Kauli za LATRA kuhusu namba za magari, kuelekea 17 Machi zimelenga kumhujumu Mama?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,882
35,891
Kumekuwa na matamko tata kutokea LATRA kuhusu magari yenye namba D na E kufanywa ndiyo yaliyo magari pekee.

Hali hii si ya kuvumiliwa hata kidogo. Kesho itakuwa gari kuingia Dar na labda hata kuthubutu tu kuwapo Tanzania ni F na G peke yake. Nani ajuaye?

Ni kawaida kwa wanaojidhania kuwa wako salama au kuwa haiwahusu kuonekana wakikenua (meno nje) wasijue ukiukwaki wa haki za wengine ni sawa na kula nyama ya mtu.

"Taratibu haitakuwa magari ya abiria peke yake, kama tukichagua kukaa kimya."

Kwani kwenye gari kinachogomba ni namba za usajili au ubora wake? Vipi kama mtu alinunua gari lake zamani akaamua kuliweka ndani bila kulitumia hata kwa miaka 20? Hilo nalo LATRA hawalitaki?

Kwanini LATRA wangependa watu kununua magari mapya (kama mazuzu tu) hata kama waliyo nayo ni mazima? Au kwanini LATRA wangependa wamiliki wa magari kuyatupa au kuyaondoa magari yao kimkumbo mkumbo tu hata kama ni mazima?

Kwani LATRA wamekuwa na maslahi gani kwenye biashara ya magari? Kwamba wamekuwa madalali, washirika au wauza magari? Kwani hata magari haya yanatengenezwa hapa nchini? Vipi kuwa mawakala wa mabeberu?

"Ikumbukwe kununua gari au chochote na hasa inapokuwa si kutoka kwenye viwanda vya ndani ni kuwaneemesha mabeberu.'

Cuba yenye kutupa sisi misaada, ni moja ya nchi za kizalendo zenye kujua umuhimu wa kutunza kila walivyo navyo; ili kuepuka unyonywaji na hasa huu wa kupitia katika manunuzi yasiyo ya lazima kutoka nje:

1b847c_5415749b717047fd87eb26fac9310d1a_mv2.jpg


Pichani ndiyo yaliyo magari katika ya maana yaliyojazana kwenye barabara bora kabisa za Havana, Cuba. Magari ya miaka 1950s huko. Spares zake zote ni kutokea katika soko lao la ndani.

Huku kufunguliwa kwetu nchi kwa lazima ya kununua nje, ni ili mabeberu yavune yawezavyo, si ndiko alikokupinga sana bwana JPM (RIP)?

"LATRA mnataka magari mapya pasipo na sababu? Vipi, kwani mmeahidiwa nini na nani wenzetu?"

Kwa hakika kuelekea 17 March mnatufanya kumkumbuka sana shujaa wetu yule tuliyembeza wengine bila kujua. Kwa hakika angekuwapo huu upuuzi wa D na E usingekuwapo.

Pumzika kwa amani baba Magufuli uliowaachia nchi leo wanatusukuma kwa mabeberu kama vipi tukakamuliwe kweli kweli.

"Kwa hakika kwa mema tutakumbuka."
 
Hujaeleweka mkuu kwamba magari namba C kushuka chini hayatakiwi barabarani au... mbona hili agizo halitekelezeki ni kama wale jamaa waliokurupuka na kusema watu watoe tinted kwenye vioo vya magari.

1. Wenzetu wanatunza vyao; Cuba magari ya 1950s yako barabarani.

2. Dar es Salaam, Tanzania wanataka magari mapya kila mwaka na yanunuliwe kutoka nje.

3. Tutakuwa tumerogwa, siyo bure!
 
Hujaeleweka mkuu kwamba magari namba C kushuka chini hayatakiwi barabarani au... mbona hili agizo halitekelezeki ni kama wale jamaa waliokurupuka na kusema watu watoe tinted kwenye vioo vya magari.
Ugumu wa nchi hii tunauendekeza wenyewe kwa kuyaona na bado tukaendelea kujidanganya kuwa hayatuhusu. Hadi pale yatakapotukuta malangoni.
 
Ni namna ya kivivu ya kufanya kazi.

Njia sahihi ilikuwa kukagua gari, lakini LATRA wanajua itatembea rushwa na kila gari itakayokaguliwa itaonekana inafaa.

Kwahiyo kukata mzizi wa fitna ni kumaliza tatizo la rushwa, jambo ambalo ni 'unrealistic'.

Mwisho wa siku wanalazimika kwenda na hiyo short-cut ya kivivu ya kuyachuja magari kwa namba za usajili (uzee).
 
Kila kitu ni siasa? Nchi ya kipuuzi sana hii, kama ndio sheria zao ulitakaje? ndio maana miji yetu ni michafu saba na inanuka kabisa na ukiuliza unaambiwa hao ni wanyonge waachwe. upumbavu
 
Ni namna ya kivivu ya kufanya kazi.

Njia sahihi ilikuwa kukagua gari, lakini LATRA wanajua itatembea rushwa na kila gari itakayokaguliwa itaonekana inafaa.

Kwahiyo kukata mzizi wa fitna ni kumaliza tatizo la rushwa, jambo ambalo ni 'unrealistic'.

Mwisho wa siku wanalazimika kwenda na hiyo short-cut ya kivivu ya kuyachuja magari kwa namba za usajili (uzee).

Kama tatizo ni rushwa kwanini TAKUKURU au serikali wangali ofisini?

Mawazo yangu "mwanzo wa ngoma ni lele." Tusipokomaa kesho itakuwa F na G. Keshokutwa magari yote yakiwamo binafsi.

Muda wa kuwakomalia ilikuwa sasa. Tusikubali haki ya mtu yeyote kuchezewa.

Kama tunataka Katiba Mpya, Tusiionee "Haya" Haki ya awaye yote

Walapo nyama ya mtu huwa hawaachi.
 
Kila kitu ni siasa? Nchi ya kipuuzi sana hii, kama ndio sheria zao ulitakaje? ndio maana miji yetu ni michafu saba na inanuka kabisa na ukiuliza unaambiwa hao ni wanyonge waachwe. upumbavu

1. Siasa na upuuzi ni huu wa kwako. Sheria zao ni kutoka mbinguni?

2. Kwamba sheria zao? Kumbe wao ni nani, miungu?

3. Ninyi ndiyo haya mapoyoyo meno nje mlioangaziwa kwenye mada:

Ni kawaida kwa wanaojidhania kuwa wako salama au kuwa haiwahusu kuonekana wakikenua (meno nje) ...

Bila shaka ulipo ulikuwa kwenye kukenua, hadi uguswe binafsi.

4. Eti miji michafu.

5. Bure kabisa!
 
Mama yenu kila kitu anahujumiwa, nini maana ya kuwa mama sasa??!!, ana macho kila mahali lakini haoni, ana masikio kila mahali lakini hasikii, ni kipofu na kiziwi, hatoshi hapo alipo. Hii nchi haiwezi kuendeshwa kwa kurembua rembua, we need a Benevolent dictator, hizo 4R zake hazina uhalisia kwenye nchi ya dunia ya 3
 
Hujaeleweka mkuu kwamba magari namba C kushuka chini hayatakiwi barabarani au... mbona hili agizo halitekelezeki ni kama wale jamaa waliokurupuka na kusema watu watoe tinted kwenye vioo vya magari.
Nadhani mtoa mada ana machungu sana au hasira sana ! Tamko la latra linahusu magari hasa daladala zitakazopewa kibali kutumia kituo kipya cha mabasi mwenge….!

Latra wameweka utaratibu kuwa magari kuanazia namba DTX kwenda juu ndio yatapewa kibali cha kuchukua habaria au kutumia kituo cha mabasi kipya cha Mwenge!
 
Mama yenu kila kitu anahujumiwa, nini maana ya kuwa mama sasa??!!, ana macho kila mahali lakini haoni, ana masikio kila mahali lakini hasikii, ni kipofu na kiziwi, hatoshi hapo alipo. Hii nchi haiwezi kuendeshwa kwa kurembua rembua, we need a Benevolent dictator, hizo 4R zake hazina uhalisia kwenye nchi ya dunia ya 3

1. Kwa hakika nchi haiwezi kutembezwa ubora wa magari ukisomwa kwenye plate number.

2. Tunaandika hivi ajue ni kwanini tunakuwa na matatizo naye.

3. Kwamba kama hata goli hili wazi halioni (analikataa) na bado hajishughluishi kuoana VAR inasema je?!

4. Honestly Lucas mwashambwa, refer huyu hatuwezi kumwelewa!
 
Kumekuwa na matamko tata kutokea LATRA kuhusu magari yenye namba D na E kufanywa ndiyo yaliyo magari pekee.

