Kikwete afanye nini Kuuokoa Urais wake?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Kwa kadiri mambo yanavyokwenda na kwa kadiri siku zinavyokwenda ndivyo mzigo wa Matumaini ambao Rais Kikwete alichutuma kuubeba ndivyo unavyozidi kuwa mzito na unaozidi kumuelemea.

Kwa mtu yeyote ambaye anafuatilia hali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi bila ya shata atatambua kuwa Rais Kikwete hawezi kuwa mwenye furaha. Bila ya shaka manung'uniko yanamkera na zaidi ya yote yale yanayoendelea kwenye Chama "chake". Mgongano wa mawazo unaoendelea kwenye vyombo vya habari, masuala ya mikataba ambayo watu walifikiria yameisha na Mkapa, siyo tu vimetia doa bali vimepaka rangi mbaya kabisa kwenye utawala wake.

Kikwete sasa hivi hana jinsi bali kucheza "pata potea". Anao uamuzi wa kuendelea na timu ile ile ya watu 60, na kutarajia mabadiliko kwa kutumia makaripio na barua za maonyo na uelekezaji, au anaweza kubadili mwelekeo wa utawala wake. Vyovyote vile atakavyofanya, Rais Kikwete anakabiliwa na mtihani mkubwa kabisa wa utawala wake hadi sasa.

Je, atakuwa ni Rais ambaye atashuhudia kumeguka kwa CCM? Je atakuwa ni Rais ambaye ameshindwa kuwadhibiti watu aliowateua na kusababisha kambi siyo kwenye chama tu bali pia kwenye utendaji?

Ana uchaguzi wa kuona ni jinsi gani anaweza kuokoa Urais wake, CCM na hatimaye yeye mwenyewe kutoka katika historia ambayo imeanza kuandikwa?

Afanye nini Rais Kikwete ili auokoe Urais wake, aiimarishe CCM, na zaidi ya yote aweze kutimiza ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania?

Fuatilia sababu 51 za kwanini Kikwete asigombee tena 2010 hapa
 
Maana nina uhakika kuwa walio karibu yake (kama kawaida yao) hawamuambii ukweli isipokuwa kuendelea kumsifia kuwa watu wanampenda, alichaguliwa kwa asilimia 80, na kuwa yeye ni mtu wa watu. Sidhani kama wanamuacha aone ubovu au uchafu. Hata kama akitaka kutafuta ukweli inabidi awauliwe wale wale waliotibua isipokuwa kwa vile yeye amewaamini basi watu hao watasema kweli. Hata hivyo, bila ya shaka kama tungepewa nafasi ya kumpa maoni nje ya wale wanaomsaidia au wenye maslahi ya kisiasa, Rais Kikwete afanye nini basi hata kama atakuwa ni Rais wa Mhula mmoja , kuweza kujenga tena imani ya watu?
 
Blame it on 'mtandao' ....maslahi, halisi... sijui kwa kweli. Ila the situation is somewhat a kinfolk of inbred right now. Within that circle- everywhere you touch is condemned, everthing they do is disgraced.

SteveD.
 
Ampe uhuru Hosea wa PCCB afuatilie tuhuma nzito dhidi ya Mkapa kuhusiana na kashfa mbali mbali. Kama kuna ushahidi wa kutosha basi sheria ifuate mkondo bila kusita wala woga. Aufute mkataba kati ya Owners wa Kiwira Coal Mining (Mkapa na Yona) na TANESCO wenye thamani ya shilingi bilioni 340. BOT pia lazima ichunguzwe kwa kina na mapana katika upotevu wa $250 milioni na ujenzi wa Twin Towers ambao umegharimu pesa nyingi mno kuliko ilivyotegemewa.

Apangue baraza la mawaziri na kuwaweka nje ya baraza hilo akina Karamagi, Meghji, Msolla, Kingunge, Mramba, Magufuli, Maghembe na yeyote yule ambaye utendaji wake umekuwa ni wa kulegalega. Akifanya haya atarudisha imani ya wananchi kwake na pia kurudisha credibility yake nchi za nje na jumuiya za mataifa.

