Ushauri: Chakula Bure mashuleni kirudishwe ili kuboresha uelewa wa wanafunzi

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
15,126
22,620
Twende haraka kwenye mada.


Mama mwenye Upendo Kwa wanae, Yuko radhi ashinde njaa, ajinyime kununua kipande Cha kanga Ili mtoto wake apate kula chakula na kupata mahitaji muhimu, Watoto mashuleni katika shule za kata ni watoto wa Serikali wawapo mashuleni.

Viongozi wengi wa juu waliopo sasa ni mashuhuda kuwa zamani wanafunzi tulikula mashuleni Bure uji, ugali wa wanga, Hadi maziwa, tulionekana Kwa nje maskini lakini tulipata huduma muhimu ya CHAKULA muhimu shuleni na Elimu ilipaa na kuthaminika sana. Nini kimetokea, mbona mmebadilika ghafula?

Wazazi wanapokabidhi watoto wao Kwa Serikali kupitia shule za kata Ili wapewe Elimu, ni JUKUMU la Serikali kuhakikisha watoto wanapatachochote kitu tumboni Ili masomo yaeleweke na kumrahisishia mwalimu kufundisha Kwa muda wawapo shuleni.


ELIMU Bora inachagizwa na Mazingira Bora ya kufundishia kama madarasa, walimu wenye Viwango Bora, Madawati, nk nk

Uwezo wa kulisha wanafunzi wetu tunao, Nia tunayo? Ari tunayo kuhakikisha watoto wanapata chakula Bure mashuleni.?

Kuna watoto shule za msingi na sekondari wanatembea zaidi ya 5km kwenda na kurudi shuleni, na hurudi jioni saa kumi Hadi 12 jioni bila kula chochote shuleni, kusoma imekuwa ADHABU?

Nikisema Serikali itoe chakula Bure mashuleni, haimaanishi Bure, wazazi wanalipa Kodi serikalini Kwa njia mbalimbali.

Pia wazazi wengi Hasa wazazi wakulima wanalima chakula na kikiuza katika maghala ya Serikali.

Hivyo pakiwepo Nia thabiti, tunaweza kuhakikisha tunaanza japo na UJI mashuleni, wanafunzi wapate japo kikombe kimoja.

Shule Zina Utaratibu wa kuwafungia watoto mashuleni Hadi jioni saa kumi bila kula chochote.

Nauliza, hivi mtoto wa MKULIMA aliyetoka nyumbani bila kula chochote nyumbani wazazi wakienda shambani kulima, anawezaje kuelewa nasomo darasani bila kula chochote ?

Narudia tena, Serikali haitapata HASARA yoyote kuhakikisha wanafunzi wanapata japo kikombe Cha uji mashuleni Nchi nzima.

Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.

Angalizo: Katika chaguzi zijazo msipokuja na HOJA nzito na muhimu kama Chakula mashuleni, maji safi, Nishati ya umeme shule za vijijini Kwa wanafunzi kujisomea usiku,sahauni kuchaguliwa.

Karibuni, Amen.
 
Twende haraka kwenye mada.

Uwezo tunao, Nia tunayo? Ari tunayo kuhakikisha watoto wanapata chakula Bure mashuleni?

Nikisema Bure haimaanishi Bure, wazazi wanalipa Kodi serikalini Kwa njia mbalimbali.

Pia wazazi wengi Hasa wazazi wakulima wanalima chakula na kikiuza katika maghala ya Serikali.

Hivyo pakiwepo Nia thabiti, tunaweza kuhakikisha tunaanza japo na UJI mashuleni, wanafunzi wapate japo kikombe kimoja.

Shule Zina Utaratibu wa kuwafungia watoto mashuleni Hadi jioni saa kumi bila kula chochote.

Nauliza, hivi mtoto wa MKULIMA aliyetoka nyumbani bila kula chochote nyumbani wazazi wakienda shambani kulima, anawezaje kuelewa nasomo darasani bila kula chochote ?

Narudia tena, Serikali haitapata HASARA yoyote kuhakikisha wanafunzi wanapata japo kikombe Cha uji mashuleni Nchi nzima.

Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.

Karibuni, Amen.
Aiseh!

Nimefundisha vijana wakilalamika njaa zinawauma!hadi HURUMA kabisa!!

Wazazi wengine wazito kutoa michango ya shule!!

Watasema serikali ina majukumu na haiwezi wakati wanalipana mabilion ya pesa kama posho na mishahara!!
 
Aiseh!

Nimefundisha vijana wakilalamika njaa zinawauma!hadi HURUMA kabisa!!

Wazazi wengine wazito kutoa michango ya shule!!

