Invisible, Kiranja:
Kwa maelezo yenu ni wazi kwamba akina Rostam na mafisadi wenzake katika CCM wameamua kuutumia msiba huu na ugomvi uliokuwepo kati ya marehemu na viongozi wenzake kama njia ya kutokea. Hata hivyo mbinu hii mimi hainishangazi kwani inatarajiwa katika uongozi ambao hawana cha kujivunia na wamepoteza sifa za kutawala isipokuwa watumie ghiliba, ujanjaujanja, umafia na mapepo.
Kinanishangaza na kunisikitisha ni hawa watanzania wenzetu wanaofanya kazi ya uandishi wa habari katika haya magazeti yaliyoandika hizi habari; iweje hawa wenzetu wakubali kuuza utu na uhuru wao na kukubalika kutumika kiasi hiki? Kwa nini waandishi wa habari watanzania wamekubali kuwekwa kwenye mfuko wa mtu mmoja anayeitwa Rostam kwa visenti? Kwa nini wameamua kujidhalilisha namna hii?
Ni hawahawa waandishi waliowalisha watanzania sumu pale walipomvalisha JK ngozi ya malaika kiasi kwamba watanzania kwa mamilioni wakapagawishwa, wakiwemo viongozi wetu wa dini hadi wakaenda mbali na kusema JK ni chaguo la Mungu. Leo hii JK mambo yamemshinda, sio kwa kupenda bali kwa kuwa hakuwa na bado hana sifa alizopewa, wamebaki kukodoa macho, na visenti walivyopewa walishakula na wala havikuwasaidia kupeleka watoto wao shule. Lakini bado hawakujifunza na wanaendelea kuwalisha watanzania sumu ya habari kwa ajira ya visumuni.
Mimi nasema katika kazi kubwa tuliyo nayo huko mbele ni kuwatoa kwenye umateka hawa wenzetu wanaofanya kazi ya uandishi wa habari. Ni kazi ngumu lakini lazima tuifanye.