Naona mambo sasa yamekaa sawa.
Yale matamko yaliyokuwa yanatolewa na Makanisa (TEC) na Ule Muunganiko wa Makanisa mengine hasa kipindi cha Pasaka, Yametulia kabisa.
Huu Mwaka hakuna kanisa lenye tamko.
Achilia mbali hali mbaya ya Uchumi inayolikumba taifa kwa sasa.
Inamaana Wameshakubali...
Kumekuwa na matamko tata kutokea LATRA kuhusu magari yenye namba D na E kufanywa ndiyo yaliyo magari pekee.
Hali hii si ya kuvumiliwa hata kidogo. Kesho itakuwa gari kuingia Dar na labda hata kuthubutu tu kuwapo Tanzania ni F na G peke yake. Nani ajuaye?
Ni kawaida kwa wanaojidhania kuwa wako...
Nimeona mjadala wa “Kusoma magazeti”. Nimeelekeza TCRA kuruhusu UBUNIFU kwenye tasnia ya Habari. Staili ya usomaji we magazeti imeongeza MVUTO kwenye usomaji huo, ni jambo linapaswa KUTIWA MOYO badala ya kuzuiwa. Waandishi endeleeni na ubunifu kwenye kusoma magazeti.
Maelekezo mengine yeyote...
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza maandamano ya amani Januari 24 mwaka huu mkoani Dar es Salaam kuishinikiza Serikali kuzingatia maoni ya wadau kuhusu masuala ya uchaguzi.
Maandamano hayo kabambe ya kupigania haki yataanzia Jijini Dar es Salaam na Yatafanyika 24/1/2024...
Ninaandika kwa masikitiko makubwa kufuatia kuona watu mbalimbali maarufu (Public figures) wakitoa matamko yanayokatisha tamaa na kuwakera vijana. Siwezi kurudia yaliyosemwa ila mengi yana ukakasi. Ifike hatua serikali, CCM na upinzani wawe makini sana na watu wote hasa viongozi wanaotoa kauli za...
Nachelea kusema kuwa Tanzania hakuna kiongozi mwenye uchungu na nchi hii.
Kila mtumishi wa umma kaachwa afanye atakavyo. Akiharibu na taarifa ikifika kwenye media ndipo wanafiki (viongozi) hujitokeza kutoa kauli za kusimamisha kazi watumishi.
Tangu Januari mpaka leo matukio ni mengi ambayo ni...
Wajuzi mnijuze kwanini kanisa katoliki likitoa matamko yake juu ya Serikali huwa yanakuwa na nguvu zaidi kuliko madhehebu mengine?
Mfano tangu sakata la bandari liibuke waraka wa kanisa katoliki ndio ulipata mileage na attention kubwa tofauti na madhehebu mengine ambayo pamoja na kutoa pia...
Viongozi wengi wa dini wako kwenye payroll ya idara nyeti na wamewekwa makusudi ili kuituliza jamii kipindi cha hamkani si shwari.
Jiulize kwani mara nyingi hutoa matamko ambayo ukiyaweka kwenye mizania unayaona kabisa yako kinyume na jamii na hayana upako wa kimungu bali wa kisiasa?
Bosi wa...
Baada ya video kusaambaa ikionesha mhudumu wa afya akiosha vifaa tiba kwa maji ya baridi na kunianika juani, serikali imekuja na majibu, ila kama kawaida inaonesha huwa hawawasiliani na hivyo kutoa matamko mawili mawili.
Waziri Ummy katoa tamko kuwa ameona video hiyo na kwamba atafatilia kujua...
Mgogoro wa wafanyabiashara Kariakoo unatokana kwa kiasi flani na mazoea ya viongozi wetu kuendesha nchi kwa matamko ya jukwaani. Tangu lini tamko la kiongozi jukwaani likawa sheria?