Watasema serikali ina majukumu na haiwezi wakati wanalipana mabilion ya pesa kama posho na mishahara!!
Kikombe Cha uji tu, HAKIKA tungepata baraka kama nchi.

Viongozi wetu kuweni na huruma, punguzeni matumizi mabaya Tuhakikishe ELIMU yetu inakua.

Waziri wa ELIMU na KILIMO waliangalie hili.

Maendeleo yanaanza na chochote tumboni!!

Vijijini watoto wanaona shule ni ADHABU!!

Mwl Nyerere aliweza kuhakikisha tunakula chakula shuleni na hakuwa na wawekezaji ktk migodi,

Tunakwama wapi?
 
Twende haraka kwenye mada.


Mama mwenye Upendo Kwa wanae, Yuko radhi ashinde njaa, ajinyime kununua kipande Cha kanga Ili mtoto wake apate kula chakula na kupata mahitaji muhimu, Watoto mashuleni katika shule za kata ni watoto wa Serikali wawapo mashuleni.

Wazazi wanapokabidhi watoto wao Kwa Serikali kupitia shule za kata Ili wapewe Elimu, ni JUKUMU la Serikali kuhakikisha watoto wanapatachochote kitu tumboni Ili masomo yaeleweke na kumrahisishia mwalimu kufundisha Kwa muda wawapo shuleni.


ELIMU Bora inachagizwa na Mazingira Bora ya kufundishia kama madarasa, walimu wenye Viwango Bora, Madawati, nk nk

Uwezo wa kulisha wanafunzi wetu tunao, Nia tunayo? Ari tunayo kuhakikisha watoto wanapata chakula Bure mashuleni.?

Kuna watoto shule za msingi na sekondari wanatembea zaidi ya 5km kwenda na kurudi shuleni, na hurudi jioni saa kumi Hadi 12 jioni bila kula chochote shuleni, kusoma imekuwa ADHABU?

Nikisema Serikali itoe chakula Bure mashuleni, haimaanishi Bure, wazazi wanalipa Kodi serikalini Kwa njia mbalimbali.

Pia wazazi wengi Hasa wazazi wakulima wanalima chakula na kikiuza katika maghala ya Serikali.

Hivyo pakiwepo Nia thabiti, tunaweza kuhakikisha tunaanza japo na UJI mashuleni, wanafunzi wapate japo kikombe kimoja.

Shule Zina Utaratibu wa kuwafungia watoto mashuleni Hadi jioni saa kumi bila kula chochote.

Nauliza, hivi mtoto wa MKULIMA aliyetoka nyumbani bila kula chochote nyumbani wazazi wakienda shambani kulima, anawezaje kuelewa nasomo darasani bila kula chochote ?

Narudia tena, Serikali haitapata HASARA yoyote kuhakikisha wanafunzi wanapata japo kikombe Cha uji mashuleni Nchi nzima.

Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.

Karibuni, Amen.
Naunga mkono hoja suala la diko shulen ni muhim san, huez soma class na yaingie akilin huku una nenge!!
 
Kikombe Cha uji tu, HAKIKA tungepata baraka kama nchi.

Viongozi wetu kuweni na huruma, punguzeni matumizi mabaya Tuhakikishe ELIMU yetu inakua.

Waziri wa ELIMU na KILIMO waliangalie hili.

Maendeleo yanaanza na chochote tumboni!!

Vijijini watoto wanaona shule ni ADHABU!!

Mwl Nyerere aliweza kuhakikisha tunakula chakula shuleni na hakuwa na wawekezaji ktk migodi,

Tunakwama wapi?
kilimanjaro asilimia kubwa za shule wanakula shuleni sijajua kwa miongo ya karibuni ila nimesoma msingi toka std 3 mpaka O level nikiwa nakula shuleni.

Na Sec ilikuwa pia shule ya kata tena ugali maharage,wali nyama, wali maharahe, ugali nyama, makande. asubuhi uji wa sukari unatiwa mafuta na mboga za majani tulikwa na bustani za kutosha.
 
kilimanjaro asilimia kubwa za shule wanakula shuleni sijajua kwa miongo ya karibuni ila nimesoma msingi toka std 3 mpaka O level nikiwa nakula shuleni.
Na sec ilikuwa pia shule ya kata tena ugali maharage,wali nyama, wali maharahe, ugali nyama, makande. asubuhi uji wa sukari unatiwa mafuta na mboga za majani tulikwa na bustani za kutosha.
Ndugu apeche alolo, nakubaliana nawe kabisa,

Kilimanjaro wameweza sana ktk hili.