Hali hii si ya kuvumiliwa hata kidogo. Kesho itakuwa gari kuingia Dar na labda hata kuthubutu tu kuwapo Tanzania ni F na G peke yake. Nani ajuaye?

Ni kawaida kwa wanaojidhania kuwa wako salama au kuwa haiwahusu kuonekana wakikenua (meno nje) wasijue ukiukwaki wa haki za wengine ni sawa na kula nyama ya mtu.

"Taratibu haitakuwa magari ya abiria peke yake, kama tukichagua kukaa kimya."

Kwani kwenye gari kinachogomba ni namba za usajili au ubora wake? Vipi kama mtu alinunua gari lake zamani akaamua kuliweka ndani bila kulitumia hata kwa miaka 20? Hilo nalo LATRA hawalitaki?

Kwanini LATRA wangependa watu kununua magari mapya (kama mazuzu tu) hata kama waliyo nayo ni mazima? Au kwanini LATRA wangependa wamiliki wa magari kuyatupa au kuyaondoa magari yao kimkumbo mkumbo tu hata kama ni mazima?

Kwani LATRA wamekuwa na maslahi gani kwenye biashara ya magari? Kwamba wamekuwa madalali, washirika au wauza magari? Kwani hata magari haya yanatengenezwa hapa nchini? Vipi kuwa mawakala wa mabeberu?

"Ikumbukwe kununua gari au chochote na hasa inapokuwa si kutoka kwenye viwanda vya ndani ni kuwaneemesha mabeberu.'

Cuba yenye kutupa sisi misaada, ni moja ya nchi za kizalendo zenye kujua umuhimu wa kutunza kila walivyo navyo; ili kuepuka unyonywaji na hasa huu wa kupitia katika manunuzi yasiyo ya lazima kutoka nje:

View attachment 2934577

Pichani ndiyo yaliyo magari katika ya maana yaliyojazana kwenye barabara bora kabisa za Havana, Cuba. Magari ya miaka 1950s huko. Spares zake zote ni kutokea katika soko lao la ndani.

Huku kufunguliwa kwetu nchi kwa lazima ya kununua nje, ni ili mabeberu yavune yawezavyo, si ndiko alikokupinga sana bwana JPM (RIP)?

"LATRA mnataka magari mapya pasipo na sababu? Vipi, kwani mmeahidiwa nini na nani wenzetu?"

Kwa hakika kuelekea 17 March mnatufanya kumkumbuka sana shujaa wetu yule tuliyembeza wengine bila kujua. Kwa hakika angekuwapo huu upuuzi wa D na E usingekuwapo.

Pumzika kwa amani baba Magufuli uliowaachia nchi leo wanatusukuma kwa mabeberu kama vipi tukakamuliwe kweli kweli.

"Kwa hakika kwa mema tutakumbuka."
Naota si kuwa nasoma! Huyu ni wewe brazaj mbaya wa JPM aliyefurahia kifo chake! Nadhani naota na nikiamka sitauona uzi huu
 
Nadhani mtoa mada ana machungu sana au hasira sana ! Tamko la latra linahusu magari hasa daladala zitakazopewa kibali kutumia kituo kipya cha mabasi mwenge….!

Latra wameweka utaratibu kuwa magari kuanazia namba DTX kwenda juu ndio yatapewa kibali cha kuchukua habaria au kutumia kituo cha mabasi kipya cha Mwenge!

Marekebisho tafadhali kulikoni nikuache kupotosha lolote hali ningalipo?

1. Mleta mada hana "machungu sana wala hasira" kama unavyodhani bila shaka kutokea LATRA pale.

2. Nina mashaka kuwa utaratibu huu wa LATRA ni wa kibaguzi usiokuwa na chembe ya haki.

3. Hapo #2 nimeweka sababu za wazi.

4. Wasiwasi wangu hii ni mwanzo tu wa kufikia kwenye magari yote yakiwamo ya binafsi kupigwa kalamu baadaye.

5. Hapo #4 ni wangapi wenye uwezo wa kununua gari jipya kila mwaka?

6. Kumbe ya zamani hata kama ni mazima yakatupwe wapi?
 
Hao latra wako chini yao, kama anaona wanamhujumu ai awatoe? Kwanini mnamfanya victim? Km yanafanyika anayaangalia bas kabariki
 
Kumekuwa na matamko tata kutokea LATRA kuhusu magari yenye namba D na E kufanywa ndiyo yaliyo magari pekee.