Jambo kubwa kama ukusanyaji wa kodi na msamaha wa kodi kwa miaka 3-5 linatamkwa tu jukwaani bila maandishi...
Tumefika hapa tulipo kwa sababu hatuna mifumo ya kuongoza nchi.
Inashangaza kuona anatokea mtu mmoja mjinga anavunja katiba ya nchi na bado anaendelea kuwa kiongozi.
Hatuwezi kupiga hatua kama Taifa liashindwa kuwa na mfumo sahihi.
Wasomi hakikisheni mnalikomboa Taifa kila kitu kinabi kuwa...
Wiki iliyopita nilitazama taarifa moja ambao nainukuu hapa ilivyoanza;
“Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo wahakikishe wanamfikisha katika vyombo vya sheria baba mzazi wa mwanafunzi wa darasa la pili (7) Jijini Arusha...
Ni Jambo la kusikitisha na la hatari sana kwenye utawala wa sheria katika zama hizi za upotoshaji wa kimtandao “misinformation era” Teuzi na tenguzi au maTangazo ma kubwa yanayohusu mustakabali wa nchi tunajulishwa kwa barua za msemaji, binafsi nilitegemea liwe Tangazo la serikali “government...
1. Aamrishe aliyewadanganya Watanzania katika 23.3% ya Mishahara akamatwe upesi na ashtakiwe afungwe Jela kabisa.
2. Aamrishe wale Wote waliofanya na Wanaofanya Uharamia wa Wanyama katika Mbuga zetu na Kusafirisha Nyara zao ( Ivory and Tusks ) si tu Wakamatwe upesi bali Wauwawe kabisa hata kama...
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, amegiza Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD) kufumuliwa na kusukwa upya ndani ya miezi sita hilo likienda sambamba na kuondoa watumishi waliokaa zaidi ya miaka 20.
Waziri Ummy amesema kumekuwapo na tuhuma kubwa za rushwa MSD na licha ya kuondoa wakuu wa...
Machinga sio kikundi cha watu ambao ukishawasikiliza wao na kuwatekelezea kilio chao basi umemaliza, hapana. Watu wanaweza kudhani kuwa machinga ni vijana tu, hapana, ndani ya machinga kuna watoto, vijana, watu wazima na wazee. Mbaya zaidi wadau wa machinga wamo watu wenye wenye ajira zao na...
Ukubwa wa seal za vizibo vya chupa za maji hauna tofauti na ukubwa wa vifungashio vya karanga na pipi.
Seal za vizibo vya chupa za maji zilikuwa ni uhakika kwa mtumiaji kuwa maji hayajachakachuliwa
Unapozuia maji kuwekewa seal una maana gani? Maji fake yaingie mitaani?
1) Mheshimiwa Waziri wa Nishati January Makambaanadai kwamba:
a) Tatizo la Mgao wa Umeme limesababishwa na Uchakavu wa Miundombinu ambayo haijafanyiwa Matengenezo kwa miaka 5!!
b) Tanesco hawajafanya Matengenezo katika kipindi kilichopita cha miaka 5 (soma: Awamu ya 5) kwa sababu eti kila...
Sio utamaduni wa chombo cha utangazaji cha Chanel Ten kutangaza habari za vyama vya upinzani nchini.
Tangu wiki lililopita wamekuwa wakitangaza taarifa za Chadema wakidai wao ni wanachama wa chadema bile kujitaja wadhifa wao kichama.
Pia najiuliza juhudi ya channel Ten kuwa mstari wa mbele...
Nachokiona ni mparaganyiko wa viongozi.
Leo atatoa tamko Mkuu wa Mkoa kesho Mkuu wa Wilaya.
Leo utasikia ya Dodoma, kesho Tanga, kesho kutwa Kiteto. Mimi nafikiri mnatuchosha wananchi.
Inaonekana viongozi mnaogopa Covid kuliko sisi wananchi.
Tunaomba mjipange then mje na tamko moja...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.