Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

Mkapa aliacha fedha nyingi alivyotoka madarakani, na yeye JK alikiri hivyo, nakumbuka katika speech yake ya bunge kama sijakosea.

Hebu fafanua Mkapa aliacha pesa nyingi kivipi ikiwa miaka yote tuna budget deficit na ingawa aliongeza makusanyo ya kodi lakini asilimia kubwa ya pesa hizo ziliishia kulipa madeni na nyingine ndizo hizo zilizochotwa miezi michache kabla ya Mkapa kumaliza muda wake kupitia ufisadi wa Kagoda shilingi bilioni 40, Meremeta shilingi bilioni 155 na ununuzi wa ndege ya Rais ambayo nayo ilinunuliwa akiwa amebakisha miezi mitatu Ikulu na magari na helicopters za jeshi yaliyonunuliwa kupitia yule wakala fisadi Vithlani.

Hebu tufafanule kuhusu hizi pesa nyingi alizoziacha Mkapa ili na wengine tuelewe unamaamisha nini unaposema "Mkapa aliacha pesa nyingi na JK alikiri hivyo"
 
Huyo mmoja mhh!
1.Je, Kunayo succession plan for this? au ni kubahatisha tu halafu tuje tulalamike tena?
2.Tunadanganyika ni vitu ambavyo havina mchango mkubwa kwenye results mwisho wa siku.
3. Hata aje malaika kutawala.... itachukua miaka zaidi ya 200 kabla ya kuona mabadiliko ya kweli.
4.Tatizo liko kwenye mind-set na siyo vingine.Mindsets za viongozi na waongozi...kote ni problem.

J, Majirani zetu Wanyarwanda waliuana na idadi ya waliouwawa kufikia karibu 900,000 miaka 15 tu iliyopita na sasa hivi chini ya Kagame nchi hiyo inafanya vizuri sana katika nyanja mbali mbali ikiwemo uchumi. Hivyo sikubaliani na kauli kwamba hata kama Watanzania tukipata malaika itachukua miaka 200 kuona mabadiliko ya kweli.

Kwa maoni yangu ni miaka 5 tu inatosha kabisa kuona mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu kama vile kuwa na madarasa ya shule za msingi yenye hadhi ya kuitwa madarasa pamoja na madawati na vitabu vya kutosheleza watoto wote wenye umri wa kwenda shule, kuwa na hospitali zenye vifaa vya kileo na madawa na vitanda katika hospitali zetu na kuondoa adha iliyomtoa machozi mlimbwende Naomi Campbell baada ya kuona chumba kinachostahili kukaa mama wajawazito wanne kina wajawazito zaidi ya 20 na wengi wao wakishare kitanda kimoja wakati mwingine hadi 7 kushare kitanda kimoja kitu ambacho hakiingii akilini kabisa.


Na mengi mengineyo, kama vile kuhakikisha tunafaidika na rasilimali zetu kama madini badala ya kusaini mikataba ya kupata 3% tu, yanayoweza kufanywa katika miaka mitano tu na Watanzania tukaanza kupiga makofi na vigelegegele kwa nguvu zetu zote kutokana na mabadiliko ya kuridhisha na ya kutia moyo sana.
 
Hadi hii leo ameshindwa kuyaweka hadharani majina ya mafisadi wa EPA "Waliorudisha shilingi 70 billioni" na kiasi kilichorudishwa na kila mmoja wa mafisadi hao.

Aligawa kama pipi "Mabilioni ya Kikwete" bila kuwa na ufuatiliaji wowote. Akiulizwa leo "Mabilioni ya Kikwete" yamefanya shughuli gani ili kuinua viwango vya maisha ya Watanzania atashikwa na kigugumizi. Miezi michache iliyopita alisikia akisema kwamba mabank wamrudishie "mabilioni yake" 😕 bahati mbaya mafisadi walishayachangamkia siku nyingi sana.
 
Utake Usitake JK atagombea 2010 na bila ubishi ndiye Rais wetu mpaka 2015.Haya mengine ni kama gumzo la kitaa...

