juvenile davis
JF-Expert Member
- Apr 13, 2015
- 4,752
- 4,449
Habari za usiku wanajukwaa. Ni muda mrefu sijachangia chochpte humu wala kuweka bandiko lolote humu zaidi tu ya kusoma mawazo yenu.
Naomba nieleweke kwamba mimi ni mfuasi mtiifu wa chadema na nitaendelea kukitii siku zote.na niweke wazi kwamba sijawahi kukihujumu chama wala sifikirii kufanya hivyo. Nije kwenye mada sasa. CHADEMA tunataka katiba mpya lakini kiukweli suala la katiba mpya haliwezekani.
Kwanini nasema haliwezekani? Kwasababu wakati wa kuitengeneza Rasimu ya pili ya warioba 2014 ili iwe the proposed constitution hawahawa viongozi wetu walikuwa ni wajumbe pale bungeni lakini walishindwa kuendelea kukaa pale bungeni na wenzao wengine kwa sababu tu ya suala la serikali mbili na serikali tatu. Wakabishana weeee hadi kufikia kuiambia serikali ilete hati ya muungano.
Ukiangalia hilo suala la muungano halikuwa na athari yoyote lakini wao wakasusa na kukimbia pale bungeni wakiongozwa na lipumba ambaye leo wanamuona sio mpinzani.ndani ya ile rasimu kuna mambo mengi ya muhimu sana wangeweza kuyapambania ambayo kama wangesusa kwa sababu ya hayo tungewaona ni mashujaa.
Mfano suala la Wabunge kuongoza miaka 10. Waziri na spika kutokuwa wabunge, matokeo ya raisi, wabunge na madiwani kuhojiwa mahakamani, tume huru ya uchaguzi, Mamlaka ya Rais kupunguzwa, mgombea binafsi, mbunge anapofariki basi aliyeshika nafasi ya pili wakati wa uchaguzi basi anakuwa mbunge na wananchi kuwawajibisha wabunge wavivu, mbunge akihama chama basi anahama na ubunge wake na sio mambo ya by election. Mengine nadhani kama ulibahatisha kuyaona kama ulisoma ile draft.
Sasa, ukiangalia kilichowafanya wakasusa ni kitu kidogo na kisicho na maana yoyote ile kwa wananchi.
Binafsi nahisi Rais Samia ameshagundua kwamba hata akisema mchakato urudi upya mambo yatakuwa ni yaleyale business as usual. Yaani CCM watataka serikali mbili huku CHADEMA wakitaka serikali tatu na mwisho hawataelewana na mchakato utakwama tena na hivyo kodi za wananchi zitakwenda bure Maana kumbuka walikuwa wanakula posho daily Tsh laki 3. Hivyo Rais sidhani kama atakubali huu mchakato urudiwe maana mambo yatajirudia ni yaleyale tu. Itakuwa ni uharibifu wa fedha..ni vizuri wang’ang’anie tu hii iliyopo ifanyiwe amendments baadhi ya vipengele lakini suala la katiba mpya hilo I’m sure halitafanikiwa.
Kitu kingine wanachohitaji viongozi wetu ni political rallies kuruhusiwa ni kweli hilo sio hisani bali ni takwa la kikatiba iliyopo lakini kuhusu hilo nadhani mheshimiwa Rais ashalitolea ufafanuzi tayari.kwamba tusubiri kwanza ajenge uchumi wawekezaji waje wakute nchi ikiwa tulivu haina labshalabsha zozote ndipo turudi majukwaani (angalau huyu katoa sababu zenye mashiko kidogo kuliko mwendazake).
Maana usisubiri hadi Raisi aongee direct kwamba “jamani utawala ulopita nilikuwa nikimshauri hiki na kile mwenzangu hakuwa akinisikiliza ndio Maana uchumi umeyumba”kwa sababu hakuna asiyejua kwamba Mzee alikuwa hashauriki.sasa Mama hawezi kuanza kumkandia na kuanza kujitetea.
Mimi nadhani tuwe watulivu tukisubiri huo uchumi unaojengwa then tukiona labda miaka miwili au mmoja unakata tunaweza kurudi kumkumbusha.lakini kwa style kama ya kuwapa vipaza watu kama mdude halafu kwa kauli kama zile kiukweli haipendezi na mwisho tutampa hasira Raisi asije akawa kama mwendazake tuanze kubambikiwa makesi na kufurushwa hata kwenye mikutano ya ndani.
Chadema chama langu waelewe tu upinzani upo ndani ya damu. Kumbuka Magufuli alipiga ban mikutano na kufunga wanasiasa na kununua wabunge na madiwani ila ilipofika wakati wa uchaguzi bado alisumbuka sana kuona nyomi la Chadema mwisho akapora uchaguzi kwa nguvu(nilisimamia uchaguzi so niliona ujinga uliofanyika) niwatakie siku njema na niwaase mfanye kazi kwa bidii na kama wewe ni mwanafunzi basi soma kwa bidiii.na msisahau kumuabudu mwenyezi Mungu.
