Katiba Mpya: Mimi ni CHADEMA lakini kwa hili nasema NO, tena Big No

Kwa hiyo wewe unataka kusema kila alitakalo Lissu ndilo lafaa kuwa kwenye Katiba?
Mantiki ya andiko inakosa maana. Sioni umuhimu wa kuandika wewe ni CHADEMA au CCM.

Jenga hoja yako. Katiba tunayoongekea ni ya nchi. Siyo ya CCM wala CHADEMA. Kwa fikra zako unaamini kuwa CHADEMA wote wanataka katuba mpya, na CCM wote hawataki katiba mpya?

Wananchi walio wengi, webye vyama na wasio na vyama, wanataja katiba mpya. Hilo lilidhihirishwa kwa data, na tume ya Warioba. Kwa sasa, zaidi kinachogomba miongoni mwa wananchi, ni timing.
 
Mkuu nami nakuunga Mkono 100%
Vyama vya siasa wanaangalia tuu maslahi yao.
Na Hapa Tuweke wazi Chadema maana ndio tunaowajadili!
Serikali 2,3
Zinamanufaa gani Kwa Mwananchi wa Kawaida!
Ina Maana Mambo Mengine kama Tume huru,Mawaziri kutokuwa wabunge,kuomba baadhi ya nafasi ziwe za Ku apply na Sio Kuteuliwa,Na Masuala Mengine waliyapuuza na Kuona Lenye Umuhimu kwao Ni La Muungano tuu,Hivyo likishindikana bora Kususa Hayo Mengine sio Kipaumbele Kwao!
Namuunga Mkono RAISI SAMIA SULUHU HASSAN haina Haja ya Kuanzisha sijui bunge la Katiba,Ni Either tuendelee pale tulipoishia,Wao wanaangalia Maslahi yao sio ya Wananchi,Wakiulizwa wananchi wataje Vipaumbele vyao 5 tuu,Hutosikia Suala la Muungano hapo!likiwepo litakuwa la mwisho.
Labda Ndio linawapa Kiki!
 
Kumbe hata rasimu ya pili ya Warioba ilikuwa haifai.

Swala la mbunge kuhama chama na ubunge wake halifai. Hiyo rasimu ingepita nadhani kipindi kile cha hamahama cha wabunge wangeweza kuhama bila hata kununuliwa kwa bei kubwa, wangepozwa kwa hela kidogo tu ya mboga na kuhama chama.

So binafsi hiyo rasimu ya Warioba ilikuwa haifai pia, japo CHADEMA walisusia mchakato kwa hoja dhaifu ila kumbe subconciously walifanya la maana sana. Mambo gani ya mtu kuhama chama anahama na ubunge wake? Huko ni kuwasaliti wananchi. Wananchi walimpa ubunge kutokana na sera za chama chake hivyo anapohama chama anaenda kinyume na makubaliano ya wapiga kura wake.

Uzuri pia wa katiba hiyo hiyo na eneo hilo la ubunge, kulikuwa na kifungu cha kumuwajibisha mbunge bila kusubiri miaka mitano kuisha iwapo ataonekana hafikii matakwa ya jimbo lake.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Naitaka katiba mpya . lakini hapa mkuu unahoja kubwa. Lile liumoja lao ukawa lilisababisha mkwamo wa katiba. Cuf walikuwa lazima wasikilizwe na ukawa wenzao kuhusu mamlaka ya Zanzibar. Ndio maana hoja ya serikaki tatu isiyo na msingi wowote ikavuruga mchakato
 
Nimekuona hamnazo uliposema swala la Serikali 2/3 lilikuwa halina maana.
Hivi unajua muundo wote wa kiutawala utategemeana ni aina gani ya Serikali inayohitajika?
Kwa ushauri rudia kusoma rasimu ya Katiba ya Warioba,kisha chukua ile nakala ya Katiba pendekezwa ndio uje na hitimisho.
 
Naitaka katiba mpya . lakini hapa mkuu unahoja kubwa. Lile liumoja lao ukawa lilisababisha mkwamo wa katiba. Cuf walikuwa lazima wasikilizwe na ukawa wenzao kuhusu mamlaka ya Zanzibar. Ndio maana hoja ya serikaki tatu isiyo na msingi wowote ikavuruga mchakato
Sasa hoja ya Serikali Tatu kama ilikuwa haina msingi kwa maelezo yako inakuwaje tena iharibu mchakato wa kupata katiba nzima?.
Usilolijua ni kuwa ufafanuzi pale kwenye utangulizi kwamba Tanzania ni Nchi either ni Jamhuri ya Muungano inayohusisha Nchi ngapi? Ndio Jambo LA msingi kuliko mengine yote.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
😂😂😂😂😂mkuu acha uongo, hata mtoto mdogo anajua KATIBA mpya ni muhimu. Mkuu hebu jaribu kuvuta picha na utulize akili yako, utagundua KATIBA ni muhimu.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Ivi nyie kipindi hicho mlikuwa watoto? Chukua rasmu ya warioba ambayo ndio maoni ya wananchi halisi na chukua Katiba pendekezwa Soma between the lines utuambie hazifanani kwa kiasi gani na utuambie kilicho andikwa kwenye Katiba pendekezwa ni nini na walipata hizo baraka wapi? Ni wehu tu na waganga njaa wanaweza kukubali na kubaki bungeni kwa kilicho fanywa na bunge la katiba

