BongoTz
JF-Expert Member
- Nov 3, 2006
- 272
- 3
Viongozi hao pia walithibitisha habari zilizoandikwa na vyombo vya habari kuwa vurugu zilizotokea siku ya yalipoahirishwa maziko ya Wangwe zilisababisha baadhi ya viongozi kuamriwa na Polisi kuondoka eneo hilo. Hali ilikuwa mbaya sisi wenyewe tuliingizwa kwenye chumba cha maiti kuhemea humo tukakaa dakika 10 na akina Mbowe (Mwenyekiti wa Chadema) ndipo tukaondoka katika eneo hilo, alisema Mrema.
Naye Mbatia alikiri kuwa vijana walikuwa wamebeba silaha za jadi na kama isingekuwa busara ya Polisi na ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Issa Machibya, kulikuwa na uwezekano wa kutokea vurugu. Alisema viongozi wengi wakiwamo wabunge na mawaziri waliruka uzio kutokana na hali kuwa tete kwenye msiba na hiyo inatokana na utata wa kifo cha Wangwe.
Alisema hata fulana zilizoandaliwa kwa heshima ya marehemu zilichomwa moto pamoja na bendera za baadhi ya vyama vya siasa. Hata hivyo hakutaja vyama ambavyo bendera zake zilichomwa moto. Juzi Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, alikanusha habari zilizoandikwa na vyombo vya habari kuhusiana na vurugu hizo. Alizielezea habari hizo kuwa zilikuwa za uzushi zenye lengo la kukiua chama cha Chadema.
Habari yote hii hapa;
ikumbukwe kwamba wanazi wa chama fulani walisema hakupakuwa na tatizo lolote.
Oh, please! And you believe all those craps!!