GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

Kusema ukweli, hili tukio linatia huruma sana. Ni vema CCM wakaliangalia hili upya. Kwa matukio haya, hata JK mwenyewe atakosa ujasiri katika baadhi ya mambo, na hivyo kushindwa kuwa kiongozi mzuri. Kwa kweli ni bora uchaguzi uchelewe, lakini asimamishwe mgombea mwingine. Hizi si dalili nzuri kabisa. Mtu mzima kuanguka vile kwa kweli haileti picha kabisa. Nimesikitika sana.

anatia huruma kwa kweli hasa ukizingatia kuwa kampeni ndio imeanza na kesho yupo mwanza ni wazi aatkuwa na woga ...wa kuanguka tena kirumba kesho ....hasa ukizingatia ratiba zimefuatana....so sad.....itabidi kesho ahutubie kwa dakika 5 tu....na ikibidi ahutubie akiwa amekaa ....la sivyo pia akiamua anaweza kujitoa..
Kamati kuu ... ina mpango wa kukaa kutafakari mambo hasa baada ya huu mwereka!!!
 
Tatizo la chadema mnafikiri mtakwenda Ikulu kwa matusi ya kisiasa dhidi ya wapinzania wenu CCM. Mnajitafutia ajali ya kisiasa bure. mwaka huu kikwete katangaza kampeni za kistaarabu na kaagiza kila mgombea CCM afanye hivyo. Hii ni kete ya ushindi.
Hivi kuanguka kwake na Chadema kuna uhusiano gani aaahgggg, kwani alitumwa na Chadema kuanguka hilo ni tatizo lake kama anatafuta huruma kama mnavyosema basi aendelee kuanguka ili apate huruma nyingi, mnafanya utetezi bogus kabisa.
 
Pole Rais mtarajiwa, najuwa wengi watashtuka, lakini ndio hali halisi na ndivyo ilivyo kwani Watanzania wana huruma sana tena sana, na kutokana na huruma zao basi zitapelekea siku ya uchaguzi kumuonea huruma rais mtarajiwa na kumchaguwa tena ili kumaliza nngwe ya miaka mitano mingine. Nawajuwa mimi Watanzania, hawabadiriki hata ukiwa-ahidi nini subirini tu mwezi wa kumi mtaona maajabu.
 
Kama wewe una wasiwasi usifikirie ni watanzania wote!!!! Una wasiwasi wa nini?
Ahaa ni ile slumdog millionaire,macho diliko, uwezo wako wa kuextra polate situations bahati mbaya ni mdogo sana.
We ulizia tu sahani yako ya ubwabwa.
 
Naona hii imewashitua sana, Michuzi aliweka video ya JK anaenda chini huku akisema maneno yasiyoeleweka lakini naona kapigwa mkwara kaitoa haraka na video kaidelete kwenye uploads zake za youtube
 
hapa ndugu yangu tuongee ukweli kabisa mimi au umma wa Tz haujaona mahali popote amkekuwa mtu wa kisasi watu wamekuwa wakimsema lakini amekuwa mpole. me nafikiri ingekuwa wakati wa uwazi na ukweli hapa hata hizi blog zisingekuwepo

..technologia imeendelea ...hizi blog zimesajiliwa marekani,,...na ukitaka kuzifuta lazima ziwe zimekiuka content rights za marekani...ambao wapo soo liberal.....huko kwenyewe wanamtoa bush anakanyagwa...itakuwa kuwaambia wafute website ambayo haijakiuka sheria.......scenerio ya UTAMU blog ni tofauti kabisa na website ya jamii kama JF..........UTAMU blog ilikuwa inatukaana hadi kukiiuka baadhi ya vipengele vya sehemu iliposajiliwa ......hasa kwa kusababisha chuki na vitu kama hivyo .....na hata hivyo ilikuwa kazi sana kushawishi ifungwe,,,ni wazi pia TISS walitumia pesa nyingi sana hasa baada ya mkubwa kutolewa anakanyagwa!!
 
hapa ndugu yangu tuongee ukweli kabisa mimi au umma wa Tz haujaona mahali popote amkekuwa mtu wa kisasi watu wamekuwa wakimsema lakini amekuwa mpole. me nafikiri ingekuwa wakati wa uwazi na ukweli hapa hata hizi blog zisingekuwepo

Muulize Babu Seya!
 
