Kibanda azidi kufunguka, CHADEMA kikaangoni

Kibanda azidi kufunguka, CHADEMA kikaangoni

Dogo unajua TISS ni nini maana majibu yako yanautata inawezekana ludovic ni cdm lakini ni memba wa TISS UMEELEWA?
we mtoto acha kuingia kichwa kichwa maana naona hujaelewa umedandia treni kwa mbele.
Nasema hivi: Ludovic alimrekodi kiongozi wa chadema akipanga mauaji, hajawarecodi TISS!
 
Mkuu hauko serious.
Dr Slaa anawezaje kuhojiwa kwa volunteers wa chama walioko kila kona ya nchi hii. Unajua maana ya volunteer? Maana yake ni mtu anayejitolea kufanya kazi za chama bila malipo. Watu wa namna hii wako ktk kila ngazi- usiwapotoshe watu humu bila sababu. Wako wanaojitolea au kuvolunteer ktk ngazi za kijiji/mtaa, kata, wilaya mkoa au Taifa. Na watu hawa huwezi kuwatawala ktk utendaji wao wa kila siku kwa sababu hujawaajiri.

Kwa hiyo, volunteer anaweza kwenda ktk eneo analojitolea mara mbili kwa wiki kwa wiki au mara 1 kwa mwezi ktk ngazi yo yote. Sasa, kutaka kumhoji Dr Slaa kwa sababu ya Volunteer ambaye hujatumbia alitolea mara ngapi kwa mwezi au mwaka makao makuu ni upotoshaji wa makusudi ambao hauwezi kuijenga ccm.
Hizi spinning zako za meaning of volunteer wa CHADEMA haziwezi kusimama kwenye macho ya sheria.

Ninaamini unachokisema ndicho unachokielewa kutokana na akili na fikra zako. Kama ndiyo hivyo, I hope your ready after Lwakatare case to eat CHADEMA humble pie.

Kama hiki unachokisema ni kutokana na kumkopesha mtu mwingine akili na fikra zako basi hili wewe ni mtu wa kusikitikiwa na kusamehewa kwa sababu huwezi kuupambanua ukweli katika network iliyo complex ambayo imewekwa na Dr.Slaa ndani na nje ya chama. Sana sana , you just have to get ready for political bewilderment and bumper ride.
 
Kwani mtu akifanya kazi kwenye chama cha upinzani hawezi kuwa agent wa TISS??

Hebu kamuulize Mrema, Bagenda na wenzao...!!

ndiyo hapo sasa ,tena unaweza kuta alikuwa ni undercover agent kwa kazi maalumu huko chadema ambalo hitimisho lake ndiyo hii cheap propaganda.
 
Nadhani kibanda nae anatumika na serikali ya ccm ktk kuididimiza CDM hata huyu ludovick a takuwa ashanunuwa
 
Ha ha ha Hamy D leo uneingia na mguu mbaya, kila kitu kinafahamika hakuna jipya kwetu ila kwako.......nafikiri ushapata somo kuwa uncle Nchemba ndio alimtuma Ludo so CCM wanayo script yote ya hii movie.
 
Sasa kama ishu ndo ikohivyo sasa mbona polisi wanasema hawajaweza kumkamata mtu yeyote wakati Kibanda anawafahamu? Wafanye mahojiano na Kibanda na Ludovick.
 
Wana-JF!!

Mnamkumbuka mhariri ABSALOM KIBANDA? AMBAE ALITEKWA NA KUTESWA?, amesema yafuatayo kuhusu wahusika ambao walimfanyia vitendo hivyo vya kinyama ambavyo vimempa ulemavu wa kudumu wa jicho lake.
Ndugu unaweza kushabikia habari hii ukidhani watakao umbuka ni CDM kumbuka mahusiano ya Ludovick na Mwigulu ambayo nina uhakika yatatufikisha kupata kitu ambacho kitakuacha kimya na hautathubutu kushabikia habari hii.
 
