Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

Amemzidi vasco da-gama na Chritopher columba kwa kukazungukia haka kasayari ketu.
 
hata hazihitajiki kufika hamsini, watu ni kufikiri kitu kidogo tu..toka 2005 mpaka leo kuna nini mtanzania anaweza akasema kafaidika au kaona impact ya utawala huu?.tumeona Obama kaja tu juzi unaona kaanza kuweka health care reforms na mambo mengine mengi. Kwa JK hakuna jipya nchi ipoipo tu.....

Labda JK aweke health care reform program ya afya yake kwanza maana amedondoka mara 3, mara apimwe akili...!
 
afya yake haieleweki na ina mgogoro, alianguka jukwaani na daktari wake aka funika funika ukweli akasingizia uchovu,,,rais ambaye afya yake ina question marks hafai kugombea tena...
 
mnhhhhhhhh...hivi inawezekana kuwa kweli enheeee???...huyu jamaa mie hata sijui haki ya mungu amefanya nini....na muda ndio huooo unayoyoma anakuja tena kuomba KULA zetu....duuuuhhh

kwani hana hata washkaji zake wanao-visit home of great thinkers ..wakatusaidie kumuuliza kuwa wadau wanauliza UMEFANYA NINI JAPO KIMOJA TUUU....ili tumpatie kula zetu arudi tena 2010.
 
all in all tuone inawezaje hii kampeni ikatoka nje ya jamvi ili iwakute majority..

Mungu aliwapa wanaisraeli sauli kwa sababu waling'ang'ania. lakini baadae aliwahurumia akamleta DAUDI- anaetamkwa 'rafiki wa Mungu'.

by faith we can stop this gentleman next year....
 
Haya mambo muulize Nkapa! JK anajitahidi kurekebisha uozo wake..sasa contract iliyofanyika kisheria huwezi kuzivunja bila kufuata taratibu za kisheria...labda kama unataka awe dicteta...na huo si ushauri mzuri ndio hajishughulishi na watu kama nyinyi

Usisahau kwamba JK aliwahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Fedha,..., kwa hiyo Mkataba ya Madini sio migeni kwake!
 
Anawajua waalifu wa madawa ya kulevya kwa sura na sehemu wanazokaa. Alishasema hayo kuwa ana majina yao. Lakini mpaka sasa hivi amewaacha waendelee kuharibu vijana wa kitanzania. Hii ni kinyume na katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
 
Usisahau kwamba JK aliwahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Fedha,..., kwa hiyo Mkataba ya Madini sio migeni kwake!

Nkapa gani bana? We hujui Richmond ni zigo la awamu yanne Pia TRL? Toto ya nyoka nae nyoka bana!!
 
Tunaweza kurudi nyuma tukawakumbuka wale wanaosema hii ni serikali ya kishkaji. Kwa sababu urais ni taasisi sio mtu mmoja, na rais ana wasaidizi wake. Cha ajabu ina maana anapoahidi kitu hakuna ufuatiliaji na ndio maana ahadi ni nyingi na utekelezaji zero. Point ya ushkaji inakuja pale ambapo kazi hazifanyiki, ahadi ya raisi hazitekelezwi hata kwa vitu vinavyo wezekana kabisa yote hii ni sababu y ushkaji ndani ya utawala. Vinginevyo angetimua wote wanaoendeleza ushkaji kazini, lakini kwa kuwa ni wanamtandao ina kuwa hakuna noma.
 
40: Yeye pamoja na CCM wamewafanya watz wasiaminike tena. Hata sisi kwa sisi. Majibu ya waziri hayana baraka za Mbunge? tena wa chama kimoja?
 
ni kweli!ila ni vizuri ukbainisha nawewe sera zako tukuchague wewe.au tumchague nani?
 
Ni coward.
Hana ubavu wa kufanya maamuzi magumu kwa maslahi ya Taifa lake.
Obama aliweka wazi juzi: Hakuna sababu ya mtu kuomba urais kama ni coward.
 
Baada ya kutafakari sana, nimepata sababu 51 za kwanini Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama chetu Cha Mapinduzi aamue kutoshiriki kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu mwakani. Ninajua kwamba ni "mtaji" kwa upande wa kina Makamba na vile vile ana "sura nzuri" na bla bla bla..

Sasa kati ya hizo 51 nitaanza na zile mbili za mwisho yaani ya 50 na 51. Bila ya shaka na wewe unaweza kuwa na za kwako.. hivyo nawakaribisha wale ambao wanaweza kukisikia au kuchangia sababu zile nyingine 49!