Hivi kuanguka kwake na Chadema kuna uhusiano gani aaahgggg, kwani alitumwa na Chadema kuanguka hilo ni tatizo lake kama anatafuta huruma kama mnavyosema basi aendelee kuanguka ili apate huruma nyingi, mnafanya utetezi bogus kabisa.

CHADEMA/CUF/UDP Etc... hawana ubavu wa kumloga JK akaanguka ...hata kama JK alimbip Slaa...[Slaa alijikabidhi kwa Mungu].......JK anakabiliwa na upinzani mkubwa ndani ya chama chake na kama kumalizana watamalizana wenyewe...tatizo analijuwa jk ..kwani nayeye ameumiza wengi ndani ya chama tangu 1995...kufika hapo....hayakuwa mapenzi ya Mungu JK kuwa rais,....ametumia nguvu nyingi za kibinaadamu...
 
Aiseee Namtakia Rais wetu apone na awe na afya njema.

Lakini mi nadhani kuna watu Ikulu hawafanyi kazi zao na home work zao. Hivi Daktari wa rais anachaguliwa na Ikulu au ni rais mwenyewe ndo anajichagulia daktari wake

Kama rais anaanguka kwa sababu ya kufunga daktari wake alikuwa wapi kumshauri kuwa aahane na kufunga?Mwishowe tutauliza kama Rais wetu naye anatumia chandarua? Tumejifunza hata bilogy O level. Kuan njia za Kuavoid, prevent na cure.

Kwa nn tusiwe na wasi wasi kuwa hawamshauri vizuri zaidi ili wapate safari za nje au wamtibu kwa gharama zao za juu. Au ndo Wanamuogopa wanaogopa kumpa ushauri utakaomchukiza. Lakini hata JK hawezi kubisha KINGA NI Bora kuliko TIBA

Kuna mambo yanatokea unaona kabisa kuna udhaifu somewhere ambao ulitakiwa umeshafanyiwa kazi.
 
hapa ndugu yangu tuongee ukweli kabisa mimi au umma wa Tz haujaona mahali popote amkekuwa mtu wa kisasi watu wamekuwa wakimsema lakini amekuwa mpole. me nafikiri ingekuwa wakati wa uwazi na ukweli hapa hata hizi blog zisingekuwepo
Nachingwea,
Umechelewa sana ndugu yangu. Hata China ambako wakomunisti bado wanashika hatamu wamepata kazi ya ziada kuzuia blogs. Tunaenda na wakati na hakuna kurudi nyuma.
 
Katiba yetu inasemaje.

37​
(2) Endapo Baraza la Mawaziri litaona kuwa Rais hawezi kumudu kazi zake kwa sababu ya maradhi ya mwili au ya akili, laweza kuwasilisha kwa Jaji Mkuu azimio la kumwomba Jaji Mkuu athibitishe kwamba Rais, kwa sababu ya maradhi ya mwili au ya akili hawezi kumudu kazi zake. Baada ya kupokea azimio kama hilo, Jaji Mkuu atateua bodi ya utabibu ya watu wasiopungua watatu atakaowateua kutoka miongoni mwa mabingwa wanaotambuliwa na sheria ya matababu ya Tanzania, na bodi hiyo itachunguza suala hilo na kumshauri Jaji Mkuu ipasavyo, naye aweza, baada ya kutafakari ushahidi wa kitabibu kuwasilisha kwa Spika hati ya kuthibitisha kwamba Rais kutokana na maradhi ya mwili au ya akili, hamudu kazi zake; na iwapo Jaji Mkuu hatabatilisha tamko hilo ndani ya siku saba kutokana na Rais kupata nafuu na kurejea kazini, basi itahesabiwa kwamba kiti cha Rais ki wazi, na masharti yaliyomo katika ibara ndogo ya (3) yatatumika.
 
Sasa wakuu nani tena nang'oa ile clip ya Muzee naanguka?
Au ni Mkuu Maskini Jeuri naamua ku-edit kwa ku-delete link kabisa?
 
Du !

Haya kumekucha huko Jangwani mwenye news zaidi atujulishe hii ni kwa mujibu wa TBC ndo naangalia hapa, Rais Kikwete kadondoka live akihutubia.

2yz9yxh.jpg

Rais Jakaya Kikwete akiwa amebebwa na walinzi pamoja na wasaidizi wakati alipoanguka Jukwaani Jangwani

5yhkip.jpg

Masononeko na vilio mara baada ya Rais Kikwete kuanguka (photo: PwaniRaha.com)

VIDEO:
SEHEMU YA KWANZA



SEHEMU YA PILI



Mkuu hiyo video ya mwisho Michuzi atakuwa katiwa msukosuko kaiondoa haraka. Ila kama ingepatikana kwa western media ingemdhalilisha sana rais, haifai kabisa kuwa online yaani nimeiangalia mpaka machozi yamenitoka aisee, rais wetu mgonjwa maana kabla hajaenda chini alianza na kusema "Aisee!!" ikiashiria gonjwa linakuja. Nafikiri hahitajiki kutembea nchi nzima kwa campaign, aende sehemu muhimu tu. Ila sisi kama raia tuna haki ya kujua afya ya rais wetu mambo ya kufichaficha si kitu kizuri. Nina uhakika kama tungekuwa tunajua afya yake tusingeshtuka kwa hili. Inatisha sana
 
Last edited by a moderator:
Wazee

Mimi nionavyo hapa tuna hatari kubwa lakini kwa sababu ya ushabiki, haitashughulikiwa ipasavyo. Kuanguka hadharani, si mra moja bali mara tatu na zaidi, kunaleta fedhea (shame). Fedhea hii inaleta kutojiamini kila mara Rais atakaposimama kuhutubia. Hali hii itaongeza frequences of attack kwa Rais. Lakini pia hali inaongeza panic kwa walinzi wa Rais ambao sasa watakuwa wengi na kukaa karibu naye kila wakati. Kabla ya leo, daktari wa Rais alikuwa visible mno katika misafara akitembea na cooler iliyojaa madawa kila wakati, na hili lilileta huzuni katika misafara ya Rais.

Aibu hii kisaikolojia inaweza kuzalisha magonjwa mengine mabaya zaidi kama ya moyo na mifadhaiko mingine isiyotakiwa kwa afya ya mtu mwenye majukumu makubwa. Wote mnajua kuwa watu wenye kifafa wanavyochukua tahadhari kubwa kukaa mbali na moto au mbali na madimbwi ya maji, au mbali na penye kusanyiko la watu, kelele, n.k. Sasa Rais ataweza haya?
 
Mkuu hiyo video ya mwisho Michuzi atakuwa katiwa msukosuko kaiondoa haraka. Ila kama ingepatikana kwa western media ingemdhalilisha sana rais, haifai kabisa kuwa online yaani nimeiangalia mpaka machozi yamenitoka aisee, rais wetu mgonjwa maana kabla hajaenda chini alianza na kusema "[B]Aisee!![/B]" ikiashiria gonjwa linakuja. Nafikiri hahitajiki kutembea nchi nzima kwa campaign, aende sehemu muhimu tu. Ila sisi kama raia tuna haki ya kujua afya ya rais wetu mambo ya kufichaficha si kitu kizuri. Nina uhakika kama tungekuwa tunajua afya yake tusingeshtuka kwa hili. Inatisha sana



Hakika ila nashangaa kwa nini asingeomba msaada wakati huo maana alishajua!
 
Kama nilivyokuwa nahisi na ndivyo ilivyotokea. Wameitoa video clip. Wapumbavu sana hawa. Sijui wanachoogopa ni nini?

Acha waendelee kujaribu kuuficha huo ugonjwa alionao huyo jamaa. Safari ijayo wataumbuka zaidi atakapo kata roho hadharani....(nategemea hii comment kuhaririwa pia)
 
Ile video ya kudondoka imeshaondolewa na "user" (Michuzi)
 
Back
Top Bottom