Naomba nieleweke kwamba mimi ni mfuasi mtiifu wa chadema na nitaendelea kukitii siku zote.na niweke wazi kwamba sijawahi kukihujumu chama wala sifikirii kufanya hivyo. Nije kwenye mada sasa. CHADEMA tunataka katiba mpya lakini kiukweli suala la katiba mpya haliwezekani.
Kwanini nasema haliwezekani? Kwasababu wakati wa kuitengeneza Rasimu ya pili ya warioba 2014 ili iwe the proposed constitution hawahawa viongozi wetu walikuwa ni wajumbe pale bungeni lakini walishindwa kuendelea kukaa pale bungeni na wenzao wengine kwa sababu tu ya suala la serikali mbili na serikali tatu. Wakabishana weeee hadi kufikia kuiambia serikali ilete hati ya muungano.
Ukiangalia hilo suala la muungano halikuwa na athari yoyote lakini wao wakasusa na kukimbia pale bungeni wakiongozwa na lipumba ambaye leo wanamuona sio mpinzani.ndani ya ile rasimu kuna mambo mengi ya muhimu sana wangeweza kuyapambania ambayo kama wangesusa kwa sababu ya hayo tungewaona ni mashujaa.
Mfano suala la Wabunge kuongoza miaka 10. Waziri na spika kutokuwa wabunge, matokeo ya raisi, wabunge na madiwani kuhojiwa mahakamani, tume huru ya uchaguzi, Mamlaka ya Rais kupunguzwa, mgombea binafsi, mbunge anapofariki basi aliyeshika nafasi ya pili wakati wa uchaguzi basi anakuwa mbunge na wananchi kuwawajibisha wabunge wavivu, mbunge akihama chama basi anahama na ubunge wake na sio mambo ya by election. Mengine nadhani kama ulibahatisha kuyaona kama ulisoma ile draft.
Sasa, ukiangalia kilichowafanya wakasusa ni kitu kidogo na kisicho na maana yoyote ile kwa wananchi.
Binafsi nahisi Rais Samia ameshagundua kwamba hata akisema mchakato urudi upya mambo yatakuwa ni yaleyale business as usual. Yaani CCM watataka serikali mbili huku CHADEMA wakitaka serikali tatu na mwisho hawataelewana na mchakato utakwama tena na hivyo kodi za wananchi zitakwenda bure Maana kumbuka walikuwa wanakula posho daily Tsh laki 3. Hivyo Rais sidhani kama atakubali huu mchakato urudiwe maana mambo yatajirudia ni yaleyale tu. Itakuwa ni uharibifu wa fedha..ni vizuri wang’ang’anie tu hii iliyopo ifanyiwe amendments baadhi ya vipengele lakini suala la katiba mpya hilo I’m sure halitafanikiwa.
Kitu kingine wanachohitaji viongozi wetu ni political rallies kuruhusiwa ni kweli hilo sio hisani bali ni takwa la kikatiba iliyopo lakini kuhusu hilo nadhani mheshimiwa Rais ashalitolea ufafanuzi tayari.kwamba tusubiri kwanza ajenge uchumi wawekezaji waje wakute nchi ikiwa tulivu haina labshalabsha zozote ndipo turudi majukwaani (angalau huyu katoa sababu zenye mashiko kidogo kuliko mwendazake).
Maana usisubiri hadi Raisi aongee direct kwamba “jamani utawala ulopita nilikuwa nikimshauri hiki na kile mwenzangu hakuwa akinisikiliza ndio Maana uchumi umeyumba”kwa sababu hakuna asiyejua kwamba Mzee alikuwa hashauriki.sasa Mama hawezi kuanza kumkandia na kuanza kujitetea.
Mimi nadhani tuwe watulivu tukisubiri huo uchumi unaojengwa then tukiona labda miaka miwili au mmoja unakata tunaweza kurudi kumkumbusha.lakini kwa style kama ya kuwapa vipaza watu kama mdude halafu kwa kauli kama zile kiukweli haipendezi na mwisho tutampa hasira Raisi asije akawa kama mwendazake tuanze kubambikiwa makesi na kufurushwa hata kwenye mikutano ya ndani.
Chadema chama langu waelewe tu upinzani upo ndani ya damu. Kumbuka Magufuli alipiga ban mikutano na kufunga wanasiasa na kununua wabunge na madiwani ila ilipofika wakati wa uchaguzi bado alisumbuka sana kuona nyomi la Chadema mwisho akapora uchaguzi kwa nguvu(nilisimamia uchaguzi so niliona ujinga uliofanyika) niwatakie siku njema na niwaase mfanye kazi kwa bidii na kama wewe ni mwanafunzi basi soma kwa bidiii.na msisahau kumuabudu mwenyezi Mungu.