Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Lowassa karibu sana na waitee na wengine waambie bado nafasi wanayo ya kutubu na kuwatumikia watanzania kwa upendo, huna mpango na urais lakini Monduli Ubunge kama kawaida kupitia CHADEMA .

Wataisoma namba CCM huu mwaka.

Lowassa kaja direct chadema na kuwa mgombea urais na kuwa juu ya Akna slaa ambao walimkashfu jamaa ni fisadi dah kituko cha Mwaka sijui slaa ataweka wapi sura yake Hahaha na mbowe kashanunuliwa na Lowassa basi kimya
 
Kumpokea yeyote hata Lucifer ni kuonyesha chama hakina agenda, hakina manifesto ya kuwashawishi wapiga kura wakichague kiwaongoze. Shame on CHADEMA kama hii ni kweli.
Unasema agenda au manifesto! Hujui kuwa walikuwa nazo lakini kwa miaka ishirini watu hawajazielewa. Nadhani hii wataielewa, ni ubunifu mzuri wala usikutishe.
 
Mkuu kama LOWASA anaweza kuindoa CCM acha apeperushe bendara ya CHADEMA/UKAWA we are so tidy with CCM haina haja ya kueleza kwa nini tumechoka najua, unajua

Hilo ndilo jambo la msingi,tuungane na yeyote anayetaka mabadiliko! Jambo la msingi ni kuondoa mfumo dhalimu uliopo,Kama Lowassa anaweza kusimama na CCM wakakaa basi asimame tu,binafsi sioni tatizo!
 
Kwa fununu watanzania wamekasirika sana juu ya ukigeu geu wa CHADEMA. Kipindi wanatangaza majina ya list of shame, watanzania walifurahi sana na CHADEMA walipata umaarufu. Moja ya fisadi papa ndani ya CCM na aliyetakiwa kujivua gamba tangu mapema alikuwa Lowassa. Ila cha ajabu aliendelea kukomaa ndani ya CCM akijua kwamba anaweza kuwanunu wajumbe mpaka rais na baraza la ushauri la wazee. Ila kumbe system (UT) waligundua kuna mtu anataka kuuza nchi. JK ukamuingia uzalendo na kufanya maajabu ya kutuletea mgombea asiye kuwa na doa. Sasa upande mwingine wa shilingi.

Iwapo Lowassa angepitishwa na CCM, tungeshuhudia magazeti kama ya Tanzania daima yakilemba;
  • CCM wapitisha fisadi urais
Je ndani ya CDM sasa watamuitaje??? Je hii si ndiyo dalili kufa CDM?
"Kilichowapa umaarufu Dr. Slaana CHADEMA ndicho kinawashusha."

Zitto aliitwa na anaendelea kuitwa Yuda Msaliti, wakati Mbowe ana damu za wana CDM waliokufa kwenye maandamano na mikutano ya CDM Kwa mil 10!! Inasikitisha.

Umeongea maneno ambayo yanaumiza sana.Ninajiuliza kama Dr.Slaa ataendelea kuwa kiongozi ndani ya CDM sitakaa nimuamini au kumuheshimu kama mtu aliyeukataa ufisadi na akaonekana hivyo.

Sababu kama viongozi wameshindwa kutuheshimu watanzania tunaumia au tulioumia na uzembe,rushwa na ufisadi uliofanywa na viongozi wakiwa ndani ya uongozi ambao walishindwa hata kusema ni nani muhusika mkuu wa ufisadi ule,leo Wanamkaribisha Lowassa,atakuja na akina Rosatam na Chenge,utawa kimbiza hao?

Itabidi viongozi wa CDM watueleze vigezo walivyotumia kumteua Lowassa awe Mgombea urais,hivi pesa alizotapanya wakati akigombea kuteuliwa kuwa Mgombea kwa tiketi ya CCM anazirudishaje?Hivi viongozi wetu hata hili wameshindwa kuliona?

Ninajiuliza wamelipwa kiasi gani cha kutudhalilisha wanachama wa CDM kwa kiasi hicho?Hivi nani mwenye ubavu atakayekuja kumnadi Lowassa?

Kwa kweli kwangu KURA yangu sitompa FISADI hata siku moja.

Mbowe,Dr.SLaa na Tundu Lissu mtueleze mmelipwa kiasi gani na Lowassa?
 
Jamani watu wote sasa hivi wamekuwa wakiongelea lowassa kusimamishwa ukawa kupitia chadema. Lakini siyo chadema wala ukawa wanaojiuliza je, wakishindwa urais 2015 hatma yao itakuwaje?

Kwani unaposhindana si kuna matokea ya aina mbili? kushinda au kushindwa! alishajiandaa kwa yote. Anaweza kushindwa Urasi kwa goli la mkono kutumika ila tunashinda kwenye ubunge, yote huu ni ushidi tu. Hii tabia ya kuunga mkono 100% na baadae kutoa matatizo kibao mtakoma.
 
Ccm haitakufa kwa mizaha mliyonayo na watanzania wanataka maendeleo c kuondoa ccm au kuiweka upinzani madarakani.
 
Kama kawaida tulitaraji CCM ndiyo wafurahi maana CDM inaenda kujifia wao ndiyo wanaongoza kulialia.
Hii inanikumbusha enzi za kumfukuza Zitto waliyokuwa wakilalamika walikuwa ni CCM.
Viva CHADEMA.
ukiona maccm yanakataa jambo ujue hilo ndo linalotakiwa na Watanzania. Ukiyaona yanakubali jambo jua hilo kwa Watanzania ni kifo. Ukitaka kusimama kwenye haki basi simama kinyume na ma ccm.
 
ni wiki ya tatu sasa kila mahali ni ukawa ukawa ukawa mbowe lipumba slaa lowasaa ndio talk of the town , kwa mkakati huu wa kuteka media mmeonesha kuwa mpo vizuri hata kuwashinda ccm, licha ya kwamba mengi yanayo semwa pengine ni fununu na hayana ukweli lakini habari ndio hiyo sio ccm sio ACT sio tadea sio ukawa wooootee mguu pande kulia geukia ukawa na wamekubali
 
Kumbe sikulijua hilo kabla basi MAMVI unasubiri nini fursa ndio hiyoooooo!!!
 

It is really unbelievable, hivi kumbe sisi Watanzania karibu wote ni wachumia tumbo? Hivi ni kweli hili limetokea? Sipati picha hawa waliomsema Lowassa ni fisadi mkubwa mpaka wakamtaja kwenye list of shame leo hii wanakaa meza moja na kujadiliana apate nafasi ya kuwa rais.Shame. Mbowe anakiua chama. Hivi huyo Slaa anajisikiaje? anakula matapishi yake mwenyewe? Yaani hainingii akilini kwa kweli. Mnyika, Tundu Lisu, Lema, Mdee mmekubali kweli haya yatokee? Kweli sasa nimeamini pesa inavunja milima!!!
 
Back
Top Bottom