51: Alisema kuwa akichaguliwa tena ataleta vijana na kuwa watu wa rika "lake" waanze kuachia ngazi. Well, kwa vile yuko rika moja nao basi na yeye aungane nao!

50: Hajui kwanini Tanzania ni maskini licha ya kuwa kwenye utumishi wa serikali kwa karibu miaka 30 sasa! Kiongozi asiyejua chanzo cha tatizo ataweza vipi kuliondoa isipokuwa kuziba tu dalili zake.

49: Aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania. Ahadi hii haionekani kutekelezeka. Inaonekana ametimiza ahadi ya maisha bora kwa kila muwekezaji wa kigeni!

48:Alitangaza kuwa wizi umefanyika Benki Kuu kwa kukombwa mabilioni; badala ya kuacha uchunguzi wa jinai akaunda Kamati kuchunguza jinai. Matokeo yake ni kucheleweshwa kwa upatikanaji wa haki.

47: Serikali yake imeshindwa kutekeleza maazimio yote ya wananchi wa Tanzania kama yalivyoanishwa na wawakilishi wao Bungeni katika maazimio kufuatia Kamati Teule ya Kuchunguza Richmond. Matokeo yake ni kuchochea mgawanyiko mkubwa kabisa wa kimaslahi katika historia ya taifa letu.

46: Aliahidi kupitia mikataba yote mikubwa ya madini ili kutengeneza hali ya "win win win". Hadi hivi sasa hakuna mkataba hata mmoja uliopitiwa na kusahihishwa na badala yake serikali yake imetangaza kuwa mabadiliko ya sheria ya madini yataendelea kuwanufaisha wawekezaji wa sekta hiyo.

45: Akiwa ni Mwenyekiti wa Chama Tawala ameshindwa kuleta nidhamu ndani ya chama na matokeo yake wanachama wake mashuhuru wanatukanana na kuitana majina hadharani. Kile kilichoitofautisha CCM miaka ya nyuma sasa hakipo tena.

44: Aligawa fedha za walipa kodi wa Tanzania kwa kile kilichojulikana kama "mabilioni ya Kikwete" Hadi hivi sasa haijaoneshwa ni kiasi fedha hizo zimeweza kubadilisha maisha ya waliozipata na kurudisha faida.

43: Aliahidi kuunda Baraza dogo la Mawaziri lakini matokeo yake Baraza lake limekuwa kubwa na lenye ufanisi mdogo.

42:

Labda umzuie asigombee kupitia chama chako mwenyewe, lakini kwa CCM, ni sawa na kupoteza muda bure kujadili kupitishwa ama kutopitishwa kwake kugombea urais. Na haya mawazo yanaonyesha jinsi gani hii nchi itaendelea kuwa chini ya CCM kwa miaka mingi ijayo, maana kama ni kiongozi bora anaweza toka upinzani pia, lakini inavyoonyesha walio wengi wameshakata tamaa na upinzani na tegemeo limebaki kwa CCM tu.

Kuna aliyesema kwamba wapiga kura wa vijijini hawajui upinzani, na ndiyo wanaoipa CCM ushindi. Hajui alisemalo. Tangu siasa za vyama vingi zimeanza, asilimia kubwa ya madiwani na wabunge wametoka vijijini na wala siyo mijini. Mjini ni usanii mtupu, maneno mengi lakini vitendo hakuna.

Hata uchaguzi wa majuzi tu wa serikali za mitaa unaonyesha hali halisi ya vijijini vs mijini. Kwa hiyo ni dharau kubwa kudai kwamba wananchi wa vijijini ni mambumbu.
 
Jakaya aliahidi kuwa hakuna mwanafunzi anayestahili kupewa elimu ya juu atakayenyimwa sponsorship ya serikali lakini tumeshuhudia watoto wa watanzania maskini wanaosoma vyuo vya juu wakimyimwa ufadhili wa serikali; licha ya wale waliorudishwa toka Ukraine!!!

Sababu nyingine ambayo inamdisqualify Jakaya asigombee ni kutoipenda nchi yake na watu wake; angekuwa anawapenda watanzania angehakikisha kwanza kabisa mafisadi wote wanaouathiri uchumi wetu wanashuhurikiwa ipasavyo na sio kiusanii; pia angepunguza matumizi ya ofisi yake hasa mabilioni ya mapesa anayotumia yeye na wapambe wake kwa kusafiri nje ya nchi. Utafiti umeonyesha kuwa safari zake nyingi za nje hazina tija wala mpamgilio na ndio maana alijikuta yuko Cuba bila watanzania kujua kuwa rais wao alikuwa na ziara kule!!
 