Tuige mfano huo iwe sera ya nchi nzima,

Wazazi waelimishwe na kuhamasika kushirikiana na shule kuhakikisha wanafunzi mashuleni wanapata chakula.

Watoto wengine wakishakula shuleni nyumbani huenda kulala njaa sababu ya Umaskini.

Upendo huonyeshwa Kwa mambo madogo.
 
Ndugu apeche akili, nakubaliana nawe kabisa,

Kilimanjaro wameweza sana ktk hili.

Tuige mfano huo iwe sera ya nchi nzima,

Wazazi waelimishwe na kuhamasika kushirikiana na shule kuhakikisha wanafunzi mashuleni wanapata chakula.

Watoto wengine wakishakula shuleni nyumbani huenda kulala njaa sababu ya Umaskini.

Upendo huonyeshwa Kwa mambo madogo.
kanisa mkuu kama kule iko hivi kila mwanafunzi wa shule ya msingi kwa mwaka mzazi anatoa mahindi debe na maharage sado moja na kuna stoo za shule zenye matank ambapo kila aletae anapewa na risiti anarudisa kwa wazazi. pili kwa swala la kuni ilikuwa ni kila week kuna kuwahi kushika namba mwisho saa 1 watakaokuja baada ya hapo adhabu ni kuleta kuni 5 kila mmoja kwa shule nzima walio chelewa sasa kwa mfumo huu mdogo hawpati shida
 
Nashukuruu sana kwa mchango wako na wazo lako lenye lengo la kuona shule panakuwa mahali ambapo mwanafunzi anafurahia kujifunza na siyo kuwa kama gereza kwa kuteseka na njaa kwakuwa mrefu.

Lakini kitu ambacho ningependa kukwambia ni kuwa mimi niliko na maeneo mengi tu wanafunzi wanapata uji asubuhi na chakula cha mchana pia.Hii inafanyika kwa michango inayotolewa na wazazi wenye watoto katika shule husika. Ambapo kikao cha wazazi huitishwa na walimu huwaeleza wazazi juu ya umuhimu wa wanafunzi kupata chakula shuleni na mwisho wazazi kushirikiana na walimu hupanga kiasi cha mchango wa vyakula vitakavyo changa na kila mzazi kwa kila mwanafunzi.

Hivyo kama huko uliko hakuna utaratibu huo nakushauri peleka wazo katika kikao cha wazazi ili kuanze utaratibu wa wanafunzi kupata chakula shuleni kama ilivyo kwa maeneo mengi tu nchini
 
Nashukuruu sana kwa mchango wako na wazo lako lenye lengo la kuona shule panakuwa mahali ambapo mwanafunzi anafurahia kujifunza na siyo kuwa kama gereza kwa kuteseka na njaa kwakuwa mrefu.

Lakini kitu ambacho ningependa kukwambia ni kuwa mimi niliko na maeneo mengi tu wanafunzi wanapata uji asubuhi na chakula cha mchana pia.Hii inafanyika kwa michango inayotolewa na wazazi wenye watoto katika shule husika. Ambapo kikao cha wazazi huitishwa na walimu huwaeleza wazazi juu ya umuhimu wa wanafunzi kupata chakula shuleni na mwisho wazazi kushirikiana na walimu hupanga kiasi cha mchango wa vyakula vitakavyo changa na kila mzazi kwa kila mwanafunzi.

Hivyo kama huko uliko hakuna utaratibu huo nakushauri peleka wazo katika kikao cha wazazi ili kuanze utaratibu wa wanafunzi kupata chakula shuleni kama ilivyo kwa maeneo mengi tu nchini
Ni KAZI na wajibu wa wizara ya ELIMU kuhakikisha inakuja na mpango kabambe kuhakikisha jambo hili linafanikiwa Nchi nzima.

Mazingira ya sehemu au wazazi eneo Moja Si sawa Nchi nzima,

Hivyo jambo Hilo liangaliwe Kwa makini.

Mfano Kilimanjaro mwamko ni mkubwa, lakini yapo maeneo kutokana na Umaskini mkubwa jambo hili linakuwa gumu, hivyo mkono wa sirikalini unahitajika.
 
Ni KAZI na wajibu wa wizara ya ELIMU kuhakikisha inakuja na mpango kabambe kuhakikisha jambo hili linafanikiwa Nchi nzima.

Mazingira ya sehemu au wazazi eneo Moja Si sawa Nchi nzima,

Hivyo jambo Hilo liangaliwe Kwa makini.

