Magabe Kibiti
JF-Expert Member
- Jan 20, 2008
- 292
- 2
Hapo sasa polisi inabidi waanike ukweli kabisa watu saizi wanafuatilia dot baada ya nukta wakituchuuza watakiona cha moto ni bora waweke wazi hiki kifo wamechemka kama mpirani hii ni rafu mbaya wamechemka.
Moto walianza kuuona polisi wa Tarime ambao walitaka kuleta siasa kama kawaida yao. Mimi nawapa ushauri polisi kuwa waendelee kulinda usalama wa wananchi wa Tarime na wasijaribu hata kidogo kukubali kuyumbishwa na wanasiasa na kuingilia kinachoendelea hapa kwenye msiba mkubwa uliowakumba raia wa Tarime.
Ninaamini kuwa watu wa Tarime ni watu makini na hawatafanya mambo ya ajabu kwa kukubali ushawishi wa wanafiki wachache wanaotumia vyombo vya habari TBC1 na magazeti ya Rostam Azizi kutaka kuwavuruga na kuleta fujo.