Kanisa Katolike ni Kasa la Majeshi, kama Mungu aitwavyo Mungu wa Majeshi. Katika Historia ya kanisa katoliki, vita vilishawahi kuanzishwa na viongozi wake. Pia amani ilishalindwa na viongozi wa kanisa katoliki. Hata kwa nyakati tulizonazo ni ukweli usiopingika kuwa Kanisa katoliki limehifadhi amani ya dunia. Bila uongozi dhabiti wa kanisa katoliki amani ya dunia ingekuwa imetikiswa vibaya kuliko ilivyotikiswa na vita vikuu vya dunia. Kiongozi wa kaniza Papa Mtakatifu ana nguvu nyingi na ambazo wengi hawazifahamu, zingine zikiwa ni siri kuu.
Mbali na yaho kanisa katoliki ndilo pioneer mkubwa wa elimu na afya duniani. Kanisa katoliki kwa enzi na enzi limekuwa likitoa elimu kwa jamii, tena elimu bora kabisa. Limejenga mashule na vyuo. shule zingine zilikabidhiwa kwa serikali za nchi husika. Pia Kanisa katoliki limesaidia katiaka huduma za kijamii hasa afya kila lilipopita. zahanati na hospitali nyingi zilijengwa na kanisa, na hadi leo kuna hostpitali na zahanati zinazotoa huduma nzuri na za kutegemewa, zote zimejengwa na kanisa katoliki. Mengine ni maji, na barabara kwa baadhi ya maeneo.
Historia inalibeba kanisa hili. Ni kanisa la kwanza kabisa kuasisiwa na jamii ya kikristo ilyoanzishwa miaka takribani 50 baada ya Yesu kuzaliwa. Mtume Petro ndiye kiongozi wake mkuu wa kwanza. Alikuwa Papa wa kanisa katoliki baada ya kufika Roma na kuliasisi kanisa kama Yesu alivyomuahidi. Makanisa yote ya kikristo yameanzia katika kanisa katoliki baada ya kuasi na mengine kujitenga.
Kanisa Katoliki ndio kanisa kongwe zaidi duniani. Kila mtu analionea husuda zaidi ya anavyoonea husuda dini yake.