Mkuu yawezekana wewe ndio mtoto.sisi wengine tunajua tangu yanaundwa mabaraza ya kata.then soma vizuri andiko langu
 
Huwezi kuwa chadema wewe mpumbavu na dhuluma ya uchaguzi wa Mwaka Jana ukiongea mambo ya ki mat*ko hapa wakati watu wameumia! Sitaki kukutukana!

Kaa huko CCM na akili za kipumbabu!
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
wewe bora ungebaki msomaji milele, maana una uwezo mdogo sana wa kuchambua mambo.BAKI KUA MSOMAJI TU MKUU UTAJIFUNZA MENGI.
 
Kwan nn faida na harasa ya serikali 3 na zipi faida na harasa za serikali 2? Wenda kila upande ulikuwa unajaribu kujitengenezea mazingira ya upataji kiurahis ndio maana hawakuona vitu vingne zaid ya hilo.
Je, huoni kuwa ni Zanzibar ni nchi , ina katiba, ina bunge lake, ina rais wake, ina wimbl waje wa taifa? xHii Zanzibar iliungana na nani mpaka tukapata Tanzania? Hiyo nchi iko wapi?
Kama Zanzibar ni nchi mbona haichangii cho chote kwenye muungano?
Wabunge wa Zanzibar hushiriki kwenye vikao vya bunge la Tanganyika ni serikaliinayolipa kila kitu chao, posho, mpaka pesa za majimbo wkt skule kuna serikali inayojitegemea.

Sasa hivi tuna rais anatawala Tanganyika kwa kuwa Zanzibar haichangii kwenye muungano.

Wengine wanasema Waziri mkuu anatawala Tabganyika sio kweli.bAnayetawala ni yule anayemteua ndiye mtawala. Rais aliyepo Mzanzibari anasimamia serikali ya Tanaganyika lakini sio ya Zanzibar. Kwa kuwa Zanzibar ina rais wake na serikali yake. Anayetawala Tanganyika mbona siye aliyechaguliwa na Watanganyika kama Zanzibar wanavyoteua wao. Kwanini tunyimwe haki hii yetu ya kikatiba ndio maana tunataka serikali yaTanganyika kwenye muungano usoeleweka
 
Habari za usiku wanajukwaa. Ni muda mrefu sijachangia chochpte humu wala kuweka bandiko lolote humu zaidi tu ya kusoma mawazo yenu.

Naomba nieleweke kwamba mimi ni mfuasi mtiifu wa chadema na nitaendelea kukitii siku zote.na niweke wazi kwamba sijawahi kukihujumu chama wala sifikirii kufanya hivyo. Nije kwenye mada sasa. CHADEMA tunataka katiba mpya lakini kiukweli suala la katiba mpya haliwezekani.

Kwanini nasema haliwezekani? Kwasababu wakati wa kuitengeneza Rasimu ya pili ya warioba 2014 ili iwe the proposed constitution hawahawa viongozi wetu walikuwa ni wajumbe pale bungeni lakini walishindwa kuendelea kukaa pale bungeni na wenzao wengine kwa sababu tu ya suala la serikali mbili na serikali tatu. Wakabishana weeee hadi kufikia kuiambia serikali ilete hati ya muungano.

Ukiangalia hilo suala la muungano halikuwa na athari yoyote lakini wao wakasusa na kukimbia pale bungeni wakiongozwa na lipumba ambaye leo wanamuona sio mpinzani.ndani ya ile rasimu kuna mambo mengi ya muhimu sana wangeweza kuyapambania ambayo kama wangesusa kwa sababu ya hayo tungewaona ni mashujaa.

Mfano suala la Wabunge kuongoza miaka 10. Waziri na spika kutokuwa wabunge, matokeo ya raisi, wabunge na madiwani kuhojiwa mahakamani, tume huru ya uchaguzi, Mamlaka ya Rais kupunguzwa, mgombea binafsi, mbunge anapofariki basi aliyeshika nafasi ya pili wakati wa uchaguzi basi anakuwa mbunge na wananchi kuwawajibisha wabunge wavivu, mbunge akihama chama basi anahama na ubunge wake na sio mambo ya by election. Mengine nadhani kama ulibahatisha kuyaona kama ulisoma ile draft.

Sasa, ukiangalia kilichowafanya wakasusa ni kitu kidogo na kisicho na maana yoyote ile kwa wananchi.

