Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

37. Anapenda kusafiri safiri sana huku akikimbia matatizo lukuki ya wantanzania aliowachagua bila kuyatafutika ufumbuzi wa kudumu.
 
psssssssss....DON'T DISTURB PLEASE, PRESIDENT YUPO KWENYE BEMBEA NA WIFE, ANABEMBEA JAMAICA!!!!!!!!!!!!
hahaahha
hahahaha
 
anajuwa kama yeye ni mgonjwa na kutokana na ugonjwa wake hapaswi kuwa kwenye madaraka yoyote (labda ujumbe wa shina), lakini yeye anangangania tu.
 
Kwanza nawataka radhi wadau wa JF kwa kuchelewa kutoa maoni yangu. Hat hivyo, pia napenda kumpongeza mwanakijiji kwa kufafanua kwa ufasaha kabisa sifa zinazoonyesha mapungufu ya Kikwete kushiriki uchaguzi mkuu ujao kama mgombea kwa kiti cha Urais.

Sifa kubwa inayoonyesha Kikwete kutofaa kuwa mgombea wa Urais uchaguzi wa mwakani ni "KUKOSA DIRA YA KULIONGOZA TAIFA". Hayo yote aliyoyataja Mkjj yamemezwa ndani ya hili lililoandikwa kwa maandishi makubwa. Mfano, utamuona anapoenda nje ya nchi (Kikwete), hotuba zake kwanza ni ndefu pasipo sababu maana zinaongelea upuuzi tu. Haziongelei kile Watanzania wanachokihitaji ili kujinasua na umasikini ambao ni takribani miaka 50 sasa imekaribia tangu Uhuru. Juzi nilikuwa nachangia hoja moja nikatolea hotuba zake za Cuba na Italia alizozitoa mwaka huu! Hakika ni kutuaibisha sisi anaotuwakilisha kutosema vitu ambavyo Tanzania inavihitaji vifanyike ili watu wake waendelee kiuchumi, kijamii na kisiasa. Vyote vinavyosemwa havina dira kabisa. Ni kule kujaribu kutatua tatizo kumbe hujui tatizo lenyewe ni nini na badala yake unaishia tu kukata majani na kuacha mizizi ikinawilisha mti kama kawaida.

Tunahitaji mtu anayefahamu matatizo ya nchi yetu ili hata akiwa anasikiliza ushauri wa kitaalamu naye aweze kupima kama ushauri husika unafaa au haufai kulingana na matatizo menyewe. Wewe utaona wapi kusema mataifa waje kuwekeza nchini wakati nchi iko gizani? Wawekeze, je bidhaa zao zitanunuliwa na akina nani wakati watanzania waliowengi wanaishi chini ya dolla maja kwa siku?

Kwa Kikwete kuwa na matatizo haya yote, ndiyo maana sasa hivi hata mfumko wa bei umefikia 18%, hebu linganisha na kipindi kabla hajaingia! Hivyo, mfumko wa bei kuwa juu, maana yake ni kwamba watanzania waliowengi sasa wameathirika zaidi na kipato chao duni maana uwezo wa kununua sasa umekwenda chini zaidi kwa kipato kilekile cha awali. Hajui hilo, kwamba ni tatizo! Inabidi tupate mtu mbadala, sasa ili kufanikiwa katika hili ni Kumuomba MUNGU kwa nguvu zetu zote zilizobaki kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
 
39. Ameshindwa kuilinda na kuitetea Katiba ya nchi: Uongozi wa sheria, ubadilishaji wa siasa ya nchi kutoka ujamaa hadi ubepari
38. Amedidimiza utawala bora. Kila kiongozi amekuwa mropokaji. Hakuna uwajibikaji
37. Ongezeko la umasikini linakuwa siku hadi siku kwa kukosekana mikakati ya kukuza uchumi na ushirikishwaji wa wananchi katika maendeleo ya nchi
36. Serikali yake imeshindwa kusimamia mfumuko wa bei
35. Amesimamia chama chake kutaka/kukusudia kupora mamlaka na uhuru wa Bunge
 
Amekuwa akíishi kwa namna ambayo anawaambia wananchi,fuateni maneno yangu usiangalie matendo yangu. Badala ya kuishi kwa mifano ya kimatendo.
Vipi ataweza kumkanya mamamkwe Sofia Simba.......ama....
 
Amelidhalilisha taifa letu kwa kuomba omba misaada isiyo na maana kutoka nchi za nje wakati nchi yetu ina rasilimali nyingi ambazo zingeweza kukidhi mahitaji yetu kama kungekuwa na uongozi makini.

