Kasoro kubwa katika video ya Lwakatare

Kasoro kubwa katika video ya Lwakatare

Tatizo la Tanzania sio CCM tu ni watanzania wote kwa nafasi zetu mbali mbali tulizokuwa nazo.

Hebu niambie:

1) CCM itajuaje kama mimi nikiwa mtumishi wa TRA nimeshirikiana na wafanyabiashara katika kukwepa kodi (Collusion)?

2) CCM itajuaje kama nyara za serikali zimetoroshwa nje ya nchi ikiwa watanzania waliopewa nafasi kwenye maeneo hayo watashirikiana na maharamia kutosha nyara za serikali (collussion)?

3) CCM itajuaje kama kuna watumishi wa umma wanaoongeza bei katika manunuzi kwa kushirikiana na wauzaji na hivyo kupandisha gharama za manunuzi ya serikali (procurement frauds)?

4) Zile overtime mnazopewa wakati muda wa kawaida mnautumia kukesha JF na kucheza karata. Unafikiri ni CCM pia?

Tatizo sio CCM pekee na serikali, ni sisi watazania kwanza inabidi tubadilike kuwa na moyo wa uzalendo ndipo mambo yatakapobadilika for good katika nchi yetu.

Bila kuwajibika, si CHADEMA wala chama chochote cha upinzani kitakachoweza kuleta the so called mabadiliko ya kweli Tanzania.

Amka usidanganywe badilika wewe kwanza na umwambie mwenzako abadilike.

Pamoja tunaweza.
Bocho kwa sehemu uko sahihi lakini ujue huu ni mfumo (system) na mfumo hujengwa kwa sheria, kanuni na taratibu ambazo sheria mama yake ni Katiba! Katiba yetu mbovu hatujaweza kusimamisha mihimili 3 ya dola ambayo inajitegemea..Rais (Executive) ana mkono kwenye mhimili wa Sheria (Judiciary) na Wawakilishi wa wananchi (Parliament) hili ni kosa kubwa sana ambalo Katiba yetu inalo! Na usidhani hii ilikuja tu, iliwekwa na watu kwa lengo la kumfanya Rais atawale na siyo kuongoza! Sasa unayoyaona leo katika nchi hii ni matokeo ya katiba hiyo! Inakuwaje mfano waziri awe na uwezo wa kulifungia gazeti (Mf Mwanahalisi issue)? Serikali (Executive) ilitakiwa iende mahakamani kulalamika na ipeleke ushahidi utolewe Gazeti husika likionekana na hatia ndipo lifungiwe au lipigwe faini! Sasa unachokiona ndio kiini macho tulichonacho kwenye Katiba yetu! Watu hawawajibiki kwa sababu Executive haiwajibiki (Top-down), executive ipo corrupt so are other officials because that's what they see from their bosses up there!! Ukweli ni kwamba accountability Tanzania ipo kwa kiwango kidogo sana siyo zaidi ya 25%, kwingine kote ni ujanja ujanja tu! It is very pathetic! Gharama ya kuubadilisha mfumo inaweza kuwa detrimental kwa Chama tawala, hilo wanalijua na ndio maana wameamua ni heri hali ibaki kama ilivyo (STATUS QUO & BUSINESS AS USUAL) maana watakuwa na uhakika wa kuendelea kutawala!!
 
Lwakatare sio Mungu wala Malaika, hivyo anaweza kutenda uovu kama mwanadamu mwingine yeyote yule, kuhusu hii video inaweza kuwa ya ukweli lakini vilevile inaweza kuwa ya kupika, wazungu walisema LOVE IS BLIND wale wenzangu na mie wa CCM watatafuta kila uhalali wa kushabikia na kusema ni video ya kweli ,aidha CDM nao watatafuta kila jinsi ya kuhalalisha kuwa video hiyo ni danganya toto. Chamsingi ndugu zangu tutulie tuviachie vyombo vya usalama vifanye kazi zake, tusiporidhika na majibu ndio tuchukue hatua nyingine, may b The Hague teh teh teh!
 