KIBANDA AKIWA AFRIKA YA KUSINI ALITANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE - JIMBO LA RUNGWE MASHARIKI 2015 na thread imo humu JF.

Na mchuano wa mchujo ndani ya chadema atashindana na YUSUFU ASUKILE na OSCAR MWAMBENE!!!... HUYU JAMAA KWAO NI RUNGWE KARIBU NA KIWIRA.

kwa hiyo???
 
Siku ya tukio Ludovick alikuwa na Mjengwa. Alitoa maelezo yake mwenyewe facebook. Kawaida kwenye matukio ya namna hii Mjengwa ndie angekuwa wa kwanza kuunganishwa naye kadiri ya maelezo ya Ludovick mwenyewe.
.
'Leo usiku, yapata saa tano na nusu, niliachana na Maggid Mjengwa maeneo ya Shekilango tukitokea Rose Garden. Yeye alielekea hotelini alikofikia sehemu fulani Kariakoo nami nikasubiri kigari kuelekea nyumbani kwangu.

Hapo Shekilango, magari yalichelewa kidogo, pembeni ilipaki bajaji ikiwa na watu wawili na dereva ndipo wakaniambia twende tuchangie mia tano tu kwenda Ubungo Mataa, nikakaa katikati ya hao jamaa.

Ghafla wakakata kona na kuanza kuelekea Mabibo huku wakiulizana kama wako kamili na mwingine kujibu yuko kamili. Nikajua tayari niko mikononi mwa majambazi na sikujua wako kamili namna gani, kwa hiyo nikaamua kuwa mtulivu.

Tulipofika relini karibu na Mabibo wakanipokonya begi lakini, hawakulifungua. Ndani yake kulikuwa na laptop, toshiba kubwa na chaji yake, kamera ndogo ya digital na USB yake, modem ya zantel na card reader. Tulipofika maeneo ya Loyola Sekondari, nikawasihi wanishushe ili nirudi mwenyewe, wakaniambia safari ile inaishia Jangwani.

Nikaingiwa na wasiwasi mkubwa na nia yao hasa, maana wameshanipokonya begi kwa nini wasiniachie? Lakini niliendelea kuwa mtulivu ili kutowaprovoke.

Tulipovuka Kigogo mwisho kwenye giza karibu na msikiti, wakasimama pembeni ya barabara na kuniamuru kushuka, nikashuka na kuanza kuwadai begi langu, ndipo mmoja akasema wamekuwa wastaarabu mimi naanza kuwadharau. Ghafla akanivuta kwa nguvu kunirudisha kwenye kibajaji akamwambia mwenzie wanisachi kama nina vitu vingine, wakanisachi na kuchukua pesa, nilikuwa na elfu 35 na simu mbili ndogo za nokia moja yenye line mbili.

Kisha mmoja akatoa ‘order' nivuliwe nguo. Nikavuliwa viatu, T-shirt na suruali nikabaki na nguo za ndani pekee. Wakanishusha na kuniacha hapo.

Kurudi nyuma kama hatua kumi tu ndipo kituo kidogo cha polisi Kigogo nikaanza kutoa maelezo hapo kwa zaidi kama ya saa mbili nikiwa uchi na nguo za ndani tu. Nikiwa hapo nikasikia polisi wakiwasiliana juu ya tukio la kupigwa vibaya Absalom Kibanda, kwenye redio calls.

Ilikuwa yapata saa nane, baada ya kuchukuliwa maelezo polisi walinipatia gari nikaelekea hotelini kwa Maggid, ambaye saa kumi aliamshwa na kunichukulia chumba hapo nikapumzika. Ameniazima nguo zake ndizo nimevaa bado hadi sasa naelekea kituo cha Polisi Magomeni kwenda kupewa mpelelezi wa kesi yangu. Namba ya kesi yangu Kigogo ni KIG/RB/318/2013, wizi kutoka maungoni.'


