Kibatala: Wanaopinga Katiba Mpya wana Maslahi Binafsi

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,227
35,151
Wakili msomi bwana Peter Kibatala leo katika 360 ya clouds TV amefunguka kisomi kuhusiana na katiba mpya.







"Katiba mpya ni hitajio la watanzania wengi. Wanaopinga, ni kwa sababu tu ya maslahi binafsi yatokanayo na katiba iliyopo." -- amesisitiza wakili huyo.

Zaidi sana anasema Kibatala:

1. Si kweli kuwa katiba mpya inatakiwa na wanasiasa tu.
2. Wanaopinga kuendelezwa kwa mchakato wa katiba mpya ni wale tu wa kunufaika kibinafsi na hii iliyopo.
3. Umuhimu wa kuzifanyia marekebisho ya kisheria tume za chaguzi ya Taifa na ile ya Zanzibar zitahusika kwenye kuivusha katiba hiyo mpya.
4. Kumalizia kiporo cha mchakato uliobakia kitampa Mama Legacy ya pekee na ya kudumu.
5. Vuguvugu la kudai katiba lililoanza Halizuiliki tena.
6. Kama ilivyo kwa mbegu, walioko madarakani inabidi waoze ili yapatikane mazao mengi
7.Kikwazo ni walioko madarakani kwani wana vingi vya kupoteza kwa ujio wa katiba mpya.

Hoja hupingwa kwa hoja. Barikiwa sana wakili msomi.
 
Lipo kundi jingine la watu ambao wanaonekana kupinga suala la katiba mpya hadharani lakini deep down inside wanaitaka.
Hawa ni wanafiki kwani hata jaji Warioba alipomaliza kuwakilisha rasimu ya Katiba mpya bungeni, wengi wa wabunge wa CCM walimpogeza Mimi nikiwa naangalia luninga yangu; wanafiki tu tena wanasahau wameajiriwa na wananchi ambao ndio wanaotaka katiba ya uajibikaji.
 
Je, wanaotaka katiba mpya hawana maslahi yao binafsi na kinyume chake?
Kiswahili kimekuwa kigumu kiasi hiki?

Maslahi ya watu kwa sababu ya njaa za matumbo yao na familia zao. Vipi hayo yanaweza linganishwa na maslahi haya:

Mwananchi wa kawaida anayejielewa, anayekataa kuendelea kubambikiziwa kesi, kuendelea kudhulumiwa, kuendelea kubebeshwa mizigo ya kodi za wengine nk.

Au hata yule anayetaka mihimili ya utawala iliyo na uhuru kamili, anayetaka usawa, anayetaka uwajibikaji, anayetaka mawazo yake kusikilizwa nk.

Seriously, haikuingii akilini kuwa kwanini hapo pana tofauti?

Au ni ile mambo ya kujitia hamnazo?
 
Wakili msomi bwana Peter Kibatala leo katika power breakfast ya clouds FM amefunguka kisomi kuhusiana na katiba mpya.

"Katiba mpya ni hitajio la watanzania wengi. Wanaopinga, ni kwa sababu tu ya maslahi binafsi yatokanayo na katiba iliyopo." -- amesisitiza wakili huyo.

Hoja hupingwa kwa hoja. Barikiwa sana wakili msomi.
Anachoongea Peter Kibatala leo na wanachoongea Chadema ni vitu viwili tofauti, Kibatala anaongelea kumalizia mchakato wa Katiba pendekezwa lakini Chadema hawaongelei kumalizia mchakato. Kwa wajibu wa Mheshimiwa Mbowe "tunamtaka Rais aunde tume ya Katiba..." tume ambayo kisheria ilishamaliza muda wake, kilichosalia ni huo mchakato wa kutangazwa gazeti ni na Tume ya Uchaguzi kusimamia mchakato wa kura ya maoni. Maana yake Katiba Mpya ipo katika mhutasari wa KATIBA PENDEKEZWA Kilichosalia ni mchakato wa kuipitisha au kuikataa.
 
Hawa ni wanafiki kwani hata jaji Warioba alipomaliza kuwakilisha rasimu ya Katiba mpya bungeni, wengi wa wabunge wa CCM walimpogeza Mimi nikiwa naangalia luninga yangu; wanafiki tu tena wanasahau wameajiriwa na wananchi ambao ndio wanaotaka katiba ya uajibikaji.
Hakuna binadamu wa ovyo kama Wabunge wa Tanzania. Wakiwa bungeni wanapitisha mambo ya ovyo ovyo utadhani watakuwa Wabunge daima. Wakitoka wao ndo miongoni mwa waathirika wa hizo sheria. Juzi Ndugai anashangaa sheria ya kutaifisha mifugo ilipitishwa yeye akiwa amelala au amezimia?
 
Wanao taka katiba mpya wana maslahi binafsi? ulisha isoma rasimu ya katiba mpya lakini,nani waliipitisha,na ni kina nani wanaikataa majibu yako wazi ni CCM sasa hawa tuwaiteje?
Hakuna asie na maslahi binafsi kwenye kila jambo, kaa hapo ufikiri kuwa wanafanya kwa ajili ya nchi ahahaa!
 

Similar Discussions

22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom