Katiba Mpya: Mimi ni CHADEMA lakini kwa hili nasema NO, tena Big No

Mwaka 2010 chadema walisema uchaguzi haukuwa huru na wa haki, lakini kwa vile Mbowe na genge lake walishinda katika uchaguzi ule na kuwa na uhakika wa kuingiza ruzuku ndan ya chama kwa kila kichwa kimoja, basi waliingia bungeni na wakawa wanashiriki vikao vya bunge. Mwaka 2015 pia chadema wakaja na kilio kile kile cha kususia matokea ya uchaguzi kwa madai kwamba uchaguzi ule haukuwa huru na wa haki, lakini kwa vile Mbowe na genge lake walishinda ubunge tena katika majimbo yao na kupata uhakika wa ruzuku kupitia vichwa vyao basi walikubali kuingia bungeni na kushiriki vikao vya bunge kama kawa. Mwaka 2020 baada ya mwenyekiti na genge lake kuangukia pua ndo wanakuja na porojo ya kususia bunge kwa madai yale yale ambayo wao yaliwaingiza bungeni kwa zaidi ya miaka 10. Mbowe na genge lake wanafikiria kuwa kila mtanzania ni poyoyo kam ilivyo misukule yake. Mwambie akumbuke haya maneno ya kingereza "You can fool some people sometimes, but you can't fool all the people all the time" - Bob Marley. Mwambieni atafute vyanzo vingine vya kupata pesa za kuwalipa kina Mmawia, hizi propaganda zake za kutaka kupiga hela kupitia mchakato wa katiba wenye akili tushaugundua na hautamsaidia.

Sina tatizo na hii akili yako maana ndio upeo wako ulipoishia. Chaguzi zote hizo ulizotaja cdm na vyama vingine walienda mahakamani kwenye baadhi ya majimbo, je safiri hii walienda? Na kama ni ruzuku hata sasa ipo lakini hawaitaki na sababu ziko wazi. Hata hivyo bado kilio kikubwa cha miaka yote hiyo ni tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Na sasa katiba hiyo inadaiwa na nguvu zote ili kusiwe na kisingizio chochote. Una jingine?
 
Sina tatizo na hii akili yako maana ndio upeo wako ulipoishia. Chaguzi zote hizo ulizotaja cdm na vyama vingine walienda mahakamani kwenye baadhi ya majimbo, je safiri hii walienda? Na kama ni ruzuku hata sasa ipo lakini hawaitaki na sababu ziko wazi. Hata hivyo bado kilio kikubwa cha miaka yote hiyo ni tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Na sasa katiba hiyo inadaiwa na nguvu zote ili kusiwe na kisingizio chochote. Una jingine?
Mwaka 2010 na 2015 uchaguzi haukuwa huru na wa haki. Walioshindwa walishauriwa waende mahakamani, lakini walioshinda Mbowe na genge lake wao walikuwa wanaendelea na vikao vya bunge kama kawa na kutafuna ruzuku kila mwezi . Mwaka 2020 uchaguzi haukuwa huru na wa haki lakini cha kushangaza alieshinda kaambiwa asiende kushiriki vikao vya bunge kama walivyokuwa wanashiriki kina Mbowe katika chaguzi za nyuma ambazo pia walisema sio huru na za haki, pia walioshindwa wamejifanya kukata kwenda mahakamani kama walivyowashauri wenzao waende. Swali langu ni kwanini Mbowe na genge lake wakishinda uchaguzi ambao wanaona sio huru na wa haki wanaingia na kushiriki vikao vya bunge kwa miaka yote 10, lakini mwaka huu wao wameshindwa afu wanamtaka mbunge alieshinda asiende kushiriki vikao vya bunge? Je Mbowe ameamua kuchukua uamuzi huu mwaka huu baada ya yeye mwenyewe kuangukia pua? Kama sio hivyo ni kwanini mgomo huu hawakuufanya miaka 10 iliyopita baada ya kuona kwamba walishinda katika chaguzi ambazo sio za huru na haki?
 
Mwaka 2010 na 2015 uchaguzi haukuwa huru na wa haki. Walioshindwa walishauriwa waende mahakamani, lakini walioshinda Mbowe na genge lake wao walikuwa wanaendelea na vikao vya bunge kama kawa na kuvuta ruzuku kila. Mwaka 2020 uchaguzi haukuwa huru na wa haki lakini cha kushangaza alieshinda kaambiwa asiende kushiriki vikao vya bunge kama walivyokuwa wanashiriki kina Mbowe katika chaguzi za nyuma ambazo pia walisema sio huru na za haki, pia walioshindwa wamejifanya kukata kwenda mahakamani kama walivyowashauri wenzao waende. Swali langu ni kwanini Mbowe na genge lake wakishinda uchaguzi ambao wanaona sio huru na wa haki wanaingia na kushiriki vikao vya bunge kwa miaka yote 10, lakini mwaka huu wao wameshindwa afu wanamtaka mbunge alieshinda asiende kushiriki vikao vya bunge?

Nakwambia akili yako ni ndogo kweli kweli. Ni mbunge gani aliyeshinda wa Cdm amezuiwa kushiriki vikao?
 
Nakwambia akili yako ni ndogo kweli kweli. Ni mbunge gani aliyeshinda wa Cdm amezuiwa kushiriki vikao?
Kama haumjui mbunge wa chadema alieshinda uchaguzi mkuu mwaka 2020, basi ww sio mfuatiliaji wa mambo ya siasa.
 
