Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
jamani.... kuna neno wanasema "to err in the side of caution". Wasipofanya au kuhurusu uchunguzi huru watakuwa wanachochea hisia zote hasi ambazo zimekuwa zikienea. Ukifiria sana utaona kuwa yawezekana ilikuwa ni ajali ya kawaida na kosa kubwa ni la kijana Malya kusema kuwa yeye hakuwa dereva na baadaye kukiri alikuwa dereva; hilo ndilo lililochanganya watu sana. Yawezekana kama walivyosema wengine hana leseni n.k

So yawezekana kuwa ni kifo cha kawaida kabisa kama Katibu Tarafa anavyosema, lakini jinsi mambo yalivyokwenda na yanavyoshughulikia yanafanya kifo hiki kisiwe cha kawaida na hivyo kulazimu uchunguzi huru ili kuwahakikishia wananchi kuwa ni kifo cha kawaida kabisa na ni ajali tu.

Kuna ubaya gani kati hilo Katibu Tarafa?

Kusema alikua haendeshi harafu baada e kukili hilo sio kosa la kutia wasiwasi ,hata juzi tu jamaa yangu kafa ila driver aligonga mti upande wake akafa palepale yule aliyekua anaendesha akasema yule aliyekufa ndiye alikua anaendesha harafu akili ilipomkaa sawa akabadili usemi akasema yeye ndiye alikua mshika usukani.

Hiyo siyo hoja kabisa hoja hapa ni Je Chacha kafa kwa ajali ya gari ama Lah na kama ndiyo nani kahusika.

Ktk nyanja za ufundi kunapotokea tatizo fundi mara nyingi hukimbilia maeneo ambayo huleta tabu mara kwa mara ili afanye Troubleshooting.

Na unapomtafuta nyoka aliyeingia chini ya uvungu wako ukiwa umeshikilia tochi lazima uanzie miguuni mwako kupiga tochi na ukienda mbali sawia na mkabala zaidi.

Eneo la toableshooting ambalo tunaweza Anzia ni wale wote ambao CHACHA amekorogana nao kwa siku hizi za usoni.

Na miguuni kwa RIP Chacha pa kuanzia kupiga tochi kumsaka nyoka aliye uvunguni ni CHADEMA.
 
Nampa pole nyingi Mkwewe Marehemu na familia yake kwa ujumla. Aidha kwa wanachama wote wa chadema na Wapiga kura wa Tarime na wote walioguswa na msiba huu...
 
Mkamap.. sasa na wewe mbona unachekesha; huyo kijana si ametoka Chadema na imedaiwa alikuwa ni mwanachama or in one way or another amekuwa karibu na Chadema. Sasa huko siyo kuanzia miguuni; au unaposema Chadema unasema kitu kingine? Na kuhusu kukorogana don't be too sure kuwa Wangwe alikuwa amekorogana na Chadema tu; believe me ukizungumzia "most recent"... it is not Chadema.
 
nadhani sasa is getting out of hand; tusubiri uchunguzi kama utafanyika. kwa sababu kama nilivyosema kwenye clue ya pili; gari. Sasa hivi mimi ningekuwa niko interested kuona nani analiangalia gari na kama limesafishwa n.k sasa hivi hilo gari lilitakiwa lisiguswe wala kufanyiwa nini hadi uamuzi utakapotolewa kama kuna inquiry. kwa sababu kama bunduki n.k ushahidi uko kwenye gari zaidi. Kwa sababu mtu anaweza kuangalia majeraha aliyo sustain Wangwe na kuangalia ndani ya gari ni kitu gani kimesababisha. So, ningeuliza where is the car?

Sasa wewe unachunguza au una mwenge unamulika maana inaonekana kama kisa kizima unakijua ila unagojea hukumu imeshatoka na watu weshafunga vitabu ndio uje na mauzauza ,maana kila watu wanapopekechua unakutwa umishafika na information za kukatisha tamaa kana kwamba tuelekeako siko,una info zimwage hapa tuzione kama ni pumba au mbigili. Kuna hatari ukatuambia walimfunga miguu wakati maiti atakuwa ameshazikwa utatoa mtihani mwengine mpya.
lakini unashusha clue utafikiri tupo kwenye body language.
 