Mfano Kilimanjaro mwamko ni mkubwa, lakini yapo maeneo kutokana na Umaskini mkubwa jambo hili linakuwa gumu, hivyo mkono wa sirikalini unahitajika.
Kikubwa ni Elimu kuwapa wazazi ili watambue umuhimu wa jambo hili na kushirikiana na serikali kutoa michango itakayowezesha wanafunzi wanapata chakula wawapo shuleni,na hivyo kusoma kwa utulivu na amani pasipo kuwa na mawazo ya njaa.
 
Kikubwa ni Elimu kuwapa wazazi ili watambue umuhimu wa jambo hili na kushirikiana na serikali kutoa michango itakayowezesha wanafunzi wanapata chakula wawapo shuleni,na hivyo kusoma kwa utulivu na amani pasipo kuwa na mawazo ya njaa.
Naona Bado hunielewi Lucas,

Naongelea hapa mchango wa Sirikali kuziba gap linaloachwa Kwa wazazi wa watoto maskini wasio na uwezo,

Serikali kupitia Mkurugenzi wa Jiji au Halmashauri anaweza kukusanya michango Toka Kampuni na taasisi binafsi mbalimbali katika mji au Jiji kuhakikisha kinachopatikana kinaenda kusaidia shule husika katika himaya yake kiuongozi, mapungufu yakitokea, aombe msaada wizara husika.

Hili lifanyike Nchi nzima na liingizwe katika sera na mipango yetu kibudget.

Muhimu ni Serikali kupunguza matumizi mabaya ya pesa za umma.
 
Sio chakula tu,mpaka usafiri kwa Wanafunzibuwe bure,ifike hatua serikali iache matumizi ya anasa na kuwekeza kwenye Elimu.
Ingetungwa SHERIA kabisa sharti watoto wote wa viongozi wa umma wasome shule za kata.

Mazingira na ELIMU ingeboreshwa haraka sana.

Zamani tulisoma wote, lakini saizi viongozi wanaweka matabaka.
 
Twende haraka kwenye mada.


Mama mwenye Upendo Kwa wanae, Yuko radhi ashinde njaa, ajinyime kununua kipande Cha kanga Ili mtoto wake apate kula chakula na kupata mahitaji muhimu, Watoto mashuleni katika shule za kata ni watoto wa Serikali wawapo mashuleni.

Viongozi wengi wa juu waliopo sasa ni mashuhuda kuwa zamani wanafunzi tulikula mashuleni Bure uji, ugali wa wanga, Hadi maziwa, tulionekana Kwa nje maskini lakini tulipata huduma muhimu ya CHAKULA muhimu shuleni na Elimu ilipaa na kuthaminika sana. Nini kimetokea, mbona mmebadilika ghafula?

Wazazi wanapokabidhi watoto wao Kwa Serikali kupitia shule za kata Ili wapewe Elimu, ni JUKUMU la Serikali kuhakikisha watoto wanapatachochote kitu tumboni Ili masomo yaeleweke na kumrahisishia mwalimu kufundisha Kwa muda wawapo shuleni.


ELIMU Bora inachagizwa na Mazingira Bora ya kufundishia kama madarasa, walimu wenye Viwango Bora, Madawati, nk nk

Uwezo wa kulisha wanafunzi wetu tunao, Nia tunayo? Ari tunayo kuhakikisha watoto wanapata chakula Bure mashuleni.?

Kuna watoto shule za msingi na sekondari wanatembea zaidi ya 5km kwenda na kurudi shuleni, na hurudi jioni saa kumi Hadi 12 jioni bila kula chochote shuleni, kusoma imekuwa ADHABU?

Nikisema Serikali itoe chakula Bure mashuleni, haimaanishi Bure, wazazi wanalipa Kodi serikalini Kwa njia mbalimbali.

Pia wazazi wengi Hasa wazazi wakulima wanalima chakula na kikiuza katika maghala ya Serikali.

Hivyo pakiwepo Nia thabiti, tunaweza kuhakikisha tunaanza japo na UJI mashuleni, wanafunzi wapate japo kikombe kimoja.

Shule Zina Utaratibu wa kuwafungia watoto mashuleni Hadi jioni saa kumi bila kula chochote.

Nauliza, hivi mtoto wa MKULIMA aliyetoka nyumbani bila kula chochote nyumbani wazazi wakienda shambani kulima, anawezaje kuelewa nasomo darasani bila kula chochote ?

Narudia tena, Serikali haitapata HASARA yoyote kuhakikisha wanafunzi wanapata japo kikombe Cha uji mashuleni Nchi nzima.

Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.

Angalizo: Katika chaguzi zijazo msipokuja na HOJA nzito na muhimu kama Chakula mashuleni, maji safi, Nishati ya umeme shule za vijijini Kwa wanafunzi kujisomea usiku,sahauni kuchaguliwa.