Aliahidi kwamba angeboresha utoaji huduma wa ATCL, lakini mpaka sasa hakuna lolote la maana linalotendeka kuliwezesha shirika hilo litoe huduma kwani hata hao Wachina wanaotegemewa kuja kuwekeza wameingia mitini!!
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna watu wanajaribu kuwafanya wengine wajisikie vibaya wanapotoa mawazo yao kuwa Rais Kikwete afikirie adhma yake ya kugombea ngwe ya pili. Wanajaribu kuwafanya watu wajisikie kama wasaliti au waonevu wanapotoa mawazo kuwa Taifa letu linahitaji uongozi mpya kabisa mwakani na siyo wa Rais Kikwete. Ukweli ni kuwa watu wengi wanampenda Kikwete kama mtu binafsi; ana sura nzuri, sauti nzuri, tabasamu n.k n.k lakini linapokuja suala la uongozi wapo wanaoona kuwa ana mapungufu makubwa mno kiasi kwamba kumpa nafasi nyingine mwakani ni kuendeleza kile ambacho tayari kimeshaonekana miaka hii minne.

Tunapoelekea mwaka huu mpya ambao ni mwaka wa uchaguzi kambi za "kikwete agombee" na "Kikwete asigombee" zitazidi kuibuka na kwa mara ya kwanza tutashuhudia mgongano wa wazi kati ya kambi hizi. Tatizo kubwa ni la wale ambao wanaamini kuwa kutaka Rais aliyemadarakani asigombee tena ni sawa na uhaini na kumtaka afikirie kutokugombea ni sawa na kumsaliti.

Hii si kweli. Rais wa Tanzania anachaguliwa kwa kipindi kimoja tu na akitaka nafasi nyingine basi anapitia mchakato ule ule na hawezi kutawala kwa vipindi zaidi ya viwili. Katiba haisemi kuwa vipindi hivyo viwili ni lazima viwe vimefuatana. Kutokana na ukweli huu ni lazima watu wakubali kuwa utawala wa demokrasia una gharama yake na gharama mojawapo kubwa ni wananchi kuweza kumkataa kiongozi wao na hata kutaka asigombee!

Lakini wazo hili ni gumu kwa watu ambao wanaongozwa na ushabiki wa mtu; watu ambao wanaona kuwa Kikwete ame"fika" hapo kwenye Urais na mtu yeyote anayetoa mawazo kuwa asigombee au hana sababu ya kutosha kugombea tena basi ni kama mhaini; tumewasikia watu wazima na ambao ni wanasiasa wakongwe wakianza kutukuza huu ubia wa Bw. Kikwete na Urais wa Tanzania.

Wanataka kumfanya Kikwete kuwa ni mfalme na kuwa yeyote atakayejitokeza kupingana naye basi ni msaliti wa aina fulani au mhaini. Haya ni mawazo potofu. Kama watu hawa wanataka Kikwete agombee milele na kuwa hakuna mtu mwingine yeyote mwenye uwezo kumzidi basi wajitokeze hadharani na wabadili Katiba ili wamtangaze Kikwete kuwa ni Rais wa Maisha na sisi wengine tutakaa kimya (kwenye njozi zao).

Mwaka 2005 kinyume na inavyosemwa Kikwete hakupitia kwenye tanuru ya moto; hakuwa na rekodi ya kusimamia lakini safari hii bila ya shaka tunayo rekodi yake ya kutosha na tunaweza kumpima kwa kile alichokifanya kama Rais. Na ni kipimo hicho tu ndicho ambacho kitatuamulia kama ana sababu ya kugombea tena au tutafute mtu mwingine.

Safari hii Kikwete kama anataka kuwa Rais wetu tena itabidi ajibithibitishe kwa kufanya midahalo na wagombea wengine, kusimamia rekodi yake na kujibu hoja zitakazotolewa dhidi yake. Safari hii Urais hauji kwa kuuza jina, sura, au tabasamu; safari urais utakuja kwa kuustahili.

Na wana CCM ambao wanaona Rais Kikwete hawezi kuwa chaguo lao wasijisikie vibaya wala kujiona kama wanasaliti chama; watambue kuwa wana wito mkubwa zaidi na sababu kubwa zaidi na kama wanaona kuwa Bw. Kikwete anahatarisha hata maslahi ya Chama basi ni jukumu lao kutokumpendekeza na yeye kama Mkapa atakaa pembeni na kula pensheni yake na kuendelea kufurahia ving'ora na saluti za hapa na pale. Kama Gen. Powell aliweza kumuunga mkono Obama wakati yeye ni Republican na mtu aliyefanya kazi na marais wa Republican kama Reagan, Bush na GW Bush basi mwana CCM yeyote anaweza naye kumpendekeza mtu mwingine zaidi ya Kikwete.

Kwa upande wetu tutaendelea Jumatano hii kwenye gazeti la Mwanahalisi na fungu la pili la sababu 51 za kwanini Rais Kikwete asigombee. Ni matarajio yetu kuendelea kuwakera watu wachache na kuwaudhi wengi.
 
tatizo ni kwamba tunaweza KUTAKA ASIGOMBEE!.....tukaishia KUTAKA.Hapo ndipo huu mchezo huwa nauona mgumu
 
MMM,

Kutaka Kikwete asigombee si ni KINYUME cha "UTARATIBU" wetu CCM? Au?
 