Binafsi nahisi Rais Samia ameshagundua kwamba hata akisema mchakato urudi upya mambo yatakuwa ni yaleyale business as usual. Yaani CCM watataka serikali mbili huku CHADEMA wakitaka serikali tatu na mwisho hawataelewana na mchakato utakwama tena na hivyo kodi za wananchi zitakwenda bure Maana kumbuka walikuwa wanakula posho daily Tsh laki 3. Hivyo Rais sidhani kama atakubali huu mchakato urudiwe maana mambo yatajirudia ni yaleyale tu. Itakuwa ni uharibifu wa fedha..ni vizuri wang’ang’anie tu hii iliyopo ifanyiwe amendments baadhi ya vipengele lakini suala la katiba mpya hilo I’m sure halitafanikiwa.

Kitu kingine wanachohitaji viongozi wetu ni political rallies kuruhusiwa ni kweli hilo sio hisani bali ni takwa la kikatiba iliyopo lakini kuhusu hilo nadhani mheshimiwa Rais ashalitolea ufafanuzi tayari.kwamba tusubiri kwanza ajenge uchumi wawekezaji waje wakute nchi ikiwa tulivu haina labshalabsha zozote ndipo turudi majukwaani (angalau huyu katoa sababu zenye mashiko kidogo kuliko mwendazake).

Maana usisubiri hadi Raisi aongee direct kwamba “jamani utawala ulopita nilikuwa nikimshauri hiki na kile mwenzangu hakuwa akinisikiliza ndio Maana uchumi umeyumba”kwa sababu hakuna asiyejua kwamba Mzee alikuwa hashauriki.sasa Mama hawezi kuanza kumkandia na kuanza kujitetea.

Mimi nadhani tuwe watulivu tukisubiri huo uchumi unaojengwa then tukiona labda miaka miwili au mmoja unakata tunaweza kurudi kumkumbusha.lakini kwa style kama ya kuwapa vipaza watu kama mdude halafu kwa kauli kama zile kiukweli haipendezi na mwisho tutampa hasira Raisi asije akawa kama mwendazake tuanze kubambikiwa makesi na kufurushwa hata kwenye mikutano ya ndani.

Chadema chama langu waelewe tu upinzani upo ndani ya damu. Kumbuka Magufuli alipiga ban mikutano na kufunga wanasiasa na kununua wabunge na madiwani ila ilipofika wakati wa uchaguzi bado alisumbuka sana kuona nyomi la Chadema mwisho akapora uchaguzi kwa nguvu(nilisimamia uchaguzi so niliona ujinga uliofanyika) niwatakie siku njema na niwaase mfanye kazi kwa bidii na kama wewe ni mwanafunzi basi soma kwa bidiii.na msisahau kumuabudu mwenyezi Mungu.
Wewe siyo Chadema bali Kadema!
 
Hawana ruzuku ama wamegomea ruzuku haramu?
Mwaka 2010 chadema walisema uchaguzi haukuwa huru na wa haki, lakini kwa vile Mbowe na genge lake walishinda katika uchaguzi ule na kuwa na uhakika wa kuingiza ruzuku ndan ya chama kwa kila kichwa kimoja, basi waliingia bungeni na wakawa wanashiriki vikao vya bunge. Mwaka 2015 pia chadema wakaja na kilio kile kile cha kususia matokea ya uchaguzi kwa madai kwamba uchaguzi ule haukuwa huru na wa haki, lakini kwa vile Mbowe na genge lake walishinda ubunge tena katika majimbo yao na kupata uhakika wa ruzuku kupitia vichwa vyao basi walikubali kuingia bungeni na kushiriki vikao vya bunge kama kawa. Mwaka 2020 baada ya mwenyekiti na genge lake kuangukia pua ndo wanakuja na porojo ya kususia bunge kwa madai yale yale ambayo wao yaliwaingiza bungeni kwa zaidi ya miaka 10. Mbowe na genge lake wanafikiria kuwa kila mtanzania ni poyoyo kam ilivyo misukule yake. Mwambie akumbuke haya maneno ya kingereza "You can fool some people sometimes, but you can't fool all the people all the time" - Bob Marley. Mwambieni atafute vyanzo vingine vya kupata pesa za kuwalipa kina Mmawia, hizi propaganda zake za kutaka kupiga hela kupitia mchakato wa katiba wenye akili tushaugundua na hautamsaidia.
 
mzee huna lolote Zaidi ya kusumbuliwa na bangi ebu tuletee kipengele kinachohusu tume huru ya uchaguzi kwenye rasimu ya warioba na ulete kipengele kwenye rasimu ya CCM halafu ndio utuletee bangi zako sawa kijana kwa ushauri tu wa bure acha kuvuta bangi bora ubugie cocaine itakusaidia.
 
Back
Top Bottom