Wanapoteza Muda Mwisho Watazika Tu Hao Wanasubiri Tu!!!wagawane Mali Kabla Ya Kuzikwa!!!wamefanyiwa Sokoine Ije Kakayangu Wangwe Wapi Iliishia
R.i.p Wangwe
Tafadhalini Naombeni Mpumnzisheni Braza Wetu Msijejiundia Tume Kula Ulaji Kwa Jina La Marehemu
Ulale Pema Peponi


Bahati mbaya huwajui watu wa mkoa wa Mara na hasa wilaya ya Tarime. Huko hakuna cha msalie mtume na umeshuhudia hayo mapokezi ya simanzi kwa kushirikiana bila kubaguana. Wana Bariadi na wana Monduli wanaweza kuzugwa kirahisi lakini si wana Tarime. Kama kuna watu wameamka nchi hii, wanapatikana Tarime.
 
Kusema alikua haendeshi harafu baada e kukili hilo sio kosa la kutia wasiwasi ,hata juzi tu jamaa yangu kafa ila driver aligonga mti upande wake akafa palepale yule aliyekua anaendesha akasema yule aliyekufa ndiye alikua anaendesha harafu akili ilipomkaa sawa akabadili usemi akasema yeye ndiye alikua mshika usukani.

Hiyo siyo hoja kabisa hoja hapa ni Je Chacha kafa kwa ajali ya gari ama Lah na kama ndiyo nani kahusika.

Ktk nyanja za ufundi kunapotokea tatizo fundi mara nyingi hukimbilia maeneo ambayo huleta tabu mara kwa mara ili afanye Troubleshooting.

Na unapomtafuta nyoka aliyeingia chini ya uvungu wako ukiwa umeshikilia tochi lazima uanzie miguuni mwako kupiga tochi na ukienda mbali sawia na mkabala zaidi.

Eneo la toableshooting ambalo tunaweza Anzia ni wale wote ambao CHACHA amekorogana nao kwa siku hizi za usoni.

Na miguuni kwa RIP Chacha pa kuanzia kupiga tochi kumsaka nyoka aliye uvunguni ni CHADEMA.


Tenda haki. Kama unaweza kusema tuanzie Chadema, ndio unatuambia uchunguzi ufanyike, ili kama ni Chadema, CCM ijulikane. Lakini kumbuka Chadema, CCM, Polisi, Usalama, JWTZ kama taasisi haziwezi kuua, wanaoweza kuua ni watu ndani ya taasisi hizo. Tumewahi kusikia polisi, wanajeshi wakihusika na uhalifu, juzi mwanajeshi kaua mkewe, halafu tumesikia wanajeshi wamekamatwa na mitambo ya gongo, tukasikia, kiongozi wa CCM kakutwa na nyara za serikali, tukasikia wabunge wa CUF wamefoji document kusafirisha vimada, tukasikia kuna viongozi wa Chadema ni majambazi, huko Tarime kuna wana Chadema ni wahalifu. Uhalifu upo sehemu yoyote hata humu JF kuna wahalifu na watu wanaolipwa kuandika tofauti na wengine wanaoandika kwa kuwa ni sehemu ya "kiburudisho" cha maisha yao. Tusibadili muelekeo, TUTALAANIWA. Ingekua Waislamu, angekwisha kuwa amezikwa pale pale Dodoma juzi Jumanne, tena baada ya adhuhuri. KWa sisi kuchelewa kuzika na kunyanyasa maiti ni jambo la kawaida haswa sisi watu wa bara
 
How old was he? What was his profile?

I was just trying to make an exception to this statement:

Getting out of hand? It's beyond that my friend. No one in Tanzania can die without controversy......

Talking about age and profile changes the whole perception that no one dies without controversy. I get your point man and unfortunately enough this is how life takes some people.
 