Hata kidogo; utaratibu wa kumpata mgombea wa CCM utafanyika kama vile ni mara ya kwanza; mwana CCM yoyote ambaye anaamini ana uwezo wa kuliongoza Taifa letu atajitokeza na kuchukua fomu na kufuata mchakato ule ule. Hadi hivi sasa JK inaonekana ameshapigiwa debe na viongozi wetu; lakini miezi michache ijayo atapata upinzani wa kihistoria na mwamko huo utakapoiva atakuja na sababu ya kwanini asigombee kama nilivyodokeza karibu miezi kadhaa iliyopita.

Tunamshukuru kwa utumishi wake lakini naamini hatokuwa na kinyongo pale ambapo mtu mwingine atapitishwa badala yake.
 
Hata kidogo; utaratibu wa kumpata mgombea wa CCM utafanyika kama vile ni mara ya kwanza; mwana CCM yoyote ambaye anaamini ana uwezo wa kuliongoza Taifa letu atajitokeza na kuchukua fomu na kufuata mchakato ule ule. Hadi hivi sasa JK inaonekana ameshapigiwa debe na viongozi wetu; lakini miezi michache ijayo atapata upinzani wa kihistoria na mwamko huo utakapoiva atakuja na sababu ya kwanini asigombee kama nilivyodokeza karibu miezi kadhaa iliyopita.

Tunamshukuru kwa utumishi wake lakini naamini hatokuwa na kinyongo pale ambapo mtu mwingine atapitishwa badala yake.

Wenye Chama mnatuletea mtu safi - another 'Mr. Clean'?
 
Hata kidogo; utaratibu wa kumpata mgombea wa CCM utafanyika kama vile ni mara ya kwanza; mwana CCM yoyote ambaye anaamini ana uwezo wa kuliongoza Taifa letu atajitokeza na kuchukua fomu na kufuata mchakato ule ule.......

Nakubaliana na wewe hapo nilipo-BOLD; Lakini ndiyo maana nimetumia neno "UTARATIBU" wetu CCM.

Kwa maana tumekuwa tukitumia huo "UTARATIBU" tangia Mwinyi, Mkapa,... ni lazima tuendelee hivyo hivyo regardless of competence ya the incumbent...

On a serious note: Kama CCM ingefuata mchakato sahihi wa kumpata mgombea kiti cha URAISA, Jakaya Kikwete ASINGEKUWA Rais wa Jamuhuri ya Muungano leo - kubali kataa. Na ndiyo maana RAIA or Mwana-CCM anayepaza sauti kuwa "JK asigombee tena" 2010 anaonekana msaliti - ANASALITI "UTARATIBU" - ambao wamekuwa wakiutumia.
 
Hivi Urais wa Tanzania unatolewa kwa kutazamana usoni?

Je katiba ya CCM inalazimisha mwanachama wa CCM aliye kwenye madaraka ya Urais katika kipindi cha kwanza KUUNGWA MKONO kugombea kipindi cha pili bila kupingwa???

Je ni dhambi kwa Kikwete kuongoza kipindi kimoja kisha akapumzika??

Binafsi naamini tunahitaji Rais mpya come 2010 (si lazima atoke upinzani), naamini aliyepo madarakani hajaweza kufikia walau 15% ya matarajio yetu. Vipaumbele vyake na wasaidizi wake vinakwenda kinyume na kauli mbiu yake ya Maisha bora kwa kila Mtanzania.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Tunamshukuru kwa utumishi wake lakini naamini hatokuwa na kinyongo pale ambapo mtu mwingine atapitishwa badala yake.

JK keshajiwekea vizuri mizizi ya kutotingishwa. Chunguza vizuri hasa wale wanaopiga kura kwenye CCM Halmashauri Kuu na Kamati kuu, hapo ndo mchezo wa kumpitisha Rais unachezwa, vinginevyo hupiti hata kama unapendwa na wananchi. Labda kupata upinza kutokea vyama vingine lakini ndani ya CCM kuna mizizi yake aliyoipanda hasa kamati Kuu kama (Chenge, RA, EL, SS n.k).
 
Tatizo la viongozi wetu wanafikiri kiongozi (post yeyote0 lazima awe na hela kushinda anaowaongoza.Ndio maana leo hii kila mwanacccm anajiona anaweza so long as amekaa kwenye system muda mrefu.
Tabia ya kulindana kwa maslahi binafsi nayo ni shida nyingine kweli mtu mpaka anakuwa doctor feki ina maan kweli system haijui??????.....shem on them.........
 
Na ndio maana Kikwete hataki kuwatosa akina EL,RA,mzee wa vijisenti,mzee wa konteina hao ndio karata yake kwani kwenye CC ya CCM ndio walioshika mpini na hao ndio watakaompitisha,kwani angewatosa ndio waliokuwa na uwezo kumbomoa,kwa kuwakumbatia Kikwete anahakika ya kuingia kipindi cha pili,TANZANIA HATUCHAGUI RAISI BALI TUNACHAGULIWA RAISI
 
Back
Top Bottom