Ndani ya CCM ajaribu kurudisha umoja ndani ya chama hicho. Hili ni gumu sana maana makundi yaliyojitokeza wakati wa kinyang'anyiro cha 2005 bado yameshamiri, anaweza kufanya hivyo kama katika baraza lake jipya atawapa uwaziri wale walio nje ya mtandao pia.

Akishindwa kufanya haya, basi hata wana mtandao hawatakuwa na imani naye hapo 2010. Ana kazi kubwa, lakini kama yuko makini anaweza kuifanya.
 
Jambo la kwanza kabisa analotakiwa kufanya ni kumuondoa EL, then kudismantle mtandao
 
...i care less about CCM a.k.a mtandao na hayo ni mambo yao...NATAKA APIGANE NA RUSHWA,AKUSANYE KODI YOTE NA AMWAGE PESA KWENYE ELIMU NA INFRASTRUCURE NITAANZA KUMWAMINI
 
mwanakijiji inawezekana kabisa yeye jk mwenyewe wala wasi hana KESHO BAADA YA MECHI NA MSUMBIJI TUKISHINDA ,..UWANJA WOTE UTARINDIMA ..JK..JK,...JK,...JK...BOOOOOYS!!!!! HAPO NA MAGAZETI YA MUTAANDAAWO YATABADILI MWELEKEO WA KASHFA HIZI..NA JK KUJEUKA SHUJAA ANGALAO KWA MIEZI KADHAA...KAMA TUKIFUNGWA JK ATAKUWA NA SABABU YA KUWA NAUCHUNGU KULIKO SISI WOOOTE!!!! MUNGU IBARIKI TANZANIA!!
 
Launch the country's biggest crackdown on corruption and declare a rule of law. Strip Mkapa's immunity in order to be prosecuted of corruption practices and theft of public funds. Fire Lowassa and Karamagi, then prosecute them of stealing our national resources. Fire the least effective 30 ministers, replicate policies that prove effective, give people the material and guidance to better their lives.
 
Afanye ibada sana na inshallah mwenye Mungu atamjalia nguvu za kuweza kutambua nani ni msaada kwake na nani ni mzigo kwake kati ya wasaidizi/mawaziri wake.
 
If few things can be changed then probably JK will save the country. First, reducing the government consumption(JK Gorv is too big), get some junks ministers off his cabinet, let Balali go, control corruption, cut the inflation down( this is real killing Tanzania), create new jobs not through loaning people money random.
Leave central bank alone, no invisible hands. Reduce taxes to wazawa companies for the conditions that they have to higher certain number of Tanzanian
Last find some real economy consultants, not 28 years old kid who graduated in international relation.
 
Ouuch!!

Kama kuna Rais ambaye aliwajaza wanachi matumaini ni Rais Kikwete. Leo hiii ndani ya mwaka mmoja tumesikioa watu waliiojiua kwa kushindwa na maisha (hali ngumu, na mmoka kwa kushindwa kuwapeleka watoto wake shule). Leo gharama ya maisha imepanda kiasi cha kwamba bei za vitu zinaonekana kuongezeka mara mbili huku mfumuko wa bei ukikaribia tarakimu mbili (sitashangaa mwezi Augusti tulikuwa kwenye Asilimia 10). Ndani ya CCM wameanza kukorogana wenyewe kwa kutuhumiana rushwa kitu ambacho licha ya kudaiwa huko nyuma kilikuwemo kwenye chama hicho viongozi wake wamekuwa wakikikana kwa nguvu mno na kudai "CCM safi". Wapinzani nao wamepata nguvu kiasi cha kusababisha Rais kugomewa na wananchi, Waziri Mkuu kugomewa na wafanyabiashara (hadi anawapigia simu kuwaomba michango!) n.k Nini kinaendelea? Je, Rais Kikwete analo la kufanya la kuweza kuiokoa CCM na hatimaye kuiokoa serikali yake?

