Kero: George Marato wa ITV

Kero: George Marato wa ITV

Wengine ni wivu tuuu. Napenda Sana mtu kuwa unique. Hawa wanahabari wawili hasa hasa huyu wa michezo inaonesha walivyo iva ktk tasnia yao. Ni dalili ya kujiamini. Napenda sana. Ni sawa na wale wa DW SAA 7
 
Yani nafsi yangu inawapenda sana MARATU na KIVUYO!
 
Damn it. Hata uchawi ulianzanga hivi hivi yaani mtu kabuni ki identity chake anatafuta riziki wewe huku kisa biashara zako zimekwama unamchukia.
 
Kwani weeeeeewee kinakuuuuuuuuma nini? (katika sauti ya george}
 
Elimu,elimu elimu wakenya tutawafukuza sana na hatuta wakamata na ndio maana hapa wako wengi tu wanapiga kazi uliza kenya kuna wa tz wangapi wanafanya kazi huko-ni aibu.
Watu kama nyie huwa mnaboa sana, wakenya wakenya wewe fanya yako, ndio maana wanawadharau Kwani kila kitu lazima utaje wakenya ndio wanaokulisha au? Mbona ni binadamu km wewe tu, wewe unawaona km special saana au??
Kama unawapenda sana na wewe si uwe mkenya sasa.
 
Wasiompenda George maratu ni wale watu wenye msongo wa mawazo na wanaochukulia kila kitu serious.

Mimi namwelewa sana
 
Huyu ripota kwa kweli huwa nikisikia tu sauti yake nabadili chanel yani anatafuta attention kwa nguvu sana na utofauti usio na msingi. Yani ananikera kama sauti ya mbu ukiwa umelala . So unprofessional.

Usihangaike na huyu hata darasa la saba hakufika

Amewahi kuona ripota gani wa kuheshimika anapoteza muda kwa kuvuta maneno kama yeye? Jirekebishe unakera sana jinsi unavyovuta makusudi maneno yako. Hata haipendezi. Kero sana. Yani.
 
Simpendi hata kidogo,sijui hata kwenye usaili alipitaje
Ukikutan naye utashangaa sana kuona kuwa ndo huwa anavuta sauti namna ile,

Kwenye maisha ya kawaida anaongea kawaida kabisa, tena ni miongoni mwa watu wanaoongea haraka haraka!
 
Kumbe watz wanamfahamu Gatete Njoroge wa Citizen,ningependa sana kuwatazama watangazaji wa tv. za tz nao pia huku Kenya. Sasa sijui kama mnamfahamu huyu Hassan Juma wa KTN ananiudhi sana na bass yake ingine feki feki,duh!meno yake yote yataanguka chini siku moja,nangoja hilo sana,haaasaaaaan juuumaaaaaaaaaah,ktn michezo!Argh!
Hiki sio kiswahili cha Kenya
 
Umerogwa wewe, au una undugu na yesu - ney wa mitego
Uyo mwandishi napenda nimsikie, na irene owoya nae pia nampenda akitangaza
 
Back
Top Bottom