Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

hizi ni hoja za kuleta chokochoko miongoni mwa watu. hamna maana hata kidogo. ongeza sababu nyingine 510 ziwe 561 hoja yako itapata nguvu kutokana na maamuzi ya watanzania siyo wahuni wa blog hii.
uhuru usio na mipaka ni vurugu. Rais wa zamani wa marekani siyo Klinton wala MABUSH aliwahi kusema DON'T ASK WHAT US WILL DO TO YOU; ASK WHAT WILL YOU DO TO US!
badala ya kuangalia kwa darubini kali nini Kikwete aliahidi na hajafany jiulize umefanya nini.....
am sorry kuita blog ya wahuni ..... sina jina jingine kuipa nadhani hili lafaa na siachi membership ng'oooooooooo

Tunajua kuwa huwezi kuacha membership kwa sababu WEWE ni mhuni........... Ndo nyie kina Tambwe Hizza
 
Kuna aliyesema kwamba wapiga kura wa vijijini hawajui upinzani, na ndiyo wanaoipa CCM ushindi. Hajui alisemalo. Tangu siasa za vyama vingi zimeanza, asilimia kubwa ya madiwani na wabunge wametoka vijijini na wala siyo mijini. Mjini ni usanii mtupu, maneno mengi lakini vitendo hakuna.

Hata uchaguzi wa majuzi tu wa serikali za mitaa unaonyesha hali halisi ya vijijini vs mijini. Kwa hiyo ni dharau kubwa kudai kwamba wananchi wa vijijini ni mambumbu.


Hili ni kweli ndio maana mkakati wa kushinda mjini ndio unahitajika zaidi. Inaonekana ni Tanzania tu ambako Mjini hawajaamka na vijijini ndio wameamka zaidi.
 
Mzee Mwanakijiji, kwanza nimefurahi kutuweka wazi kuhusu 'chama chenu'. Taratibu za chama chenu kutoa malalamiko unazijua, wewe kama mwanachama mtiifu, kwanini unamvua nguo Mwenyekiti wako wa Chama na rais wako kulikopelekea kumuacha utupu na hivyo kupata matukano, kubezwa, kuchekwa na hata kudhihakiwa hivi?.

Kwanini unafikiri mawazoni mwangu Rais wetu na Mwenyekiti wetu ni "mfalme"!? Nimeamua kuvunja mwiko.

Mimi kama practical in a real sense, hizi sababu zote ni wastage of time na furahisha genge, wewe Mzee Mwanakijiji unajua wazi tena bila mashaka wala mawaa Kuwa 2010 ni JK.

Hili si kweli; ni mawazo ya kukata tamaa na kuacha fate iamue. JK hana guarantee ya Urais 2010 isipokuwa kwa watu ambao wameshakubali kushindwa. I'm not one of them.
Nilifikiri tuko timu moja ya uhamasishaji kuiamsha jamii ya Watanzania kuondokana na fikra za chama dola, kwa kumtafuta mgombea atakayaweza kukwaana na JK, kumbe sasa ni kujaribu kusafisha mumo kwa mumo kuwa 2010 asiwe JK lakini bado ni CCM.

Inategemea hizo timu nyingine zinataka nini.

Niliwahi kusema mahali kuwa CCM itatawala milele, wakati huo hata sijajua Mzee Mwanakijiji nawe ni CCM, nilikuona as a source of inspiration of changes we can belive in, kumbe ni mule mule!.

sasa ulifikiri CCM itatawala milele bila kuwa na watu wa kutawala?

Haya baada ya wabunge wenu kuvuana nguo kwenye kamati ya Mwinyi kule Dodoma, sasa ni zamu ya wanachama watiifu wa CCM, kuwavua nguo viongozi wenu na mwisho mtamalizia kwa kuvuana nguo wenyewe kwa wenyewe.

Yote ni sehemu ya mapambano yale yale. Ni bora mtu mmoja kuangamia kuliko taifa zima kuangamia.

Kwa maoni yangu, CCM is a gone case, kwa upinzani huu legelege tulionao, bado ni CCM tuu itaendelea kutuswaga mpaka watu wenye uelewa na uono wa type ya Mwanakijiji, watakapokubali to have a look outside the box.

We looked outside the box, and it sucks bigtime!

Ile mada ya wapiganaji ndani ya CCM wanapigania nini, inaniacha na swali Mwanakijiji ndani ya CCM ana maslahi gani zaidi ya kumvua nguo mwenyekiti wake na kumuacha uchi mtupu kabisa?.

well.. bado najiuliza wanapigania nini. NI lazima tupate kitu cha msingi cha kupigania.
 
Ukiangalia trend ya utawala uliopo madarakani kwa sasa ni dhahili kwamba kikwete asingeruhusiwa kugombea tena kwa sabau ahadi zote alizo ahidi kashindwa kutekeleza hata moja.

Kwanza mimi namuuliza mh. rais kikwete hivi anaweza kusimama mbele ya umma leo na kusema "kasi mpya, nguvu mpya na ari mpya??" na je, kwa nini hiyo slogan haitamkiki leo?? kuna nini??
 
Alisema ili Mtera ijae, pamoja na Kihansi inahitajika Elnino 3, lakini in just one normal rain season mabwawa yalijaa, na mtera ilibidi ifurishwe kidogo.
 
Alisema uchaguzi umekwisha na yeye ni rais wa watanzania wote, lakini tunachokishuhudia yeye ni rais wa mafisadi na washkaji zake
 
Ameamua kuendelea kuwa waziri wa mambo ya nje badala ya kuwa Rais na kutumia muda mwingi nje ya nchi huku nyumbani mambo yakienda kwa kusuasua.
 
Mkuu Mwanakijiji, sababu za JK kutogombea ni nyingi lakini moja tu ndio yenye uzito mkubwa nayo ni""

1) Kushindwa kuongoza nchi kwa faida ya wananchi wa TZ. Kwa maneno mengine ni kushindwa kuboresha maisha ya watanzania, huku akiachia makampuni ya nje yakimaliza madini yetu yenye thamani kubwa mno kwenye soko la dunia na sisi kuambulia NOTHING, na mwisho kuruhusu wizi mkubwa wa mali za umma unaofanywa na kikundi kilichomweka madarakani hence complicity yake.

kifupi ... kushindwa kuilinda na kuitetea katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kama alivyoapa .... kwa ku-create a heaven of the untouchables ....

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anakula viapo vitatu:

Kiapo cha kwanza ni cha utii, ambapo anaapa kuwa atakuwa mwaminifu kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wake wote, na kwamba ataihifadhi, kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

Kiapo cha pili ni cha Rais, ambapo anaapa kwamba atatenda kazi zake za Urais kwa uaminifu na kutimiza wajibu wa kazi hizo kwa bidii na moyo mkunjufu, na kwamba atawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Sheria, mila na desturi za Tanzania bila woga, upendeleo, huba wala chuki.

Na Kiapo cha tatu na cha mwisho alacho rais ni cha kudumisha Muungano, ambapo anaapa kwamba ataitetea na kudumisha umoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

source: www.bongotz.com
 
40. Pamoja na kwamba amepewa ushaidi wa kutosha kuwa kuna wakubwa wana degree feki lakini amekuwa mugumu kuwaambia angalau wasitumie hivyo vyeti ndani ya serikali.

Hivyo tunaongozwa na watu wenye vyeti feki na kufanya watanzania wote waone kuwa si lazima kufanya vitu kihalali hila kifeki feki.
 
Hivi yale mabilioni "ya Kikwete" yalitoka wapi, na yamerudisha kiasi gani kwenye mtaji? Yaweza kuwemo katika hizi sababu..
hivi hao mabilioni yalitoka wapi? katika bajeti ipi.

kama alikuwa na mahela mengi hivyo (binafsi) ashauriwe kupumzika ili kutenganisha uongozi na biashara. kama si ya kwake na yametoka hazina inabidi tuangalie uadilifu wake pia kwani isije ikawa ni epa nyingine.
 
39. amepewa majina ya wauza unga na majambazi tangu mwaka wa kwanza madarakani lakini hakuna jipya zaidi ya kuongezeka kwa uhalifu na biashara ya unga nchini....
 
5. Ameteua wabunge wenye elimu za utata (vilaza) na mafisadi kuwa mawaziri wa wizara nyeti nchini - Mkullo, Malima, Nchimbi na wengineo
 
40. Hana Presidential Confidence, so anabakigi kujikanyaga tu siku zote akipigwa maswali magumu
 
mtoto wa kikwere kazi unayo...mi aliniacha hoi alipokuwa ana quantify ajira zilizoongezeka kwa kuwauliza wabunge eti wale ulioajiri nyumbani kwako vijana wa ng'ombe ,house girld ndo ajira zenyewe hizo...hahaaaaa Mr.prezident kazi unayo usipotoa majibu nakini watu watakulima karate kama PM wa Italy
 
Personally sioni lawama kwa JK ni sahihi waliomchagua ndio walaumiwe yaani sijaona raisi msanii kama JK.
Yaani he is never serious alafu hawa wapambe wake akina makamba wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa mwambieni ukweli aachie ngazi next year ataheshimika.
Ila watz walivyo wa ajabu utashngaa next year anapita kwa kishindo bila kupinga.
Big up mwanakijiji kwa kuspare mda wako kumuanalyse uyu mwenzetu though mimi naona ndo uwezo wake JK ulipofikia alistep down itakuwa vyema though to Afrikan leaders ni ngumu.
 
39. Pamoja na kupewa picha ya hali katika uchimbaji wa madini ambapo watanzania wamekuwa wakiangaika na kemikali zitokazo katika Machimbo ya migodi, Amekuwa kimya na hakuweza kuchukua hatua yoyote kitendo ambacho wananchi wameendelea kuteseka na kuteswa na sumu hivyo kusababisha hata vifo vyao. Mfano mara.

38. Wananchi wa kimasai wamehamishwa kutoka katika makazi yao kwa nguvu kwa masilahi ya wawekezaji (majangili) na pia wamefikia wakati wa kuitwa kuwa ni waamiaji kutoka Kenya huku yeye kama kiongozi wan chi aliyeteuliwa kuwalinda akiwatelekeza na kusababisha matatizo makubwa kwa watanzania.
 
Back
Top Bottom