Hali hii si ya kuvumiliwa hata kidogo. Kesho itakuwa gari kuingia Dar na labda hata kuthubutu tu kuwapo Tanzania ni F na G peke yake. Nani ajuaye?

Ni kawaida kwa wanaojidhania kuwa wako salama au kuwa haiwahusu kuonekana wakikenua (meno nje) wasijue ukiukwaki wa haki za wengine ni sawa na kula nyama ya mtu.

"Taratibu haitakuwa magari ya abiria peke yake, kama tukichagua kukaa kimya."

Kwani kwenye gari kinachogomba ni namba za usajili au ubora wake? Vipi kama mtu alinunua gari lake zamani akaamua kuliweka ndani bila kulitumia hata kwa miaka 20? Hilo nalo LATRA hawalitaki?

Kwanini LATRA wangependa watu kununua magari mapya (kama mazuzu tu) hata kama waliyo nayo ni mazima? Au kwanini LATRA wangependa wamiliki wa magari kuyatupa au kuyaondoa magari yao kimkumbo mkumbo tu hata kama ni mazima?

Kwani LATRA wamekuwa na maslahi gani kwenye biashara ya magari? Kwamba wamekuwa madalali, washirika au wauza magari? Kwani hata magari haya yanatengenezwa hapa nchini? Vipi kuwa mawakala wa mabeberu?

"Ikumbukwe kununua gari au chochote na hasa inapokuwa si kutoka kwenye viwanda vya ndani ni kuwaneemesha mabeberu.'

Cuba yenye kutupa sisi misaada, ni moja ya nchi za kizalendo zenye kujua umuhimu wa kutunza kila walivyo navyo; ili kuepuka unyonywaji na hasa huu wa kupitia katika manunuzi yasiyo ya lazima kutoka nje:

View attachment 2934577

Pichani ndiyo yaliyo magari katika ya maana yaliyojazana kwenye barabara bora kabisa za Havana, Cuba. Magari ya miaka 1950s huko. Spares zake zote ni kutokea katika soko lao la ndani.

Huku kufunguliwa kwetu nchi kwa lazima ya kununua nje, ni ili mabeberu yavune yawezavyo, si ndiko alikokupinga sana bwana JPM (RIP)?

"LATRA mnataka magari mapya pasipo na sababu? Vipi, kwani mmeahidiwa nini na nani wenzetu?"

Kwa hakika kuelekea 17 March mnatufanya kumkumbuka sana shujaa wetu yule tuliyembeza wengine bila kujua. Kwa hakika angekuwapo huu upuuzi wa D na E usingekuwapo.

Pumzika kwa amani baba Magufuli uliowaachia nchi leo wanatusukuma kwa mabeberu kama vipi tukakamuliwe kweli kweli.

"Kwa hakika kwa mema tutakumbuka."
Mkuu shida siyo LATRA bali ni CCM.

Tamko lolote la Serikali ni MAAGIZO ya chama tawala
 
Naota si kuwa nasoma! Huyu ni wewe brazaj mbaya wa JPM aliyefurahia kifo chake! Nadhani naota na nikiamka sitauona uzi huu

1. Siwezi kufurahia kifo cha mtu. Huwezi kulIona hilo popote.

2. Kwamba nilikuwa na taabu na mengine yake yakiwamo kuhusu corona, chanjo, kutekana, kukandamiza demokrasia nk. Kulikoni nisimbumuke kwa mema?

3. Sang'udi, Manjagata, Etwege na genge zima la Wana chattle tulindane ndugu zangu.

4. Zaidi sana kwenye mada kuko wazi kuhusu hata wale waliokuwa na tofauti naye:

Kwa hakika kuelekea 17 March mnatufanya kumkumbuka sana shujaa wetu yule tuliyembeza wengine bila kujua. Kwa hakika angekuwapo huu upuuzi wa D na E usingekuwapo.

Pumzika kwa amani baba Magufuli uliowaachia nchi leo wanatusukuma kwa mabeberu kama vipi tukakamuliwe kweli kweli.

"Kwa hakika kwa mema tutakumbuka."


5. Kulikoni kuniwekea mihemko isiyokuwa yangu ndugu?
 
Back
Top Bottom