Aliwatahadharisha watendaji/washkaji zake kwamba wasimwangushe kwenye mkataba wa richmondi kwa kuleta kampuni lisilo na uwezo. Matokeo yake pamoja na angalizo la rais wasaidizi wake walimpuuza na kuendeleza njaa zao kwa kuingia mkataba na kampuni sii tu isiyo na uwezo bali hewa
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama chetu Cha Mapinduzi.
[/SIZE][/FONT][/B]
Mzee Mwanakijiji, kwanza nimefurahi kutuweka wazi kuhusu 'chama chenu'. Taratibu za chama chenu kutoa malalamiko unazijua, wewe kama mwanachama mtiifu, kwanini unamvua nguo Mwenyekiti wako wa Chama na rais wako kulikopelekea kumuacha utupu na hivyo kupata matukano, kubezwa, kuchekwa na hata kudhihakiwa hivi?.

Mimi kama practical in a real sense, hizi sababu zote ni wastage of time na furahisha genge, wewe Mzee Mwanakijiji unajua wazi tena bila mashaka wala mawaa
Kuwa 2010 ni JK.

Nilifikiri tuko timu moja ya uhamasishaji kuiamsha jamii ya Watanzania kuondokana na fikra za chama dola, kwa kumtafuta mgombea atakayaweza kukwaana na JK, kumbe sasa ni kujaribu kusafisha mumo kwa mumo kuwa 2010 asiwe JK lakini bado ni CCM.

Niliwahi kusema mahali kuwa CCM itatawala milele, wakati huo hata sijajua Mzee Mwanakijiji nawe ni CCM, nilikuona as a source of inspiration of changes we can belive in, kumbe ni mule mule!.

Haya baada ya wabunge wenu kuvuana nguo kwenye kamati ya Mwinyi kule Dodoma, sasa ni zamu ya wanachama watiifu wa CCM, kuwavua nguo viongozi wenu na mwisho mtamalizia kwa kuvuana nguo wenyewe kwa wenyewe.

Kwa maoni yangu, CCM is a gone case, kwa upinzani huu legelege tulionao, bado ni CCM tuu itaendelea kutuswaga mpaka watu wenye uelewa na uono wa type ya Mwanakijiji, watakapokubali to have a look outside the box.

Ile mada ya wapiganaji ndani ya CCM wanapigania nini, inaniacha na swali Mwanakijiji ndani ya CCM ana maslahi gani zaidi ya kumvua nguo mwenyekiti wake na kumuacha uchi mtupu kabisa?.
 
Kwa maoni yangu, CCM is a gone case, kwa upinzani huu legelege tulionao, bado ni CCM tuu itaendelea kutuswaga mpaka watu wenye uelewa na uono wa type ya Mwanakijiji, watakapokubali to have a look outside the box.

Jamani tuseme kwamba CCM hatuiwezi kuifukuza madarakani, tusilete visingizio.Hivi ni ulegelege gani huo ambao upinzani unao ambao CCM hawana?

Okay, kama wapinzani ni legelege, vipi makundi mengine? Walio wanachama wa vyama vya siasa Tanzania hawazidi milioni 6, kati ya wapiga kura milioni zaidi ya 18, vipi makundi mengine yanafanya nini, au na yenyewe ni legelege? Kote huko ambapo vyama tawala viling'olewa havikung'olewa na vyama vya upinzani pekee. In fact vyama vya upinzani viltumika kama tu'vehicles'; waliongoza mapamabano (Kenya, Zambia, Malawi, etc) walikuwa ni vyama vya kiraia, mashirika ya dini, wafanyakazi, wanafunzi, wasomi na vyama vyao vya kitaaluma, n.k. Kwetu vipi haya makundi yanafanya nini?

Sisi tumebaki kulaumu vyama vya upinzania kama vile ndivyo vyenye jukumu pekee la kuleta ukombozi katika nchi hii.

Hapa tulipofikia, anybody can be better than CCM. Hawa jamaa wameperform at the lowest level you can imagine. Sasa kama tunaona hawa bado ni bora kuliko mtu mwingine, then inabidi tukiri kwamba sisi kama nchi tupo hoi kabisa kiuwezo. then we need to shut up!

But I don't believe so; Tuache woga, CCM inang'oleka, play your part!
 
Baada ya kutafakari sana, nimepata sababu 51 za kwanini Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama chetu Cha Mapinduzi aamue kutoshiriki kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu mwakani. Ninajua kwamba ni "mtaji" kwa upande wa kina Makamba na vile vile ana "sura nzuri" na bla bla bla..

Sasa kati ya hizo 51 nitaanza na zile mbili za mwisho yaani ya 50 na 51. Bila ya shaka na wewe unaweza kuwa na za kwako.. hivyo nawakaribisha wale ambao wanaweza kukisikia au kuchangia sababu zile nyingine 49!