Nimeeleza kwa kirefu na mawazo yangu yanakubaliana sana na watu wengi humu. Tumaini la JK ni Taifa Stars Jumamosi.. aombee siyo tu ishinde bali Senegal ishindwe ili TAifa STars isonge mbele!! Vinginevyo.. jumatatu.. itakuwa ngumu kweli. Labda jambo moja analoweza kufanya ni kukaa ofisini, hivi kwanini yeye na WAziri wake mkuu wote wanakata mbuga.. haiwezekani kupokezana? au Shein ndiyo Rais hasa?
 
Launch the country’s biggest crackdown on corruption and declare a rule of law. Strip Mkapa’s immunity in order to be prosecuted of corruption practices and theft of public funds. Fire Lowassa and Karamagi, then prosecute them of stealing our national resources. Fire the least effective 30 ministers, replicate policies that prove effective, give people the material and guidance to better their lives.

DEVIL YOU ARE RIGHT ..BUT PLEASE I BEG YOU TO DIFFER ON THIS...
we will not get any where with witch hunting....wanasema " mwarabu mbaya kiatu chake ni dawa!!!"....AFTER NYERERE ...mkapa is THE BEST PRESIDENT we have have had...pamoja na mabaya yoote yanayosemwa leo ..mkapa alifanikiwa katika mambo ya msingi..tulikuwa na uchumi mbovu kabisa..aliyeingia angehitaji kurekebisha basi makosa yake na kuongeza ufundi wake..mambo yende ...kumshitaki mkapa au kwa sababu kina jk wanazojua na mengi[mnafiki]..kumuanzishia magazeti ya kumchimba mkapa hakujaweza kutuongezea pato ka taifa hata dhumuni...hii habari ni nzito na watu wanajua fika hizi mbinu za "funika kombe.."ili tukeshe tunajadili mabaya ya mkapa na tusahau kuvurunda kwa serikali hii ni PROPAGANDA MBAYA KABISA...sio lazima ukubaliane na mimi lakini huo ndo ukweli halisi..

what i say is ya MKAPA TUMESHAYAONA ..YAKWENU YAKO WAPI WANDUGU..MSITAKE MKIONDOKA TUWAKUMBUKE KWA KUPIKA MAJUNGU..MTATUACHIA NINI WANANCHI???
 
Fire EL? Duh! hapo atakuwa amecheza kweli, maana hata hao wengine watajua yuko serious na wataanza kujisafisha au kujiuzulu.
Kwa upande mwingine EL akiondolewa kwa style hiyo utakuwa ndio mwanzo mzuri wa kuvunjika CCM maana lazima alipize kwa kuimega apate kundi lake, its a nice dream though

Taifa stars..hii imekuwa ni karata nyingine ya JK kujipatia umaarufu..ajue tu kuwa hii ni ya muda mfupi sana, punde tu ligi itaisha, walalahoi watakuwa hawana cha kuongelea zaidi ya maovu ya serikali ya CCM, so, badala ya kujificha kwenye kivuli cha uyoga JK aanze mkakati wa kudumu wa kurejesha matumaini ya watanzania
 
Jambo la kwanza apunguze ukubwa wa baraza la mawaziri na utitiri wa manaibu waziri wasio na kazi yeyote kwa kuanzia nashauri wizara zifuatazo ziunganishwe na kuwa wizara moja

Wizara Mifugo na Kilimo kuwa wizara moja; Maji na Nishati kuwa wizara moja, Usalama wa raia, katiba, sheria na mambo ya ndani wizara moja,Mambo ya nje na afrika mashariki wizara moja, Kazi, ajira, habari utamaduni na maendeleao ya vijana wizara moja.

