njwanjwanjwa
Member
- Jul 28, 2022
- 8
- 11
Moja ya Vitu ambavyo Serikali inapaswa kupongeswa navyo katika swala la Elimu ukiachilia mbali miundombinu ya madarasa nk basi huachi kabisa kuipongeza serikali hii inayoongozwa na Dk. Samia Suluhu pamoja na ile ya mtangulizi wake Hayati John Magufuli kwa katazo na marufuku ya Michango mashukeni kwa kuleta Elimu bure.
Hili nalo lilikuwa ni kichaka cha baadhi ya Wakuu wa shule kujinemeesha kupitia hiyo Michango na mwisho wa siku ilikuwa ni mzigo mkubwa kwa wananchi wa hali ya chini kisomesha watoto wao.
Kwa kufuta Ada pamoja na michango mingine mashuleni hii ninpongezi kubwa sana kwa Serikali yetu.
NB: Japo kuwa serikali ilifanikisha kupiga marufuku na kuzuia michango mashuleni , huu mchango wa chakula Bado ni sugu na mwiba kwa wananchi. Wengi wanashindwa kuumudu na shule za hapa nchini zina viwango tofauti vya mchango huo na umekuwa njia ya kupitisha na kuhalalisha Michango mingine. Huwezi Amani kuna baadhi ya shule mchango wa chakula umefika Hadi Laki moja na usheee!
Chukulia mwananchi wa hali ya chini mwenye watoto watutu (3) shule moja na wote anapaswa kuwalipia mchango wa chakula kila mmoja tsh 100,000 maana yake anapaswa kulipa tsh Laki tatu.
Na mbaya zaidi kwa baadhi ya shule Hata kama mtoto hajala chakula cha shule kwa Mwaka mzima au kwa miaka minne alazimika kulipa gharama zote za Mchango chakula kwa miaka minne amalizapo kidato cha Nne. ( 10,000 x 4)
Wazazi wengi na wadau wengi wa Elimu wanashauli na kupendekeza yafuatayo kuhusu mchango sugu wa chakula kwa baadhi ya shule
1. Serikali iweke fungu la Chakula kwenye ile hela ya Ruzuku (capitation fee) mashuleni ili kutamatisha huu usemi wa Elimu bila malipo maana mchango wa chakula umekuwa mzigo mzito kwa maananchi mlala hoi.
Kama Serikali itaendelea kuruhusu mchango wa chakula mashuleni ulipwe na WAZAZI tafsiri yake ni kwamba Serikali imewapunguzia tu Michango kwa kumlioia mwanafunzi Michango ya Ada ya mitihani, Ada ya Shule (20000) nk na kumwachia mzazi au Mlezi atoe mchango wa 80,000 Hadi 100,000+ kwa ajili ya chakula kwa baadhi ya shule maana si shule zote hapa nchini wanafunzi wanakula chakula.
2. Mchango wa chakula mashuleni ufutwe kama Michango mingine maana ni kichaka cha kuhalalisha na kupitisha michango mingine.
3. Mchango wa chakula uwe hiari katika halmashauri na shule zinazotoa chakula. Wachangishwe wanaokula au waliokula chakula hicho na shule ziwe na data base y’a wanafunzi wanaokula.
4. Kama maanafunzi hajala chakula cha shule kwa term nzima ama mwaka mzima ama kwa kipindi chote alichosoma shule husika basi amalizapo kidato cha Nne asilipishwe mchango wa chakula ambacho hakula.
5. Shule ziruhusu bidhaa ya chakula kuuzwa maeneo ya shule maana kuna baadhi ya shule hupiga stop uuzwaji wa aina yoyote ya chakula hata mihogo, maandazi nk kwenye vipindi vya breakfast na lunch ili iwe kama adhabu ya kuwashindisha njaa wanafunzi na aone umuhimu wa kulipia mchango wa chakula.
Mwisho,
Katika pita pita zangu nimekutana na hii Parent Report form ya mwanafunzi x kwa Mzazi wake Mwaka 2014. Aloo kwa sasa ukiisoma kwenye kipengele cha mengineo kinachohusu Michango na Ada utastaajabu sana. Si chini ya michango 10 mzazi aliyokuwa akichangishwa katika shule husika.
1. Ada: 20,000 /=
2. Mchango wa chakula: 80,000/=
3. *Mchango wa watumishi: 21,000/=
4. Mchango wa Taaluma: 20,000/=
5. *Mchango wa Uzio : 15,000/=
6. Ada ya mtihani pre-national kidato cha pili: 10,000/=
7. Necta kidato cha pili: 10,000/=
8. Pre- National kidato cha Nne: 15,000/=
9. Necta kidato cha Nne. 35,000/=
10. *Mchango ujenzi choo cha watumishi: 15,000/=
Nadhani kwa sasa wazazi wanaowapeleka watoto wao shule hiyo wanafurahia sana kukisekana kwa michango na fedha hizo ambazo wangetoa kulipia michango bila Shaka zinatumika kwenye shughuli nyingine za maendeleo hivo kupiga vita Umasikini. Viva Awamu ya Sita Viva Dkt Raisi Samia Suluhu Hassani unaeishi na kutekeleza ndoto za myangulizi wako hayati JPM kwenye swala la Elimu bure. Kazi Iendeleeeeee!