Hii ni kweli kabisa - kwa wadanganyika ninaowafahamu, CCM hata ikimsimamisha Kiwete atapita tuu, sembuse JK. Hata hivyo aliahidi hatakuwa na ubia kwenye serikali yake, lakini sasa wabia yaonekana wamemzunguka na wamempiku - moja wapo, Makamba, amekuwa msemaji wa serikali na wakati huo huo anabakia balozi wa Mafisadi. Aliahidi serikali ndogo lakini hivi sasa idadi ya mawaziri wake karibu inaingia kwenye guiness book of records. Aliitisha orodha ya wauza unga na matokeo yake wamekuwa washikaji wake wakuu na vijana huko Zenj wanazidi kuathirika kwa kilevi. Aliingia kwa gear ya ari, nguvu na kasi mpya lakini sasa twashuhudia uchovu, unyonge na uwoga kwa kiwango cha kutisha - si ajabu mara azimie, mara abebwe na mara apimwe akili. Jamani hapana na imetosha asigombee tena asilani.
 
Hii ni kweli kabisa - kwa wadanganyika ninaowafahamu, CCM hata ikimsimamisha Kiwete atapita tuu, sembuse JK. Hata hivyo aliahidi hatakuwa na ubia kwenye serikali yake, lakini sasa wabia yaonekana wamemzunguka na wamempiku - moja wapo, Makamba, amekuwa msemaji wa serikali na wakati huo huo anabakia balozi wa Mafisadi. Aliahidi serikali ndogo lakini hivi sasa idadi ya mawaziri wake karibu inaingia kwenye guiness book of records. Aliitisha orodha ya wauza unga na matokeo yake wamekuwa washikaji wake wakuu na vijana huko Zenj wanazidi kuathirika kwa kilevi. Aliingia kwa gear ya ari, nguvu na kasi mpya lakini sasa twashuhudia uchovu, unyonge na uwoga kwa kiwango cha kutisha - si ajabu mara azimie, mara abebwe na mara apimwe akili. Jamani hapana na imetosha asigombee tena asilani.
Mkuu,ni kweli ulikuwa unataka kumaanisha 'kiwete' in your post.Naona kama haijakaa vizuri.Is it?
 
Sababu nyingine ni kwamba JK si kiongozi, hajawahi kuwa kiongozi na nadhani hajui kuwa kiongozi maana yake nini
 
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, AKIFUNGUA RASMI BUNGE JIPYA LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA, 30 DESEMBA 2005

Nanukuu...

Mheshimiwa Spika:
Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2005 imetamka bayana majukumu mawili ya msingi ya Serikali ya Awamu ya Nne:.

· Kwanza, kuitoa Tanzania kutoka kwenye dimbwi la uchumi ulio nyuma na tegemezi na kuiingiza katika mkondo wa uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea.

· Pili, kuwashirikisha wananchi wote kwa njia ya uwezeshaji katika ujenzi wa uchumi na kuutokomeza umaskini.

Mheshimiwa Spika:
Kwa kuzingatia majukumu haya ya msingi, na mbinu na mikakati mbalimbali ya kuyatekeleza, Watanzania watarajie mambo kumi yafuatayo katika miaka mitano ijayo:

· Kwanza, Serikali ya Awamu ya Nne itahakikisha kuwa Amani, Utulivu na Umoja wa nchi yetu na watu wake vinadumishwa;

My opinion: hakuna Utulivu wala Umoja kitaifa

· Pili, Serikali ya Awamu ya Nne itadumisha na kuendeleza mafanikio yaliyopatikana tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza hadi leo;

My opinion: hakuna kilichodumishwa

· Tatu, Serikali ya Awamu ya Nne itaendeleza vita dhidi ya umaskini, ujinga na maradhi, tena kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya;

My opinion: Tena hapa ndio amefeli kabisa

· Nne, Serikali ya Awamu ya Nne itatimiza ipasavyo wajibu wake wa utawala na maendeleo, na itaendesha dola kwa misingi ya utawala bora na uwajibikaji; utawala wa sheria unaoheshimu na kulinda haki za binadamu; itaendeleza mapambano dhidi ya rushwa bila ya woga wala kuoneana muhali.

My opinion: hivi kweli alikua anajua anachokisema..???

