saigilomagema
JF-Expert Member
- Jun 5, 2015
- 4,174
- 6,158
Suluo mkurungenzi mkuu binafsi nakuamini, pale Arusha kuna mabasi yameandikwa Oldonyosambu-King'ori via stand ndogo, Intel-Kikatiti-via stand ndogo na kadhalikq maana vituo viko viko vingi. Mh. Suluo ukweli ni kwamba hakuna anayeshimu hiyo ratiba. Hakuna basi linaanzia huko yote yanaanzia stand ndogo na yanaishia Maji ya Chai. Taarifa ni kwamba hayo mabasi ni ya matrafiki na maafisa wa LATRA ndio maana hayaguswi. Abiria wanateseka, km unafikiri ni umbeya fuatilia wape watanzania.mrejesho. Tayari tuna video na picha zenye namba za magari ambazo zimeandikwa zinakotakiwa kuishia zikiwa zinageuziwa maji ya chai polisi wakiaangalia. Mmiliki aombe leseni ya kuishia maji ya chai siyo Kikatiti au King'ori ambapo gari yake haiendi. Mh. Rais wetu tunaomba utusaidie, Arusha imejaa rushwa ondoa RTO, Mkuu wa LATRA. Hakuna anayeshimu leseni yake, kiujumla mama Arusha hakuna serikali. Km mm ni mwongo pengine tuma watu wako ktk hii sekta ya usafiri. Mh. Rais hata waziri haielewi hii nchi na hataki kuijua, nasikia ni mpemba, sazingine ndio maana watu wana hasira kwamba mpemba hajui wala hajihangaishi na matatizo yetu jambo ambalo mi sipendi hata kuliwaza.