Kama haumjui mbunge wa chadema alieshinda uchaguzi mkuu mwaka 2020, basi ww sio mfuatiliaji wa mambo ya siasa.
Narudia tena, huyo mbunge aliyeshinda alizuiliwa kuingia bungeni? Nakushauri rudi kwa anayekumezesha maneno, umuulize vizuri kuhusu huyo mbunge mmoja.
 
Narudia tena, huyo mbunge aliyeshinda alizuiliwa kuingia bungeni? Nakushauri rudi kwa anayekumezesha maneno, umuulize vizuri kuhusu huyo mbunge mmoja.
Naona unajaribu kuukwepa ukweli.. Haya turudi katika sababu zilizosababisha mwaka 2010 na 2015 Mbowe akubali kuingia bungeni na wabunge wake wa viti maalumu kwa takribani miaka 10 kupitia tume ambayo sio huru na uchaguzi usio wa haki, lakini mwaka 2020 baada ya yeye kushindwa na genge lake basi haoni sababu ya wabunge wa viti maalum kuingia bungeni kushiriki vikao vya bunge huu sio ubinafsi?
 
Naona unajaribu kuukwepa ukweli.. Haya turudi katika sababu zilizosababisha mwaka 2010 na 2015 Mbowe akubali kuingia bungeni na wabunge wake wa viti maalumu kwa takribani miaka 10 kupitia tume ambayo sio huru na uchaguzi usio wa haki, lakini mwaka 2020 baada ya yeye kushindwa na genge lake basi haoni sababu ya wabunge wa viti maalum kuingia bungeni kushiriki vikao vya bunge huu sio ubinafsi?

Sioni kama una jipya, umesema sijui hawana ruzuku nimekwambia ruzuku ipo ila hawaitaki. Umesema wanawazuia wabunge waliochaguliwa, nimekwambia mbunge wa kuchaguliwa ni mmoja, na hajazuiwa. Chaguzi zote za nyuma walikuwa wanasema sio za haki, ila walienda mahakamani wangalau, ila safari hii hata mahakamani hawakwenda kutokana na kilichoendelea. Je unataka miaka yote wabaki wanalalamika bila kuchukua hatua stahiki ili kuondokana na dhuluma Hizo?

Hilo suala la viti maalum unajua likoje? Kwanza cdm hawakupeleka majina ya hao wabunge, kwani hawautambui mchakato mzima na uhalali wake. Na ushahidi ni kugomea hata ruzuku yenyewe. Je hiyo miaka yote waligomea hiyo ruzuku? Sasa hapo kwenye mjadala wetu nakwepa ukweli gani? Acha kuwa bendera fuata upepo Boss.
 
wewe bora ungebaki msomaji milele, maana una uwezo mdogo sana wa kuchambua mambo.BAKI KUA MSOMAJI TU MKUU UTAJIFUNZA MENGI.
Eti Hawa ndo wametumwa na lumumba kuja kutwist agenda ya katiba mpya

Ccm imekufa kabisa
 
Kiukweli CHADEMA hawana long term strategy, ubabaishaji na kutukanana tu, ukishauri unaishia kutukania tu. Waendelee tu.

Nilichogundua, zimwi lao wanalitengeneza wenyewe na imekuwa mtaji kwa CCM.

Heri shetani unayemjua kuliko malaika usiyemjua. Done
 
Anajihami kabla ya kuanza kushambuliwa na kuitwa mataga. Chadema wanaamini kwamba mtu yoyote mwenye mawazo tofauti na Mbowe ni msaliti au ni CCM, na yule anaekubaliana na mawazo au fikra za Mbowe ndio chadema kindaki ndaki hata kama mawazo au fikra hizo ni za kipuuzi inakubadi ukubaliane nazo tu ili kujinusuru na matusi. So usimshangae jamaa kujihami mapema japo najua na hiyo haitomsaidia kwa sababu tayar kimawazo kaishatofautiana na mwenyekiti.
Nilichokuja kugundua Hawa watu lugha zao ni matusi tu. Hakuna anayeweza kufikiri hata Jambo kwa undanikidogo na kusema hili ni sahihi.

Namna hii hakuna chama hapo ni kupotezeana muda tu.
 
Je, huoni kuwa ni Zanzibar ni nchi , ina katiba, ina bunge lake, ina rais wake, ina wimbl waje wa taifa? xHii Zanzibar iliungana na nani mpaka tukapata Tanzania? Hiyo nchi iko wapi?
Kama Zanzibar ni nchi mbona haichangii cho chote kwenye muungano?
Wabunge wa Zanzibar hushiriki kwenye vikao vya bunge la Tanganyika ni serikaliinayolipa kila kitu chao, posho, mpaka pesa za majimbo wkt skule kuna serikali inayojitegemea.

Sasa hivi tuna rais anatawala Tanganyika kwa kuwa Zanzibar haichangii kwenye muungano.

Wengine wanasema Waziri mkuu anatawala Tabganyika sio kweli.bAnayetawala ni yule anayemteua ndiye mtawala. Rais aliyepo Mzanzibari anasimamia serikali ya Tanaganyika lakini sio ya Zanzibar. Kwa kuwa Zanzibar ina rais wake na serikali yake. Anayetawala Tanganyika mbona siye aliyechaguliwa na Watanganyika kama Zanzibar wanavyoteua wao. Kwanini tunyimwe haki hii yetu ya kikatiba ndio maana tunataka serikali yaTanganyika kwenye muungano usoeleweka
Kuna uwezekano ukawa na serikali mbili kwenye srikali ya muungano serikali ya mapinduzi ya zanzibar na serikali ya Tanganyika lakini siyo kwenye mfumo wa shrikisho no!
 
Back
Top Bottom