Wakati Ludovick akiwa ametoa maelezo hayo kwa jamii kupitia mitandao ya kijamii, polisi wameshindwa kuthibitisha taarifa za kutekwa, kuporwa na kupokea taarifa yake aliyodai kuitoa kituo kidogo cha polisi Kigogo.

Polisi katika kituo kidogo cha Kigogo waliohojiwa na MTANZANIA Jumapili kuhusiana na taarifa za Ludovick, walionekana kurushiana mpira kuzizungumzia.

Wapelelezi walio mahiri wangeunganisha Ludovick alikuwa na nani siku hiyo kabla ya tukio na baada ya tukio.

Tumeona mara baada ya tukio hilo Ludovick alienda Iringa kwa kuitwa na Mjengwa, na Polisi walimkamata akiwa Iringa kwa kazi za Mjengwa.

Ndugu zangu,
Usiku huu nikiwa kwenye shughuli ya shule ya watoto wangu pale Highlands Hall Iringa nilifikiwa na habari kuwa Kijana Ludovick amekamatwa na polisi kuhusiana na tuhuma za kuhusika na kuteswa mwandishi Absalom Kibanda.

Namfahamu kijana Ludovik tangu akiwa Chuo Kikuu ( DUCE). Ni mmoja wa Watanzania wengi walionifahamu kupitia kazi zangu za magazetini.

Kwangu Ludovick ni kijana mtaratibu na mpole sana, na hata niliposikia habari hizi kwa namna fulani nimeshtushwa nazo.

Ludovick ambaye amekuwa akiishi Dar ni mmoja wa vijana waliokuwa wakinisaidia kwa kujitolea kwenye kazi zangu za mitandaoni, hususan kwenye Mjengwablog na website ya Kwanza Jamii. Amekuwa na mchango mkubwa, na hata katika miezi ya karibuni,ndiye yeye aliyekuwa akifanya kazi ya kuingiza magazeti kwenye Mjengwablog kila asubuhi.

Akiwa Dar na mimi nikiwa Iringa, Ludovick hakuwa mwajiriwa wangu kama wanavyodhani wengine, bali , amekuwa ni mmoja wa vijana waliokuwa tayari kunisaidia kwa kazi za hapa na pale ikiwamo kunipelekea invoice kwa watangazaji kwenye Mjengwablog.

Mara nyingi nimekuwa nikimtambulisha kama ' Msaidizi wa Mwenyekiti'.

Na jana nilimwomba aje Iringa aniletee vitabu vyangu vya invoice na risiti kwa vile nilitarajia ugeni wa kutoka TMF- Mfuko wa Ruzuku kwa vyombo vya habari. Kwamba huenda vitabu hivyo vingehitajika wakati wa mazungumzo na watendaji wa TMF yaliyofanyika leo asubuhi.

Hata hivyo, katika hili lililomtokea, siwezi hapa kumtetea wala kumtia hatiani. Maana, naye ni binadamu kama wengine, siwezi kusema kuwa ninamfahamu sana. Kwa vile yuko mikononi mwa vyombo vya usalama , nina imani, kuwa vyombo hivyo vitafanya kazi yake ili kutusaidia katika kupata ukweli wa jambo zima.

Na kama ni kweli kwa namna yoyote ile itathibitishwa kuwa ameshiriki njama za kupanga mikakati hiyo ya kigaidi, basi, ahukumiwe kwa dhambi hiyo.
Ni mimi:
MAGID MJENGWA
Credit: Mjengwablog

Hatimaye Mjengwa alitoa tamko rasmi
TAARIFA RASMI KUTOKA Mtandao Wa Kijamii Wa MJENGWABLOG

Sunday, 17 March 2013 | Written by Mjengwa Blog

Ndugu zangu,
Kutokana na kuwepo kwa taarifa rasmi za kipolisi zenye kumtuhumu Ludovic Joseph kuhusika na matukio ya kigaidi.

Uongozi wa Mtandao wa Kijamii wa Mjengwablog unasitisha rasmi, kuanzia leo Jumapili, Machi, 17,2013, kuwa na Ludovick Joseph kama msaidizi wa Mtandao wa Kijamii wa Mjengwablog na website ya Kwanza Jamii.

