nzuri mjadala wa katiba mpya uko mbele yetu na kama tukiutumia vizuri tunaweza kupata suluhisho la kudumu la matatizo kama haya.


Mwenzetu uko hapa kwa interest ya nani?? If I may ask Bro'........................???
 
Kama amekiri wazi kuwa Richmond/Dowans kampuni hewa, sasa basi Rostam Aziz, mbunge wake aliyehusika kuisimamia Kampuni hii feki kuchukua tenda, anamfanyaje???????????? Atueleze bayana hapo.

Hili nalo neno!
 
Kwa wale wanaodhani hawana Rais watafute nchi nyingine ya kwenda kuishi.

Hawa ni wale wenye kushabikia uongo na waongo.

Watanzania tuna akili ya kuelewa mambo na tunaona.

Nyuma ya hao kuna Kanisa.
 
Kwa wale wanaodhani hawana Rais watafute nchi nyingine ya kwenda kuishi.

Hawa ni wale wenye kushabikia uongo na waongo.

Watanzania tuna akili ya kuelewa mambo na tunaona.

Nyuma ya hao kuna Kanisa.

Tunabanana hapa hapa Yeye ndiyo atatoka atuachie nchi yetu.Hanan hadhi ya kuwa Rais aliwahadaa watanzania
 
Hivi, siku zote hizo Bwana Kikwete alikuwa anasubiri tar 5 Feb kuwaeleza Watz uhusiano wake na dowans. Sasa kama Rais mwenyewe hajui wamiliki, sasa nani ajue? Wale wa Ngeleja walitoka wapi? I don't think tuna rais imara. Hivi baraza la mawaziri halikukaa wakati wa Richmond? Nani mwenyekiti wake?? Yeye alikuwa wapi?
 
Sijaona wala kusikika Rais mvivu wa kufikiri kama huyu

La, ni lazima anahusika tu. Yote majizi haya ambayo kama Ben Ali wa Tunisia na Mubarak wa Misri walifikiri mapinduzi ya wananchi ni ndoto za Alinacha. Hii ni dunia nyingine, ngoja mapinduzi ya vijana na waliowengi, na hela wanazokazania kuiba wataziona chungu na zitarudi tu hata wakizificha Jersey.
 
Back
Top Bottom