Kauli ya Waziri wa Elimu ya kwamba walimu wafanye mtihani kabla ya ajira ni ya udhalilishaji

Mganguzi

JF-Expert Member
Aug 3, 2022
1,032
2,769
Watabisha sana lakini kauli ya waziri wa elimu kuhusu ajira za walimu ni kauli za udhalilishaji wa waalimu na Maprofesa wa vyuo husika!

Kama mitaala ya vyuo vya walimu inasimamiwa na wizara ya elimu! Kama vyuo vyetu vina ubora unaokidhi vigezo! Kwanini waziri anawataka walimu wafanye mitihani Tena kabla ya ajira? Mbona madaktari na wauguzi wasifanyiwe mitihani upya?

Ni kwa sababu waziri wa elimu ana hisi vyuo vyetu ni takataka! Na wahitimu wa vyuo vyenyewe ni mapompopo! Fikiria kwamba zaidi ya waalimu laki mbili Hawana ajira na viwango vyao vya elimu vinatofautiana hiyo mitihani itazingatia muda wao waliokaa bila ajira?

Hiyo gharama ya kuisimamia hiyo mitihani sio matumizi mabaya ya fedha? Kama vyuo vyetu vimekosa ubora basi tuambiwe ili na sisi wazazi tusipeleke watoto wetu kwenye vyuo ambavyo serikali Haina Imani navyo.

Kama serikali imekosa Imani na vyuo vyetu, tafadhali wizara itoe tamko rasmi tuvisusie hivyo vyuo havitufai kabisa ! Watoto wetu kwa sasa Wana stress kwa kuwa hawajui ninini kitatokea!

NB: Waziri wa Elimu kabla hujafanya maamuzi shirikisha wadau! Usiamue mambo peke yako kama Mtemi Mirambo wa Tabora.
 
Kwahiyo vyuo vinavyotoa ma HR, wahasibu, wahandisi, marubani n.k vilikosa sifa tangu zamani?

Wenzako tulifanya usaili ili tuajiriwe na hatukupiga kelele.

Unafanya interview mbili mpaka 3.

Unakwenda Dodoma unatumia zaidi ya laki 3 ukipata poa ukikosa unatulia unasubiri mkeka mwingine mpaka unapata.

Acheni ujinga nyie walimu.

Kada ya wajinga.

Ni kada pekee inayompiga mteja wake.
 
Tangu zamani walimu ndivyo wanavyoonekana kwa kuwa wamejidharaulisha wao wenyewe mbele ya jamii kwa mambo yao ya ovyo.
 
Malalamiko yako hayana maana, Uliona wapi mtu anakuwa daktari kabla ya kupitia mafunzo ya vitendo zaidi ya mwaka mmoja? Walimu mnakimbia interview hii ni dalili hatarishi.
 
Kwahiyo vyuo vinavyotoa ma HR, wahasibu, wahandisi, marubani n.k vilikosa sifa tangu zamani?
Wenzako tulifanya usaili ili tuajiriwe na hatukupiga kelele
Acha kuwadharau walimu wetu kuita majina ya ajabu,labda kama hujasoma ila kama umesoma na ulifundishwa na hao walimu ambao sasahiv unawakejeli basi ulikuwa unasomea ujinga na wewe.
 
Acha kuwadharau walimu wetu kuita majina ya ajabu,labda kama hujasoma ila kama umesoma na ulifundishwa na hao walimu ambao sasahiv unawakejeli basi ulikuwa unasomea ujinga na wewe.
Haya nitajie kada nyingine inayompiga mteja wake ukiondoa kada ya ualimu
 
Magereza,polisi.Alafu wanaolipwa ada si watoto ni wazazi.Waheshimu walimu wetu hata kwa mapungufu unayoyaona kwao.
 
Ninatafuta license ya kufundisha middle na high school kwa district ya Columbia, nina mitihani Kama 8 hv lazima nifanye ndio nipate license, sasa kama States na nchi zilizoendelea lazima ufanye paper ndio uruhusiwe kufundisha , mbona bongo mnakuwa wakali?🤦🏾‍♂️🤔
 
Kama engineers wanafanya..!
Pamoja na kada zingine, kwanini nyie mnahofu?

Je! Ni uwezo mdogo?
 
Watabisha sana lakini kauli ya waziri wa elimu kuhusu ajira za walimu ni kauli za udhalilishaji wa waalimu na Maprofesa wa vyuo husika!

Kama mitaala ya vyuo vya walimu inasimamiwa na wizara ya elimu! Kama vyuo vyetu vina ubora unaokidhi vigezo! Kwanini waziri anawataka walimu wafanye mitihani Tena kabla ya ajira? Mbona madaktari na wauguzi wasifanyiwe mitihani upya?

Ni kwa sababu waziri wa elimu ana hisi vyuo vyetu ni takataka! Na wahitimu wa vyuo vyenyewe ni mapompopo! Fikiria kwamba zaidi ya waalimu laki mbili Hawana ajira na viwango vyao vya elimu vinatofautiana hiyo mitihani itazingatia muda wao waliokaa bila ajira?

Hiyo gharama ya kuisimamia hiyo mitihani sio matumizi mabaya ya fedha? Kama vyuo vyetu vimekosa ubora basi tuambiwe ili na sisi wazazi tusipeleke watoto wetu kwenye vyuo ambavyo serikali Haina Imani navyo.

Kama serikali imekosa Imani na vyuo vyetu, tafadhali wizara itoe tamko rasmi tuvisusie hivyo vyuo havitufai kabisa ! Watoto wetu kwa sasa Wana stress kwa kuwa hawajui ninini kitatokea!

NB: Waziri wa Elimu kabla hujafanya maamuzi shirikisha wadau! Usiamue mambo peke yako kama Mtemi Mirambo wa Tabora.

TATIZO LA ELIMU YETU HASA SHULE ZA MSINGI KWA ASLIMIA 95% NI UKOSEFU WA WAALIMU WA HESABU.
SEKONDARI PIA KUNA UPUNGUFU MKUBWA.
WAKIAJIRI WAALIMU WA HESABU WALAU KILA SHULE YENYE MKONDO MMOJA IPATE WAWILI UFAULU UTAONGEZEKA PENGINE MARA 10 YA SASA NA MENGINE YOOOTE YATAKWISHA HATA HIYO MITIHANI HAINA HAJA.
WATOTO WAKIFAULU HESABU HUFAUKU NA MASOMO MENGINE!!!!!!
Kila mwaka watoto wanafeli hesabu kwa asilimia 90% watafiti wetu wanakuja na hoja nyepesi nyepesi badala ya kutaja tatizo linalobela 80% kuwa, hakuna waalimu wa Hesabu huko mashuleni waliopo WENGI WAO huko primary hawana sifa za kufundisha Hesabu!
 
Back
Top Bottom