· Tano, Serikali ya Awamu ya Nne itaimarisha uwezo wake wa kulinda maisha na mali za raia wake. Tutapambana na uhalifu wa kila aina, na majambazi hayataachwa yatambe yatakavyo;

My opinion: hapa kachemsha vibaya sana

· Sita, Serikali ya Awamu ya Nne itahakikisha mipaka ya nchi yetu ipo salama. Hatutamruhusu mtu au nchi yeyote kuchezea mipaka ya nchi yetu na uhuru wetu;

My opinion: hivi suala la silaha zinazopita bila serikali kujua na bado mipaka yetu ipo salama??? kafeli tena hapa

· Saba, Serikali ya Awamu ya Nne itafanya kila iwezalo kuhakikisha Tanzania ina mahusiano mazuri na mataifa yote duniani, pamoja na mashirika ya kimataifa na kikanda;

My opinion: Pengine hili kalifanikisha kwa gharama kubwa sana,lakini vipi hii ripoti ya silaha haiwezi kutuweka kwenye nafasi mbaya ya kimahusiano na majirani zetu? nampa nusu maksi

· Nane, Serikali ya Awamu ya Nne itajali sana maslahi na mahitaji ya makundi maalum katika jamii kama vile wanawake, vijana, watoto, wazee, walemavu na yatima;

My opinion: Kashindwa kuwalinda maalbino na vikongwe

· Tisa, Serikali ya Awamu ya Nne itaongoza mapambano mapya ya kuhifadhi mazingira ili vizazi vijavyo virithi nchi nzuri, na msingi imara wa maendeleo endelevu;

My opinion: Jitihada haziridhishi...!

· Kumi, Serikali ya Awamu ya Nne itaendeleza michezo, na shughuli za utamaduni na burudani.

My opinion: Kwenye burudani sioni! utamaduni ndio unazidi kupotea! michezo hakuna kitu, watetezi wake watazungumzia soka! soka sio mchezo pekee!

Mwisho wa kunukuu.
 
Nitarudi badae kufafanua maoni yangu kwa kirefu...! Na kwenye sababu 51 iliyokuu inayotufanya tusimchague tena ni baada ya kuikana ilani ya uchaguzi tuliyomchagua kwayo! kwa kifupi tuliuziwa mbuzi kwenye gunia..!
 
Lets try to be a little bit more specific kuliko kuwa general..


JK NI MBABAISHAJI AND IS ALWAYS DREAMING.

He just don't know what it takes to accomplish a thing. He can not form a winning team and I believe he's not a team player. He is just a populist leader na above all he has lack of memory. Can not link past, present and the foreseeable future.
 
JK NI MBABAISHAJI AND IS ALWAYS DREAMING.

He just don't know what it takes to accomplish a thing. He can not form a winning team and I believe he's not a team player. He is just a populist leader na above all he has lack of memory. Can not link past, present and the foreseeable future.

this is an indictment!
 
(......)yupo tayari kuiingiza nchi kwenye matatizo/vita kwa kufagilia udini ,kuruhusu kodi za watz kujadili udini na kunyamazia udini kwa maslahi ya dini fulani WAKATI KATIBA YA NCHI IKO WAZI NAE ALIAPA KUITETEA NA KUILINDA.
 
(.....)WA KULAUMIWA KATIKA YOTE NI SISI WATZ kwa kuangalia zaidi sura kuliko uwezo wa mtu
 
Nitarudi badae kufafanua maoni yangu kwa kirefu...! Na kwenye sababu 51 iliyokuu inayotufanya tusimchague tena ni baada ya kuikana ilani ya uchaguzi tuliyomchagua kwayo! kwa kifupi tuliuziwa mbuzi kwenye gunia..!
hapa mdau umenikuna......................MBUZI KWENYE GUNIA!!!!!!!!!!!!!!!!!!TENA GUNIA LA UKWELI
 
Ni rais ambaye yuko rahisi sana alafu ni mwongo sana...........alisema anawajua kwa majina vigogo wanaojihusisha na madawa ya kulevya....mpaka sasa kimya
alisema anawajua kwa majina vigogo wanaokwepa kulipakodi....mpaka sasa kimya...........
 
kwa akili za Watanzania atapita tu mwakani-2010
 
Anakimbia matatizo ya msingi kwenye nchi na kwenda nje kwa ajili ya kupumzika na maneno ya Watanzania
 
Back
Top Bottom