Afute wizara kabisa mawaziri Waziri wa nchi Siasa na uhusiano wa jamii (Kingunge analala tu hana kazi) Waziri wa nchi Muungano Dr Mwinyi, Waziri wa nchi mazingira ( Mwandosya) apelekwe Miundo mbinu Mramba atupishe na shughuli za mazingira zitafanywa na kitengo kimoja ktk ofisi ya makamu wa Rais.

Baada ya zoezi hili kukamilika abadilishe na kuwaacha baadhi wa mawaziri mzigo, The like of Karamagi, Mramba, Kingunge, Mungai, Nagu, Magufuli, Ngasongwa nk

Kuhusu manaibu waziri hakuna haja ya kuwa manaibu waziri wawili mpaka watatu kwa kila wizara. Kila wizara naibu waziri mmoja tu.

Jambo la pili aget rid off mtandao, kuna mesmo unasema once ukishakuwa President jambo la kwanza ni ku get rid off ur best friends.

Matumizi ya yasiyo ya lazima na safari zisizo kichwa wala miguu ni mzigo kwa serikali.

Akianza na hayo nadhani kutakuwa na mwelekeo kidogo.
 
kaka philemon una mawazo kama yangu...nadhani Muungwana kwa sasa kitakachompa matumaini ni "ushindi" dhidi ya Msumbiji,na kweli kwa jinsi walivyonunua WAHANDISI wa habari watajaribu kumliwaza muungwana na wtz kwa ujinga huo...but as koba said,I for one do not give a damn on mpasuko wa kimakundi ndani ya ccm,only what is at staek here is the welfare of our nation,strip mkapa of his immunity,prosecute all thieves of our resource whom of course he knows and he incorporate the likes of Zitto,otherwise naona Muungwana na yeye kama kachoka kabisa na ingekuwa inawezekana kupokezana uirais nadhan long time angekuwa ameshampatia Dr.Salim..kwikwikwikwikwi!!!
 
Mimi natabiri kesho tunafungwa kwa hiyo hilo la ushindi tuliondowe kabisa why?

Msumbiji wamempoteza beki wao katika ajali yeye na familia yake hivyo watataka washinde ili kumuenzi mwenzao hivyo ndugu zangu tusijipe moyo sana kwa hilo.....
 
Mimi natabiri kesho tunafungwa kwa hiyo hilo la ushindi tuliondowe kabisa why?

Msumbiji wamempoteza beki wao katika ajali yeye na familia yake hivyo watataka washinde ili kumuenzi mwenzao hivyo ndugu zangu tusijipe moyo sana kwa hilo.....

Good prediction keep it up! Viva Mozambique, Viva Frelimo...
 
If few things can be changed then probably JK will save the country. First, reducing the government consumption(JK Gorv is too big), get some junks ministers off his cabinet, let Balali go, control corruption, cut the inflation down( this is real killing Tanzania), create new jobs not through loaning people money random.
Leave central bank alone, no invisible hands. Reduce taxes to wazawa companies for the conditions that they have to higher certain number of Tanzanian
Last find some real economy consultants, not 28 years old kid who graduated in international relation.

Rais ambaye ameweka pamba masikioni hawezi kuona hilo. Leo hii tumekuwa na haraka ya kuingiza ati maconsultants wageni ambao hawana experience na wanakuja kujifunzia kazi kwetu. Mifano ipo mingi sana, angalia shirika la simu lilivyouzwa kwa bei ya peremende na ndio tatizo letu hilo ukiambiwa kuna consultant wa nje unaruka kama kima.
 
Mimi natabiri kesho tunafungwa kwa hiyo hilo la ushindi tuliondowe kabisa why?

Msumbiji wamempoteza beki wao katika ajali yeye na familia yake hivyo watataka washinde ili kumuenzi mwenzao hivyo ndugu zangu tusijipe moyo sana kwa hilo.....

Tukishinda kesho utasema nini? Hiyo sababu uliyosema sioni kama ina msingi wowote.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom