Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Adui ni adui tu. Unapodhamiria kummaliza adui na hasimu wako mkuu unapaswa kutumia kila njia kummaliza. Na njia rahisi ya kummaliza ni kujiunga na wale wote waliojeruhiwa na adui yako ili muweze kumsawazisha kwa nguvu kidogo. Our enemy is the ccm which has been on power for almost 50yrs with sufferings and backward development. Welcome Lowasa to fight our biggest snake (ccm). "Aluta continua"
 
Teh teh teh siasa hizi! Mkuu achana na hiyo picha inamuonyesha Lowassa akilisilimiana na viongozi wa CHADEMA. Jaribu kuangalia ile picha aliyokaa meza kuu na viongozi wa CHADEMA kwa umakini kabisa nayo unaweza kusema ni edited?
Mimi picha hiyo ya chini nilisema wazi ni edited lakini hiyo ya juu hakika ni halisi kabisa na ni wazi Chadema hawakutaka picha hii ivuje na Mbowe ana sema za kutengenezwa lakini kwa aliyo yasema mbele ya wahariri ni wazi picha hizo ni halisi kabisa sema imembidi azikane tuu!
 
Yaan style hiii kula yang kuanzia mjumbe wa nyumba.10 hadi raisi inarud CCM...maana sas naona CDM wanaleta michezo ya kitoto...mda wote CDM tunapambana yey alikuwa wapi mpak aone kanyimwa madaraka uko ndo arud kwetu..mtu tulyemponda kwa ufisadi leo hii tunamshuhudia Kama hero wetu..
 
Umeongea maneno ambayo yanaumiza sana.Ninajiuliza kama Dr.Slaa ataendelea kuwa kiongozi ndani ya CDM sitakaa nimuamini au kumuheshimu kama mtu aliyeukataa ufisadi na akaonekana hivyo.

Sababu kama viongozi wameshindwa kutuheshimu watanzania tunaumia au tulioumia na uzembe,rushwa na ufisadi uliofanywa na viongozi wakiwa ndani ya uongozi ambao walishindwa hata kusema ni nani muhusika mkuu wa ufisadi ule,leo Wanamkaribisha Lowassa,atakuja na akina Rosatam na Chenge,utawa kimbiza hao?

Itabidi viongozi wa CDM watueleze vigezo walivyotumia kumteua Lowassa awe Mgombea urais,hivi pesa alizotapanya wakati akigombea kuteuliwa kuwa Mgombea kwa tiketi ya CCM anazirudishaje?Hivi viongozi wetu hata hili wameshindwa kuliona?

Ninajiuliza wamelipwa kiasi gani cha kutudhalilisha wanachama wa CDM kwa kiasi hicho?Hivi nani mwenye ubavu atakayekuja kumnadi Lowassa?

Kwa kweli kwangu KURA yangu sitompa FISADI hata siku moja.

Mbowe,Dr.SLaa na Tundu Lissu mtueleze mmelipwa kiasi gani na Lowassa?

Pole dada, ninajua unaumia sana kutokana na haya maamuzi.

Ila jua kwamba hivyo ndivyo siasa(haswa za Kiafrika) zilivyo.
 
mhn! haya bana!
sijachangia toka mchakato wa kutafuta urais uanze lakini kwa hili na mimi nafikiri nivunje ukimya kwa maneno machache na hasa kwa chama hiki ambacho watanzania wengi wanaimani nacho kuwa kinaweza kuwa hakiwezi kufanya mambo ya hovyo.
ikiwa ni lengo ni kuwa na kura nyingi za urais wanaweza kuzipata lakni si urais ila baya zaidi ni kuwa thamani halisi ya chama hiki kwa watu wengi itashuka na hawataaminiwa tena kama mwanzo hilo walitegemee.
hata wabunge ambao watachaguliwa si kwasababu ya chama tena bali ni kwakuwa watu wanataka ushindani wa maana katika bunge lao kwa kupunguza idadi ya chama kinachotawala kuwa na wabunge wengi.
kiukweli kama kweli huyu jamaa anaenda huko basi jambo la busara ni kwamba asiwe mgombea tena wa urais vinginevyo ndio safari imekwisha.
chadema tusipo angalia ni kwamba tumeuza uhuru wetu kwa kipande cha mkate.
jinsi ilivyokuwa inaonekana ilikuwa kama ifuatavyo
mwaka huu viti kwa wapinzani zilitegemewa kuwa kati ya asilimia 40-50 na kama ikienda kama itegemewavyo na wananchi wakaaamini uchanguzi mwingine ingekuwa kati 50-70.
hii ingewewawezesha kuwa na uhakika wa kushika dola na kutoa rais ifikapo 2025 lakini kwa hili sina uhakika kama tutafika hapo vinginevyo jamaa asiwe mgombea urais.
linaloendana na hilo hata hawa wagombea waliohama au wabunge watakao hamia ukiacha esta bulaya ambaye yeye alionekana yuko huku toka mwanzo lakini wengine wote walizofata ni nafasi zao za madaraka katika majimbo yao. kama kweli wanataka kuwa wapinzani wa kweli waendelee kuwapigia debe wagombea waliojitokeza awali na chadema au vyama vingine vya upinzani na sio vinginevyo.
nia aibu kwa vyama vilivyo aminiwa na wananchi kula matapishi yao.
hata wakati wa njaa haitokei wenye njaa kula matapishi yao.
utetezi wa jamaa kwa sasa kwa kashfa mbalimbali alizohusishwa nazo kwa kuhisi au kuhisiwa azitakuwa na maana sana kwa macho na masikio ya watanzania kwakuwa hili walilitegemea mwanzo na sio sasa hili haliwezi kujenga uaminifu kwa muda huu ni kama kusema ng'ombe hanenepi siku ya mnada.
ukweli ni kwamba wabunge binafsi nipo tayari kuwaona wanasimama ukawa lakni kwa hili kama mkitupa mgombea huyo sioni kama kutakuwa na mafanikio ya kushinda dola.
ikumbukwe kuwa katika taifa hili haijawahi kutokea mwanachama aliyependekezwa na rais anayeondoka akashika nchi vilevile waziri mkuu akashika nchi.hivyo huyu jamaa angepumzika mfano mdogo nauhakika nyerere angekuwepo angeulizwa kutoka moyoni ni kwamba mwinyi halikuwa chaguo lake hivyo hivyo mwinyi alimpenda marechela na mkapa japo hakuonyesha wazi sana lakini alimpenda sumaye hii ya mwisho simo.
na rais aliyestaafu ananafasi kubwa na ushauri mkubwa kwa nafasi hii ni kama nyerere kwa mkapa, mwinyi kwa kikwete na mkapa kwa magufuri.
hivyo tujipange kwa maslahi ya taifa na sio kumwangalia mtu na fedha zake
najua nimewaudhi sana lakin huu ndio mchango wangu na mawazo yangu na ndicho ninachokiona.
 
Inatia huzuni sana,najiuliza mara mbili mbili sipati jibu.Wametuona watanzania wapuuzi sana.Yaani ninaumia nikikumbuka wanachama walivyojitoa muhanga kuitetea CDM,wamepoteza familia na wengine viungo vyao,leo wanamuweka mtu ambaye hata kuwatetea BUNGENI tu hakuthubutu,leo wanamuona wamaana kuliko hawa wanachama?

J J Mnyika atuambie Bungeni alikuwa anatetea nini?Na sasa anafanya nini?Ngoja nifanye maamuzi magumu sasa.

Watanzanzania wote wenye mapenzi mema sema HAPANAAAAAAAAAAAA kwa Lowassa

Mkuu adui wa nchi yetu sio Lowasa

Sio membe

Sio Kikwete

Sio Mwigulu

Adui yetu ni Mfumo wa CCM...Hicho tu

Failure ziko ngapi kweye uchumi wetu...Is it about Lowasa au mismanagement ya mfumo wa serikali ya CCM

I believe you are learned enough.......Our goal is to take out CCM.....Baada ya hapo ni effectivenesss ya serikali ya UKAWA kuweka uwajibikaji
 
Mke wa mtu unaweza kumuowa akishaachwa na mumewe. Kwa hivyo hata LOWASA amekua safi baada ya kukatwa na CCM laiti angepewa nafasi ya kupeperusha bendera ya MAGAMBA heeeeeeeeeeeeee UKAWA wasingeona cha kukampeni zaidi ya Lowasa + Richmind. Tutaendele kuyaona maajabu

Hapo maajabu yake nini sasa? Hata kama Mbowe hatasema hadharani ila sababu ya lowasa kukaribishwa ukawa, ni kwamba kila mtu mwenye akili timamu anajua kabisa lowasa ana hasira na kisasi, kwa kitendo cha kitengo kukata jina lake. Achilia mbali ufisadi wake na madhambi mengine, tayari huyu bwana amejaa sumu ya kisasi. kwa vyovyote vile cdm kwao ni mtaji mkubwa, make kwa sasa lowasa ni adui wa kitengo, na cdm adui yao kisiasa ni ccm,kwa iyo lazima sapoti ya mamvi waikubali tu. Ni kweli hata mamvi asingepigwa rafu na kushinda, bado majukwaani cdm wangemnanga make ni rafiki wa adui yao.
 
Chiwa are you serious

Unaongelea 2025....unaona hali ya uchumi wa nchi yetu ulivyo sasa?

CCM has to go NOW.......Hakuna muda wa kusubiri

Sometimes ni bora kuharibu mfumo uliopo na kuanza kuijenga nchi upya...hAKuna haja ya kusubiri subiri

Sikia ndugu yangu....Viongozi waliopita ni binadamu...sio Miungu...wana madhambi yao pia....na ni hao hao walioifikisha nchi yetu katika hali hii mbaya.

Kwa hio hata wanapotoa maoni yao wanaangalia nani atawalinda

Lowasa ni mtu ambaye hua hana compromise na Ujinga

Tuepuke kuangalia mtu mmoja mmoja...Adui yetu ni CCM
 
Last edited by a moderator:
Mimi picha hiyo ya chini nilisema wazi ni edited lakini hiyo ya juu hakika ni halisi kabisa na ni wazi Chadema hawakutaka picha hii ivuje na Mbowe ana sema za kutengenezwa lakini kwa aliyo yasema mbele ya wahariri ni wazi picha hizo ni halisi kabisa sema imembidi azikane tuu!

Kwahiyo Mbowe anajidai kukana teh teh teh siasa hizi! Mkuu acha movie iendelee!
 
BAVICHA acheni kulia lia. Siasa za kufuata mkumbo ndio zimewafikisha hapa.
 
Chiwa are you serious

Unaongelea 2025....unaona hali ya uchumi wa nchi yetu ulivyo sasa?

CCM has to go NOW.......Hakuna muda wa kusubiri

Sometimes ni bora kuharibu mfumo uliopo na kuanza kuijenga nchi upya...hAKuna haja ya kusubiri subiri

Sikia ndugu yangu....Viongozi waliopita ni binadamu...sio Miungu...wana madhambi yao pia....na ni hao hao walioifikisha nchi yetu katika hali hii mbaya.

Kwa hio hata wanapotoa maoni yao wanaangalia nani atawalinda

Lowasa ni mtu ambaye hua hana compromise na Ujinga

Tuepuke kuangalia mtu mmoja mmoja...Adui yetu ni CCM
Kamwe hakuna chama cha kuiondoa CCM madarakani kamwe...
 
Last edited by a moderator:
Kwa kauli yako ni kuwa waTanzania ni wajinga kweli yaani wanakusanyika na kupoteza muda wao kumshabikia FISADI? ebu changanya akili yako kidogo na utafakari kwa kina.

MMGL2436.jpg


MMGL2535.jpg


MMGL2536.jpg


MMGL0846.jpg


MMGL0984.jpg


MMGL0158.jpg


MMGL0175.jpg

Hebu changanya na zile picha za Kuhama kwa Lembeli, Mwanza, Iringa kwa Msigwa, kumbuka na umati wa Arusha kwenye mikutano ya makamanda yaani hapo mtu mwenue akilia timamu hawezi kuiona fursa ya kuizika CCM? Au wa nataka wabaki pembeni wakiimba ufisadi hukubo yanaendelea kama kawaida, bado naona taifa za Lowassa ni kubwa kuliko hasara. Bahati mbaya watakaoondoka warudi CCM maana kwa kwa kuondoka Lowassa imeshafishika. Pity
 
Ngoja nikuambie ukweli.Kakini una kifua?Ukweli ni huu,CCM inakufa.Kila ukipita mtaani jina ni Lowasa tu.Nilikuwa nadhani Lowasa karubuni watu kwa fedha.Ni kweli karubuni wachache, lakini ingekuwa wachache,not this much.Sjui huyu bwana katumia mbinu gani.Magufuli si lolote kwa Lowasa hasa ikizingatiwa kwamba kapitishwa na chama kiovu.Wanasema uovu wa Lowasa ni bora kuliko uovu wa CCM!CCM inakufa hivi hivi naiona,thankyou God,umesikia sala zetu.
Yaani uzuri w CCM ni kubadilika badilika kulingana na hali husika ktk wakati muafaka kama hili ni kweli la Lowassa ,? Ni ushindi wa wazi ktk opresheni ya kuvua gamba na muonekno mpya wa CCM imara inayozidi kukomaa kila leo. Magufuli kamaliza yote!!!!
 
Kama kweli CHADEMA kwisha kazi. Wamejipeleka kaburini huku wakiona na kutizama. Inatia huruma kwa Watanzania waliokuwa na matumaini kwa chama chao cha CHADEMA. Watakimbilia wapi??? Sitashangaa wakirudi kwa CCM ambao wameonyesha kuanza vita dhidi ya ufisadi kwa kumuengua Lowasa kwenye kugombea urais wa nchi.

Ccm hamuwezi kutoa ushauri cdm ili kisonge mbele, tulieni kimbuga kinakuja
 
Back
Top Bottom