Tenda haki. Kama unaweza kusema tuanzie Chadema, ndio unatuambia uchunguzi ufanyike, ili kama ni Chadema, CCM ijulikane. Lakini kumbuka Chadema, CCM, Polisi, Usalama, JWTZ kama taasisi haziwezi kuua, wanaoweza kuua ni watu ndani ya taasisi hizo. Tumewahi kusikia polisi, wanajeshi wakihusika na uhalifu, juzi mwanajeshi kaua mkewe, halafu tumesikia wanajeshi wamekamatwa na mitambo ya gongo, tukasikia, kiongozi wa CCM kakutwa na nyara za serikali, tukasikia wabunge wa CUF wamefoji document kusafirisha vimada, tukasikia kuna viongozi wa Chadema ni majambazi, huko Tarime kuna wana Chadema ni wahalifu. Uhalifu upo sehemu yoyote hata humu JF kuna wahalifu na watu wanaolipwa kuandika tofauti na wengine wanaoandika kwa kuwa ni sehemu ya "kiburudisho" cha maisha yao. Tusibadili muelekeo, TUTALAANIWA. Ingekua Waislamu, angekwisha kuwa amezikwa pale pale Dodoma juzi Jumanne, tena baada ya adhuhuri. KWa sisi kuchelewa kuzika na kunyanyasa maiti ni jambo la kawaida haswa sisi watu wa bara

Haya ndiyo maneno mkuu Halisi,

Watu walitaka kupaint picha mbaya sana kuwa watu wa Tarime ni wapenda fujo, wasio make sense, hadi kufikia wengine kusema kuwa watagombania rambirambi.

Haya ya kuwazushia wananchi na viongozi wa Chadema wa Tarime kuwa ni majambazi yamesemwa sana kwenye vyombo vya habari vya wanafiki. Kama ilivyokuwa makosa kumuunganisha Chenge na wasukuma wote, ni makosa pia kuwajumuisha wakurya wote kwa vitendo vya watu wachache.

Vyombo vya habari vimejaribu kuanzisha uchonganishi na vurugu kwa raia wa Tarime ili wapigane wenyewe kwa wenyewe (ccm vs chadema) watimbaru vs wanyabasi, wakurya vs wachaga kwenye msiba wa Wangwe lakini wamekosa pa kushika.

Watu wa Tarime hawatamwaga damu kama wanafiki wachache wanavyotaka hili litokee. Kilichowatokea viongozi wa serikali na baadhi ya wabunge waliotaka kuleta unafiki msibani liwe fundisho tosha. Huu msiba ni mkubwa sana na hizi report za kuchanganya toka polisi kuhusu kilichotokea kwa sasa hazitoi msaada bali kulipaka matope jeshi la polisi.
 
NN.. there is nothing more sensational than death; kwani Marilyn Monroe ilikuawaje? JF ilikuwaje, MLK Jr ilikuwaje, it is by very nature sensational.

I guess it's human nature.......

I can't wait for the day when you (Mwanakijiji) die (knock on wood)....not that I 'm wishing you death but all the conspiracy theories and the sensation that will follow afterwards....
 
Tarime palikuwa na mpango uliopangwa tangia jana kuwa watu wa CHADEMA na haswa Mbowe wazomewe na kujenga image kuwa wanahusika na msiba huo na hilo lingeondoa mpango wao wa kutaka ifanyike independent investigation.

Leo asubuhi walipofika huko wakina Mbowe pamoja na viongozi wengine wa vyama vya upinzani wakapokelewa na hakukuwa na hicho walichopanga, sasa kuna juhudi zinafanywa kwa kumshirikisha RPC atoe statement kuwa wamemnusuru Mbowe kuuwawa ,sasa sijajua kama ataitoa wapi ila najua kuwa kuna waandishi wameitwa kwa ajili ya kupata hiyo statement japo kwa umakini mkubwa.

Vyombo vya habari vimechaguliwa mahususi kuwa ni vyombo gani vihusike kupata hiyo statement.

Mtindo huu wa kutaka kutwist mambo huko yanaweza kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa sana ambayo wanaopanga ,na haswa waliokaa nyumbani kwa waziri mmoja wa serikali mjini Dodoma na kuandaa mpango huo mahususi eti kwa vile Mbowe alimshinda Kikwete kura huko Tarime utakuwa na matatizo kwao binafsi.

Vijana waliokuwa wamendaliwa wamesema kuwa wataweka mambo hadharani na kusema mpango huo na haswa baada ya kuona utata wa kifo hiki.

Nawatakia kila la kheri.
 