Ingekuwa umefuatilia vizuri post zangu ungegundua kwamba sijakataa uwepo wa hiyo teknolojia.....hoja yangu wangu ni kwamba, huwezi ku-link a real voice kwenye video ikaenda beyond 5 minutes! Umeangalia hiyo ya Obama? Ni ya dakika ngapi? Umesikiliza vizuri hiyo sauti?!
NasDaz habari yako mkuu, naomba nikukumbushe tu ufup wa video ya Obama haimaanish walioiandaa walishindwa kwenda zaid ya hapo. Hiyo iliandaliwa specifically for that short event. Kutoshabihiana kwa sauti ile pia haimaanish utaalam ndo uliishia hapo au that should always be the case, we have not been told yet, kuwa that was the best case scenario. Ile video iliwekwa kuelezea kuwa Technologia ya kulishana maneno ipo hapa dunian ingawa sikusema kuwa Lwakatare kalishwa maneno, naiman post ile bado inasomeka vzr.
 
kitu kikubwa kwenye video hii ukiangalia kwa makini utagundua kuwa lwakatale alikua hajui kama anareodiwa utajuaje?angalia uhusiano wa macho na camera utaona haoneshi kabisa kuangalia camera sababu hana habari na kinachoendelea ni kama wewe unapomchungulia mtu chumbani kwa kupitia dirisha lake mtu huyo akionesha kukaza macho au kuangalia kwa makini dirishani huyo ndio uhusiano wa macho na camera na ukiangalia kwa makini mwanzo kabisa camera inaoneshwa ilikuwa imewashwa na kufichwa chini kisha kuinuliwa mara tu alipoanza kuongea hivyo inaonesha wazi kua ni usaliti aliofanyiwa na wenzake
 
kitu kikubwa kwenye video hii ukiangalia kwa makini utagundua kuwa lwakatale alikua hajui kama anareodiwa utajuaje?angalia uhusiano wa macho na camera utaona haoneshi kabisa kuangalia camera sababu hana habari na kinachoendelea ni kama wewe unapomchungulia mtu chumbani kwa kupitia dirisha lake mtu huyo akionesha kukaza macho au kuangalia kwa makini dirishani huyo ndio uhusiano wa macho na camera na ukiangalia kwa makini mwanzo kabisa camera inaoneshwa ilikuwa imewashwa na kufichwa chini kisha kuinuliwa mara tu alipoanza kuongea hivyo inaonesha wazi kua ni usaliti aliofanyiwa na wenzake
Karibu jamvini kaka...........
 
Mimi najiuliza Lwakatare alikuwana interest gani na mpango huo????
 
Hili si suala la CHADEMA au CCM ni suala la usalama wa nchi kwani wewe unafikiri hiyo CCM ni zaidi ya TANZANIA? hakuna chama cha siasa ambacho ni zaidi ya nchi elewa vizuri siasa tumechoka na madudu ya CCM tunataka kuwapa CCM muda wa kujitafakari kutambua wamekosea wapi sababu sasahivi hawakosoleki kuwasaidia ni kuwatoa madarakani ndipo watakapo pata nafasi ya kujitafakari. Mimi nimecheza Chipukizi najua siasa na ninauchungu wa nchi yangu niko tayari kwa lolote kwa manufaaya nchi yangu.


Chadema mbona mnahangaika sana na Video ya Lwakatare! Tumeiona tume ielewa!
 
Mwigulu nchemba ni mtu ambaye alitakiwa kuwa wa kwanza kuhojiwa kuhusu video aliyosema anayo ikionesha viongozi wa cdm wakipanga mikakati ya kudhuru watu. Ingetakiwa atoe maelezo ya namna alivyoipata hiyo rekodi, ila polisi wetu km kawaida yao hawakuchukua hatua yoyote hadi pale video ya lwakatare ilipo wekwa kwenye mtandao,ndipo walipokurupuka kumkamata lwakatare bila hata ya kuufanyia uchunguzi huo mkanda kama ni wa kweli au ni feki
 
Kitu ambacho watawala hawajaelewa, na hawataelewa hadi watakapotoka madarakani, ni kuwa wao wanafikiri wanapambana na CHADEMA kama CHADEMA. Ukweli ni kwamba CHADEMA ni alama tu ya wale wote wanaotaka mabadiliko katika nchi hii. Yeyote anayekerwa na kuona kuwa mambo hayaendi vizuri, na anayeamini kwamba tupo hivi tulivyo kwa sababu ya CCM na utawala wake, analazimika kuunga mkono CHADEMA, sio tu kama chama, lakini kama alama ya mabadiliko. Kwa hiyo kujaribu kuizima CHADEMA ni kujaribu kuzima dhamira ya ndani kabisa ya mabadiliko ambayo imejikita ndani ya watanzania walio wengi leo. Wafuatiliaji mabadiliko duniani wanaelewa kuwa haiwezekani kuzima kiu na dhamira ya mabadiliko kwa sababu ipo ndani sana ya mioyo ya watu. Ndio maana mipango yote ya kijinga kama hii na isiyo ya kijinga itafeli na CHADEMA itaibuka imara zaidi!