Hili nalo lilikuwa ni kichaka cha baadhi ya Wakuu wa shule kujinemeesha kupitia hiyo Michango na mwisho wa siku ilikuwa ni mzigo mkubwa kwa wananchi wa hali ya chini kisomesha watoto wao.
Kwa kufuta Ada pamoja na michango mingine mashuleni hii ninpongezi kubwa sana kwa Serikali yetu.
NB: Japo kuwa serikali ilifanikisha kupiga marufuku na kuzuia michango mashuleni , huu mchango wa chakula Bado ni sugu na mwiba kwa wananchi. Wengi wanashindwa kuumudu na shule za hapa nchini zina viwango tofauti vya mchango huo na umekuwa njia ya kupitisha na kuhalalisha Michango mingine. Huwezi Amani kuna baadhi ya shule mchango wa chakula umefika Hadi Laki moja na usheee!
Chukulia mwananchi wa hali ya chini mwenye watoto watutu (3) shule moja na wote anapaswa kuwalipia mchango wa chakula kila mmoja tsh 100,000 maana yake anapaswa kulipa tsh Laki tatu.
Na mbaya zaidi kwa baadhi ya shule Hata kama mtoto hajala chakula cha shule kwa Mwaka mzima au kwa miaka minne alazimika kulipa gharama zote za Mchango chakula kwa miaka minne amalizapo kidato cha Nne. ( 10,000 x 4)
Wazazi wengi na wadau wengi wa Elimu wanashauli na kupendekeza yafuatayo kuhusu mchango sugu wa chakula kwa baadhi ya shule
1. Serikali iweke fungu la Chakula kwenye ile hela ya Ruzuku (capitation fee) mashuleni ili kutamatisha huu usemi wa Elimu bila malipo maana mchango wa chakula umekuwa mzigo mzito kwa maananchi mlala hoi.
Kama Serikali itaendelea kuruhusu mchango wa chakula mashuleni ulipwe na WAZAZI tafsiri yake ni kwamba Serikali imewapunguzia tu Michango kwa kumlioia mwanafunzi Michango ya Ada ya mitihani, Ada ya Shule (20000) nk na kumwachia mzazi au Mlezi atoe mchango wa 80,000 Hadi 100,000+ kwa ajili ya chakula kwa baadhi ya shule maana si shule zote hapa nchini wanafunzi wanakula chakula.
2. Mchango wa chakula mashuleni ufutwe kama Michango mingine maana ni kichaka cha kuhalalisha na kupitisha michango mingine.
3. Mchango wa chakula uwe hiari katika halmashauri na shule zinazotoa chakula. Wachangishwe wanaokula au waliokula chakula hicho na shule ziwe na data base y’a wanafunzi wanaokula.
4. Kama maanafunzi hajala chakula cha shule kwa term nzima ama mwaka mzima ama kwa kipindi chote alichosoma shule husika basi amalizapo kidato cha Nne asilipishwe mchango wa chakula ambacho hakula.
5. Shule ziruhusu bidhaa ya chakula kuuzwa maeneo ya shule maana kuna baadhi ya shule hupiga stop uuzwaji wa aina yoyote ya chakula hata mihogo, maandazi nk kwenye vipindi vya breakfast na lunch ili iwe kama adhabu ya kuwashindisha njaa wanafunzi na aone umuhimu wa kulipia mchango wa chakula.
Mwisho,
Katika pita pita zangu nimekutana na hii Parent Report form ya mwanafunzi x kwa Mzazi wake Mwaka 2014. Aloo kwa sasa ukiisoma kwenye kipengele cha mengineo kinachohusu Michango na Ada utastaajabu sana. Si chini ya michango 10 mzazi aliyokuwa akichangishwa katika shule husika.
1. Ada: 20,000 /=
2. Mchango wa chakula: 80,000/=
3. *Mchango wa watumishi: 21,000/=
4. Mchango wa Taaluma: 20,000/=
5. *Mchango wa Uzio : 15,000/=
6. Ada ya mtihani pre-national kidato cha pili: 10,000/=
7. Necta kidato cha pili: 10,000/=
8. Pre- National kidato cha Nne: 15,000/=
9. Necta kidato cha Nne. 35,000/=
10. *Mchango ujenzi choo cha watumishi: 15,000/=
Nadhani kwa sasa wazazi wanaowapeleka watoto wao shule hiyo wanafurahia sana kukisekana kwa michango na fedha hizo ambazo wangetoa kulipia michango bila Shaka zinatumika kwenye shughuli nyingine za maendeleo hivo kupiga vita Umasikini. Viva Awamu ya Sita Viva Dkt Raisi Samia Suluhu Hassani unaeishi na kutekeleza ndoto za myangulizi wako hayati JPM kwenye swala la Elimu bure. Kazi Iendeleeeeee!