51: Alisema kuwa akichaguliwa tena ataleta vijana na kuwa watu wa rika "lake" waanze kuachia ngazi. Well, kwa vile yuko rika moja nao basi na yeye aungane nao

50: Hajui kwanini Tanzania ni maskini licha ya kuwa kwenye utumishi wa serikali kwa karibu miaka 30 sasa! Kiongozi asiyejua chanzo cha tatizo ataweza vipi kuliondoa isipokuwa kuziba tu dalili zake.

49: Aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania. Ahadi hii haionekani kutekelezeka. Inaonekana ametimiza ahadi ya maisha bora kwa kila muwekezaji wa kigeni!

48:Alitangaza kuwa wizi umefanyika Benki Kuu kwa kukombwa mabilioni; badala ya kuacha uchunguzi wa jinai akaunda Kamati kuchunguza jinai. Matokeo yake ni kucheleweshwa kwa upatikanaji wa haki.

47: Serikali yake imeshindwa kutekeleza maazimio yote ya wananchi wa Tanzania kama yalivyoanishwa na wawakilishi wao Bungeni katika maazimio kufuatia Kamati Teule ya Kuchunguza Richmond. Matokeo yake ni kuchochea mgawanyiko mkubwa kabisa wa kimaslahi katika historia ya taifa letu.

46: Aliahidi kupitia mikataba yote mikubwa ya madini ili kutengeneza hali ya "win win win". Hadi hivi sasa hakuna mkataba hata mmoja uliopitiwa na kusahihishwa na badala yake serikali yake imetangaza kuwa mabadiliko ya sheria ya madini yataendelea kuwanufaisha wawekezaji wa sekta hiyo.

45: Akiwa ni Mwenyekiti wa Chama Tawala ameshindwa kuleta nidhamu ndani ya chama na matokeo yake wanachama wake mashuhuru wanatukanana na kuitana majina hadharani. Kile kilichoitofautisha CCM miaka ya nyuma sasa hakipo tena.

44: Aligawa fedha za walipa kodi wa Tanzania kwa kile kilichojulikana kama "mabilioni ya Kikwete" Hadi hivi sasa haijaoneshwa ni kiasi fedha hizo zimeweza kubadilisha maisha ya waliozipata na kurudisha faida.

43: Aliahidi kuunda Baraza dogo la Mawaziri lakini matokeo yake Baraza lake limekuwa kubwa na lenye ufanisi mdogo.


42: Aliahidi kuwa mgao wa umeme utakuwa historia lakini hadi sasa yeye ndo amekuwa historia akiacha mgao UNATAMALAKI kwa jinsi unavyotaka.................
 
Jamani tuseme kwamba CCM hatuiwezi kuifukuza madarakani, tusilete visingizio.Hivi ni ulegelege gani huo ambao upinzani unao ambao CCM hawana?

Okay, kama wapinzani ni legelege, vipi makundi mengine? Walio wanachama wa vyama vya siasa Tanzania hawazidi milioni 6, kati ya wapiga kura milioni zaidi ya 18, vipi makundi mengine yanafanya nini, au na yenyewe ni legelege? Kote huko ambapo vyama tawala viling'olewa havikung'olewa na vyama vya upinzani pekee. In fact vyama vya upinzani viltumika kama tu'vehicles'; waliongoza mapamabano (Kenya, Zambia, Malawi, etc) walikuwa ni vyama vya kiraia, mashirika ya dini, wafanyakazi, wanafunzi, wasomi na vyama vyao vya kitaaluma, n.k. Kwetu vipi haya makundi yanafanya nini?

Sisi tumebaki kulaumu vyama vya upinzania kama vile ndivyo vyenye jukumu pekee la kuleta ukombozi katika nchi hii.

Hapa tulipofikia, anybody can be better than CCM. Hawa jamaa wameperform at the lowest level you can imagine. Sasa kama tunaona hawa bado ni bora kuliko mtu mwingine, then inabidi tukiri kwamba sisi kama nchi tupo hoi kabisa kiuwezo. then we need to shut up!

But I don't believe so; Tuache woga, CCM inang'oleka, play your part!
Kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, haki ya raia kushiriki politics haipo, imemezwa na sheria kwamba lazima upitie kwenye chama cha siasa.

CCM ndio chama tawala, mategemeo ya mabadiliko ni kwenye upinzani, kumbe hata wanaharakati makini kama Mwakijiji ni CCM, ndio maana nikamuomba aangalie outside the box to join forces Tanzania ikombolewe, vinginevyo tutatawaliwa milele!.
 
Back
Top Bottom