Tarime palikuwa na mpango uliopangwa tangia jana kuwa watu wa CHADEMA na haswa Mbowe wazomewe na kujenga image kuwa wanahusika na msiba huo na hilo lingeondoa mpango wao wa kutaka ifanyike independent investigation.

Leo asubuhi walipofika huko wakina Mbowe pamoja na viongozi wengine wa vyama vya upinzani wakapokelewa na hakukuwa na hicho walichopanga, sasa kuna juhudi zinafanywa kwa kumshirikisha RPC atoe statement kuwa wamemnusuru Mbowe kuuwawa ,sasa sijajua kama ataitoa wapi ila najua kuwa kuna waandishi wameitwa kwa ajili ya kupata hiyo statement japo kwa umakini mkubwa.

Vyombo vya habari vimechaguliwa mahususi kuwa ni vyombo gani vihusike kupata hiyo statement.

Mtindo huu wa kutaka kutwist mambo huko yanaweza kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa sana ambayo wanaopanga ,na haswa waliokaa nyumbani kwa waziri mmoja wa serikali mjini Dodoma na kuandaa mpango huo mahususi eti kwa vile Mbowe alimshinda Kikwete kura huko Tarime utakuwa na matatizo kwao binafsi.

Vijana waliokuwa wamendaliwa wamesema kuwa wataweka mambo hadharani na kusema mpango huo na haswa baada ya kuona utata wa kifo hiki.

Nawatakia kila la kheri.


Kwa CCM kila kitu ni SIASA.... Na wapinzani nao wajifunze, wangejipanga na kufanya siasa, lakini jambo baya ni kwa CCM kutumia Dola kufanya siasa
 
Tarime palikuwa na mpango uliopangwa tangia jana kuwa watu wa CHADEMA na haswa Mbowe wazomewe na kujenga image kuwa wanahusika na msiba huo na hilo lingeondoa mpango wao wa kutaka ifanyike independent investigation.

Leo asubuhi walipofika huko wakina Mbowe pamoja na viongozi wengine wa vyama vya upinzani wakapokelewa na hakukuwa na hicho walichopanga, sasa kuna juhudi zinafanywa kwa kumshirikisha RPC atoe statement kuwa wamemnusuru Mbowe kuuwawa ,sasa sijajua kama ataitoa wapi ila najua kuwa kuna waandishi wameitwa kwa ajili ya kupata hiyo statement japo kwa umakini mkubwa.

Vyombo vya habari vimechaguliwa mahususi kuwa ni vyombo gani vihusike kupata hiyo statement.

Mtindo huu wa kutaka kutwist mambo huko yanaweza kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa sana ambayo wanaopanga ,na haswa waliokaa nyumbani kwa waziri mmoja wa serikali mjini Dodoma na kuandaa mpango huo mahususi eti kwa vile Mbowe alimshinda Kikwete kura huko Tarime utakuwa na matatizo kwao binafsi.

Vijana waliokuwa wamendaliwa wamesema kuwa wataweka mambo hadharani na kusema mpango huo na haswa baada ya kuona utata wa kifo hiki.

Nawatakia kila la kheri.

Kuna watu wanataka kuanzisha vurugu Tarime kwa visingizio vya msiba wa Wangwe ili kupoteza ukweli wa kilichotokea. Wananchi wa Tarime tumekataa kuwa hatutagawanywa na vyombo vya habari na habari zao za kinafiki na ndio maana viongozi wote wa upinzani na ccm waliokuwa fair wamepokewa vizuri sana ikiwemo suala la Zitto kusikilizwa na wananchi wachache ambao walikuwa too emotional.

Wanasiasa wanaotaka kuleta siasa kwenye huu msiba waache kabisa maana sio jambo zuri. Kwa vile familia na wakazi wa Tarime wamekataa kuzika mpaka uchunguzi mwingine binafsi ufanyike, basi polisi waendelee na kazi yao ya kulinda amani na usalama wa wananchi wote wa Tarime na sio kukubali kutumiwa na wanafiki wachache.
 
Kwani wakuu kweli mtu hawezi kuuwawa kwa kutumia vyuma vizito na gari kweli ikasetiwa accelerator ikaonekana ajali? Mbona kweli hili suala pia halitiliwi maanani?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom