Netanyahu
Senior Member
- Oct 2, 2008
- 147
- 22
Bunge katika kikao chao cha sasa limekataa kujadili hotuba tata ya Kikwete aliyoitoa bungeni kikao cha bunge kilichopita kwa kile ofisi ya spika ilichosema kuwa muda ni mfupi na hautoshi.
Muda usingetosha kweli kwani wabunge walikuwa wajadili si hotuba yake tu bali pia walipania kumjadili yeye na utendaji wake usioridhisha ikiwemo kitendo chake cha kuvunja katiba kwa kuingiza mambo ya kidini kama kadhi na OIC na kuwagawa watanzania kwa mipasuko mikubwa na kutaka hatua zichukuliwe dhidi yake.
Ofisi ya spika baada ya kuona kuwa kuna jambo la kihistoria linakuja ambalo lingetikisa vyombo vya habari duniani na kutoa hatima ya Raisi Kikwete madarakani ofisi ya spika ikaamua kuichomoa hoja ili kumnusuru Raisi Kikwete.
Ofisi ya spika kukataa kuingiza hoja kumjadili Rais ni kuahirisha tu tatizo.TIME IS RUNNING OUT.Ni vizuri bunge limjadili na lichukue hatua kuliko kuachia wananchi wamjadili Raisi na kumchukulia hatua zikiwemo za kumrushia mawe kama ilivyofanyika Mbeya.
Bunge kuahirisha kumjadili na kumchukulia hatua kwa sababu ya kisingizio cha muda,kujikomba au chochote hiyo ni PANADOL APPROACH ambayo inasaidia tu kupunguza maumivu ya Raisi kwa muda na baadaye yatamlipukia tena kama habadiliki katika utendaji wake ukiwemo uvunjaji katiba kwa ukumbatiaji hoja za kidini.
Kushindwa kumjadili bungeni ni kituko kinachoweza zalisha vituko mitaani.Bunge ndiyo mahali sahihi pa kumvalia njuga Raisi na penye heri kuliko wananchi kumvalia njuga.
Muda usingetosha kweli kwani wabunge walikuwa wajadili si hotuba yake tu bali pia walipania kumjadili yeye na utendaji wake usioridhisha ikiwemo kitendo chake cha kuvunja katiba kwa kuingiza mambo ya kidini kama kadhi na OIC na kuwagawa watanzania kwa mipasuko mikubwa na kutaka hatua zichukuliwe dhidi yake.
Ofisi ya spika baada ya kuona kuwa kuna jambo la kihistoria linakuja ambalo lingetikisa vyombo vya habari duniani na kutoa hatima ya Raisi Kikwete madarakani ofisi ya spika ikaamua kuichomoa hoja ili kumnusuru Raisi Kikwete.
Ofisi ya spika kukataa kuingiza hoja kumjadili Rais ni kuahirisha tu tatizo.TIME IS RUNNING OUT.Ni vizuri bunge limjadili na lichukue hatua kuliko kuachia wananchi wamjadili Raisi na kumchukulia hatua zikiwemo za kumrushia mawe kama ilivyofanyika Mbeya.
Bunge kuahirisha kumjadili na kumchukulia hatua kwa sababu ya kisingizio cha muda,kujikomba au chochote hiyo ni PANADOL APPROACH ambayo inasaidia tu kupunguza maumivu ya Raisi kwa muda na baadaye yatamlipukia tena kama habadiliki katika utendaji wake ukiwemo uvunjaji katiba kwa ukumbatiaji hoja za kidini.
Kushindwa kumjadili bungeni ni kituko kinachoweza zalisha vituko mitaani.Bunge ndiyo mahali sahihi pa kumvalia njuga Raisi na penye heri kuliko wananchi kumvalia njuga.