Maggid Mjengwa,
Mmiliki wa Mjengwablog /Kwanzajamii

Kwa hiyo Ludo alikuwa ana shughuli nyingi tu. Chadema alikuwa Volunteer, kwa Mjengwa alikuwa Msaidizi wa Blog.

Katika tukio la Kibanda sijui wapi pa kuanzia uchunguzi hapo, yule waliyekuwa naye siku hiyo na ambaye baadaye alimwita Iringa au kule ambako ni volunteer!

Tafakari mwenyewe na usiache akili ya mwingine ikuamulie
 
Hizi spinning zako za meaning of volunteer wa CHADEMA haziwezi kusimama kwenye macho ya sheria.

Ninaamini unachokisema ndicho unachokielewa kutokana na akili na fikra zako. Kama ndiyo hivyo, I hope your ready after Lwakatare case to eat CHADEMA humble pie.

Kama hiki unachokisema ni kutokana na kumkopesha mtu mwingine akili na fikra zako basi hili wewe ni mtu wa kusikitikiwa na kusamehewa kwa sababu huwezi kuupambanua ukweli katika network iliyo complex ambayo imewekwa na Dr.Slaa ndani na nje ya chama. Sana sana , you just have to get ready for political bewilderment and bumper ride.

Wewe mwanadiwani najua una hasira kubwa sana na mimi kwa sababu nimegusa Mwigulu Nchemba NA nitaendelea kumwanika. Wewe huku JF kwa nini unongoza kwa kumtetea Mwigulu Nchemba kuliko hata ccm yenywe? Kwani mwigulu ni nani wako?

Pili, hiki ulichokiandika hapa mkuu bado hujaelweka na umezungumzia mambo mengi sana mpaka nashindwa kuelewa. Nakushauri utoe ushahidi wa hicho unachokisema.
 
Mkuu HAMY-D leo umebuma kamanda, naona unajaribu kuongeza chumvi kwenye udaku wako.
 
Last edited by a moderator:
Wewe mwanadiwani najua una hasira kubwa sana na mimi kwa sababu nimegusa Mwigulu Nchemba NA nitaendelea kumwanika. Wewe huku JF kwa nini unongoza kwa kumtetea Mwigulu Nchemba kuliko hata ccm yenywe? Kwani mwigulu ni nani wako?

Pili, hiki ulichokiandika hapa mkuu bado hujaelweka na umezungumzia mambo mengi sana mpaka nashindwa kuelewa. Nakushauri utoe ushahidi wa hicho unachokisema.
naona mmekutana, ww unamtetea sana slaa na mwenzako anamtetea mwigulu..hapo ni sawa na mbwa na paka wamekutana
 
Kwani mtu akifanya kazi kwenye chama cha upinzani hawezi kuwa agent wa TISS??

Hebu kamuulize Mrema, Bagenda na wenzao...!!

Asiende mbali sana Chadema tunae Mabere Marando na ni haki yake kuwa katika chama chochote
 
Mbona mwigulu haji kuchangia hata sentensi moja tu? Ritz? Chama?


Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
attachment.php
 
acheni kukumbatia waovu, wauwaji, watembea na sumu, warusha mabomu na watishia watu kwa bastola

Labda nitumie maneno mengine inawezekana utanielewa, kwa serikali yoyote makini yenye jeshi, usalama wa taifa nk isingeruhusu raia wake kunyanyaswa na kikundi chochote kutoka ndani au nje ya mipaka yake. kwa mtazamo wangu matukio hayo ya mauaji, utekaji, utesaji ulipuaji mabomu, na uvunjifu huu wa sheria usingetokea kama kusingekuwa na mkono wa serikali. BELIEVE ME OR NOT ONLY THE GOVERNMENT CAN STOP ALL THESE PROBLEMS BY DOING THE RIGHT THINGS TOWARDS HIS PEOPLE
 
Back
Top Bottom