GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

Mkuu Nachingwea ana post nne tu hapa kazi ipo.


Siri wakati anatumia kodi za wananchi? Kama anataka kuweka siri aache kazi ya urais.

Nafikiri watu wengine wanashindwa kutambua na hii ni kwa sababu ya ufinyu kufikiri na pia helimu duni... hivi kwa kutumia mfano rahisi mke wako akiwa amepima kipimo cha ukimwi na kwa sababu wewe ni mume wake basi unaruhusa ya kupewa majibu ya mke wako..
Watu hapa mchangie mada kwa kufikiri na kutumia akili zaidi
 
Kikwete kama binadamu ana mapungufu yake.Hili la mtu kumdhihaki mtu mwingine wakati tunajua nafssi yake kwa muda huo inateseka ni kukosa uungwana.Lile usilopenda kutendewa usilitende.Kama JK ana kifafa,ukimwi,tetekuwanga au ungonjwa uletao sononeko la moyo na mwili , ni vema waTanzania tukaliombea tukio hili ambalo si la kawaida.
Kuugua kwa JK ni zaidi ya ugonjwa kwani Rais wa nchi pamoja na afya yake ni taasisi inayohimili kila uweza wa uendeshaji wa nchi.
Tukumbuke kuwa kuna wanaomtakia mabaya ili wafaidike na kuna wale wenye moyo mwema nia ya kuwezesha hali ya nchi kurudi katika hali ya kawaida.
Watanzania tuombee sana ili amani na mshikamano iendelee kuwapo wakati wa muda huu wa wasiwasi.
 
Nafikiri watu wengine wanashindwa kutambua na hii ni kwa sababu ya ufinyu kufikiri na pia helimu duni... hivi kwa kutumia mfano rahisi mke wako akiwa amepima kipimo cha ukimwi na kwa sababu wewe ni mume wake basi unaruhusa ya kupewa majibu ya mke wako..
Watu hapa mchangie mada kwa kufikiri na kutumia akili zaidi
helimu ni nini?
 
Mwanza pia palibarikiwa na Papa huyohuyo, mwaka huo huo
Mwanza JK alikamatwa miguu na kuangushwa jukwaani kirumba
Mwanza alianguka Jk akihutubia katika ibada ya miaka 100 ya kanisa la AIC
Mwanza ameanguka Dr. Slaa, bafuni wakati anaoga,
Haijulikani JK ameanguka mara ngapi in private
Tofauti ya Dr. Slaa na JK ni kuwa mmoja ni Rais na mwingine ni mgombea
Tuna haki ya kuwa concerned na afya Rais
 
Nasikia TV za nyumbani nyingi hazikulionesha tukio hili kwenye taarifa za usiku, ni kumlinda rais? Kwani ni aibu kuonwa na watanzania? Ni rais wa CCM au Rais wa watanzania?

Kuanguka kwa JK kumezidi, something is VERY WRONG somewhere!

Waliosoma hesabu hasa probability watusaidie;Is it possible for "coincidence"to come twice on the same person from the multitude of more than 40 million people?

Historia inaonyesha kuwa JK kule Mwanza alianguka pia na wakasema ni uchovu wa kusimama jukwani kwa muda mrefu,leo kaanguka pia tena ikiwa ni siku ya kwanza tu toka zianze kampeni kwa maana hiyo basi issue kama kachoka haipo!

Sasa CCM wameanza kuhusisha na kuanguka kwa JK na swaumu,sidhani kama kuna ukweli wowote wa hilo maana kuna watz kibao wana funga na kufanya kazi ngumu hata za mashambani na swaumu zao lkn hawaanguki!Tunataka majibu ya kisayansi sio majibu ya kulinda kura zao ili Rais asionekane kuwa ni mgonjwa

Nakubaliana na washika dau,there are something wrong na afya ya Rais wetu na ndiyo sasa muda muafaka wa sisi anaotuongoza tuambiwe na Ikulu nini chanzo cha kilichompata leo Rais wetu Jangwani sambamba na majibu ya kupimwa uimara wa ubongo wake aliyofanyiwa mwaka juzi hospitalini Havana-Cuba!
 
Kikwete kama binadamu ana mapungufu yake.Hili la mtu kumdhihaki mtu mwingine wakati tunajua nafssi yake kwa muda huo inateseka ni kukosa uungwana.Lile usilopenda kutendewa usilitende.Kama JK ana kifafa,ukimwi,tetekuwanga au ungonjwa uletao sononeko la moyo na mwili , ni vema waTanzania tukaliombea tukio hili ambalo si la kawaida.
Kuugua kwa JK ni zaidi ya ugonjwa kwani Rais wa nchi pamoja na afya yake ni taasisi inayohimili kila uweza wa uendeshaji wa nchi.
Tukumbuke kuwa kuna wanaomtakia mabaya ili wafaidike na kuna wale wenye moyo mwema nia ya kuwezesha hali ya nchi kurudi katika hali ya kawaida.
Watanzania tuombee sana ili amani na mshikamano iendelee kuwapo wakati wa muda huu wa wasiwasi.
Kama wewe una wasiwasi usifikirie ni watanzania wote!!!! Una wasiwasi wa nini?
 
Mungu hadhihakiwi... Mungu hasikilizi sala za wanafiki... waongo....

Macho wapi Mungu amedhiakiwa!!!!!, ikiwa hatakama Adui yako mpende!!! hapo ambapo Mungu amedhiakiwa ni wapi...yaani humu nadi kuna watu vichwa maji sijapata kuona mimi nilikuwa nadhani all are great thinkers kumbe kuna .........jibu mwenyewe
 
Heri kabisa ameaibika jamaa anasema eti wanapambana na Rushwa akabaki kusema aiseee aiseee Giza na mweleka!
 
Macho wapi Mungu amedhiakiwa!!!!!, ikiwa hatakama Adui yako mpende!!! hapo ambapo Mungu amedhiakiwa ni wapi...yaani humu nadi kuna watu vichwa maji sijapata kuona mimi nilikuwa nadhani all are great thinkers kumbe kuna .........jibu mwenyewe
Adui gani? wacha siasa zako za enzi za wakati wa mawe hapa!
 
Heri kabisa ameaibika jamaa anasema eti wanapambana na Rushwa akabaki kusema aiseee aiseee Giza na mweleka!

Halafu kama alivyokwisha sema Mag3... baada ya kuanguka anaibuka mtu na kupayuka.... CCM OYEEEEE
 
Mimi nimeangalia clip ya kudondoka kutoka blog ya michuzi, alianza kusihiwa nguvu wakati akisema kuwa tuleifanya mengi na tunaahidi kufanya zaidi kama mkitupa ridhaa, tuta... tu...nyaaa-- then kwisha. Nadhani hizi ahadi zinampa shida kwa kuwa anajua hazitekelezeki, alikuwa anasema uongo, na mwili wake ukakataa kabisa. This is very sad, na nadhani huyu bwana ana kaugonjwa hako na lazima kanampata mara kwa mara, ndio maana alijua kanakuja akasema "aisee"

I can be sure kuwa sio kitu kigeni kwake, so kuna haja ya yeye kuamua kwa amani tu aache!!

Nafikiri hapo kulikuwa na mgongano wa dhamira mbili tofauti (malaika wa bwana na wa shetani) moja ilikuwa inamwambia sema ukweli nyingine ilikuwa inamwambia danganya, nafikiri iliyokuwa inamwambia danganya ikashinda alipotaka kuendelea roho na mwili vikakataa.
 
Mimi nikiwa kama mtanzania mwenye mapenzi maema na nchi yangu na watu wake akiwepo Raisi JK, ninamuombea Mungu ili amjalie afya njema na kuendelea kuingoza nchi ya Tanzania. Tunajua mangapi ambayo ameyafanyia Tz. Ufisadi si jambo dogo linahitaji uwe na uwezo thabiti wa kupambana nayo na uwezi kupambana ufisadi kwa kuhisi tuu.
Nyieeeeeee aliyewatuma bahati mbaya kawatuma kumsafisha JK akiwa kachelewa mno kwani macho yetu yalishafunguka na tumemwona mfalme uchi.
 
Yah! I hate CCM, Yah I hate Kikwete as a president but not as a personal, tukio lililotokea leo limefanya nitokwe na chozi. The guy is serious sick na kama CCM wanampenda huyu mtu basi ni heri wampumzishe
 
Nyieeeeeee aliyewatuma bahati mbaya kawatuma kumsafisha JK akiwa kachelewa mno kwani macho yetu yalishafunguka na tumemwona mfalme uchi.
Mimi siyo mpenzi wa chama chochote, lakini Kikwete ni raisi wetu na nafikiri hakuna mwingine zaidi yake hata huyo unayemfikiria mwenyewe alikuwa hajiamini kupambana kwa nafasi hiyo utampaje mtu urais hata yyeye mwenyewe hajiamini.. urais siyo sehemu ya kujifunzia
poleni sana, kama ma fisadi wamewatuma mmeshindwa,
 
Neno au lugha nzuri pale mtu apatwapo na tatizo au misukosuko, sie waungwana huwa nalo moja tu... Pole au Poleni kwa yote yaloku/wa fika.
 
Mimi siyo mpenzi wa chama chochote, lakini Kikwete ni raisi wetu na nafikiri hakuna mwingine zaidi yake hata huyo unayemfikiria mwenyewe alikuwa hajiamini kupambana kwa nafasi hiyo utampaje mtu urais hata yyeye mwenyewe hajiamini.. urais siyo sehemu ya kujifunzia
poleni sana, kama ma fisadi wamewatuma mmeshindwa,

wewe ni mtetezi wa mafisadi wa ccm .... acha unafiki wako
 
Back
Top Bottom