Mkuu Kitila Mkumbo, heshima mbele, kwanza nakubaliana na wewe kuwa kwa sasa Chadema hapa ilipofika sio chama tuu kama chama, its a "movement for change" and as the "wind of change" "sweeping across Tanzania" is gaining more and more momentum, wako wengi watakaozolewa na upepo huu, hivyo kufikia kiwango na kuifanya Chadema iwe "unstoppable" kuingia ikulu 2015!, lakini lazima "chadema" ikubali "ukweli" kuwa inaongozwa na watu na sio malaika!, sasa linapofanyika kosa "dhahiri" lazima "chama" kiwe tayari kuukubali "ukweli" na kubeba "responsibilities" za ukweli huo na sio kwa "negation" kama inavyofanyika sasa!. Nimeisikiliza clip ni "bonafide genuine!".

Pasco.

Pasco najua wewe ni mfuasi wa magamba lakini nilikuwa nakuchukulia ni mtu mwelewa na asiyeweza kusimama upande fulani kama una makosa/au umefanya jambo lisilo jema eti kwa sababu yu wa upande huo..yawezekana nilikuwa wrong. Kwa mazingira ya video ile,timing ya kutolewa kwake na jinsi tu ilivyotolewa inaonyesha dhahiri video hii si ya ukweli ila kwa sababu nawe umekomalia hivyo na kuto reason nje ya gamba la CCM,naomba niseme na mimi nataka kukubaliana na wewe kwamba kweli hii video ni genuine kama utanijibu maswali yangu yafuatayo kwa ufasaha na sio kukwepa kwepa

1. Mwigulu Nchemba alisema anayo video ya viongozi wa chadema wakipanga kufanya mauaji mwanzoni mwa mwaka huu. Swali hapa je kwa ufahamu wako,hii ndiyo video aliyosema anayo au hii ni sehemu tu ya video hiyo,au ni kwamba anazo nyingi au hii video si kati ya zile za mwigulu ni mtu mwingine tu ameiposti? na kama ni mtu mwingine unakubaliana nami kwamba lazima atakuwa ni mwana CCM kama wewe?

2. Hivi unapopanga mauaji,unapanga na watu ambao ulishafanya nao hayo mambo kabla au unaajili mtu na kumfundisha jinsi ya kwenda kuua/kuteka?kama unafanya na watu ulizooea kufanya nao kama Lwakatare anavyomueleza msikilizaji "Kama tulivyofanya kule Igunga" kwa nini uanze kumfundisha mbinu mtu ambaye mlishafanya nae matukio kabla huku naye anaitika tu? Pili ina maana naye hawezi kutoa ushauri kwamba mkuu naona kwa huyu jamaa tufanye hivi....yaani kila kitu yeye ni ndiooo,yap....Utakubaliana nami kwamba kwa hii video yaonekana kabisa Lwakatare yuko na mtu mwingine mmoja tu ikwa sababu sauti zinazooongea ni mbili tu,hivyo basi hata anayemrekodi Lwakatare ni huyo huyo mtu mmoja anayeongea naye? Kama ndivyo na kwa kuwa tukio la kumteka,kumtesa,kumpiga mtu haliwezi kufanywa na mtu mmoja unakubaliana nami kwamba huyu anayeelekezwa hapa ni kiongozi wa hao vijana wanaotumwa kufanya hiyo kazi? kama ndivyo mbona katika haya maongezi hakuonekani kuwa na maelezo elekezi kwa huyu jamaa kupelekea another party bali inaonekana dhahiri ni one to one conversation?

Nataka kwenda na wewe one to one na hii conversation nahitaji majibu yako kwa uwazi..I am waiting..maswali megine yanafuatia!!
 
Mimi nimejiuliza tu kuwa hivi hujuma nzito kama hizi zinapangwa sehemu wazi hivyo, mpaka na watu wanapita na kutoa salaam kabisa.

I hope polisi watafanya kazi yao ipasavyo, na kama kweli kuna uhusika, basi sheria na ichukue mkondo wake.

Polisi wetu ni mazuzu, kazi yao ni kuitikia tu kama huyo kikaragosi asiyeonekana kwenye hiyo video, inawezekana walioitengeneza hiyo video ndiyo hao hao waliomkamata Lwakatare.
 
Voice Changer Software Diamond 6.0 is the most advanced version of the Voice Changer Software series. The utility offers you the ability to add narrations, perform dubbing tasks for audio or video clips. You can also change song voices, create animal sounds, and you can also have so much fun creating E-greeting cards or mimics of other person's voice, for example.

This version offers a faster algorithm to work with voices and a modified interface making it ideal to work in a professional way. The program layout makes it easy to see in the same view important features like the Voice Morpher and the Parody Mixer. Another important thing to remark is the possibility to have a lot of program windows opened at the same time, which makes the work with VCS Diamond easier.
Like the lighter versions, the program works with the major VoIP and Instant Messaging programs.
This version adds other interesting possibilities to the karaoke singer. You can perform modifications to your voice to make it sound different by changing timbre and pitch. You can also add interesting effects like the used in Hollywood with the help of a wide range of presets.
 
Chadema mbona mnahangaika sana na Video ya Lwakatare! Tumeiona tume ielewa!

Mlengo wa kati nadhani wewe ni mlengo wa kulia! System ya ulinzi ya nchi ilivyoambiwa imemsulubub Dr Ulmboka ilifunga gazeti badala ya kujibu hoja sasa cdm wameambiwa wanapanga mauaji unataka watupe mawe? Lah! Wanatumia haki yao ya halali kuonesha hawahusiki!
 
Hii video itawatesa sana naona mnajaribu kufanya cover up lakini ukweli huu wa vitendo vya utesaji ambao umekua ukifanywa na kitengo cha ulinzi na usalama ndani ya chadema utaishi muda mrefu sana.
wale polisi wote waliokuwa wamemzunguka Mwangosi wote walikamatwa?
 
Ushabiki na mapenzi ya kisiasa hapa JF umefikia pabaya sana, hasa ukiangalia juhudi hapa jamvini za kukivisha Chama cha Chadema ngozi ya kondoo wakati ni mbwa mwitu wa kali!!!! Hivi kweli badala ya kulaani kilichofanywa na Rwakatare eti hapa mashabiki wanajitokeza na kujaribu kupotosha ukweli kwa kisingizio cha matumizi ya technolojia.....nasema huu ni uhuni wa ajabu...kwa huu unyama Chadema hamtoki...ni bora mtuambie ukweli kwanini mnapanga mauji wakati nyie ni Chama cha siasa?!!!
wale polisi wote waliomzunguka Mwangosi wakati anauwawa wanastahili kukamatwa maana walitumwa na chadema kumuua Mwangosi, kanzia wao mpaka yule aliyetaka kusema uongo kwamba alitupiwa kitu kutoka kwa waandamanaji
 
ni kweli even me nimesomea hio technolojia lakini huwezi badli lips za mtamkaji msitake kuchange mind za watu kama wana saikolojia
 
wale polisi wote waliomzunguka Mwangosi wakati anauwawa wanastahili kukamatwa maana walitumwa na chadema kumuua Mwangosi, kanzia wao mpaka yule aliyetaka kusema uongo kwamba alitupiwa kitu kutoka kwa waandamanaji

nawashaurini wana JF kuachana na huu mjadala sasa.mliyoyasema yanatosha kama wahusika watachukua maoni yetu na kuyafanyia kazi,that's ok.turudi katika mijadala yetu ya maana zaidi katika kuibana serikali kutenda haki!wale nguli wetu wa kufukunyua mambo hebu mwageni ishu mpya watu tuchangie.tukiendelea na huu kwa muda mrefu jamaa watakuwa wamefanikiwa kuteka mijadala yetu humu tutakalia kuzungumza mambo ambayo Lumumba wanataka tuongee kila siku watatenda tukio na kuvijaza vyombo vya habari na mijadala kuhusu hayo matukio ya kipuuzi huku watu hawana umeme,maji,dawa n.k.hii kesi ya Lwakatare kwa wanaojua sheria ni ndogo tu,hakuna ushahidi mzito.atachomoka tu lakini lengo la kuipaka matope chadema na kuwasahaulisha watu mambo ya msingi kwa kuteka mijadala yao litakuwa limefanikiwa.na wataleta movies kibao kufikia 2015 ili kuua hoja nzito zinazowasambaratisha jukwaani.kuweni na jicho la tatu!
 
Hakika ccm inachelewesha watu kufikiri juu ya mambo ya msingi ya kufanya! Hebu fikiri hii propoganda imefanya uongozi wote wa juu wa cdm kuacha kufikiria mambo ya kuimarisha chama na wamekaa kujadili huu upuuzi wa you-tube feki ya kupika! Wana jf badala ya kupost mambo ya maana wote tumebaki kujadili huu upuuzi! Na watahakikisha watoto wetu mwisho ni form four failure ili kuweza kututawala!:A S shade:
 
Back
Top Bottom