Karibuni, Amen.
Unatuomba sisi au unamwambia SAMIA
 
Twende haraka kwenye mada.


Mama mwenye Upendo Kwa wanae, Yuko radhi ashinde njaa, ajinyime kununua kipande Cha kanga Ili mtoto wake apate kula chakula na kupata mahitaji muhimu, Watoto mashuleni katika shule za kata ni watoto wa Serikali wawapo mashuleni.

Viongozi wengi wa juu waliopo sasa ni mashuhuda kuwa zamani wanafunzi tulikula mashuleni Bure uji, ugali wa wanga, Hadi maziwa, tulionekana Kwa nje maskini lakini tulipata huduma muhimu ya CHAKULA muhimu shuleni na Elimu ilipaa na kuthaminika sana. Nini kimetokea, mbona mmebadilika ghafula?

Wazazi wanapokabidhi watoto wao Kwa Serikali kupitia shule za kata Ili wapewe Elimu, ni JUKUMU la Serikali kuhakikisha watoto wanapatachochote kitu tumboni Ili masomo yaeleweke na kumrahisishia mwalimu kufundisha Kwa muda wawapo shuleni.


ELIMU Bora inachagizwa na Mazingira Bora ya kufundishia kama madarasa, walimu wenye Viwango Bora, Madawati, nk nk

Uwezo wa kulisha wanafunzi wetu tunao, Nia tunayo? Ari tunayo kuhakikisha watoto wanapata chakula Bure mashuleni.?

Kuna watoto shule za msingi na sekondari wanatembea zaidi ya 5km kwenda na kurudi shuleni, na hurudi jioni saa kumi Hadi 12 jioni bila kula chochote shuleni, kusoma imekuwa ADHABU?

Nikisema Serikali itoe chakula Bure mashuleni, haimaanishi Bure, wazazi wanalipa Kodi serikalini Kwa njia mbalimbali.

Pia wazazi wengi Hasa wazazi wakulima wanalima chakula na kikiuza katika maghala ya Serikali.

Hivyo pakiwepo Nia thabiti, tunaweza kuhakikisha tunaanza japo na UJI mashuleni, wanafunzi wapate japo kikombe kimoja.

Shule Zina Utaratibu wa kuwafungia watoto mashuleni Hadi jioni saa kumi bila kula chochote.

Nauliza, hivi mtoto wa MKULIMA aliyetoka nyumbani bila kula chochote nyumbani wazazi wakienda shambani kulima, anawezaje kuelewa nasomo darasani bila kula chochote ?

Narudia tena, Serikali haitapata HASARA yoyote kuhakikisha wanafunzi wanapata japo kikombe Cha uji mashuleni Nchi nzima.

Kiongozi wetu mkuu wa sasa ni mama na mwenye vichengerwa kadhaa, tafadhali unaweza kukumbukwa hata Kwa hili jambo dogo lenye mchango mkubwa sana mbeleni.

Angalizo: Katika chaguzi zijazo msipokuja na HOJA nzito na muhimu kama Chakula mashuleni, maji safi, Nishati ya umeme shule za vijijini Kwa wanafunzi kujisomea usiku,sahauni kuchaguliwa.

Karibuni, Amen.
What do you mean? What is kirudoshwe, kwani kilikuwapo? Hii ni hoja nzuri, weka kwenye Ilani akiiweka mbowe itasikika vizuri. Ila kama ni tundulissu hata hawo watoto wa shule watatapoka kwanza matusi yatakayotolewa something like MACCM WANAIBA CHAKULA CHENU WANAWAPA WAARABU. Ni hoja nzuri lakini.
 
Wazo zuri, sema wazazi waelimishwe kutoa michango, ila kusema serikali iwalipie kila kitu ni kulemezana,
Halafu hapo hapo serikali itapata kichaka cha kutoongeza mishahara au kuajiri
 
What do you mean? What is kirudoshwe, kwani kilikuwapo? Hii ni hoja nzuri, weka kwenye Ilani akiiweka mbowe itasikika vizuri. Ila kama ni tundulissu hata hawo watoto wa shule watatapoka kwanza matusi yatakayotolewa something like MACCM WANAIBA CHAKULA CHENU WANAWAPA WAARABU. Ni hoja nzuri lakini.
Chakula kinachogharimiwa na sirikali kilikuwepo, hata ukimuuliza Ndugu Wassira atakubaliana nami.

Kwann kimeondoshwa wakati wao walinufaika nacho?

NB:Naongea Leo Ili Ilani za vyama viyachukue,

Mwenye kuja na Ilani nzuri ndiye atakayepewa kuongoza.
 
Back
Top Bottom